mr mkiki
JF-Expert Member
- Sep 22, 2016
- 5,717
- 11,917
Plata o plomo/Fedha au risasi.
Ni msemo wa kispaniola uliobuniwa na akina Pablo Escobar, bwana unga maarufu nchini Colombia mwishoni mwaka miaka ya 1970s. Kauli mbiu hii iliwalenga marafiki na mahasimu wa Pablo waliopo nje au ndani ya serikali. Pablo na wenzake walikuwa wakitoa ujumbe kwamba wasipokubali fedha watatunukiwa kifo.
Wakati akina Pablo wakifanya biashara zao za dawa za kulevya wakikutana na vikwazo vya wanausalama, walichagua kuwapa fedha ili waachwe na mambo yao yaende. Askari au mwanausalama au kiongozi aliyekataa fedha, alitafutwa na kuuawa kwa risasi. Plata o Plomo.
Mbinu hiyo imeigwa na makundi mengi duniani, aghalabu makundi yote ni ya kihalifu. Bila kujali kikundi fulani kinavaa bendera za Taifa au/na kutumia ofisi na malia za umma, kama kikundi hiko kinatumia mbinu hiyo ya kuhonga au kuua anayekataa kuhongwa, hiko ni kikundi cha uhalifu.
Mungu awarehemu viongozi wote wa kisiasa wanaoendelea kupoteza maisha kwa kusimamia misimamo yao. Tumeshahama kutoka kwenye siasa za uadui, sasa hivi siasa ni kifo.
Plata o Plomo.
Watanzania ni lazima tuishi kama mashetani.
mr mkiki.
Ni msemo wa kispaniola uliobuniwa na akina Pablo Escobar, bwana unga maarufu nchini Colombia mwishoni mwaka miaka ya 1970s. Kauli mbiu hii iliwalenga marafiki na mahasimu wa Pablo waliopo nje au ndani ya serikali. Pablo na wenzake walikuwa wakitoa ujumbe kwamba wasipokubali fedha watatunukiwa kifo.
Wakati akina Pablo wakifanya biashara zao za dawa za kulevya wakikutana na vikwazo vya wanausalama, walichagua kuwapa fedha ili waachwe na mambo yao yaende. Askari au mwanausalama au kiongozi aliyekataa fedha, alitafutwa na kuuawa kwa risasi. Plata o Plomo.
Mbinu hiyo imeigwa na makundi mengi duniani, aghalabu makundi yote ni ya kihalifu. Bila kujali kikundi fulani kinavaa bendera za Taifa au/na kutumia ofisi na malia za umma, kama kikundi hiko kinatumia mbinu hiyo ya kuhonga au kuua anayekataa kuhongwa, hiko ni kikundi cha uhalifu.
Mungu awarehemu viongozi wote wa kisiasa wanaoendelea kupoteza maisha kwa kusimamia misimamo yao. Tumeshahama kutoka kwenye siasa za uadui, sasa hivi siasa ni kifo.
Plata o Plomo.
Watanzania ni lazima tuishi kama mashetani.
mr mkiki.