Fedha za dhamana zitolewazo mahakamani huwa zinaenda wapi?

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
719
1592886507342.png

BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA
Salamu wakuu, naona weekend nayo inasogea taratibu.

Nimewaza tu hapa. Kumekuwa na fedha nyingi sana inayotolewa mahakamani na watuhumiwa mbalimbali kuhusu kesi kadhaa ili wapewe dhamana.

Utasikia "ameachiwa kwa dhamana ya TZS 10 Millioni, ameachiwa baada ya kutoa TZS 2 Million, wamekamilisha masharti ya dhamana wakatoa TZS 5 Million kila mmoja, nk".Mfano Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, kila siku iendayo kwa Mungu, mamilioni yanaingia pale kama benki vile.Na mahakama zinginezo huko mikoani nako watu wanatoka kwa dhamana ya hela nyingi sana.

Je,fedha hii itolewayo mahakamani kama dhamana, huenda wapi au hufanya kazi zipi?Hazina wanazichukua au ni mapato ya ndani ya Halmashauri husika?

Asanteni
---
Salaam,

Nimekuwa nikisikia mara kadhaa watuhumiwa hutakiwa kutoa kiasi fulani cha fedha kama dhamana dhidi ya mashtaka yanayowakabili ili waachiwe kutoka mahabusu.

Je, fedha hizi huwa zinarudi?

Asante.

BAADHI YA MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU
Dhamana sio mapato mkuu, dhamana (kama ni fedha taslimu) hurudishwa kwa mhusika (mdhamini) baada ya kuisha kesi au muda wowote atakapoamua kujitoa kama mdhamini wa mtuhumiwa, itaingizwa kama mapato pale tu mtuhumiwa atakapokiuka masharti ya dhamana kwa kutoroka na mdhamini ashindwe kumfikisha mahakamani au kueleza mahali alipo ili asaidiwe kumpata.

Hata hivyo mahakama itampa muda mtu huyu amtafute huyo mtuhumiwa na atakaposhindwa kumfikisha mahakamani mpaka muda aliopewa kuisha..basi ndio watakapoichukua hiyo pesa (kutaifisha) na kama dhamana ni mali (nyumba au kiwanja) watavutaifisha na kuvipiga mnada
---
Dhamana nyingi ambazo hazihusishi kesi za wizi wa pesa, ambapo dhamana inahusisha kuweka hati zisizohamishika zenye thamani ya nusu ya pesa unayodaiwa kuiba.

Dhamana zingine una sign hati (bond) sio cash!!! Mnadhimi anakuja na vitambulisho na barua zake za ofisini au mtendaji wa mtaa na ku sign hizo bond sio cash.
 
Asilimia 90 huwa ni katika maandishi tu. Kama mtu akikwepa hiyo dhamana,mdhamini ataleta hiyo milioni 10. Mara chache sana mshtakiwa hutakiwa kuweka dhamana ya pesa taslimu hutokea kwenye kesi nzito
Kama za Ngada?
 
Dhamana nyingi ambazo hazihusishi kesi za wizi wa pesa, ambapo dhamana inahusisha kuweka hati zisizohamishika zenye thamani ya nusu ya pesa unayodaiwa kuiba.

Dhamana zingine una sign hati (bond) sio cash!!! Mnadhimi anakuja na vitambulisho na barua zake za ofisini au mtendaji wa mtaa na ku sign hizo bond sio cash.
 
Hiyo no dhamana tu...kesi ikiisha zinarudi kwa wadhamini!
 
Ni kwamba unasaini bond kuwa utawasilisha fedha hizo ikiwa uliemdhamini atatoroka hivyo hutoi pesa taslim lakini ikikulazimu kutoa pesa taslim unatakiwa upewe/ udai risiti ya fedha hizo ili dhamana inapokwisha urudishiwe mpunga wako.
 
Hizo dhamana na faini zinakwenda kwenye mapato ya serikari japo ujanja ujanja mwingi
Dhamana sio mapato mkuu, dhamana (kama ni fedha taslimu) hurudishwa kwa mhusika (mdhamini) baada ya kuisha kesi au muda wowote atakapoamua kujitoa kama mdhamini wa mtuhumiwa, itaingizwa kama mapato pale tu mtuhumiwa atakapokiuka masharti ya dhamana kwa kutoroka na mdhamini ashindwe kumfikisha mahakamani au kueleza mahali alipo ili asaidiwe kumpata.

Hata hivyo mahakama itampa muda mtu huyu amtafute huyo mtuhumiwa na atakaposhindwa kumfikisha mahakamani mpaka muda aliopewa kuisha..basi ndio watakapoichukua hiyo pesa (kutaifisha) na kama dhamana ni mali (nyumba au kiwanja) watavutaifisha na kuvipiga mnada
 
Nimejifunza, kumbe hela za dhamana hurudishwa?
Naomba kuuliza, kama umemdhamini mtu mahakama ya Mwanzo amepangiwa tarehe ya kurudi Mahakamani, ikifika tareh husika kwani ni lazima mdhamini uwepo au yey mtuhumiwa akienda si basi inatosha?

Au??
 
Okay nashukuru kwa shule
Kwa kuongezea ni muhimu uwepo ili kama uliemdhamini akiwa hafiki basi upate taarifa na upewe amri ya kumfikishamtu huyo mahakamani kuliko. wote kuonekana watoro.
 
Back
Top Bottom