Fedheha kubwa viongozi wa Mbeya

Fedheha kubwa viongozi wa Mbeya

BAPUPEGHE

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2012
Posts
220
Reaction score
38
Ndugu wanabodi, siyo siri ni fedheha na usanii mkubwa kupeleka Makao makuu ya Mkoa Mkwajuni.

Naomba nieleweke kuwa sina nia mbaya na jina la Mkoa Wa Songwe. Shida yangu kwa nini Makao Makuu yanaenda Mkwajuni? Ni vigezo vipi vinatumika Kupata Makao Makuu ya Mahali furani? Kwa mfano Mtu wa Ileje ambaye anatembea umbali wa km 220 mpaka Mbeya Mjini, sasa atatembea km 305 hali kadharika Tunduma na Momba. Kwanini wasingeweka makao Makuu Mlowo ili kuwianisha Umbali?

Zipo taarifa ambazo siyo rasimi kuwa wapo watu wametumia pesa nyingi kufanikisha hili. Mimi nafikiri sasa ni wakati wa Wapenda Maendeleo wa Mbozi na Ileje kusimama kupinga upuuzi na Utupu wa wazi kabisa kama huu.

Makao Makuu yangefaa kuwa Mkwajuni endapo tu hata Tabora ingekuwa sehemu ya huu Mkoa Mpya. Haya ni Maajabu Mengne ya ulimwengu kama yalivyo Maajabu yaliyotangulia kwenye rasmu ya Katiba kuwa kuwe na Serikari Tatu.

Kwa manufaa ya watu ambao hawafahamu vizuri huu mkoa, ni kwa Mfano utoe makuu ya Tanzania kwa sasa toka Dodoma upeleke Mara au Mwanza, je utakuwa umewatendea haki wenzetu wa songea, mtwara na mby?

Twende barabarani kabla Rais haja tia saini yake. Silinde ongoza jahazi. Tunajua wenzako Zambi na Kibona hawana lolote maana Kama Kibona mbunge wa Ileje sidhani kama hata alichangia chochote.

Hao wakuu wa Wilaya, wakurugenzi ni wapita njia, watatuacha sisi na adhaa. Wao wamelishwa pesa na wakaunga Mkono hoja. Hata hivyo baada ya kumaliza kikao walienda hotelini na Mfanyabiashara Maarufu wa Madini wakiongozwa na moja ya kiongozi wa juu wa Serikali ambaye alikuwa Mjumbe wa kikao hicho ktk hotel Moja iliyo Maeneo ya Sowete kwa Mwaisabila.

Haikubaliki, ni hujuma, unafiki, uzandiki na utupu!! Tusimame kuondoa udharimu Mpya. Hii sasa ni vita ileje na Mbozi funga mikanda. Bora kwenda Malawi au zambia lakni siyo udikiteta wa pesa.
NAWASILISHA.
 
He he he heeee...!!! wanataka wai promote Chunya..!?? No way... watachemsha. wakifanya hivyo basi watu wa Ileje nawashauri wawe.wanaenda kumalizia shida zao Chitipa na wa Mbozi waende Nakonde maana ndo itakuwa karibu.. hizi politiki hizi... my chinese mobile.
 
Ingieni mitaani kupinga mipango miovu kama hii. swali la msingi,Mby mna mambo mengi makubwa ya kufanya, hili la kugawanywa kataeni kabisa. Ni upuuzi mtupu.
 
Kama CCM itaendelea kuwepo madarakani hata kale kakijiji ketu katakuwa mkoa ili huduma ziwafikie wananchi. Haaaaaaaaaah!

Huu uchizi, hakuna kitu kama hicho kugawa mikoa kila kukicha. Kikwete amezalisha mikoa zaidi ya 4 sasa, Njomba mmoja (Manyara).

Sasa maendeleo yanaletwa na Mkuu wa Mkoa au mipango bora ya maendeleo?
 
Nasikia Philipo Mulogo jana amefanya party kubwa sana. Nimepata taarifa kuwa hiyo ni kete kubwa sana kwa wapiga kura wake. Anajaribu kughiribu wananchi wa Chunya kuwa ni yeye ndiye aliyefanikisha kuwapelekea mkoa mpya! Siasa bwana!
 
Kama CCM itaendelea kuwepo madarakani hata kale kakijiji ketu katakuwa mkoa ili huduma ziwafikie wananchi. Haaaaaaaaaah!

Huu uchizi, hakuna kitu kama hicho kugawa mikoa kila kukicha. Kikwete amezalisha mikoa zaidi ya 4 sasa, Njomba mmoja (Manyara).

Sasa maendeleo yanaletwa na Mkuu wa Mkoa au mipango bora ya maendeleo?

Manyara hakuanzisha JK, alianzisha Mkapa kwa kuimega Arusha. JK kaanzisha Katavi (kwa Pinda), Njombe (kwa Makinda), Geita (Ngeleja) na Simiyu (kwa Chenge). Napinga Mbeya kugawanywa, watengeneze kwanza miundombinu ya Chunya na Ileje ili nao wa enjoy matunda ya uhuru
 
Mtoa hoja yaani umeshindwa hata kuwataja walio nyuma ya movie hii. Hebu wataje nasi tuwajue, manake sikuhizi ccm kuna ugonjwa wa kuhonga hata jambo lisilohitaji hongo. Sijui wana hela sana, au ndo vile tena kuthibitisha kuwa chama kilishaporwa kutoka mikononi mwa Wakulima na Wafanyakazi, na sasa kiko mikononi mwa Wafanyabiashara.
 
hawa hawafai hata kuwa viongozi kwani maamuzi yao ni bora hata yangefanywa na walevi waliolewa chakali tungesema hizo ni pombe tu zikiisha kichwani watabadilisha maamuzi. badala ya kupunguza umbali kupata huduma wao wanawaongezea watu umbali.
 
Ulaji tu na ujinga chunya haina hata mtaa mmoja pale mjini na ileje haina hata mtaa mmoja si waboreshe hizo wilaya kwanza ujinga usio na mkia
 
Ndugu wanabodi, siyo siri ni fedheha na usanii mkubwa kupeleka Makao makuu ya Mkoa Mkwajuni.

Naomba nieleweke kuwa sina nia mbaya na jina la Mkoa Wa Songwe. Shida yangu kwa nini Makao Makuu yanaenda Mkwajuni? Ni vigezo vipi vinatumika Kupata Makao Makuu ya Mahali furani? Kwa mfano Mtu wa Ileje ambaye anatembea umbali wa km 220 mpaka Mbeya Mjini, sasa atatembea km 305 hali kadharika Tunduma na Momba. Kwanini wasingeweka makao Makuu Mlowo ili kuwianisha Umbali?

Zipo taarifa ambazo siyo rasimi kuwa wapo watu wametumia pesa nyingi kufanikisha hili. Mimi nafikiri sasa ni wakati wa Wapenda Maendeleo wa Mbozi na Ileje kusimama kupinga upuuzi na Utupu wa wazi kabisa kama huu.

Makao Makuu yangefaa kuwa Mkwajuni endapo tu hata Tabora ingekuwa sehemu ya huu Mkoa Mpya. Haya ni Maajabu Mengne ya ulimwengu kama yalivyo Maajabu yaliyotangulia kwenye rasmu ya Katiba kuwa kuwe na Serikari Tatu.

Kwa manufaa ya watu ambao hawafahamu vizuri huu mkoa, ni kwa Mfano utoe makuu ya Tanzania kwa sasa toka Dodoma upeleke Mara au Mwanza, je utakuwa umewatendea haki wenzetu wa songea, mtwara na mby?

Twende barabarani kabla Rais haja tia saini yake. Silinde ongoza jahazi. Tunajua wenzako Zambi na Kibona hawana lolote maana Kama Kibona mbunge wa Ileje sidhani kama hata alichangia chochote.

Hao wakuu wa Wilaya, wakurugenzi ni wapita njia, watatuacha sisi na adhaa. Wao wamelishwa pesa na wakaunga Mkono hoja. Hata hivyo baada ya kumaliza kikao walienda hotelini na Mfanyabiashara Maarufu wa Madini wakiongozwa na moja ya kiongozi wa juu wa Serikali ambaye alikuwa Mjumbe wa kikao hicho ktk hotel Moja iliyo Maeneo ya Sowete kwa Mwaisabila.

