Filikunjombe VS Mtikila - mtendaji VS mwenye blabla

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,899
Mtikila(24).jpg Mtikila VS Filikunjombe 06.jpg

Kusini Nyanda za Juu kumeibua wanasiasa wengi wenye umaarufu ndani ya chama tawala na upinzani. Mmoja ambaye amefanikiwa kutikisa anga la Tanzania kisiasa ni Mtikila ambaye ni mzaliwa wa wilaya ya Ludewa ambayo ni jimbo la uchaguzi la Mbunge Filikunjombe. Ikumbukwe kwamba mara moja Mtikila alishawahi kugombea ubunge kule Ludewa na kurudi kwa aibu bila hata kuambulia theluthi moja ya kura.

Filikunjombe alipoenda kugombea kule hakuwa na umaarufu wa kujulikana kisiasa kitaifa kama ilivyo kwa mchungaji Mtikila, lakini kwa kipindi kifupi tu amejizoelea umaarufu mkubwa jimboni mwake na hata kitaifa kwa msimamo wake kujali utaifa na kutetea haki za wengi na pengine hata kudiriki kuinyoshea kidole serikali bila woga.

Mtikila pamoja na kuwa mwanasiasa aliyediriki kuanzisha chama cha siasa ambacho hakionyeshi kukua ameonekana kutopokeleka kwao kwa vile ni mtu wa blabala za mdomoni licha ya kujenga hoja za msingi. Lakini je, ili kupokeleka kwa wananchi ni kufungua kesi mahakamani na kuishtaki seirkali tu bila kuwasogelea karibu wananchi? Sina mazoea ya kuona Mtikila akifanya mkutano ya hadhara ila mikuano yake ni mahakamani mahakimu na wanasheria.

Wote wawili ni maarufu, lakini mmoja anaonekana kutambulika zaidi kwa wananchi si kwa maneno bali kwa matengo kinyume na mwingine yupo zaidi kwa kauli na mara anaingia mitini, atakaporudi huko sijua atakuna na lipi.
 
Huyu Filikunjombe mnayemmwagia misifa hapa anaonekana mchapa kazi kitaifa kwa sababu hajagusa maslahi ya mafisadi mchini. Huyu hajaitingisha system inayohodhi siasa na uchumi nchini lakini pia, kiwango cha umasikini mkubwa na mwamko katika jimbo lake kuwa chini ndiyo inamfanya aonekane mchapa kazi jimboni kwake hata akifanya mambo kidogo lakini kwao yanaonekana ni makubwa.

Nadhani unafahamu nini kilimtokea Mtikila baada ya kugusa maslahi ya Watanzania ambao ni movers and shakers in the political and economic.

Siasa mara nyingi zinachagizwa na historia kwa maana kuwa, utendaji kisiasa unapimwa mara nyingi na milinganisho ya utendaji uliopita na uliopo.

Labda nitoe mfano mdogo sana ili watu wa enzi hizo wanielewe. Mh. Salim Ahmed Salim alipata umaarufu sana nchini wakati akiwa Waziri Mkuu baada ya kuruhusu nguo za "Mitumba" kuingizwa nchini kwa sababu hali ilikuwa ni mbaya kimavazi kwa sababu kuna maeneo mengi mengine nchini ambapo watu walikuwa wamefikia hatua ya kutengeneza magunia na kuwa ni nguo za kuvaa. Huu ulikuwa ni uamuzi wa kawaida sana lakini kwa vile nchi ilikuwa katika mazingira ya chini sana kimavazi, basi alionekana ni shujaa na mchapa kazi kutokana na milinganisho.

Sijaona kitu cha ajabu kisiasa anachokifanya Mh. Filikunjombe kupewa sifa za aina hii.
 
---- mambo ya msingi ambayo wananchi wanatambua uwepo wa viongozi wao na kuwajali kwa kuwatembelea kusikiliza matatizo yao na kuyafikisha kunakohusika ndilo linalotazamiwa kwa hawa wawakilishi wa wananchi. Pengine yanayofanywa kutoa misaada ingawa wananchi wanafikiri ni haki yao ni ziada tu kwa vile sheria na taratibu hazijaainisha wawakilishi hawa kufanya hayo, huu ni utashi wa mwakilishi mwenyewe anavyoweza kuwajali wananchi wake.

Mchungaji Mtikila ni mtu wa kudandia hoja fulani kitaifa, ni mzuri kujenga hoja nzuri na kuitetea anapoona kuna udhaifu fulani. Lakini udhaifu alio nao ni huu wa kutokuwa karibu na wananchi. Hata masuala muhimu kama haya anayotetea huwa hafanyi jitihada kuelimsha wananchi. Toka hapo ni likizoni hadi anapoona kuna jambo la kwenda mahakamani.

