Fastjet Interview inapaswa kuigwa na makampuni mengine Tanzania

Fastjet Interview inapaswa kuigwa na makampuni mengine Tanzania

BURUDIKA

Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
91
Reaction score
8
Habari wana JF.

Jamani wana JF nashuhudia kitu nilicho kiona ktk interview ya kampuni ya ndege FASTJET iliyofanyika tar 4 mwezi huu pale Accomondia Hotel kuwa hakuna mtu kupendelewa yani ni fair na haki kiasi kwamba kila mtu anaondoka ameridhika tena kwa moyo mmoja. Nilitegemea nitakuta MAGUMASHI kama nilivozoea kwenye makampuni mengine ila wale jamaa ni noma na wanafaa kuigwa, kama ww ni mzuri wa interview za written utapata haki yako na kama ww ni mzuri wa interview ya oral utapata haki yako pia.

Naombeni makampuni mengine muige inteview za hawa jamaa mtapata watu wa kuwasaidia kwenye kazi zenu mlizo panga mwombaji azifanye baada ya kumuajiri.
 
Kwani fastjet wanafanyia interview kwenye ndege??? Halafu nilisikia wataanza kwenda usa na uk kwa laki 5. Ni kweli??
 
unakumbuka community air line!!!???ilikufa km analogia!!!cha msingi reasonable price with maximum profit!!!
 
unakumbuka community air line!!!???ilikufa km analogia!!!cha msingi reasonable price with maximum profit!!!

Dah community airline..nlivuta mwanasheria hadi Mwanza thru hawa jamaa bana sjui walienda api
 
jamaa wale walikuwa ni watanzania waliojiunga na kukodi ndege nje na kufanikiwa kununua moja,bahati mbaya nadhani hawakuelewana miongoni mwa share holders hasa ktk bodi ya wkurugenzi,wakashindwa kuendesha kampuni wakagawan kila mtu chake kampuni ikafa!!!makampuni mengi ya kizalendo(ya watanzania) yaishiaga kufa tu,cjui watanzania tuna nn!??
 
jamaa wale walikuwa ni watanzania waliojiunga na kukodi ndege nje na kufanikiwa kununua moja,bahati mbaya nadhani hawakuelewana miongoni mwa share holders hasa ktk bodi ya wkurugenzi,wakashindwa kuendesha kampuni wakagawan kila mtu chake kampuni ikafa!!!makampuni mengi ya kizalendo(ya watanzania) yaishiaga kufa tu,cjui watanzania tuna nn!??

Mkuu Community airline ilikufa kutokana na matatizo ya uendeshaji ambayo yalisababishwa na aina ya mkataba wa ndege walizozikodisha. Kwenye masuala ya kukodi ndege kuna aina mbili za mikataba, dry na wet. Dry unapewa ndege tu halafu wewe unaajiri marubani, engineers na wafanyakazi wengine wote. Wet unapewa ndege pamoja na marubani, engineers, na pengine usipokuwa makini utapewa mpaka airhostless. Community airline walikodisha ndege kwa mkataba wa wet hivyo marubani na most of the employee kwenye hiyo ndege hawakuwa Watanzania. Hawa jamaa badala ya kuwasikiliza na kupokea order na maelekezo kutoka kwa waliokodisha ndege wao walikuwa wanariporti kwa walitoa ndege. Hii ilileta mkanganyiko kiutendaji. Lakini tatizo zaidi ilikuwa ni kuingiza uswahili kwenye operations. Kwa mfano marubani wana masaa ambayo hawapashwi kuyazidisha wakiwa angani kwa siku, kwa wiki na kwa mwezi. Hawa washwahili wenzetu walikuwa wanapata route nyingine kubeba wanasiasa au wafanyabiashara kinyume na route zilizokubalika hivyo walikuwa wanawataka marubani kuacha route za kawaida na kuchukua hizo tenda. Hii ilkuwa ngumu kwa marubani kwani kwa kufanya hivyo wangeruka masaa zaidi ya yale waliyopangiwa. Wakawa wanagoma kuruka as a result, wenye biashara yao wakaamua kusitisha mkataba na kurudisha ndege.

Nafikiri walikuwa hawajajipanga kukutana na challenges kama hizi.

Tiba
 
nimekusoma sn ndugu,kumbe kny kuchange route c daladala tu hata ndege???dah wabongo nouma sn!!!wajipange upya kwa kubadilisha aina ya mikataba,pia kufanyia kazi challenges zote zilizopelekea wao kucollapse,nadhani nao walileta ushindani mzur sana kipindi hicho,sasa wakirudi watakimbizana na fastjet duhh wateja tutafaidi kwa mapunguzo ya bei kila siku!!
 
tiba tunashukuru kwa shule uliyotupa
ila fastjet wamejipanga na wanasaidia sana hasa huku mwanza na mbeya
maana wale wazee wa swala wana bei utadhani ndege walioandikiwa kupanda ni watu flani tu
hongereni sana fastjet
 
bosi msigwa,community ndio hii hapa fastjet na nyingine imeanzishwa juzi kenya ni gharama kama hizi kutokea nai kwenda kisumu na mombasa ni kama 50,000/- so hii ndio community bana hata bata na kuku wanabeba.
 
Mleta mada ss ulichoelezea ni wasifu we thank i.
Ss hw wz it?!
 
Kwani fastjet wanafanyia interview kwenye ndege??? Halafu nilisikia wataanza kwenda usa na uk kwa laki 5. Ni kweli??

Kuna siku ceo alikuwa kwenye page yao aliruhusu ushauri maswali namalalamiko nikamshauri route za Guangzhou na Dubai zina vichwa vingi akasema hawana mpango wa route yoyote ya nje ya bara.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom