Faili kutoka ofisi moja ya ardhi kwenda ofisi nyingine ya ardhi latumia miaka mitatu

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,902
52,003
Jana kwenye kipindi cha TBC saa tatu usiku kwenye kipindi cha siku 100 za MAGUFULI kinachorushwa mfululizo kila siku waziri Lukuvi alikutana na Kituko cha mwaka pale alipofanya ziara ya kustukiza masjala na alipokuta faili la hati ya mtu limekaa miaka mitatu kwenye ofisi ya Ardhi kwamba haliwezi toka ofisi moja kwenda ofisi ya Ardhi makao makuu liandikiwe hati kwa sababu shilingi elfu ishirini hazijaletwa na wizara ya ardhi kwenye hiyo ofisi ya Ardhi iliyokalia hilo faili la mteja ambaye kutwa kucha anapiga kiguu na njia kuuliza hati yake imefikia wapi kwa miaka mitatu.

Waziri alipowabana kuwa mlimwambia mwenyewe kuwa tatizo ni hiyo Elfu ishirini? Wakasema hapana.Waziri alionyesha kukerwa mno.

Yaani Ardhi kuna baadhi ya watendaji wa ajabu sio wabunifu wa kutatua kero za wananchi kama kero ndogo kama hiyo.Looo! Faili lilionekana limechoka limejaa vumbi hadi basi.Ni kama waliliweka kwenye kaburi la masjala.

Kuna mwingine ambaye faili lake la kero limekaa muda mrefu hebu atupe uzoefu wake na elezea ni wapi huko sio lazima iwe ardhi tu.
 
Jana kwenye kipindi cha TBC saa tatu usiku kwenye kipindi cha siku 100 za MAGUFULI kinachorushwa mfululizo kila siku waziri Lukuvi alikutana na Kituko cha mwaka pale alipofanya ziara ya kustukiza masjala na alipokuta faili la hati ya mtu limekaa miaka mitatu kwenye ofisi ya Ardhi kwamba haliwezi toka ofisi moja kwenda ofisi ya Ardhi makao makuu liandikiwe hati kwa sababu shilingi elfu ishirini hazijaletwa na wizara ya ardhi kwenye hiyo ofisi ya Ardhi iliyokalia hilo faili la mteja ambaye kutwa kucha anapiga kiguu na njia kuuliza hati yake imefikia wapi kwa miaka mitatu.

Waziri alipowabana kuwa mlimwambia mwenyewe kuwa tatizo ni hiyo Elfu ishirini? Wakasema hapana.Waziri alionyesha kukerwa mno.

Yaani Ardhi kuna baadhi ya watendaji wa ajabu sio wabunifu wa kutatua kero za wananchi kama kero ndogo kama hiyo.Looo! Faili lilionekana limechoka limejaa vumbi hadi basi.Ni kama waliliweka kwenye kaburi la masjala.

Kuna mwingine ambaye faili lake la kero limekaa muda mrefu hebu atupe uzoefu wake na elezea ni wapi huko sio lazima iwe ardhi tu.
Yaani hiyo miaka mitatu ni michache, mimi nafuatilia hati yangu ya kiwanja kilichoko kibamba mwaka wa tano sasa, hakuna kinachoeleweka, Huu mradi wa kibamba ni jipu kubwa sana, Tunamuomba Mheshimiwa Lukuvi atusaidie, wala sio mimi tuu wapo wengi wa kibamba na maeneo mengine ya Dar es salaam wana matatizo kama hayo.
 
Katika watu ambao moto wa milele utawachoma vibaya sana ni watu wa wizara ya ardhi, namaanisha wale wa wizarani na sio kwingineko. Kuna wazee wamesumbukia hati kwa zaidi ya miaka 20. Kuna wazee wamebomolewa nyumba zao kwa makusudi tu kwa sababu ya networks za kishenzi ambazo source yake ni pale wizarani. Miaka ya nyuma kulikuwa na utapeli ambao unahusisha watu wa wizara.

Ukitaka kujua umuhimu wa watanzania kubadilika kiutendaji nenda pale wizara ya ardhi. Angalau baada ya awamu ya tano kuanza wale wafanyakazi wanaonekana kuwachangamkia wateja wao. Ukizingatia kuwa kwa sasa TAKUKURU wamekuja kivingine, angalau kuna some changes lakini ile wizara imechangia sana katika kuwaumiza watu wengi. Na sio wale ambao ni watu wa maisha ya hali ya chini, anadhulumiwa kiwanja mtu aliyefanya kazi serikali kwa miaka zaidi ya 30, anayeishi mbezi beach au mikocheni.

Let's hope awamu ya tano itakuja na mabadiliko mengi makubwa.
 
Mimi nilipeleka kupata hati,sasa mwaka wa saba hapo hapo kwa wizara ya Lukuvi mpaka leo,ila ya kiwanja wanachukua.Mimi kiwanja kilikuwa na offer sasa niliomba hati.Jamani hii ni Tanzania yetu
 
ile wizara ukitaka mambo yako yaende fasta utoe rushwa na hiyo rushwa utoe huku ukisukuma watu na vitip tip tena ...
 
