Fedha za Stanbic ziligharimia kampeni UKAWA?

Fedha za Stanbic ziligharimia kampeni UKAWA?

Mbona hujawataja Marehemu Mgimwa na mwanae??
Ondoa u-Lumumba wako hapa.

MsemajiUkweli,wetu wa CCM wako wapi? Kuna hadi Mawaziri na mtoto wao. Mbona huwataji? Acha double standards Mkuu!

Mzee Tupatupa
Lowassa alikuwa na mamluki wa kutosha. Wengine mliwaona wakitoa matamko hadharani kule Dodoma. Wengine mkawapatia na zawadi ya ubunge. Hivyo mngetulia kwanza mahakama ya mafisadi iwe fully operational
 
Last edited by a moderator:
haahaaaahh..familia ya Kikwete haita jinusuru kwa post za kitoto kama zako jamaa yangu,come with evidence mh.Nape nauye a.k.a Msemaji Ukweli
 
UCHUNGUZI unaoendelea wa serikali kuhusu ufisadi wa takribani shilingi bilioni 13 katika mkopo uliochukuliwa kupitia Benki ya Stanbic unaonyesha kuwagusa watu ambao walikuwa mstari wa mbele kwenye kampeni za vyama vilivyo kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imefahamika.

Ingawa kiwango halisi cha mkopo ambao serikali ilichukua kupitia benki hiyo ni dola milioni 600 (shilingi trilioni 1.3), ufisadi unaonekana katika kiwango cha dola milioni sita (shilingi bilioni 13) ambazo sasa imethibitika zilitumika kuwahonga viongozi wa serikali ili wauruhusu.

Kinara Bashir Awale
Huyu ndiye aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Stanbic wakati wa kutafuta na hatimaye kupatikana kwa fedha hizo. Kwa mujibu wa taarifa za kimahakama kutoka Uingereza, huyu ndiye alikuwa mtengenezaji wa mpango wote wa kupatikana kwa rushwa hiyo.

Mara baada ya kuondoka kutoka Stanbic mwaka 2013, kutokana na kukataa kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo, mara nyingi Awale alionekana akiwa na aliyekuwa mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowassa.

Ndani ya kambi ya Lowassa haikuwa siri kwamba endapo angeshinda urais, Awale angeweza kupewa nafasi ya Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Yeye ni mmoja wa watu waliokuwa wakitajwa kama wasaka fedha wakuu wa Ukawa na Lowassa. Akiwa na uzoefu wa muda mrefu katika eneo la benki na fedha, Awale alikuwa miongoni mwa wana Ukawa walioweza kujigamba kwamba wako karibu na Lowassa.

Kwa sasa, Awale amefukuzwa nchini kwa madai ya kutokuwa raia wa Tanzania lakini ukaribu wake na Lowassa unaonekana katika baadhi ya picha zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa katika mojawapo ya mikutano ya kisiasa ya Chadema, akiwa amekaa karibu na mtoto mkubwa wa Lowassa, Fred.

Uchunguzi wa vyombo vya usalama vya Uingereza unaonyesha kwamba wakati wa fedha hizo kulipwa kutoka Stanbic kwenda kwa kampuni ya EGMA, fedha zilikuwa zikitolewa kwenye akaunti na kwenda kwanza kugawiwa kwenye ofisi yake kabla ya kutoka nje ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Kinara Shose Sinare
Taarifa za kikachero kutoka Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Kijinai ya Uingereza (SFO), zinamtaja mfanyakazi huyu wa zamani wa Stanbic kama SS, na aliwahi kuwa Miss Tanzania mwaka 1996.

Katika ufisadi huu, Shose anatajwa kama msaidizi wa karibu wa Awale na mtu ambaye ukiondoa bosi wake huyo, alifanya kazi kubwa kuhakikisha mpango huo unafanikiwa. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kumhusisha Shose na Ukawa zaidi ya hatua ya mama yake, Dk. Eve Sinare, aliyekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutangaza kuhama chama hicho katika siku za mwisho za kampeni za Uchaguzi Mkuu.

Wakati Dk. Sinare akitangaza kuhama CCM, watu wengi walishangazwa na uamuzi wake huo kwa vile yeye si mmoja wa wanachama maarufu wa chama hicho na hatua yake hiyo haikuonekana kumsaidia yeyote. Mara baada ya kuibuka kwa kashfa hii ya Stanbic, maswali yameanza kuibuka kuhusu mwenendo wao katika wakati huo wa kuelekea Uchaguzi Mkuu. Inadaiwa kuwa kwa kawaida Dk. Sinare na Shose ni watu walio karibu sana.

