Fm academia, akudo impact nani zaidi?

Fm academia, akudo impact nani zaidi?

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,073
Reaction score
34,844


Hizi ni bendi mbili tofauti zinazopiga muziki wa dansi hapa nchini, ambazo kwa kiasi kikubwa zimejizolea umaarufu kutokana na umahiri wa tungo zao kiasi cha kuwapa wakati mgumu mashabiki kuamua nani mkali kuliko mwenzake katika tasnia ya burudani ya muziki wa dansi hapa nchini... Miongoni mwa masongi ambayo yameimbwa na Bendi hizi na kufanikiwa kuwateka mashabiki vilivyo, ni pamoja na ‘Dunia kigeugeu’ wa Fm Academia a.k.a 'Wazee wa Ngwasuma' na ‘Sifa kwa mwanamke’, wimbo ulioipaisha sana bendi hiyo.

Kwa upande wa Akundo Impact a.k.a 'Wazee wa Masauti', wao wana nyimbo kama ‘Yako wapi mapenzi’ , ‘Mama Vanessa’ na ‘Safari Siyo Kifo’, huku wakitarajia kuachia albamu yao mpya iliyobatizwa jina la History no Change na ndani yake kukiwa na ngoma kama ‘pongezi kwa wenye ndoa’ na Ubinafsi’

Dondosha kura yako utuambie nani yuko juu zaidi kati ya bendi hizi mbili.
 
Back
Top Bottom