Kuwa kiongozi wa wananchi mwakilishi au kiongozi anatakiwa kuwajongea wananchi si kubaki ofisini na kuongoza wananchi kwa kutumia vyombo vya habari.
 
Mambo aliyoyafanya Mtikila yana impact kitaifa kuliko ya Filikunjombe.
1. Kupigania mgombea binafsi
2. Kupigania serikali ya Tanganyika
 
Mambo aliyoyafanya Mtikila yana impact kitaifa kuliko ya Filikunjombe.
1. Kupigania mgombea binafsi
2. Kupigania serikali ya Tanganyika

Binafsi mambo mengi ambayo Mtikila amepigania ni muhimu kitaifa, pengine anapigania ya juu zaidi ambayo wananchi walio wengi hawayajui umuhimu wake ila watu wa kiwango chako na changu tunaweza kuelewa hivyo.

Ninachoona Mtikila anakosa ushawishi kwa wananchi wa kawaida ila kwa wasomi, hivyo kipimo ni pale aliposhindwa uchaguzi wa ubunge jimboni Ludewa na kuambulia pengine kura yake na ya familia yake tu.

Jambo la msingi katika uongozi wa kisiasa mtu unatakiwa kuwateka wananchi wa kawaida ambao ndio idadi kubwa ya wapiga kura. Hilo limeshindikana kwa Mtikila ndio maana pamoja na umaarufu wake lakini chama chake hakina umaarufu wakati wanasiasa wengine umaarufu wao hukuza vyama vyao vya siasa.
 
Kumbe wewe hujui, mzee Mtikila pamoja na mapungufu yake yupo kitaifa zaidi. Amepambana na swala la Tanganyika na kufikia kusimama nalo mahakamani. Mgombea binafsi alishinda ila waziri mkuu Pinda akalifunika kibabe. Kuelekea katiba mpya tumeelekea kulekule alipopapigania mwenyewe. Kwa wazalendo wa nchi hii, hawawezi kumbeza mzee Mtikila.
 
Ili nchi iamke tunahitaji akina mtikila wengi, wenye uthubutu wa kutikisa mbuyu! So far, zaidi ya publicity anayopewa ndiyo inayomfanya aonekane anafaa. Jambo la kujiuliza nani anampa publicity Filikunjombe? Aliyopigania mtikila yamegusa 'interest' za kila mtanganyika anayejitambua, japo naye kama binadamu ana mapungufu yake.
 
Huyu Filikunjombe mnayemmwagia misifa hapa anaonekana mchapa kazi kitaifa kwa sababu hajagusa maslahi ya mafisadi mchini. Huyu hajaitingisha system inayohodhi siasa na uchumi nchini lakini pia, kiwango cha umasikini mkubwa na mwamko katika jimbo lake kuwa chini ndiyo inamfanya aonekane mchapa kazi jimboni kwake hata akifanya mambo kidogo lakini kwao yanaonekana ni makubwa.

Nadhani unafahamu nini kilimtokea Mtikila baada ya kugusa maslahi ya Watanzania ambao ni movers and shakers in the political and economic.

Siasa mara nyingi zinachagizwa na historia kwa maana kuwa, utendaji kisiasa unapimwa mara nyingi na milinganisho ya utendaji uliopita na uliopo.

well said. The truth is bitter but must be told!
 
Filikunjombe hawezi kumkuta Mtikila

Mtikila alisukumwa kwa gari akikatiza mitaa ya Nkuruma. Kidongo chekundu aiwafokea Magobacholi
Filikunjombe yeye na Wananchi wa Ludewa baada ya kuacha uPOLISI hajawahi hata kusukumwa kwa baiskeli

Mtikila kasukumwa kwa kuzima Gari Dodoma alipofungua Kesi dhidi y Serikali na kushinda
Filikunjombe hathubutu wakati ni POLISI

Mtikila kavurumishwa Tarime wakati wa Kampeni
Filikunjombe hajawahi hutubia hata Mkutano wa Kata zaidi ya Ludewa

Mtikila kampa za Uso Paul Kagame LIVE kuhusu unyama wa Watutsi
Filikunjombe hajafikia kuisema ngazi ya kimataifa.

Mtikila kashtaki Rostam, Mchungaji wake nk kashtakiwa nk

yaani usipime na huyu jamaa aliyeitangaza Bia ya Safaru Lager ikabatizwa Mtikila


 
Mgombea binafsi, serikali ya Tanganyika, kesi kadhaa notable kushinda...ni baadhi ya vitu vinavyomtofautisha na wanasiasa kadhaa
 
Filikunjombe hawezi kumkuta Mtikila

Mtikila alisukumwa kwa gari akikatiza mitaa ya Nkuruma. Kidongo chekundu aiwafokea Magobacholi
Filikunjombe yeye na Wananchi wa Ludewa baada ya kuacha uPOLISI hajawahi hata kusukumwa kwa baiskeli

Mtikila kasukumwa kwa kuzima Gari Dodoma alipofungua Kesi dhidi y Serikali na kushinda
Filikunjombe hathubutu wakati ni POLISI

Mtikila kavurumishwa Tarime wakati wa Kampeni
Filikunjombe hajawahi hutubia hata Mkutano wa Kata zaidi ya Ludewa

Mtikila kampa za Uso Paul Kagame LIVE kuhusu unyama wa Watutsi
Filikunjombe hajafikia kuisema ngazi ya kimataifa.

