Fastjet kupunguza wafanyakazi

Fastjet kupunguza wafanyakazi

NBC nao wanapiga restructuring ya kufa mtu..

baclays bank anaondoka africa nae.. hapo lazima tuisome namba
 
Kampuni binafsi ya usafiri wa anga, Fast Jet imeamua kupunguza wafanyakazi ili kwenda sambamba na gharama za uendeshaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Fast Jet, John Corse ametoa taarifa kwa gazeti la The Citizen inayoeleza kuwa watapunguza wafanyakazi kutokana na mabadiliko ya kimuundo na uendeshaji.

“Wateja wamepungua, hawapandi ndege sasa. Hivyo ili kampuni ipate faida, ni lazima ipunguze baadhi ya wafanyakazi ili kuendana na gharama za uendeshaji,” anasema Corse kwenye taarifa hiyo.

Alipoulizwa kama sababu ya kupunguza wafanyakazi inaweza kuwa inatokana na mikakati ya kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Corse amejibu: “Si kwa sababu ATCL inafufuliwa bali ni changamoto za kibiashara.”

Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alitangaza kuwa ndege mbili ambazo Serikali iliahidi kuzinunua zitafika nchini kati ya Septemba 19 na 25.


Chanzo: Mwananchi
 
kampuni binafsi ya usafiri wa anga, Fast Jet imeamua kupunguza wafanyakazi ili kwenda sambamba na gharama za uendeshaji.



Mkurugenzi Mtendaji wa Fast Jet, John Corse

ametoa taarifa kwa gazeti la The Citizen inayoeleza kuwa watapunguza wafanyakazi kutokana na mabadiliko ya kimuundo na uendeshaji.



“Wateja wamepungua, hawapandi ndege sasa. Hivyo ili kampuni ipate faida, ni lazima ipunguze baadhi ya wafanyakazi ili kuendana na gharama za uendeshaji,” anasema Corse kwenye taarifa hiyo.



Alipoulizwa kama sababu ya kupunguza wafanyakazi inaweza kuwa inatokana na mikakati ya kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Corse amejibu: “Si kwa sababu ATCL inafufuliwa bali ni changamoto za kibiashara.”



Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alitangaza kuwa ndege mbili ambazo Serikali iliahidi kuzinunua zitafika nchini kati ya Septemba 19 na 25.

Chanzo:Mwananchi
mfupa aliyo ushindwa fastjet ATCL itauweza?
 
Ndege inafanya safari abiria wakifika hata robo tatu wanashukuru mungu maana hali ilivyo tete kujaza ni ishu,wana haki ya kupunguza wafanyakazi hakuna mfanyabiashara anaependa hasara..siku hizi hata wenye mabasi wanaomba shule zifungwe hata kesho wapakie wanafunzi sababu mabasi hayajazi watu wamefunga kusafiri..
 
Kama walisave misharaha yao,basi ni suala dogo tu la kubadilisha Fedha kweda kwenye Mawazo,na kisha kuwekeza.

Wao wafanyakazi kama wanalia,je wale ambao hataneno ajira kwao ni tatizo inakuwaje.

So,wao wana advantage kubwa sana,this is a worldwide issue.
Nchi nyingi sana mabadiliko haya hutoke,mwenye akili atatumia akiba yake kwa kujikwamua zaidi,ila bongo lala hapo lazima ataisoma.
Na wapo watu ambao wanaweza kufanikiwa zaidi baada ya kutoka kwenye ajira,na mifano ipo
Mungu awape wepesi na uwezo wa kufikiri.
 
Kwenye kila mada yake lazima aweke link za mada zake za nyuma, huko ni kulazimisha ugwiji wa JF kama jamaa mmoja hivi...
Ni kweli na ni kwasababu kuna watu huwa ni wabishi sana hivyo yanapotimia huwa ni budi tuwakumbueshe na kuwaonya waache ubishi.
 
Ni kweli na ni kwasababu kuna watu huwa ni wabishi sana hivyo yanapotimia huwa ni budi tuwakumbueshe na kuwaonya waache ubishi.
Lakini na wewe ni mpenda umaarufu mwepesi. Vipi tabiri zenu za duru za kisiasa zikienda fyongo, huwa mnafufua thread pia?
 
Back
Top Bottom