Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
.... i hope hii haihusiani na wale "farasi wanne".... !!!
Inasemekana eti yeye ni "Paulo Usije Kucheza na Sisi... Una...."
Rev.Kishoka,
..wachumi na wataalamu wetu wa fedha wanaamini kwamba tutafaidika na 3% royalty na tax breaks za kila aina.
..hata tupate AG toka mbinguni bado hatuwezi kufaidika na rasilimali zetu ktk mazingira ya sasa.
..mwanasheria mkuu hapangi wala hapatani bei.
---kwa vile "walioogopa kuchafuliwa mikono" wametenda yote haya ndani ya miaka 6-7 iliyopita, je "paulo" alikuwa wapi na kwanini hakuweza hata "kuwarushia uchafu huo" walau kwa proxy...alimradi tu angewachafua na kuutaarifu ulimwengu kuwa kuna wenye mikono michafu pahala fulani?!
Rais Jakaya Kikwete `ameicharukia` Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Barabara nchini TANROADS kutowapa kazi wakandarasi wababaishaji, pia kutowalipa wanaojenga barabara chini ya viwango.
``Wakandarasi wababaishaji wasipewe kazi, wanatufikisha pabaya,`` alisema.
Aidha, aliwataka wizara ya ujenzi wanapotoa tenda wamchague yule aliyetoa hesabu kubwa na sio kuangalia mwenye hesabu ndogo kwani wao pia ukubwa wa kazi wanaijua.
``Hakuna sababu wizara, TANROADS kumchagua mtu mwenye hesabu ndogo, mnapotangaza tenda lazima kuangalia kama kazi ataiweza, ingawa wale watakaokosa watasema mnajali mafisadi,... hayo msiyajali!,`` alishauri.
Aidha, amesema yapo makampuni kadhaa hapa nchini ambayo kazi yao ni kudanganya pindi wanapokuwa wamepewa tenda za kutekeleza miradi mbalimbali.
Alisema hayo jana mjini hapa wakati akizindua barabara ya Isuna hadi Manyoni yenye urefu wa kilomita 55 baada ya mkandarasi aliyepewa kazi ya kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kushindwa kazi kwa visingizio.
Rais Kikwete yuko mkoani humu kwa ziara ya siku sita kwa ajili ya kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua mwaka 2005.
Rais Kikwete alisema awali barabara hiyo ya Isuna-Manyoni, ilikuwa ikijengwa na mkandarasi kutoka China ambaye alishindwa kukamilisha kazi kama ilivyotakiwa.
Alisema kilichotokea hapo iwe ni fundisho na kwamba tatizo la namna hiyo lisijitokeze tena.
Aidha Rais Kikwete alibainisha kuwa kupewa tenda kwa mkandarasi mwenye hesabu ndogo ndiko kunakosababisha matatizo ikiwa ni pamoja na miradi kutokamilika kwa wakati uliotakiwa.
Alisema wakiendelea na utaratibu huo wa kuangalia hesabu ndogo watakwama wakati nchi bado ni maskini.
``Ninaomba sana, bure ni ghali sana, kwani angalia sasa tunaingia gharama nyingine tena kubwa zaidi kuliko zile za awali,`` alisema.
Aliongeza kuwa mzabuni atakayekiuka utaratibu unaotakiwa wanapaswa kumuita na kumuuliza ili wasimamie katika ukweli na haki na sio kuwachanganya.
Kuhusu makampuni yanayodanganya alisema hapa nchini yapo kadhaa na kazi yao ndio hiyo halafu badaye huhitaji majadiliano.
``Simamieni wataalamu mlio nao, makampuni yawe yanasema ukweli kuepusha hasara katika nchi,`` alisema.
``Nchi hii ni maskini, ujenzi huu unagharamiwa na fedha za wananchi, epukeni kuingia gharama mara mbili, kwani wanaofanya hivyo wanakuwa wanyonya damu,`` alisema.
Pia aliwataka kukasirika na kuwachukulia hatua makampuni yanayokiuka utaratibu ikiwa ni pamoja na kuwaambia kwa herini (byebye) wakatafute tenda nyingine nje ya nchi.
Rais aliongeza kuwa mhandisi mshauri naye hatakiwi kulipwa malipo yake endapo ujenzi hautakuwa umekamilika kwa kiwango kinachotakiwa kwani wasipofanya hivyo Tanzania itakuwa shamba la wajinga.
Lazima Watanzania waone uchungu na kutekeleza miradi ya wananchi katika kiwango kinachotakiwa, alisisitiza.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Bw. Omar Chambo alisema barabara hiyo itagharimu kiasi cha Sh. bilioni 30.43 na ujenzi wake ulisainiwa Desemba 11, mwaka 2007.
Alisema barabara hiyo ilisainiwa kati ya TANROADS na Kampuni ya China Geo Engineering kutoka nchini China na kwamba sehemu ya barabara hiyo inatarajiwa kukamilia ifikapo mwaka 2010.
