Faragha (UWATA) Tanzania

Faragha (UWATA) Tanzania

nani mwanzilishi
Capture.PNG
 
Hao jamaa wana shule zao zinafanya vizuri mno, wana Hospitali, pia ni taasisi ya DINI.

WAGUGO utawajua vizuri
 
Mwanzilishi anaitwa Mwakiswalele, alianzia huduma yake Mbeya, na alifariki miaka ya 90 licha ya kwamba kuna watu wanaamini hakufa ila alikimbilia Uingereza

kwa Mujibu wa hapo amefariki mwaka 91, kwann wanaamini alikimbilia uingereza??
 
UWATA (Uamsho wa Wakristo Tanzania) ni dhehebu la dini ya kikristo kama yalivyo madhehebu mengine. Dini na dhehebu lolote anakaribishwa kujiunga dhehebu hili.
Kujiunga nao, unatakiwa kutubu dhambi na kuziacha kabisa.
Utambulisho wao wa mavazi kwa wanawake ni sketi ndefu ya marinda na blauzi au gauni ndefu yenye marinda, kukata nywele, kutovaa heleni, bangili, cheni, rozari wala mapambo aina yoyote. Kwa wanaume, suruali ya kitambaa na shati au tisheti, suruali za jeans haziruhusiwi.
Nyumba yao ya ibada wanaiita "faragha", yaani wanakutana na kusali pasipo kujionyesha machoni pa watu. Faraghani huwa hakuna mabenchi wala viti, bali kuna mikeka tu, hii wanaenzi agano la kale la mitume na kinabii.
Mwanzilishi wa imani hii anaitwa Harrison Mwakiswalele.
 
UWATA (Uamsho wa Wakristo Tanzania) ni dhehebu la dini ya kikristo kama yalivyo madhehebu mengine. Dini na dhehebu lolote anakaribishwa kujiunga dhehebu hili.
Kujiunga nao, unatakiwa kutubu dhambi na kuziacha kabisa.
Utambulisho wao wa mavazi kwa wanawake ni sketi ndefu ya marinda na blauzi au gauni ndefu yenye marinda, kukata nywele, kutovaa heleni, bangili, cheni, rozari wala mapambo aina yoyote. Kwa wanaume, suruali ya kitambaa na shati au tisheti, suruali za jeans haziruhusiwi.
Nyumba yao ya ibada wanaiita "faragha", yaani wanakutana na kusali pasipo kujionyesha machoni pa watu. Faraghani huwa hakuna mabenchi wala viti, bali kuna mikeka tu, hii wanaenzi agano la kale la mitume na kinabii.
Mwanzilishi wa imani hii anaitwa Harrison Mwakiswalele.
Nashukuru sana mkuu .... Nimekuelewa, niliuliza hili swali baada mke wangu kuanza kusali huko sasa Imekua changamoto maana Mimi nasali Lutheran yeye anasali huko faragha na huku Lutheran sasa nashindwa kuelewa which is which.....

Ushauri plz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru sana mkuu .... Nimekuelewa, niliuliza hili swali baada mke wangu kuanza kusali huko sasa Imekua changamoto maana Mimi nasali Lutheran yeye anasali huko faragha na huku Lutheran sasa nashindwa kuelewa which is which.....

Ushauri plz

Sent using Jamii Forums mobile app

Wale jamaa ni Muunganiko wa makanisa mbalimbali wapo waroma, waKKT, wa moravian,wasabato, angalikana etc etc, mule huwa wanasoma sana bibilia na kuomba, wnasali kila siku mchana.

ondoa mashaka kabisa.
 
Tatizo litakuja pale atakapogoma watoto kupelekwa hospitali na kukazana kukemea magonjwa.
Acha uzushi wewe, vitu usivyovijua ni bora kukaa kimya, wale watu hospital huwa wanaenda, na zaidi ya hayo wao wenyewe wanamiliki hospital kubwa kabisa ya kisasa ipo mbeya maeneo ya ivumwe, ni hospitali bora kabisa kwa nyanda za juu kusini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom