Ni kweli, wanahitaji kupata mafunzo ya customer care! lakini saa ingine utakuta tu ni hulka zetu sisi wa rangi nyeus!Si precision wala fastjet wote wababaishaji tu.
Pole sana kwa matukio na samahani kwa nitakayoyasema.
Nilishaona kwa macho yangu, desk check ya Turkish Air ikiwa imefungwa saa moja kabla. Ila alikuwepo Mbabe mmoja akapiga simu kwa mama mmoja ndani na wakafungua ingawa wafanyakazi wa Turkish Air walishasema kuwa hadi kesho.
Naona nyie mlikosa mtu kama huyo.
Ila nashindwa kuelewa kitu kimoja, ninavyofahamu mie ni kuwa kwa sasa kwa sheria za ulinzi zilivyo uwanja wa ndege, unatakiwa ufike masaa mawili kabla yaani dakika 120 kabla. Sasa wewe nani alikuambia unafika dakika 40 kabla? Dakika 40 kabla ni kuwa ndiyo mnajiandaa kwenda kuingia kwenye ndege tayari na si kwamba ndiyo unafanya Check-In.
Naona ukaja tena kuchelewa hata Bus la kwenda KIA. Yaani hata Bus likakuacha jamani? Nalo sijui utasingizia nini?
Pole sana kwa tukio ila kumbuka kuwa uwanja wa ndege unatakiwa kufika saa MBILI kabla popote pale duniani labda kama umesha Check-In online na huna mzigo, yaani unafika tu na kuingia ndani kusubiri kupanda ndege.
Kwa ARUSHA hiyo ni sawasawa MACHIMACHI RESORT ya Kinondoni Shamba!....:heh::heh::heh::heh::heh:
Umeona eeeh!!!!Sisi wa mabasi hata getini unafunguliwa mlango unarukia na safari inaunga, huko angani mtanisimulia tuuuuuuuuuuu
Pamoja na hayo yote, bado inavyoonekana wewe sio wa status ya kusafiri kwa Bus.Mkuu Asante kwa ushauri, lakini kumbuka walioweka usafiri wa ndege sio wajinga kivile, kuna mazingira inafaa kusafiri kwa gari na mazingira mengine yana dictate matumizi ya usafiri mbadala. On this particular case, ilikuwa ni muhimu kusafiri kwa ndege kurudi Dar ili kupambana na muda!!!!
Tiba
Mkuu inawezekana wewe sio mzoefu wa usafiri wa anga hapa Tanzania. Hao Precision unaowasifia ipo siku utakuja hapa kuwaanzishia uzi wa kuwaponda. Kifupi inategemea tu bahati ya safari ya siku hiyo.
Mkuu waijua Machimachi?ha ha haaaa!
Umeona eeeh!!!!
Hadi raha. Sisi watanzania tuliochoka tutaendelea na usafiri wetu wa Analogia(Bus) mpaka hapo Digitali(Ndege) watakapokuwa wamejipanga(Ustaarabu) na pia sisi tukiwa tumeandaliwa vema(Kipato).
Na ole wake serikali kama itajaribu kufuta usafiri wa Analogia(Bus) ili tuhamie Digital(Ndege) kilazima.
Patachimbika!!!
Herg, am I wrong?, ndivyo ilivyo mkuu kwa ufahamu wangu na hii si story ni utaratibu wao.
Tiba
Pamoja na hayo yote, bado inavyoonekana wewe sio wa status ya kusafiri kwa Bus.
Nimekusoma kwenye maelezo yako hapo juu, sioni mahali popote ambapo wazo la kusafiri kwa Bus linaweza kujitokeza. Ninaona kabisa ni lazima ungesafiri na Ndege ama Private Car lakini sio Bus kwa namna yoyote ile.
Usafiri wa jamii(Daladala, Bus, Treni, Bodaboda, Baiskeli Mtumbwi, Malori) inaonekana ulishaachana nao zamani sana. Uko juu ndugu na usirudi nyuma.
Hongera ndugu!!!
Kwa domestic flight hii ni sawa kwani counter inatakiwa kufungwa 30min kabla ya ndege kuruka. Useme tu ukweli ni kwamba walishauza nafasi yako ndio maana hata ndege ilipozuiwa kuruka hawakukupa nafasi.