Harry Kitilya
Huyu alipata kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Ushiriki wake katika kashfa hii umewashangaza wengi kwani kwenye jamii alijenga picha ya kiongozi msafi. Kitilya alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya EGMA ambayo ndiyo ilipewa kiasi hicho cha shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ?kulainisha viongozi wa serikali? kukubali kuchukua mkopo huo kutoka Stanbic.

Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, jina la Kitilya lilikuwa likitajwa kama mmoja wa watu waliokuwa wakichangisha fedha za kusaidia Lowassa ashinde uchaguzi.

Tofauti na watu kama Awale waliokuwa wakimuunga mkono Lowassa hadharani, Kitilya hakuwahi kutamka hadharani kumuunga mkono mwanasiasa huyo wala kuonekana kwenye mikutano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Kitilya, kwa nafasi aliyokuwa nayo TRA, ni mmoja wa watu waliokuwa wakiombwa ushauri na serikali iwapo ichukue mkopo au isichukue. Kwa maana hiyo, Kitilya alilipwa fedha hizo ili pia naye ?alainike? na ?kuishauri? serikali ichukue mkopo huo hata kama masharti yake hayakuwa muafaka.

Kwa mfano, wakati riba ya kawaida ya mikopo ilikuwa ni asilimia 1.4, mkopo huo ulichukuliwa kwa riba ya asilimia 2.4. Ongezeko hilo la asilimia moja ndilo lililoleta kiwango hicho cha shilingi bilioni 13. Ili kuhakikisha EGMA inapata fedha nyingi kupitia asilimia hiyo moja, badala ya serikali kukopa dola milioni 550 ilizotaka kukopa awali, ikakopa dola milioni 600. Kama ingekopa dola milioni 550, EGMA ingepata dola milioni 5.5 tu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa SFO, ingawa Kitilya ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya EGMA, hakuwahi kwenda kuchukua fedha hizo Stanbic na badala yake kazi hiyo ilifanywa na wabia wenzake, Dk. Fratern Mboya na Peter Nyabuti.

Peter Nyabuti
Uchunguzi wa SFO unamtaja Nyabuti kama raia wa Kenya na hakuna taarifa nyingi zinazomhusu. Hata hivyo, katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Nyabuti alikuwa mmoja wa wateja maarufu katika baa ya Kruz In iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kwa kipindi kirefu, baa hiyo imefahamika kama kambi rasmi ya ?Marafiki wa Lowassa? ambapo ni kawaida kwa watu waliokuwa kwenye kambi yake; tangu akiwa CCM, kujumuika na kubadilishana mawazo katika eneo hilo. Kwa sababu hiyo, Nyabuti aliyekuwa akichanganyika na watu kama Awale na Fred Lowassa, alikuwa akifahamika kama mmoja wa wapanga mipango na mikakati wa Ukawa.

Ingawa Chadema na vyama vilivyo kwenye Ukawa vimekuwa vikifahamika kwa kupinga ufisadi, hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa kambi hiyo aliyetoa kauli ya karipio dhidi ya ufisadi huo wa Stanbic.

Kwa sasa serikali inafanya uchunguzi kuhusu suala hilo na tayari imeahidiwa kwamba itarejeshewa shilingi hizo bilioni 13 zilizotolewa kama hongo.

Kwa hisani ya RaiaMwema
Hivi wakati ufisadi huo unafanyika ilikuwa mwaka gani vile? Hao uliowataja walikuwa UKAWA? Kwanza UKAWA yenyewe ilikuwepo? Huo ufisadi una harufu ya CCM kama ufisadi mwingine wote uliokwishatokea nchi hii. Wacha waendelee kufukunyua yatajulikana na mengine tu
 
Which means ninyi CCM (choo) mmeukubali kwa dhati ufisadi (kinyesi)...maana ndio mahali pake haswaa!
CCM ilikuwa ndiyo kiwanda cha kuzalisha mafisadi.

Mvumbuzi, mjenzi na msimamizi wa kiwanda hicho alikuwa ni Lowassa!
 
Unaweza kupata ndondoo kidogo za huyu Mama kupitia thread hii,


Si unakumbuka fedha za escrow zilitoka mkombozi kwenda stanbic bank kwa majunia. Sasa mkurungezi wa mkombozi bank alikuwa sinare. Unganisha dotii. Na stanibic kulikuwa na sinare mwingine junior. Ha ha ha ha
 
Mapendekezo ya Baraza la Maadili ya Utumishi wa Umma bado hayajawekwa hadharani!

Wengi waliopelekwa kwenye baraza la maadili walikuwa ni wale waliokuwa karibu sana na mkweree na ndio maana hata baada ya baraza kumaliza kazi yake mtawala wetu akaamua kuchukua hatua reja reja kwa wahusika mpaka muda wake ulipomalizika; mfano ni huyo Gurumo , yeye alichofanya binamu yake ni kumuondoa kama mnikulu basi!!! Mkweree was an accomplice to many atrocious crimes that were committed during his presidency!!!
 
UCHUNGUZI unaoendelea wa serikali kuhusu ufisadi wa takribani shilingi bilioni 13 katika mkopo uliochukuliwa kupitia Benki ya Stanbic unaonyesha kuwagusa watu ambao walikuwa mstari wa mbele kwenye kampeni za vyama vilivyo kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imefahamika.

Ingawa kiwango halisi cha mkopo ambao serikali ilichukua kupitia benki hiyo ni dola milioni 600 (shilingi trilioni 1.3), ufisadi unaonekana katika kiwango cha dola milioni sita (shilingi bilioni 13) ambazo sasa imethibitika zilitumika kuwahonga viongozi wa serikali ili wauruhusu.

Kinara Bashir Awale
Huyu ndiye aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Stanbic wakati wa kutafuta na hatimaye kupatikana kwa fedha hizo. Kwa mujibu wa taarifa za kimahakama kutoka Uingereza, huyu ndiye alikuwa mtengenezaji wa mpango wote wa kupatikana kwa rushwa hiyo.

Mara baada ya kuondoka kutoka Stanbic mwaka 2013, kutokana na kukataa kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo, mara nyingi Awale alionekana akiwa na aliyekuwa mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowassa.

Ndani ya kambi ya Lowassa haikuwa siri kwamba endapo angeshinda urais, Awale angeweza kupewa nafasi ya Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Yeye ni mmoja wa watu waliokuwa wakitajwa kama wasaka fedha wakuu wa Ukawa na Lowassa. Akiwa na uzoefu wa muda mrefu katika eneo la benki na fedha, Awale alikuwa miongoni mwa wana Ukawa walioweza kujigamba kwamba wako karibu na Lowassa.

Kwa sasa, Awale amefukuzwa nchini kwa madai ya kutokuwa raia wa Tanzania lakini ukaribu wake na Lowassa unaonekana katika baadhi ya picha zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa katika mojawapo ya mikutano ya kisiasa ya Chadema, akiwa amekaa karibu na mtoto mkubwa wa Lowassa, Fred.

Uchunguzi wa vyombo vya usalama vya Uingereza unaonyesha kwamba wakati wa fedha hizo kulipwa kutoka Stanbic kwenda kwa kampuni ya EGMA, fedha zilikuwa zikitolewa kwenye akaunti na kwenda kwanza kugawiwa kwenye ofisi yake kabla ya kutoka nje ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Kinara Shose Sinare
Taarifa za kikachero kutoka Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Kijinai ya Uingereza (SFO), zinamtaja mfanyakazi huyu wa zamani wa Stanbic kama SS, na aliwahi kuwa Miss Tanzania mwaka 1996.

Katika ufisadi huu, Shose anatajwa kama msaidizi wa karibu wa Awale na mtu ambaye ukiondoa bosi wake huyo, alifanya kazi kubwa kuhakikisha mpango huo unafanikiwa. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kumhusisha Shose na Ukawa zaidi ya hatua ya mama yake, Dk. Eve Sinare, aliyekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutangaza kuhama chama hicho katika siku za mwisho za kampeni za Uchaguzi Mkuu.

Wakati Dk. Sinare akitangaza kuhama CCM, watu wengi walishangazwa na uamuzi wake huo kwa vile yeye si mmoja wa wanachama maarufu wa chama hicho na hatua yake hiyo haikuonekana kumsaidia yeyote. Mara baada ya kuibuka kwa kashfa hii ya Stanbic, maswali yameanza kuibuka kuhusu mwenendo wao katika wakati huo wa kuelekea Uchaguzi Mkuu. Inadaiwa kuwa kwa kawaida Dk. Sinare na Shose ni watu walio karibu sana.

Harry Kitilya
Huyu alipata kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Ushiriki wake katika kashfa hii umewashangaza wengi kwani kwenye jamii alijenga picha ya kiongozi msafi. Kitilya alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya EGMA ambayo ndiyo ilipewa kiasi hicho cha shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ?kulainisha viongozi wa serikali? kukubali kuchukua mkopo huo kutoka Stanbic.

Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, jina la Kitilya lilikuwa likitajwa kama mmoja wa watu waliokuwa wakichangisha fedha za kusaidia Lowassa ashinde uchaguzi.

