Faragha (UWATA) Tanzania

Faragha (UWATA) Tanzania

Nashukuru sana mkuu .... Nimekuelewa, niliuliza hili swali baada mke wangu kuanza kusali huko sasa Imekua changamoto maana Mimi nasali Lutheran yeye anasali huko faragha na huku Lutheran sasa nashindwa kuelewa which is which.....

Ushauri plz

Sent using Jamii Forums mobile app
Fanya maamuzi kama Mwanaume uliekamilika,piga stop haraka unakaribisha matatizo makubwa nyumbani kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Any feedback mkuu
Yaa nikweli kabisa ni zaidi ya miaka 5 nilikuja hapa JF kuomba ushauri lkn kwa kifupi tuu ni kwamba ilinibidi kukubaliana na hali kwanza Cz haikua rahisi ukizingatia mwenzangu (mke) alikua serious sana na hakua tayari kuacha kwenda kwa namna yoyote Ile so nilimwacha aendelee na hicho kikundi chake baada yakujiridhisha kupitia baadhi ya viongozi wa dini kua ni sehemu salama na sio dhehebu ila nikikundi cha maombi ambacho mtu yoyote wadhehebu lolote anaweza kujiunga lakini bado akabaki kwenye dhehebu lake.
Mpaka Sasa mama watoto yupo huko pia nilicho observe kwenye hiki kikundi ; upendo, utii kwa mke/mme na jamii kwa ujumla, Kwa ujumla advantage ni nyingi kuliko disadvantage.
 
Yaa nikweli kabisa ni zaidi ya miaka 5 nilikuja hapa JF kuomba ushauri lkn kwa kifupi tuu ni kwamba ilinibidi kukubaliana na hali kwanza Cz haikua rahisi ukizingatia mwenzangu (mke) alikua serious sana na hakua tayari kuacha kwenda kwa namna yoyote Ile so nilimwacha aendelee na hicho kikundi chake baada yakujiridhisha kupitia baadhi ya viongozi wa dini kua ni sehemu salama na sio dhehebu ila nikikundi cha maombi ambacho mtu yoyote wadhehebu lolote anaweza kujiunga lakini bado akabaki kwenye dhehebu lake.
Mpaka Sasa mama watoto yupo huko pia nilicho observe kwenye hiki kikundi ; upendo, utii kwa mke/mme na jamii kwa ujumla, Kwa ujumla advantage ni nyingi kuliko disadvantage.
Na wewe ujiunge sasa
 
Harrison uwata mbeya umenikumbusha mbali kidogo kifupi ni wazuri Wana misimamo mizuri sana wanakata nywele na ni safi mda wote wanavaa sketi za marinda wanaongea taratibu ni wasafi sana wa mwili kifupi ni wazuri
 
Ndugu yangu, kama mke wako ameamua kuingia faraghani, mshukuru Mungu na mwache aendelee, utanishukuru kesho.
 
UWATA (Uamsho wa Wakristo Tanzania) ni dhehebu la dini ya kikristo kama yalivyo madhehebu mengine. Dini na dhehebu lolote anakaribishwa kujiunga dhehebu hili.
Kujiunga nao, unatakiwa kutubu dhambi na kuziacha kabisa.
Utambulisho wao wa mavazi kwa wanawake ni sketi ndefu ya marinda na blauzi au gauni ndefu yenye marinda, kukata nywele, kutovaa heleni, bangili, cheni, rozari wala mapambo aina yoyote. Kwa wanaume, suruali ya kitambaa na shati au tisheti, suruali za jeans haziruhusiwi.
Nyumba yao ya ibada wanaiita "faragha", yaani wanakutana na kusali pasipo kujionyesha machoni pa watu. Faraghani huwa hakuna mabenchi wala viti, bali kuna mikeka tu, hii wanaenzi agano la kale la mitume na kinabii.
Mwanzilishi wa imani hii anaitwa Harrison Mwakiswalele.
Umesahau kusema wanavua viatu waingipo Faraghani.
 
Back
Top Bottom