Mtikila kashtaki Rostam, Mchungaji wake nk kashtakiwa nk

yaani usipime na huyu jamaa aliyeitangaza Bia ya Safaru Lager ikabatizwa Mtikila



Ukisoma vema maelezo yangu unaweza kubaini kwamba Mtikila mdandiaji mzuri wa hoja zinazoonekana kumjengea mazingira ya kupata mwanya katika uongozi, alidandia hoja ya ugombeaji binafsi baada ya kuona kupitia chama chake kuna ukakasi fulani usiompa nafasi.

Mtikila anakubalika kwa hoja lakini hakubaliki kwa wananchi katika kuongoza nchi, na hapana shaka hata akigombea tu udiwani au uenyekiti hataambulia kitu, hiyo ni ishara wazi ya kutokukubalika kwake.

Siasa ya leo ni sayansi, si kuvimbisha mishipa tu kama Mtikila. Wakaribie wananchi ufahamu matatizo yao na wakufahamu ukaribo na unavyowajali si nadharia anayofanya mtikila.

Mtikila ni mbinafsi, hata siku moja hajaonekana kuunga mkono hoja ambazo pengine zinakubalika naye, na pale kambi ya upinzani inapoibua mambo muhimu kitaifa utamwona anakuwa kinyume na kuwasema wenzake, jambao ambalo alitakiwa kuungana na wenzake kuongeza nguvu. Hiyo ni dalili tosha Mtikila ni mbinafsi asiyefaa kuwa kiongozi.

Tangu aanzishe chama cha siasa kiongozi wa juu ni yeye tu wakati vyama vingine walishabadilisha uongozi.
 
MImi namshukuruni sana Mch Mtikila mtujasiri namba moja aliyewahi miezi yakaribuni kutoa waraka nafikiri wanajamvi muliuona uliokuwa ukihamasisha serikali ya nchi yetu kufanya jitihada za haraka juu ya uvamizi wa waharamiaji haramu walio shamiri hasa mikoa yakanda ya ziwa na kigoma wahamiaji hao kutoka nchi za Rwanda,Burundi na nchi nyingine za ukanda huo.Si mwingine ni mchu ngaji huyuhuyu bilakujificha alielezea jinsi wananchi hasa wa jimbo la Muleba,na sehemu nyingine kama Ngote,Karambi Kyebitebe na nyamiranda na vijisehemu vidogovidogo siwezi kuvimalizana jinsi viongozi wa maeneo hayo wanavyo hongwa ng,ombe na waharamiaji hao na akawataja wavamizi na vigogo wakuu kutoka Rwanda wa kuwa ni Kafurama na Mugisha wanaomiliki maelfu ya mifugo katikapori la burigi na kasindaga Nafikili mzee wakaya alipousoma waraka huu hakulala usingizi ulipaa asubuhi yake alipanga safari ya ghafla kuelekea mikoa ya kanda ya ziwa na Kigoma kwakuangalia hali ilivyo nakweri alikuta hivyo na kutangaza rasmi OPERATION KIMBUNGA.wanajanvi naomba tujadili hili....
 
Hawa wote ni magamba tu, kama wanajitambua kweli na wapo kwa maslahi wananchi, ni vyema wakatoka hapo walipo, wakaungana na wapigania haki, kinyume na hapo ni mazuzu, huwezi sema wewe ni mzuri, harafu unaogelea kwenye bwawa linalonuka damu.

:mullet::hand:Hivi wewe sikuelewi hivi unajua nani aliyeanzisha vuguvugu laoperation kimbunga mpaka mzee wa kaya anaingilia kati jamani mnyonge mnyongeni haki yake mpatie.
 
Candid Scope pamoja na kwamba simkubali MTIKILA lakini ni kitu gani alichofanya DEO cha kumlinganisha na MTIKILA ? UMEKOSEA SANA !
 
Candid Scope pamoja na kwamba simkubali MTIKILA lakini ni kitu gani alichofanya DEO cha kumlinganisha na MTIKILA ? UMEKOSEA SANA !