Tofauti na watu kama Awale waliokuwa wakimuunga mkono Lowassa hadharani, Kitilya hakuwahi kutamka hadharani kumuunga mkono mwanasiasa huyo wala kuonekana kwenye mikutano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Kitilya, kwa nafasi aliyokuwa nayo TRA, ni mmoja wa watu waliokuwa wakiombwa ushauri na serikali iwapo ichukue mkopo au isichukue. Kwa maana hiyo, Kitilya alilipwa fedha hizo ili pia naye ?alainike? na ?kuishauri? serikali ichukue mkopo huo hata kama masharti yake hayakuwa muafaka.

Kwa mfano, wakati riba ya kawaida ya mikopo ilikuwa ni asilimia 1.4, mkopo huo ulichukuliwa kwa riba ya asilimia 2.4. Ongezeko hilo la asilimia moja ndilo lililoleta kiwango hicho cha shilingi bilioni 13. Ili kuhakikisha EGMA inapata fedha nyingi kupitia asilimia hiyo moja, badala ya serikali kukopa dola milioni 550 ilizotaka kukopa awali, ikakopa dola milioni 600. Kama ingekopa dola milioni 550, EGMA ingepata dola milioni 5.5 tu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa SFO, ingawa Kitilya ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya EGMA, hakuwahi kwenda kuchukua fedha hizo Stanbic na badala yake kazi hiyo ilifanywa na wabia wenzake, Dk. Fratern Mboya na Peter Nyabuti.

Peter Nyabuti
Uchunguzi wa SFO unamtaja Nyabuti kama raia wa Kenya na hakuna taarifa nyingi zinazomhusu. Hata hivyo, katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Nyabuti alikuwa mmoja wa wateja maarufu katika baa ya Kruz In iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kwa kipindi kirefu, baa hiyo imefahamika kama kambi rasmi ya ?Marafiki wa Lowassa? ambapo ni kawaida kwa watu waliokuwa kwenye kambi yake; tangu akiwa CCM, kujumuika na kubadilishana mawazo katika eneo hilo. Kwa sababu hiyo, Nyabuti aliyekuwa akichanganyika na watu kama Awale na Fred Lowassa, alikuwa akifahamika kama mmoja wa wapanga mipango na mikakati wa Ukawa.

Ingawa Chadema na vyama vilivyo kwenye Ukawa vimekuwa vikifahamika kwa kupinga ufisadi, hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa kambi hiyo aliyetoa kauli ya karipio dhidi ya ufisadi huo wa Stanbic.

Kwa sasa serikali inafanya uchunguzi kuhusu suala hilo na tayari imeahidiwa kwamba itarejeshewa shilingi hizo bilioni 13 zilizotolewa kama hongo.

Kwa hisani ya RaiaMwema

Kila nikisikia jina sinare natamani kulia hii familia ni moja ya familia zilizotufisadi sana nchi yetu
 
Wengi waliopelekwa kwenye baraza la maadili walikuwa ni wale waliokuwa karibu sana na mkweree na ndio maana hata baada ya baraza kumaliza kazi yake mtawala wetu akaamua kuchukua hatua reja reja kwa wahusika mpaka muda wake ulipomalizika; mfano ni huyo Gurumo , yeye alichofanya binamu yake ni kumuondoa kama mnikulu basi!!! Mkweree was an accomplice to many atrocious crimes that were committed during his presidency!!!
Kuna mambo mabaya sasa yamefanyika nchini!

Ukweli huchelewa kufika na naamini kuna siku ukweli zaidi utatufikia.

Ukweli kama kutumia zaidi ya bilioni 2 kwa ajiri ya semina elekezi ni ufisadi wa aina yake.
 
nilipomuona mzee warioba anapanda jukwaani kuhakikisha lowassa haingii ikulu, nikaanza kupata picha halisi ya lowassa na genge lake.

Mzee warioba ni kati ya wazee wachache wenye busara na hekima waliobaki nchini. Maneno na matendo yake yanabeba fikra fikirishi kwa watu wapevu kifikra.

Nchi yetu ilikuwa mbioni kutumbukia kwenye shimo la mauti. Mungu amefanya kazi yake iliyotukuka kupitia kwa wazee kama mzee warioba ili lowassa na genge lake wasiingie ikulu.

Chadema kama chama kupitia kwa mbowe na tundu lissu kilikuwa kinajinadi kama mkombozi wa watanzania, kimegeuka kuwa maajenti wa kuididimiza tanzania.

Mungu bado analipenda taifa letu.

wanaccm ni vinara wa ufisadi
 
Mleta maada anasahau yoote hayo yalifanyika hso watu wakiwa wanachama wa ccm!
 
Back
Top Bottom