Faida Za Kuwa Mama Wa Nyumbani

Faida Za Kuwa Mama Wa Nyumbani

Hahahaaaaaaa.what if umekufa gafla na mke wako alishazoea kukaa nyumbani na kukuta hela bank.Hivi vitu ni rahisi sana kusema lakini kuviweka kwenye vitendo ni ishu.sasa umemkuta mwenzio wazazi wake wamemsomesha gafla unamwambia kaa home uangalie watoto na hela nitakazo kuwekea usiwasaidie ndugu yako.Haingii akilini
Unaweza kumfungulia biashara itakayowaingizia kipato kakini pia itampa muda wa kukaa na familia
 
"i believe siyo kila m/ke au m/me anafaa kuwa mke/mme ila kuna walioumbwa kuwa waume/wake za watu"
 
Mada nzuri kwa sisi wamama wa nyumbani mana nami ni mmoja wapo, watoto ukikaa nao nyumbani raha sana kwa jinc wanavyokuzoea, hata wakirudi kutoka shule, wa kwanza kuuliziwa ni mama, baba mida yake ni usiku, ikifika mida ya kwenda kulala, kama baba yao hajarudi ndio wanaanza kumuulizia, kama nikitoka kidogo, halafu niwaache nyumbani, nitaharakisha kilichonitoa ili niwawahi watoto, ndio maana wanangu wananipenda sana, kama ulivyosema mtoa mada, kuwaogesha, kuwapikia, kuwafulia, kuwasaidia wafanye h/w, na hata kucheza nao, wanafurahi sana vitu hivi niwafanyie mimi, kuliko dada wa kazi.
 
My wife stays at home and I do provide the necessities plus everything
My babies mama should be at home taking care of my family while me the baba is working for them

Wewe ni kati ya wachache wanaofanya hivyo kama ni kweli.

Mijanadume ya siku hizi haipendi majukumu.
 
Kwa kuanzia mwanamke hapaswi kudharauliwa...awe mama wa nyumbani au mfanyakazi...wote wana mchango mkubwa kwenye familia...

Ila naomba kutofautiana...hakuna ushaidi kuwa watoto waliolelewa na mama wa nyumbani wana tabia nzuri au mafanikio kuliko walio lelewa na mama wenye kazi...

Hata tuliokulia mjini mnaweza kunisaidia kwani those days kulikuwa na mchanganyiko...wengine mama zao walikuwa wafanya kazi na wengine mama zao walikuwa mama wa nyumbani...

Nimekuwa critical pia kwa sababu nimemkumbuka mwalimu wangu Japan...alikuwa anawabonda new generation kule kuwa ni wahuni tu...na aliongeza kusema ni tatizo la kulelewa na mama...kwa kuwa wanaume wa Japan ni workaholic; na mtoto analelewa kwa asilimia kubwa na mama peke yake... (mwanamke akiolewa kimila za huko anatakiwa aache kazi alee watoto)

Jaribu kuchunguza hata wewe hivi hawa watoto wa ma house wife wako na tabia nzuri kweli kuliko wa wafanya kazi?

Unasema kusaidia home work kivipi? Maana mama wa nyumbani most likely shule ndogo...atajua magazijuto...na hizi academy mtoto anakuja na home work majibu mpaka mzazi u Google
 
Ujumbe mzuri ila kwa mimi nionavyo Maisha yamebadilika sana..........

The cost of living is high kuna umuhim wa kufanya kazi ili tuweze kusaidiana wote wawili........

umuhimu wa kufanya kazi upo lakini mwanamke asielemewe na kufanya kazi akasahau jukumu lake la msingi alilopewa na Mungu la kutunza familia yake
 
Safi sana queeny wanawake tumejisahau sana kuhusu malezi ya familia yetu badala yake tumewaachia wadada wa kazi majukumu yote.... Uangalizi wa nyumba, watoto na mume ni letu tujaribu kubalance muda wetu angalau tuweze kutimiza hata kidogo wajibu wetu na si kujisahau kabisa.

HUSBAND LOVE YOUR WIFE, WIFE SERVE YOUR HUSBAND!!!!!!

haswa... hilo ndilo nalosema mimi KUBALANCE MUDA. tunaelemewa sana na kazi za ofisini tunakosa muda wa kuhudumia famiia zetu kitu ambacho si sahihi. Unakuta mama wa nyumbani anakuwa na familia bora kuliko mama wa ofisini.
 
katika mada zote nilizowahi kuzisoma humu, hakika hii imenigusa sana.
Tangu nilipokuwa natafuta mchumba moja ya kigezo kilikuwa ni akubali kuwa mama wa nyumbani, kwamba aiweke familia yetu mbele kuliko pesa. Akubali kutumia elimu yake kwa ajili ya familia na sio kutafuta pesa, kwani kutafuta ni jukumu langu.

