Wakati Rais Dkt. Samia Suluhu anaingia madarakani mwaka 2021 sekta ya utalii ilikuwa inapitia katika mazingira magumu kutokana sababu mbalimbali ikiwemo athari ya UVIKO 19
Mapato ya utalii yalipungua sana, ajira nyingi zikashuka, wanufaika wa sekta hii wakaathirika kiuchumi.
Hata hivyo, ujio wa Rais Samia mwaka 2021 ulibadilisha taswira ya sekta hii kwa kiasi kikubwa, hii ni baada ya kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kuandaa mkakati maalum wa kutangaza vivutio vyetu katika maeneo mbalimbali ya Dunia
Soma pia:
Tukio kubwa lililovutia hisia za wengi na baadae kuzaa matunda ni lile la yeye kushiriki kucheza filamu maarufu ya Royal Tour
Filamu hii iliyokidhi vigezo vya kimataifa ilisaidia sana kuwavutia watalii hasa wale kimataifa kuja nchini.
Katika kipindi kifupi idadi ya watalii ya kimataifa iliongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, ongezeko la asilimia 132.1 huku watalii wa ndani wakiongezeka, kutoka 788,933 mwaka 2021 hadi kufikia 3,218,352 mwaka 2024
Ongezeko hili la watalii limepelekea kuongeza ajira kwa watu milioni 1.5. Licha ya mafanikio haya katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake katika sekta hii, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameahidi kupitia ilani ya uchaguzi wa CCM kuongeza ajira kutoka milioni 1.5 mwaka 2025 hadi milioni 3 mwaka 2030 sambamba na kuongeza idadi ya watalii hadi milioni 8 mwaka 2030
Chanzo: ITV DIGITAL
Mapato ya utalii yalipungua sana, ajira nyingi zikashuka, wanufaika wa sekta hii wakaathirika kiuchumi.
Hata hivyo, ujio wa Rais Samia mwaka 2021 ulibadilisha taswira ya sekta hii kwa kiasi kikubwa, hii ni baada ya kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kuandaa mkakati maalum wa kutangaza vivutio vyetu katika maeneo mbalimbali ya Dunia
Soma pia:
- Pre GE2025 - Makalla: 'Royal tour' imefanya kazi kubwa mikoa ya kaskazini, mapato ya utalii yameongezeka
- Mapato ya Utalii yafikia Trilioni 9. Waliobeza "Royal Tour " wamuombe radhi Rais Samia, amekuwa ni Game Changer wa Uchumi wa Tanzania
Tukio kubwa lililovutia hisia za wengi na baadae kuzaa matunda ni lile la yeye kushiriki kucheza filamu maarufu ya Royal Tour
Filamu hii iliyokidhi vigezo vya kimataifa ilisaidia sana kuwavutia watalii hasa wale kimataifa kuja nchini.
Katika kipindi kifupi idadi ya watalii ya kimataifa iliongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, ongezeko la asilimia 132.1 huku watalii wa ndani wakiongezeka, kutoka 788,933 mwaka 2021 hadi kufikia 3,218,352 mwaka 2024
Ongezeko hili la watalii limepelekea kuongeza ajira kwa watu milioni 1.5. Licha ya mafanikio haya katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake katika sekta hii, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameahidi kupitia ilani ya uchaguzi wa CCM kuongeza ajira kutoka milioni 1.5 mwaka 2025 hadi milioni 3 mwaka 2030 sambamba na kuongeza idadi ya watalii hadi milioni 8 mwaka 2030
Chanzo: ITV DIGITAL