Jaribu kuridia mada na kuisoma, kwamba Mchungaji Mtikila alijaribu kugombea ubunge wilayani kwake Ludewa alichoambulia ni kura yake na wasindikizaji wa familia yake. Dalili tosha anapanga hoja fulani kitaifa lakini ayuko karibu na wananchi ndicho ninachojadili tofauti na kijana Filikunjombe kukubalika na wananchi.
 
Jaribu kuridia mada na kuisoma, kwamba Mchungaji Mtikila alijaribu kugombea ubunge wilayani kwake Ludewa alichoambulia ni kura yake na wasindikizaji wa familia yake. Dalili tosha anapanga hoja fulani kitaifa lakini ayuko karibu na wananchi ndicho ninachojadili tofauti na kijana Filikunjombe kukubalika na wananchi.

Mkuu, kwa nini unamsakama mzee wetu Mikila namna hii? kwani amekufanya nini? kwa nini unamlinganisha na Deo wakati yeye si mwakilishi wa wananchi? Unamsakama kwa kupata kura moja kwa sababu gani? huo ubunge aligombea mwaka gani? je mwaka huo kulikuwa na uelewa wa kiwabgo gani miongoni mwa wananchi kuhusu mfumo wa vyama vingi huko Ludewa? je iwapo Deo angegombea ubunge kupitia chama cha upinzani mwaka huo angeshinda uchaguzi?

Elewa kuwa Mtikila alishindwa kwa kuwa ni mpinzani, angekuwa CCM angeshinda kwani huko Ludewa na njombe kwa ujumla hakuna mbunge wa upinzani kwa kuwa wananchi wanaamini kuwa CCM ndio baba na ndio mama. Naomba mbadilike. Pia naomba umuheshimu mzee wetu kwa mchango wake katika harakati za kudai demokrasia katika Taifa hili ambao tunauthamini sana. Tafadhali sana usimlinganishe na Deo.
 
Mkuu, kwa nini unamsakama mzee wetu Mikila namna hii? kwani amekufanya nini? kwa nini unamlinganisha na Deo wakati yeye si mwakilishi wa wananchi? Unamsakama kwa kupata kura moja kwa sababu gani? huo ubunge aligombea mwaka gani? je mwaka huo kulikuwa na uelewa wa kiwabgo gani miongoni mwa wananchi kuhusu mfumo wa vyama vingi huko Ludewa? je iwapo Deo angegombea ubunge kupitia chama cha upinzani mwaka huo angeshinda uchaguzi?

Elewa kuwa Mtikila alishindwa kwa kuwa ni mpinzani, angekuwa CCM angeshinda kwani huko Ludewa na njombe kwa ujumla hakuna mbunge wa upinzani kwa kuwa wananchi wanaamini kuwa CCM ndio baba na ndio mama. Naomba mbadilike. Pia naomba umuheshimu mzee wetu kwa mchango wake katika harakati za kudai demokrasia katika Taifa hili ambao tunauthamini sana. Tafadhali sana usimlinganishe na Deo.

Jadili hoja iliyopo na kuleta hoja za kuzipiku hoja zangu, kwamba heshima, mara sijui nini, mara mzee wangu hayo lete mada tuijadili.

Nimeshakueleza kwamba Mtikila hayuko karibu na wananchi, ila anadandia hoja fulani na kwenda mahakamani kudai haki itendeke hilo halina ubishi. Kama mtikila yupo karibu na wananchi mbona hata uchaguzi alishindwa vibaya kiasi kwamba hana mvuto kwa wananchi wa kawaida ila tu hoja zake za kisomi zinakubalika kwa wasomi.

Mantiki ya kuwateka wananchi Deo anayo na amaefanikiwa na hata leo Mtikila akisema ajiunge na CCM na kugombea ubunge Ludewa atabwagwa vibaya kwa sababu yeye ni nadharia zaidi kwa wananchi kitu ambacho kinahitajika hivyo kwa wasomi si wananchi wa kawaida.
 
Jaribu kuridia mada na kuisoma, kwamba Mchungaji Mtikila alijaribu kugombea ubunge wilayani kwake Ludewa alichoambulia ni kura yake na wasindikizaji wa familia yake. Dalili tosha anapanga hoja fulani kitaifa lakini ayuko karibu na wananchi ndicho ninachojadili tofauti na kijana Filikunjombe kukubalika na wananchi.

Uchaguzi sio kipimo sahihi.. bado uchaguzi wa Tanzania haujawa Wa huru na haki, tafuta kipimo kingine..
 
Uchaguzi sio kipimo sahihi.. bado uchaguzi wa Tanzania haujawa Wa huru na haki, tafuta kipimo kingine..

Uchaguzi kama usingekuwa wa haki tusingekuwa na wawakilishi toka vyama tofauti ndani ya jamii yetu, kasoro fulani fulani si kiegezo kwamba uchaguzi sio huru wakati sheria za uchaguzi zinaonyesha uhuru katika uchaguzi.
 
Back
Top Bottom