Haikubaliki, ni hujuma, unafiki, uzandiki na utupu!! Tusimame kuondoa udharimu Mpya. Hii sasa ni vita ileje na Mbozi funga mikanda. Bora kwenda Malawi au zambia lakni siyo udikiteta wa pesa.
NAWASILISHA.

Nakuunga mkono mkuu,mie sio mwenyeji wa mbeya ila katika shughuli zangu za kikazi nimewahi kutembea mkoa wote wa mbeya mara mbili kila wilaya kwa undani zaidi.Hapa nawaonea huruma watu ileje kwa sababu ndio safari ambayo ilikuwa ngumu kwangu kuacha ile ya chunya na milima na barabara mbaya ila pia muunganiko wa hizi sehemu haujakaa sawa.Waliangalie hili suala upya hasa kwa watu wa ileje na wengine wa mwambao huo
 
Piga elimu uraia bila kuchoka kwani 2015 hivi vimikoa na viwilaya tutaviua vyote na kutengeneza serikali za majimbo na mambo yatakuwa mazuri mno.
 
piga elimu uraia bila kuchoka kwani 2015 hivi vimikoa na viwilaya tutaviua vyote na kutengeneza serikali za majimbo na mambo yatakuwa mazuri mno.
mkuu ileje tuna jipanga wasomi wote ileje njoo nyumbani kwenu mulugo na wenzake wametumia pesa kutaka kutupeleka mkwajuni.tutapambana naye na ccm wote walio unga mkono cc kwenda mkwajuni.hapa tuondoe tofauti zetu zote za kiitikadi tuje pamoja na tupinge hoja za mulugo na hongo zake.kibona wa ileje ndo ziiiiiii hamna kitu.zambi wa mbozi mlopokaji ameshrk kuipeleka mbozi na ileje huko mkwajuni.nitapamba mpaka kieleweke tuungane wanaileje na mbozi
 
Nasikia Philipo Mulogo jana amefanya party kubwa sana. Nimepata taarifa kuwa hiyo ni kete kubwa sana kwa wapiga kura wake. Anajaribu kughiribu wananchi wa Chunya kuwa ni yeye ndiye aliyefanikisha kuwapelekea mkoa mpya! Siasa bwana!
Hii ishu kuna jamaa yangu yupo pale Chunya kaniambia kwamba toka nchi hii imepata Uhuru hakuna mtu aliyefanikiwa kuipigania Chunya kama Mulugo, watu wanamkubali sana baada ya kufanikisha hili na wanaapa hakuna mbunge mwingine anaweza kupokelewa Chunya, anadai eti magholofa yoote yaliyojengwa Mbeya Mjini yametokana na Madini ya Chunya lakini hakuna mtu aliyeipigania na yenyewe iwe kama miji mingine iliyoendelea, nimecheka sana, kwamba hii kete itamtoa sana Mulugo
 
Naomba uje ileje tuyajadili ya mkwajuni na mulugo mtaka mkoa mpya wa songwe kuupeleka kwao cc hatuendi hatutaki
 
Under utawala wetu sio umbali bali ni maslahi zaidi. Kuna shida gani kama utatembea KM 300 kwa gari ya gharama za serikali huku mambo yako yanakwenda. Achana na watembea kwa miguu wanaotaka makao yawe karibu ili kuokoa gharama.
 
Nasikia Philipo Mulogo jana amefanya party kubwa sana. Nimepata taarifa kuwa hiyo ni kete kubwa sana kwa wapiga kura wake. Anajaribu kughiribu wananchi wa Chunya kuwa ni yeye ndiye aliyefanikisha kuwapelekea mkoa mpya! Siasa bwana!
Imesemwa an kuandikwa ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, siasa safi na uongozi bora. Tanzania uongozi bora hatuna tuna viongozi wasio bora wanaondesha siasa chafu. Huu ni msala. Kuongeza wilaya inamaana kwa mwananchi nasio mkoa.
 
Hili jambo halikubakiki hata kidogo na sijui walikuwa wanafikilia kwa kutumia utashi gani mapaka wakifikia hatua hiyo,kijiografia haviendani Mbozi,ileje Momba na chunya kuwa mkoa. Haya ni mambo ya wanasiasa kutaharibia mambo ya utawala kwa maslahi yao binafsi.
 
Back
Top Bottom