Sina tatizo na Fei Toto kua X-Factor player, kibongo bongo ana hiyo sifa. Shida yangu Mimi ni mtu kuanzisha kampeni ya utapeli ili imsaidie kuuza jezi kwa kuwadanganya watu kua X-Factor player ananunuliwa kwa michango ya mashabiki kupitia kununua jezi. Hela ya kuvunja mkataba wa Fei Toto ilikua 1B kabla hasaini mkataba mpya sijui kwasasa, ila tusimamie hapo kwenye 1B. Haya, dirisha la usajili linafungwa Jmosi hii tar.15. Zitauzwa jezi ngapi kupata hiyo 1B? Na hizo jezi mzabuni akiuza hiyo 1B yote atapeleka kumnunua Fei Toto halafu yeye anafaidikaje? Kuna mfanyabiashara anaweza kufanya hicho kitu hapa Duniani? Then ni kitu ambacho hakipo hata kwenye mkataba na Club. Mi nadhani watu wanunue jezi jamaa aridishe pesa zake kwasababu asipomleta huyo X- Factor Player hakuna cha kumfanya wala pa kumpeleka hakuna. All in all hakuna mchezaji Duniani ananunuliwa kwa style hiyo, kuna muda baadhi mashabiki na influencers wa hivi vilabu vyetu viwili wanakua kama wehu hivi.