Alisema mradi huo unasimamiwa na mhandisi mshauri Black &Veatch kutoka Afrika Kusini akishirikiana na Kampuni ya Mak Consult ya Tanzania kwa gharama ya Sh. milioni 857.23.
Mrema wa TANROADS ALIPO TETEWA NA JK KUWA ASIOGOPE KUITWA FISADI!
Mkuu Kishoka,
Heshima mbele, hata mimi nasikia kuwa hata hii deal ya Richimonduli yeye ndiye architect na ndiye hasa masterminder wa IPTL, lakini amekuwa mjanja sana na ku-lay low na hakuna mwenye shida naye kabisaa kumba mambo yote yeye ndiye chanzo!
Mushi,
Nafikiri unachanganya machungwa na maharage. Hii thread ni kuhusu Felix Mrema ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania na si Ephraim Mrema CEO wa Tanroads.
Ya Mrema wa Tanroads yaache kule kwenye thread ya Tanroads na si kuyapandikiza mahali ambapo si pake!
FMES,
Huyu jamaa alitegemewa kuwa AG kamili baada ya Uchaguzi 1995. Lakini alikwenda na kugombea Ubunge Arusha Mjini na akaupata. Wakati Mkapa anajiandaa kuunda Baraza la Mawaziri, Mrema alitgemewa kwa AG au Waziri wa Sheria, lakini akapotea na kubakia kama Mbunge wa kawaida.
He has gone quite out of the public fanfare, lakini kama ulivyosema, inasemekana yeye ndiye Architect Mkuu wa IPTL na si ajabu mkono wake ulitumika kwa Tanesco.
Kwenye ripoti ya Brian Cooksey, anawataja Chenge na Maria Kejo-Ndosi kutoka ofisi ya AG, lakini Mrema's name never surfaces!
NA PIA ULIYASEMA HAYA ULIPOMJIBU FMES...
Wewe ni mmojawapo wa wale wanaofagilia UKABILA HAPA JF!
Sasa Na wewe pia ni shabiki la KUGANGAMALA NA HUYO YUSUPH MUSHI SIMPLY KWASABABU GANI?
NA PIA ULIYASEMA HAYA ULIPOMJIBU FMES...
Wewe ni mmojawapo wa wale wanaofagilia UKABILA HAPA JF!
Sasa kama unakiri kuwa hakutajwa kwenye source...Na huku ukikiri kuwa hakuwa AG...At the same time kuwepo na utaratibu mpya hapa jf wa kuyataja majina ya wachagga na kuwahusisha na UFISADI BILA KUJALI KUWA KASHFA HIZO ZIMEANZIA KWA WAISLAM WA ccm KINA IDDI SIMBA NA WAARABU WAKE,NA NYINGINE KUTOKA KWA WATOPU AMBAO HAWANA UISLAM WALA UCHAGGA!
Sasa Na wewe pia ni shabiki la KUGANGAMALA NA HUYO YUSUPH MUSHI SIMPLY KWASABABU GANI?
AMA UNATAKA KUSEMA KUWA SIR CHANDE NI FISADI MDOGO KULIKO HUYO MUSHI?
NANI NI KINGPIN?
Hawa Mrema wote ni mrema na wanahusiana politics zetu wakati wa kueleke a UCHAGUZI NA KAMWE SITORUHUSU UKABILA NA AMA UDINI UWAPOTOSHE WANANCHI!
TUNATAKA UHURU...!
NA SAA YA UKOMBOZI NI SASA!
WE ARE PATIENTLY WANITING!
WE THE PEOPLE SHALL OVERCOME!
Again the same JMushi takeover tactics of threads are emerging.
Kwa nini usianzishe thread inayosema Maoni ya JMushi ukaandika kila unachotaka na kujijibu na kuacha Thread nyingine zisizuhusiana na mambo unayoyataka ziendelee kivyake vyake?
WEWE Ulishasema kuwa AG alikuwa CHENGE...AT THE SAME TIME...Kusema kuwa hakupewa u AG na MKAPA..Sasa kwanini usianzishe thread ya CHENGE AMA KUDAI RIPOTI ZISOMWE BUNGENI NA SI KUFLOOD JF NA MITHREAD YA UKABILA NA UDINI?
ATISHI NYAU HAPA!
UNAJUWA NILIKOTOKEA NA USIJARIBU KURUDI HUKO!
WE KAZI YAKO KUANZISHA THREADS ETI REV MNAMTAFUTA!
WAKUTAFUTE WA NINI NA WAKATI SERA ZAO ZA UKABILA UNAZIENEZA NA CHUKI ZAKO ZA WAZI?
Mushi1,'
Mimi namfahamu Reverend. Hana hata chembe moja ya ukabila. Soma tena threads zake kwa makini.