Ni kweli kabisa. Mimi katika maisha yangu sitakaa niwasahau hao Precision ambao niliapa mwaka 2002 kuwa sitapanda ndege zao tena lakini kama walivyosema "Never say Never" siku hizi napanda , kuna siku niitwa kwenye interview Mwanza kutoka Dar Es Salaam ilitakiwa iwe siku ya ijumaa. Kwa kuwa sikutaka mwajiri wangu wa wakati huo ajue nikazusha kuumwa nikaondoka ijumaa asubuhi na kufika mwanza mapema na kuwahi interview saa nne. Nilipanga nirudi jumapili ndege ya jioni. Niliambiwa niwe pale saa moja kabla.
Basi siku ya kurudi Dar niliwahi vizuri kabla hata ndege hiyo toka Dar haijafika. Nilimkuta mzee pale counter ya Mwanza pamoja na binti mmoja na jamaa mwingine ambaye alikuwa kwenye ofisi akicheza Karata kwenye Kompyuta. Nikawapa tiketi wakaniambia nisubiri, basi nikawa sina shaka nikanunua gazetu nikaanza lakini nikashangaa watu wengine wana-check in. Mimi nikaenda tena kuulizia wakaniambia niendelee kusubiri. Baadaye nikaona watu wengi wanaingia nikaenda tena kuulizia wakasema nisubiri kunaofisa anakuja kuongea nami.
Nikasubiri baada ya dk 5 hivi ndege toka Dar ikafika nikaulizia tena ndipo yule dada akaondoka akabaki yule mzee ambaye kazi yake ilikuwa kupima mizigo, ghafla akaja huyo ofisa ambaye alinitaarifu kuwa ndege imejaa kwa kuwa nilichelewa. Kwa kweli nilichanganyikiwa. nikasema nilejeshee fedha zangu nikapande basi. Wakasema eti watakata asilimia 20 nikasema sawa. Wakaniambia nisubiri baadaye wakaja kusema eti nije kesho yake saa nne, ndipo mhasibu atakapokuwa amefika. Kwa kweli nilichukia na kuchanganyikiwa. Baadaye walimwita askari mmoja ambaye alianza kunitishia kuwa angeniweka ndani, nilikuwa na simu (Mshindi) nikajaribu kupigia simu za mamaeneja zilizokuwa kwenye nembo yao ama zilikuwa hazipokelewi ama hazipatikani.
Mama mmoja alinionea huruma ndipo akaja akaniambia kuwa wakati ule ile ilikuwa kawaida. aakaniambia kuwa kuna binti wa mkubwa alipata safari ya ghafla ndiye aliyepewa nafasi yangu, na wakati nasubiri walikuwa wanaangalia kma kuna abiria ataahirisha safari lakini hakupatikana. kwa kuwa usafiori wa basi ulikuwa mgumu wakati huo, na kwakuwa ingebidi nianze safari siku ya jumanne na kufika jumatano (kwani pesa ningepewa saa nne) nilisafiri na dege yao ya jumatatu asubuhi na kufika Dar saa 5 hivi.
Kuna matukio related na hilo yalifuata ambayo yaliniathiri maishani mwangu, yaani kutosafiri kurudi Dar jumapili kama nilivyopanga. Yule binti sikuwahi kumwona tena ila yule mzee (alikuwa na jicho moja bovu akipendelea kuvaa T-shirt nyeupe) aliendelea kuwepo pale mpaka kwenye miaka ya 2006 hivi kwani nilikuwa nikipita pale na kumwona roho yangu ilikuwa inastuka sana.
Hivyo nakubaliana nawe huku Afrika wasafiri hawana haki kabisa.
Siku ya tarehe 26 April 2013, nilikutana na mkasa wa hawa jamaa zetu wa Fastjet na tangia siku hiyo nilinuia, kutokufikiria kutumia usafiri wa hii ndege tena. Kisa chenyewe kilikuwa hivi;
Nilisafiri kwa gari binafsi kutoka Dar kwenda Arusha tarehe 21 April 2013 na nilitarajia kurudi Dar Ijumaa ya tarehe 26 April 2013 kwa kutumia ndege ya Fastjet iliyokuwa iondoke Arusha (KIA) saa 3:30 usiku. Nilikuwa na tiketi mkononi. Taratibu za Fastjet ni kuripoti dakika 40 kabla ya muda wa ndege kuondoka. Nilikodisha taxi kutoka Arusha na nilifika KIA saa 2:40 usiku. Nilipofika, taxi iliyonipeleka pale iliondoka. Kufika mlangoni, walinzi wakanimbia kwamba nimechelewa na kwamba counter tayari imefungwa na hakuna mtu wa kunicheck in. Nilimkuta na Bwana mwingine aliyekuwa amenitangulia kufika na yeye akibembeleza kuruhusiwa kuingia. Wale walinzi walikataa katakata na ukweli ni kwamba pale counter hakukuwa na mtu hata mmoja. Kwa kushirkiana na msafiri mwenzangu niliyemkuta pale, tulianza jitihada za kutaka kuonana na mwakilishi wa Fastjet pale uwanjani. Jitihada zetu za kumwona mwakilishi wa Fastjet hatimae zilifanikiwa lakini to our suprise, yule Bwana alikuwa too arrogant kupita kiasi. Alitwambia hakuna msaada wowote anaoweza kutupatia. Ndege ilikuwa bado iko pale uwanjani. Wakati tukiendelea kumbembeleza, aliitwa kwenye radio call na hivyo akatutaka tutoke ofisini kwake na kwamba angekuja kutusikiliza baadae lakini akasema msaada pekee anaoweza kutupa ni kutukatia ticket nyingine kwa ajili ya ndege ya Jumamosi asubuhi tarehe 27 April 2013.
