Familia inahitaji ushauri wenu wanajf

Kitukizuri

Member
Apr 25, 2011
21
1
Tulikua na kijana wa kazi kutoka iringa,tuliishinae kwa takribani miezi kumi na tatu lakini alikuja kudhihirisha tabia zake za ulevi kupita kiasi,kiasi cha kusahau majukumu yake.mwisho wa siku yeye mwenyewe akaamua kuondoka nakusema anaenda kwao.basi tukampa chake,tukaagana.lakini inasema hakurudi kwao akawa anarandaranda mitaani..sasa leo tumeletewa taarifa amegongwa na gari amefariki.yuko chumba kuhifadha maita.sasa huku hana ndugu.watu wote wanatuangalia sisi.sisi tufanyaje ukizingatia kwao hatuna mawasiliano nao.gharama za kusafirisha kubwa,kwao iringa ndanindani huko hatupajui.
 
poleni sana, labda tuanzie hapa....mlimpataje?
\

eeeewaaaaaaaaaa!..Preta kweli umenena,mtu wamekaa nae miezi 13(zaidi ya mwaka)lakn hawajui anatoka wapi...mimi nafikiri kuna kukwepa uwajibikaji hapa.
Suala la watu kuwaangalia nyie kwa ajili ya msiba ni sahihi kabisa na inabidi muwajibike ipasavyo,....gharama za kusafirisha sio issue mnaweza hata kuzika hapo mlipo.
 
miez 13 mnakaa na mtu hampajui kwao? Ingetokea amefia mikonon mwako ungefanya nini? Jibu swali la preta then ndo tutajua cha kukushauri.
 
tulitewa na mama mmoja ambaye kwa sasa amerudi iringa na hatuna mawasiliano nae
\

halafu mkakaa nae more than a year bila kumuuliza anatoka wapi,.....anyway poleni lakn msiba unawahusu sana na msikwepe kabisaaaaaaaaaaaaaa
 
t<span style="color: rgb(0, 0, 205);">ulitewa na mama mmoja ambaye kw</span>a sasa amerudi iringa na hatuna mawasiliano nae
\<br><br>halafu mkakaa nae more than a year bila kumuuliza anatoka wapi,.....anyway poleni lakn msiba unawahusu sana na msikwepe kabisaaaaaaaaaaaaaa,...wekeni picha kwenye vyombo vya habari kama tv,magazet
 
Makosa mawili mliyofanya hayawezi kurekebishika. Kwanza kukaa naye muda wote huo bila ya kujua kwao ni wapi, wazazi wake ni akina nani, kutomuuliza huyo mama aliyewaletea habari zote zinazomhusu.
Kosa la pili ni pale aliposema anarudi nyumbani mkamwacha aondoke bila ya kujua anaelekea wapi. Laiti mmoja wenu angamsafirisha hadi kwao!
Kilichobaki ni kukubali jukumu lenu. Ikiwa hamjui kwo wapi, mzikeni hapo hapo mlipo, lakini ni lazima mbebe jukumu hili.
Poleni sana kwa msiba.
RIP HG.
 
Ni kweli tulifanya kosa,lakini cha muhimu sasa ni kuangalia nini cha kufanya.tunajaribu kufatilia kwa rafiki zake tumegundua kwao ipogolo.tunajaribu kutafuta ndugu zake
 
Makosa mawili mliyofanya hayawezi kurekebishika. Kwanza kukaa naye muda wote huo bila ya kujua kwao ni wapi, wazazi wake ni akina nani, kutomuuliza huyo mama aliyewaletea habari zote zinazomhusu.
Kosa la pili ni pale aliposema anarudi nyumbani mkamwacha aondoke bila ya kujua anaelekea wapi. Laiti mmoja wenu angamsafirisha hadi kwao!
Kilichobaki ni kukubali jukumu lenu. Ikiwa hamjui kwo wapi, mzikeni hapo hapo mlipo, lakini ni lazima mbebe jukumu hili.
Poleni sana kwa msiba.
RIP HG.

