Filamu itakayotoka miaka 100 baada ya kutengenezwa

Filamu itakayotoka miaka 100 baada ya kutengenezwa

Royal Son

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2016
Posts
1,472
Reaction score
2,767
100 Years ni filamu fupi ya majaribio ya kisayansi iliyoandikwa na kuongozwa na John Malkovich na Robert Rodriguez, kwa ushirikiano na kampuni ya vinywaji ya Louis XIII Cognac.

Kilicho cha kipekee kuhusu filamu hii ni kwamba haitatolewa hadi mwaka 2115—miaka 100 baada ya kutengenezwa.

Wazo kuu ni kuonyesha jinsi ulimwengu unavyoweza kubadilika katika karne moja. Filamu hiyo imewekwa kwenye sefu maalum ambayo itafunguliwa kiotomatiki mwaka 2115.

Hadi leo, hakuna mtu yeyote ambaye amepata nafasi ya kuiona, na tunachojua ni kupitia matangazo (teasers) machache ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja na hadithi ya filamu yenyewe.
 
Sasa mimi nitaigiza muvi ya kwenda kuvunja hiyo sefu na naibeba halafu naiweka hadharani halafu dunia kutatokea machafuko kisa hiyo muvi!, maana vitu ambavyo vitakuwemo vitawagusa watu wa karne hii tofauti na watu waliowakusudia hao wajao!.. sisi sasa tutakinukisha balaa...🤣
 
Movie ambayo hata jina hatulijui, sasa hao watu watakaokuwepo sijui watathibitishaje kuwa hiyo movie imeektiwa miaka 100 iliyopita na ulimwengu huu wa AI ikiendelea kutamalaki.
 
Back
Top Bottom