Fedha za TASAF zimeongezwa kutoka Tshs Bilioni 2 hadi bilioni 6

Fedha za TASAF zimeongezwa kutoka Tshs Bilioni 2 hadi bilioni 6

John John Msakuzi

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
279
Reaction score
99
==
Katika sekta ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Sita imetoa miongozo ya kuyawezesha makundi mbalimbali ya jamii kuimarisha uwezo wao wa kushiriki shughuli za maendeleo na kuleta usawa wa kiuchumi. Katika kipindi hiki, kumekuwa na ongezeko la vikundi vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri za Mkoa wa Mara kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kutoka vikundi 187 mwezi Novemba 2020 hadi vikundi 324 Aprili 2025. Fedha zinazotolewa kama mikopo kwa vikundi hivyo zimeongezeka kutoka shilingi bilioni 1.63 Novemba 2020 hadi shilingi bilioni 5.88 mwaka 2025.

Idadi ya vikundi vya wanawake imeongezeka kutoka vikundi 92 Novemba 2020 hadi vikundi 99 Aprili 2025, vikundi vya vijana kutoka 53 hadi 139, na vikundi vya watu wenye ulemavu kutoka 42 hadi 86. Mafanikio yaliyopatikana kutokana na vikundi hivi ni pamoja na kuongezeka kwa ajira, kuimarika kwa uchumi wa vikundi na mtu mmoja mmoja, pamoja na kupungua kwa utegemezi wa makundi haya katika jamii. Kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), Mkoa wa Mara una jumla ya wanufaika 50,934 hadi Juni 2025, ambapo wananchi hao wameweza kuboresha maisha yao kwa kujifunza na kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

Aidha, Mkoa kwa kushirikiana na Tume ya Madini na Mgodi wa Barrick North Mara umewawezesha upatikanaji wa leseni 104 kwa vikundi 48 vyenye jumla ya vijana 1,836 kutoka vijiji 13 katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime. Uwezeshaji wa makundi hayo ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) yenye lengo la kutoa fursa kwa vijana kushiriki katika mnyororo wa thamani wa madini. Vijana hao wanapatiwa elimu kuhusu uchimbaji wa madini chini ya uangalizi wa Mgodi wa Barrick North Mara, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Ofisi ya Madini Mkoa.

Hata hivyo fedha zote zilizotamkwa katika utekelezaji wa miradi ya uwezeshaji ni shilingi bilioni 5.88, huku jumla ya wanufaika wote wakiwa watu 52,770.​

Miradi20202025Ongezeko
Idadi ya vikundi vyote187324137
Vikundi vya wanawake92997
Vikundi vya vijana5313986
Vikundi vya wenye ulemavu428644
Thamani ya mikopo (TSh Bil.)1.635.884.25
Wanufaika TASAF-50,934-
Wanufaika leseni za madini-1,836-
Jumla ya wanufaika wote-52,770-
Jumla ya fedha zote (TSh Bil.)-5.88-
 
==
Katika sekta ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Sita imetoa miongozo ya kuyawezesha makundi mbalimbali ya jamii kuimarisha uwezo wao wa kushiriki shughuli za maendeleo na kuleta usawa wa kiuchumi. Katika kipindi hiki, kumekuwa na ongezeko la vikundi vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri za Mkoa wa Mara kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kutoka vikundi 187 mwezi Novemba 2020 hadi vikundi 324 Aprili 2025. Fedha zinazotolewa kama mikopo kwa vikundi hivyo zimeongezeka kutoka shilingi bilioni 1.63 Novemba 2020 hadi shilingi bilioni 5.88 mwaka 2025.

Idadi ya vikundi vya wanawake imeongezeka kutoka vikundi 92 Novemba 2020 hadi vikundi 99 Aprili 2025, vikundi vya vijana kutoka 53 hadi 139, na vikundi vya watu wenye ulemavu kutoka 42 hadi 86. Mafanikio yaliyopatikana kutokana na vikundi hivi ni pamoja na kuongezeka kwa ajira, kuimarika kwa uchumi wa vikundi na mtu mmoja mmoja, pamoja na kupungua kwa utegemezi wa makundi haya katika jamii. Kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), Mkoa wa Mara una jumla ya wanufaika 50,934 hadi Juni 2025, ambapo wananchi hao wameweza kuboresha maisha yao kwa kujifunza na kuanzisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

Aidha, Mkoa kwa kushirikiana na Tume ya Madini na Mgodi wa Barrick North Mara umewawezesha upatikanaji wa leseni 104 kwa vikundi 48 vyenye jumla ya vijana 1,836 kutoka vijiji 13 katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime. Uwezeshaji wa makundi hayo ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) yenye lengo la kutoa fursa kwa vijana kushiriki katika mnyororo wa thamani wa madini. Vijana hao wanapatiwa elimu kuhusu uchimbaji wa madini chini ya uangalizi wa Mgodi wa Barrick North Mara, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Ofisi ya Madini Mkoa.

Hata hivyo fedha zote zilizotamkwa katika utekelezaji wa miradi ya uwezeshaji ni shilingi bilioni 5.88, huku jumla ya wanufaika wote wakiwa watu 52,770.​

Miradi20202025Ongezeko
Idadi ya vikundi vyote187324137
Vikundi vya wanawake92997
Vikundi vya vijana5313986
Vikundi vya wenye ulemavu428644
Thamani ya mikopo (TSh Bil.)1.635.884.25
Wanufaika TASAF-50,934-
Wanufaika leseni za madini-1,836-
Jumla ya wanufaika wote-52,770-
Jumla ya fedha zote (TSh Bil.)-5.88-
Tasaf ni fedha za mkopo toka Bank ya Dunia.
 
akina nani?
Tangu enzi za JK, TASAF ilishakuwepo, ikaja enzi za JPM TASAF ilikuwepo hadi kipindi hiki ipo. Halafu TASAF sio mradi wa hizo billion 2 hadi 6 unzotaja, huo mradi unafika hadi trillion kadhaa na hakuna alichoongeza Wala kupunguza Samia. Na kwenye hii thread yako umeitaja TASAF mara moja tu wakati kichwa Cha habari kinahusu TASAF. Kama hamna taarifa sahihi na za kutosha msiwe mnaanzisha nyuzi na kusubiri kupata elimu kwenye comments. Akipita hapa mtu anayefanya kazi TASAF atakuona kama CHAWA pro-max kiwango cha LUCAS Muwashambwa.
 
Tangu enzi za JK, TASAF ilishakuwepo, ikaja enzi za JPM TASAF ilikuwepo hadi kipindi hiki ipo. Halafu TASAF sio mradi wa hizo billion 2 hadi 6 unzotaja, huo mradi unafika hadi trillion kadhaa na hakuna alichoongeza Wala kupunguza Samia. Na kwenye hii thread yako umeitaja TASAF mara moja tu wakati kichwa Cha habari kinahusu TASAF. Kama hamna taarifa sahihi na za kutosha msiwe mnaanzisha nyuzi na kusubiri kupata elimu kwenye comments. Akipita hapa mtu anayefanya kazi TASAF atakuona kama CHAWA pro-max kiwango cha LUCAS Muwashambwa.
kwa mkoa mmoja> au unazungumzia nchi nzima?
 
Back
Top Bottom