Umenena vema Mammamia....

Inabidi tu kukubali jukumu hilo. Poleni sana kwa msiba huo.
 
good kwa hatua mliyofikia. Huo ndo ubinadamu! Kila la kheri na poleni kwa msiba.

R . I. P kijana!
 
Ni kweli tulifanya kosa,lakini cha muhimu sasa ni kuangalia nini cha kufanya.tunajaribu kufatilia kwa rafiki zake tumegundua kwao ipogolo.tunajaribu kutafuta ndugu zake

good move,.........kila la heri na Mungu awape moyo wa ujasiri
 
Poleni sana..

Sasa..yaliyopita yamepita. Kama funzo umeshapata..kwa sasa kikubwa ni mazishi. Kumbuka kama wewe usipomsaidia marehemu kumhifadhi vizuri..basi Serikali itamzika na unajua mazishi ya serikali ..yaani wanatupa mzoga.

Marehemu ulikaa naye miezi 13..ni mingi na alikuwa na uwezo wa kukudhuru kwa masaa 24 ya mwanzo hakufanya hivyo. Nakushauri jitahidi umsaidie kumuhifadhi. Si lazima kufuata Ceremony nzima ambayo itakugharimu ..Jitahidi kama msamaria mwema na muhifadhi kwa uwezo wako.. kabla serikali haijatupa mzoga.. Kumbuka Mungu ana njia nyingi za kukupima wema wako... Usiangalie yaliyopita..angalia mbele..
 
miez 13 mnakaa na mtu hampajui kwao? Ingetokea amefia mikonon mwako ungefanya nini? Jibu swali la preta then ndo tutajua cha kukushauri.
Hayo ni matatizo tuliyonayo wengi,tunapenda kusimplelise mambo sana,huu ni wakati wa kujifunza,lakini ni bora kumshauri cha kufanya sasa!
 
Mimi nawashukuru kwa kuwa na moyo wa imani kwa kuliona hilo suala la msiba linawahusu. Nawashauri mchukue jukumu la mazishi mumzike ata hapahapa Dar, hii itawasaidia zaidi hapo baadaye ambapo ndugu zake watamtafuta. Najua kuwa serikali huwa inawazika watu wasio na ndugu kwa gharama za Serikali lakini huwa hawaziki ktk misingi ya Imani na utu wa mwanadamu hivyo mkichukua jukumu la kumzika inatosha sana na gharama zitakuwa ndogo sana.

Fundisho tunalolipata hapa ni tuwe makini na wasaidizi wetu wa kazi, inapaswa tuwe tunafahamu makwao na nivizuri kutembelea makwao pale tunapowahitaji na kuwarudisha makwao pale tusipowahitaji.
Hili limeshatoke hivyo hakuna aja ya kulaumiana bali ni kumstiri ndugu yetu kisha ndugu zake watatafutwa baadaye. Poleni sana wafiwa.
 
Ndg yangu pole kwa huo msiba, ila ulifanya kosa kubwa kukaa na kijana kwa miezi 13 bila kujua ndg zake. Sasa ulimtoa wapi? hana hata rafiki, hata mtu anayefahamiana naye wa kwao huko Iringa japo si ndugu kabisa? Ila sisi wengine tujifunze jamani, hii si tabia nzuri, unawezaje kukaa na kijana/msichana wa kazi bila kuwajua ndugu zake? so angekuibia ungeanzaje?
 
poleni na msiba na pia hili ni funzo kwa watu wengi ... tunapokuwa na wasaidizi wa kazi huwa hatujali wala kufuatilia wanakotoka au kuwa na mawasiliano na ndugu zake kwa vile hutuoni umuhimu ,... kwa hili hamna jinsi zaidi ya kuchukua au kumhifadhi au kuwatafuta ndugu ... lakini piia mnafahamu walau majina yake matatu ??? mnaweza kwenda iringa kutangaza kwenye radio za huko ..
 
Back
Top Bottom