FIU kifanye ujajusi wa kiuchumi

FIU kifanye ujajusi wa kiuchumi

Kamanda

Senior Member
Joined
Dec 5, 2007
Posts
151
Reaction score
182
Tanzania ina vitengo viiingiii ya kufuatilia masuala ya usalama. Vipo karibu kila mahali na watendaji wake siyo lazima wajulikane.

Miongoni mwa vitengo hivyo ni kile kinachoitwa Financial Intelligence Unit (FIU), ambacho nadhani kiko chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Pamoja na kwamba hakijulikani sana, lakini naambiwa kazi zake kuwa ni kufuatilia na kuchunguza fedha na mali wanazokuwa nazo wananchi, ambazo zina walakini katika upatikanaji wake.

Naomba kushauri kitu kimoja, pamoja na kazi hizo, ningependekeza FIU wapewe kazi za kufanya ujasusi wa kiuchumi; kudukua na kujua nchi nzingine zinafanyaje kuinuka kiuchumi kupitia viwanda, nguvu kazi zingine, mitaji na zaidi sana kuwa na ushawisi wa kuvuta wawekezaji wakubwa nchini.

Niko tayari kuwashauri namna ya kufanya haya yatokee.

Mnaonaje waungwana wa jukwaa hili? Ushauri wenu tafadhali ili kuboresha.
 
Wazo ni zuri sana na lenye manufaa kwa nchi, Mimi nadhani kingeanzishwa humu humu JF na kupewa jukwaa mahususi kwa ajili hiyo likishirikisha wadau walioko nchini na nje ya nchi. Itapendeza sana!.
 
Mnaonaje waungwana wa jukwaa hili? Ushauri wenu tafadhali ili kuboresha.
Mkuu umenena kitu kizuri sana. Wengi hawajui kuhusu hiki kitengo. Hata hivyo hata mimi nahitaji kukijua zaidi, maana ninaandaa chapisho kuhusu kitengo hiki
 
Mkuu umenena kitu kizuri sana. Wengi hawajui kuhusu hiki kitengo. Hata hivyo hata mimi nahitaji kukijua zaidi, maana ninaandaa chapisho kuhusu kitengo hiki

Wewe utakuwa unavuta bangi za wapi? Unaanda huku hukijui kama kipo? Muda mwingine bora unyamaze tu.
 
Wewe utakuwa unavuta bangi za wapi? Unaanda huku hukijui kama kipo? Muda mwingine bora unyamaze tu.
Ninamashaka kama unajua kusoma wewe. Hebu rudia kusoma kilichoandikwa halafu jipange kuandika. Nguruwe mkubwa wewe
 
Mbona kiko imara kama simba? bungeni mmeambiwa mbadili sheria namba 15 , 1996 TISS ifumuliwe...Zitto kamchana chana Robert Musalika huko Fb...kamsome kisha utapata mwanga wa hicho unachotaka!
 
Tanzania ina vitengo viiingiii ya kufuatilia masuala ya usalama. Vipo karibu kila mahali na watendaji wake siyo lazima wajulikane.

Miongoni mwa vitengo hivyo ni kile kinachoitwa Financial Intelligence Unit (FIU), ambacho nadhani kiko chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Pamoja na kwamba hakijulikani sana, lakini naambiwa kazi zake kuwa ni kufuatilia na kuchunguza fedha na mali wanazokuwa nazo wananchi, ambazo zina walakini katika upatikanaji wake.

Naomba kushauri kitu kimoja, pamoja na kazi hizo, ningependekeza FIU wapewe kazi za kufanya ujasusi wa kiuchumi; kudukua na kujua nchi nzingine zinafanyaje kuinuka kiuchumi kupitia viwanda, nguvu kazi zingine, mitaji na zaidi sana kuwa na ushawisi wa kuvuta wawekezaji wakubwa nchini.

Niko tayari kuwashauri namna ya kufanya haya yatokee.

Mnaonaje waungwana wa jukwaa hili? Ushauri wenu tafadhali ili kuboresha.
Wakutafute kwa ID yako hii feki?
 
Mnataka kikifanya kazi kije kwenye runinga ?
 
Back
Top Bottom