FIFA kuondoa offiside na kubadili upigaji wa penati

Hii ya offside itasababisha beki hata acheze miaka kumi hataweza kufunga labda ajifunge golini kwake, pia swala la kushika ikiwa kadi ya njano kwa mpira uelekeao golini basi kihesabike ni goli
 
Penalty , offside na Substitution zibaki kama zilivyo. zinaleta raha sana na ushindani mchezoni
 
Raisi mpya wa FIFA Gianni Infantino anaonekana kutaka kubadili sola kabisa.Infantino anaonekana kuondoa kila kitu cha Sepp Blatter na kuleta vyake.Baada ya kuongeza timu zitakazoshiriki kombe la dunia 2026 kufikia timu 48 sasa Infantino amekuja na mpya.Kwa kumtumia mkurugenzi wa mambo ya ufundi wa FIFA Marco Van Basten amependekeza baadhi ya sheria mpya katika soka.
Kuondoa offside.

Akihojiwa na gazeti la Ujerumani liitwalo Bild,Van Basten amesema wanawaza kuondoa mchezo wa kuzidi katika soka.Alisema “sipati picha soka isipokuwa na ofside,washambuliaji watapata nafasi nyingi sana za kufunga”.Van Basten alisema mpira wa miguu utakuwa wakuvutia sana kama offside itaondolewa na anaamini jambo hilo litawafurahisha mashabiko na washambuliaji.

Kubadili upigaji wa penati.Van Basten pia anaona kuna haja kubwa kwa FIFA kubadili aina ya upigaji wa penati.Kwa sasa adhabu ya penati mchezaji anauweka mpira mita kadhaa karibu na goli ma kuupiga.Lakini Van Basten anaona penati ibadilishwe.Anataka mpiga penati auweke mpira mita 25 kabla ya goli na kama anaweza atembee nao kuelekea golini kwa muda usiozidi sekunde nane.Aina hii ya upigaji penati sio ngeni kwani mwaka 1999 ilishafanyiwa majaribio nchini Marekani.

Kupunguza adhabu mipira ya kushika.Van Basten anaona kama adhabu ya kadi nyekundu ni kali mno kwa tukio hilo.Na analiona kama tukio dogo lisilohitaji kadi nyekundu na anazani inapaswa ipunguzwe adhabu hiyo.Kusitolewe kadi nyekundu mpira ukishikwa.Adhabu kam ile ya tukio la Luis Suarez mwaka 2010 wakicheza dhidi ya Ghana aliposhika mpira wakati ukiingia golini Van Basten anataka kadi iwe ya njano.

Kapteni awe mtu pekee kuongea na mwamuzi.Kama katika Rugby ni kapteni tu anayeongea na mwamuzi,asiruhusiwe mtu yeyote,mchezaji yeyote kuongea na mwamuzi.
Style ya faulu ya mchezo wa kikapu.Katika mchezo wa kikapu pale mchezaji anapocheza faulu tano anatakiwa atoke uwanjani.Na sasa Van Basten anaamini staili hiyo inapaswa kuletwa katika soka.

Kupunguza idadi ya mechi.Hii itafurahiwa sana na makocha wageni Uingereza.Alianza Van Gaal akaja Jurgen Klopp walilalamikia idadi ya mechi kuwa nyingi Epl.Van Basten anataka idadi ya mechi zipunguzwe kutoka mechi 80 kwa msimu hadi 50 kwa msimu.

Kuongeza idadi ya Substitution.Van Basten anatamani kuongeza idadi ya wachezaji wa sub kuanzia 5-7,kwa muda mrefu wadau wa soka wamekuwa wakizungumzia kuhusu suala la kuongeza wachezaji wa akiba na sasa FIFA inatarajia kuliangalia suala hili.

Kuzifanya dakika 10 za mwisho kutumika ipasavyo.”Tunajua kutokana na kuongeza idadi ya wachezaji wa akiba pamoja na aina ya upigaji penati vitachukua mda mrefu uwanjani na itatubidi kuhakikisha dakika 10 za mwisho zinatumika kiuhakika” Van Basten alisema watahakikisha hakuna upotezaji muda katika dakika zamwisho za mchezo.

Hayo ni mapendekezo tu kutoka kwa mkurugenzi wa ufundi wa FIFA.Na sasa atawasilisha mapendekezo hayo katika kamati ya FIFA yaweze kujadiliwa
Kitu kingine ninacho ina kinafaa kubadilishwa ni timu zikitoka dare mpaka dakika ya 90 basi katika muda wa nyongeza waingie kwanza wachezaji waliokuwa bench na nafasi zitakazo baki zijazwe na waliotoka itapedeza kushirikisha wote
 
filipo inzaghi,rud van neestoroy, nuno gomes

jamaa warud tu kwenye sheria mpya ikifutwa offside kila mechi watatupia goli mia
 
Kupunguza adhabu mipira ya kushika.Van Basten anaona kama adhabu ya kadi nyekundu ni kali mno kwa tukio hilo.

Kapteni awe mtu pekee kuongea na mwamuzi.Kama katika Rugby ni kapteni tu anayeongea na mwamuzi,asiruhusiwe mtu yeyote,mchezaji yeyote kuongea na mwamuzi.

Kuongeza idadi ya Substitution.Van Basten anatamani kuongeza idadi ya wachezaji wa sub kuanzia 5-7,kwa muda mrefu wadau wa soka wamekuwa wakizungumzia kuhusu suala la kuongeza wachezaji wa akiba na sasa FIFA inatarajia kuliangalia suala hili.

Nimezipenda hizo 3;

1. Kupunguza adhabu mipira ya kushika
2. Kapteni awe ndo mtu pekee kuongea na refa
3. Sub zifike 5
 
Ya offside wamechemsha coZ striker atakua anashinda na golikipa wanapiga story...wangeruhusu pia waingie na kahawa au chai wawe wanashushia huku striker anasubiri amalizie tu, itapendeza zaidi

Kwani Mabeki nao watalala?, nao si wataweka ulimzi, ni badiriko zuri tu, kwani hata lile la Kipa kutodaka backpass nalo lilikuwa gumzo na ilionekana kuwa litakuwa zoezi gumu, lakini limefanikiwa kwa ustadi mkubwa na wachezaji wameadapt vizuri tu
 
Kuondoa Offside Kutafanya Washambuliaji WAVIVU Kama CHIRWA na KICHUYA Kukaa na Golikipa Kwa dakika zote 90
 
La offside siliafiki,kuongeza sub na kupunguza adhabu kwa mpira wa kushika na kurefusha sehemu ya kupigia penati ni mawazo mazuri.Na hata hiyo ya nahodha kuwa ndio muongeaji na refa ni wazo zuri.
 
Ya offside wamechemsha coZ striker atakua anashinda na golikipa wanapiga story...wangeruhusu pia waingie na kahawa au chai wawe wanashushia huku striker anasubiri amalizie tu, itapendeza zaidi
nasikia jamaa kafurahi.
cropped_REU_2375861__2_.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom