Ni siku chache zimepita tumemsikia mkurugenzi wa NSSF Dk akieleza kamati ya mashirika ya umma fao la kujitoa kamwe halitawezekana kwa mfanyakazi atakayejitoa hadi miaka 55 au 60. Wakati tunajiunga na mfuko huu hawakutueleza hayo ila kwa sasa kwa sababu wanazifanyia biashara na zimewanogea kwa sababu wanazifanyia biashara bila riba wameamua kuziwekia sheria kandamizi ile waendelee kunufaika nazo. Ni aibu kufananisha nchi yetu na nchi za ulaya ambazo hata kodi wanazolipa zinakidhi yale mahitaji ya jamii na dhamani ya hela yao ikiendelea kupanda wakati shilingi yetu ikishuka. Je thamani ya fao langu la mwaka huu litakuwa na dhamani sawa na kusubiria miaka 20..!? Tumekuwa watu wa kuiga kila kitu hatuwezi kuwa na mfumo wa kwetu unaoendana na maisha yetu? au ni uvivu wa kufikiri ndio maana tunaiga kila kitu kwa wenzetu! wafanyakazi tumekuwa janga, kodi kubwa sisi, mshahara hautoshelezi watu wengi wameweza kufungua au kuanzisha vipato vya ziada kwa kutumia mafao ya kujitoa.
Wafanyakazi tuungane kwa pamoja kupinga na kusema hapana kwa hii sheria kandamizi. Kukaa kimya ndio mwanzo wa kuwapa nguvu akina Dk D kujiona wao wanaweza kusema wanavyojisikia.
Nawakilisha wana GT tuchangie ktk hili tuone limekaaje.
Wafanyakazi tuungane kwa pamoja kupinga na kusema hapana kwa hii sheria kandamizi. Kukaa kimya ndio mwanzo wa kuwapa nguvu akina Dk D kujiona wao wanaweza kusema wanavyojisikia.
Nawakilisha wana GT tuchangie ktk hili tuone limekaaje.