FastJet kunani

FastJet kunani

haibreus

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2009
Posts
295
Reaction score
106
Hivi kunani FastJet maana nimekata ticket online kupitia Mpesa hapa Tanzania, pesa kweli ikakatwa vizuri lakini sikupata feedback, baadae nikawapigia FastJet wakaniambia kuwa niwaambie Vodacom warudishe pesa nianze upya nikawauliza sababu wakasema hawaioni pesa yangu OK, nikapiga moyo konde nikarudi Vodacom kweli wakarudisha pesa yangu.

Nikaanza hatua upya za booking na nikalipa tena nikasubiri feedback kimya nikawapigia wakasema pesa yangu haipo labda nirudi tena Vodacom, kuanzia hapo nikakaa chini na kuanza kufanya uchunguzi nikagundua yafuatayo;

1. Customer care wa FastJet wengi wanajua English ya hali ya juu ila hawana elimu.

2. Ukifanya malipo kwa Mpesa, pesa zako huenda kwa mawakala wanaojiita Pay Pal ambao wapo Naivasha road, Kenya japo sina uhakika kama wana ofisi au ni nyumbani kwa mtu

3. Hawa PayPal Kenya wao ndio hufanya uwakala na FastJet wa kuprocess malipo na confirmation, tatizo lao hawa wanaonekana wapo kama Richmond flan hivi maana hawako active hadi uwatekenye na simu zao huwa busy all times labda utumie email.

4. Connection kati ya Vodacom ,FastJet na PayPal inaonekana sio nzuri either ni system au ni mambo ya madili au wote hawajui wanachokifanya.

5. FastJet haina tofauti na mabasi ya ubungo.

6. Wahudumu wa FastJet inaonekana ni vibarua kwa sababu wanapenda sana kuomba na kupora vipodozi vya abiria.

7. Wahudumu wa ndani ya ndege hawarudishi change na wanaover price bidhaa.

8. Hakuna uhusiano mzuri kati ya mteja na FastJet in terms of complaints and refund.

9. FastJet ni kampuni ya matapeli japo wanasifa MOJA TU NZURI

10. Sifa nzuri ya FastJet ni kutuwahisha kufika safari zetu ila mengine yote wanahitaji kufanya supplementary.

Nawasilisha
 
Mimi natafta no. Zao ofc ya Mwanza kila nikipiga inaita tuu hakuna anayepokea nyingine zote za dar haukuna inayopatikana.Kama unazo no nisaidie hasa za mwanza.
 
Wameshapihwa lidandasi bado wana stress.. Wasamehe tu hao staff wa FJ
 
Mimi natafta no. Zao ofc ya Mwanza kila nikipiga inaita tuu hakuna anayepokea nyingine zote za dar haukuna inayopatikana.Kama unazo no nisaidie hasa za mwanza.
Yes n kwel Mwanza utapiga sim siku nzima haipokelewi
 
Hiyoo no.6 mkuu ni kweli kabisaa mpka leo najiuliza ni nini sababu ya kunyang'anywa lotion,spray na mafta ya nywele na hawa wakaguzi wao fastjet.....inakera sanaa
 
Hiyoo no.6 mkuu ni kweli kabisaa mpka leo najiuliza ni nini sababu ya kunyang'anywa lotion,spray na mafta ya nywele na hawa wakaguzi wao fastjet.....inakera sanaa
Kule Marekani walishazoea. Hairuhusiwi kuingia na aina yo yote ya liquid au vilainishi. Hali hii ililetwa na yule gaidi wa Kinaijeria aliyetaka kudondosha ndege kule Detroit Marekani baada ya kuchanganya kemikali kwenye choo cha ndege. Mashirika mengi ya ndege duniani kwa sasa wanafanya hivyo kwa kisingizio cha ugaidi. Marekani vitu vyote vinavyotaifishwa kutoka kwa abiria huchomwa moto. Hapa kwetu sitashangaa kama wafanyakazi wanagawana. Kwa hili nadhani Fast Jet wanafuata protokali za kimataifa kuhusu usafiri wa anga.
 
Ndege zao nzuri,tusubirie a very big competition from ATC, nadhani wataacha maringo na ndege zqo zitaanza kwenda MTWARA sasa,maana wamedai runway ni mbovu ngoja tuone,ATC anaweza kuwa Mkombozi
 
mi nilishaacha kukwea Fastjet maana bei zao hazieleweki pia ikitokea ukapata dharura cndo imekula kwako, nilishachelewa connection NAIROBi kisa cancellation ya ndege yao ya DAR to NBO.
 
Back
Top Bottom