Ukiyapeleka mambo ki-shekh/ki-uchungaji si wizara ya ardhi pekee yake ila karibia kila taasisi za nchi hii kupata huduma kusudiwa kwa haraka sahau si miaka 3-7 hata miaka 10 watakuwa wamekuonea huruma sana,ila ukitoa hela ya maziwa ( eti kwenye kutafuta faili watakutana na vumbi ) fasta tu hata dakika 3 ni nyingi.
 
Tatizo la ardhi hasa hizo masjala ni la rasilimali watu zaidi. Watu wameajiriwa kindugu hawana taaluma yo yote ya ardhi. Badala yake maofisa wanalaumiwa.
 
Tatizo la ardhi hasa hizo masjala ni la rasilimali watu zaidi. Watu wameajiriwa kindugu hawana taaluma yo yote ya ardhi. Badala yake maofisa wanalaumiwa.

Ofisa anayehudumia hilo faili mimi naona ndie ana matatizo hilo faili kama lilikuwa mezani kwake akaliona lina kitu kimepungua mfano hiyo elfu 20.Ilibidi atafute ufumbuzi au amwambie mwenye faili lipia elfu 20 tutakatana kwenye kodi ya ardhi itakayofuata utakayotakiwa kulipa au akae nalo mezani kwake mwenyewe .Utarudishaje faili masjala wakati hujamaliza kazi yake?

Hizo lawama za kukaa masjala miaka mitatu wa kulaumiwa ni ofisa aliyepewa kushugulikia hilo faili.Mtu wa masjala kazi yake kutunza mafaili anayejua nini kimebaki kwenye hilo faili ni ofisa mhusika.Hivi akilipeleka masjala anakumbukaje kuwa kuna faili halijashughulikiwa mwaka mzima? Likishaenda masjala ni kuwa limeenda mapumziko ya milele.

Wizara iwainue maofisa wote wa Ardhi nchi nzima waende masjala zao waaangalie kila faili lile ambalo hawajashughulikia washughulikie.Wakuu wa vitengo wote wainuke wasimamie hilo zoezi wote wahamie masjala.
 
Wakati nikiwa muajiriwa wa kampuni ya uchimbaji madini ya resolute kule nzega mkoani tabora, uongozi wa kampuni uliamua kuwasimamia wafanyakazi wote kupata viwanja vilivyopimwa pale wilayani. nasema iliwasimamia kwani garama zote tulilipa kutoka katika mishahara yetu. cha kushangaza hadi leo ni asilimia kama 30 tu ya wafanyakazi ndo waliokwisha pewa hizo hati. navyaandika sasa hivi ni takribani miaka nane tangu zoezi hilo lianze na hata ile kampuni ilishawindup shughuli zake na kujiondokea. sasa sisi ambao hatukubahatika kupata zile hati tumesha hangaishwa mpaka tumekata tamaa na tumeamua kukaa kimya tu. lakini kwa spidi hii ya awamu hii naamini ni suala la kuweka wazi tu kwa lukuvi ili ajuue namna ya kutumbua maana tumechoka sasa.
 
Tatizo la ardhi hasa hizo masjala ni la rasilimali watu zaidi. Watu wameajiriwa kindugu hawana taaluma yo yote ya ardhi. Badala yake maofisa wanalaumiwa.
Vijana wengi tu pale ardhi ukiwa mbele yao unaona kabisa jinsi wanavyofanya kazi kwa kubabaisha, kila hatua ya kazi utawaona wanawasikiliza wale masenior waliowakuta kazini, yaani kujifunza kazi kwao hakujifichi.
 
Halafu haya majitu yakitimuliwa wanalalamika Magufuli dikteta! Hivi kweli kumtesa mwenzio miaka yote hiyo siyo udikteta? Tujadili
 
Wakati nikiwa muajiriwa wa kampuni ya uchimbaji madini ya resolute kule nzega mkoani tabora, uongozi wa kampuni uliamua kuwasimamia wafanyakazi wote kupata viwanja vilivyopimwa pale wilayani. nasema iliwasimamia kwani garama zote tulilipa kutoka katika mishahara yetu. cha kushangaza hadi leo ni asilimia kama 30 tu ya wafanyakazi ndo waliokwisha pewa hizo hati. navyaandika sasa hivi ni takribani miaka nane tangu zoezi hilo lianze na hata ile kampuni ilishawindup shughuli zake na kujiondokea. sasa sisi ambao hatukubahatika kupata zile hati tumesha hangaishwa mpaka tumekata tamaa na tumeamua kukaa kimya tu. lakini kwa spidi hii ya awamu hii naamini ni suala la kuweka wazi tu kwa lukuvi ili ajuue namna ya kutumbua maana tumechoka sasa.
ulikuwa kitengo gani?
 
Back
Top Bottom