Baadae tulipata taarifa kwamba ndege haiwezi kuondoka kwa kuwa imepata hitilafu na kwamba abiria ambao tayari walikuwa wamepanda wameshushwa na kurudi waiting room. Yule mwakilishi wa Fastjet hakurudi tena ofisini pale ingawaje tuliendelea kumsubiri. Kwa kuwa nilikuwa na mkutano muhimu wa kuhudhuria Dar Jumamosi tarehe 27 April 2013, nilianza kufanya mpango wa kuangalia uwezekano wa kupata seat kwenye ndege ya Precision Air iliyokuwa iondoke Arusha (KIA) saa 1:55 asubuhi kuelekea Dar. Bahati nzuri nilimpata mwakilishi wa Precision Air pale uwanjani ambaye baada ya mawasiliano alinihakikishia kunipatia seat kwenye hiyo ndege. Tatizo sikuwa na cash ya kulipia hiyo ticket ambayo gharama yake ilikuwa Tshs. 195,000 one way. Baada ya kuhakikishiwa seat, nililazimika kukodisha taxi ya kunirudisha mjini ili kupata hela za kulipia ticket ya Precision kutoka kwenye ATM. Nilifanikiwa kupata hela na baada ya hapo kazi ya kutafuta hotel ikaanza. Nilipata Hotel na nililala karibu saa 6 usiku.
Saa 11:30 alfajiri tayari nilikuwa kwenye ofisi za Precision Air pale Arusha ili kupanda shuttle kwenda KIA. Kufika tu, nikaambiwa tayari shuttle ilikuwa imeondoka hivyo nalazimika kutumia usafiri wangu kwenda KIA (Ukweli ni kwamba shuttle ilikuwa haijaondoka na wala ilikuwa haijafika ila mlinzi anashirikiana na taxi drivers kudanganya abiria ili wakodishe taxi zao). Nilifanya hivyo na kufanikwa kufika Dar kwenye saa 3:45 asubuhi Jumamosi. Wakati turuka pale KIA, ile ndege ya Fastjet tuliiacha pale na sijui iliondoka saa ngapi. Abiria walilala pale uwanjani bila huduma yoyote hata maji ya kunywa hawakupewa.
Nia ya kuleta uzi huu ni kuwaambia wana Jamvi kwamba wakati mwingine rahisi ni ghali. Safari hii ilinigharimu pesa nyingi sana kwa kuwa tu nilitaka ticket rahisi ya Fastjet (Tshs. 107,000) one way lakini matokeo yake niliingia gharama zifuatazo;
1. Ticket ya Fastjet Tshs. 107,000
2. Taxi Arusha KIA x 3 Tshs. 150,000
3. Hotel tarehe 26/4 Tshs. 50,000
4. Ticket ya Precision Tshs. 195,000
Jumla Tshs. 502,000
Nilinuia hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kujaribu kusafiri na Fastjet na ilikuwa mara ya mwisho pia. Sitakaa nithubutu kufanya makosa tena hata kama Fastjet wata improve huduma kwa wateja na kuajiri watu wanaoweza kuwasiliana kwa heshima na wateja.
Tiba [Mkuu pole sana kwa shida hizo, kwa kifupi hawa jamaa ni wasanii sana na hawajajipanga, na hizi shida za kusema kila siku ndege ina hitilafu zimekuwa nyingi sana! narudia tena chonde chonde serikali iangalieni ndege hii,Very poor customer service na hata technical part yake nadhani pia ni POOR/QUOTE]