Ilinichukua mda ila Namshukuru Mwenyezi Mungu hatimae nilimpata.
Hakika kwa sasa naenjoy maisha kupindukia.

hongera sana... inahitaji mwanamke mwenye busara sana kukubali huo utaratibu. binafsi nauona ni sawa kabisa ili mradi uwe na upendo wa dhati kwa mkeo na umsupport na sio kumsimanga. ukiweza hilo Mungu atakubariki na utafanikiwa. unaweza kumfungulia biashara ambayo haitamfanya kuwa bize sana akashindwa kuhudumia familia. watu hawajui tu lakini kipindi cha ujauzito ni wakati ambao mama anapaswa kupumzika zaidi sana kufanya mazoezi ya kutembea tembea na sio kila siku pilikapilika za makazini. hata akijifungua anahitaji muda wa kutosha kulea mtoto pasipo presha ya aina yoyote. awe na muda wa kutosha kumnyonyesha mtoto na kubond na mwanae. sio miezi mitatu tu mama ashaanza kukimbia kimbia na kazi. inakera sana.
 
Topic nzuri sana.
Mimi naunga mkono hoja. Lkn queeny wanaume wa sikuizi nao wanatuzeveza, unaweza ukasema unakaa nyumbani, mwanaume akaja kukubadikia, keshakuzalisha wtt, mara anakutelekeza na wtt, wewe ndo uanze kuhangaika na wtt. Unaanza alifu kwa ujiti.
Mi kusema kweli natamani sana to be a housewife but to be honest m scared

na hilo ndo tatizo kubwa, wanaume wamesahau majukumu yao wanaishia kuwanyanyasa wake zao ndo maana wamama inawabidi wajikaze kisabuni kutafuta riziki kuepuka masimango. laiti wanaume wangejua wajibu wao waliopewa na Mungu kusingekuwa na shida. mwanaume unamtegeshea mkeo kuleta mahitaji ya nyumbani?? si sawa kabisa.. mbona mwanamke hamtegeshei mumewe kulea mimba kujifungua?? kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake.
 
Kwa kuanzia mwanamke hapaswi kudharauliwa...awe mama wa nyumbani au mfanyakazi...wote wana mchango mkubwa kwenye familia...

Ila naomba kutofautiana...hakuna ushaidi kuwa watoto waliolelewa na mama wa nyumbani wana tabia nzuri au mafanikio kuliko walio lelewa na mama wenye kazi...

Hata tuliokulia mjini mnaweza kunisaidia kwani those days kulikuwa na mchanganyiko...wengine mama zao walikuwa wafanya kazi na wengine mama zao walikuwa mama wa nyumbani...

Nimekuwa critical pia kwa sababu nimemkumbuka mwalimu wangu Japan...alikuwa anawabonda new generation kule kuwa ni wahuni tu...na aliongeza kusema ni tatizo la kulelewa na mama...kwa kuwa wanaume wa Japan ni workaholic; na mtoto analelewa kwa asilimia kubwa na mama peke yake... (mwanamke akiolewa kimila za huko anatakiwa aache kazi alee watoto)

Jaribu kuchunguza hata wewe hivi hawa watoto wa ma house wife wako na tabia nzuri kweli kuliko wa wafanya kazi?

Unasema kusaidia home work kivipi? Maana mama wa nyumbani most likely shule ndogo...atajua magazijuto...na hizi academy mtoto anakuja na home work majibu mpaka mzazi u Google

kwanza kabisa sijasema wamama wasifanye kazi nilichosema ni kuwa, kazi ya kuondoka asubuhi mapema kurudi usiku ndiyo yenye madhara kwani muda mwingi mama anakuwa mbali na watoto na hiyo ina effect kwa watoto psychologically kwakuwa muda mwingi hawawaoni wazazi wao, hasa mama.

pia kuwa mama wa nyumbani sio kwamba unakuwa mbumbumbu au hujaenda shule. unaweza kuwa na degree ukawa mama wa nyumbani for sometime au ukafanya kazi ambayo unakuwa hauko busy sana au ukafanya ujasiriamali. kuwa mama wa nyumbani sio kuwa ZERO BRAIN
 
Mada nzuri kwa sisi wamama wa nyumbani mana nami ni mmoja wapo, watoto ukikaa nao nyumbani raha sana kwa jinc wanavyokuzoea, hata wakirudi kutoka shule, wa kwanza kuuliziwa ni mama, baba mida yake ni usiku, ikifika mida ya kwenda kulala, kama baba yao hajarudi ndio wanaanza kumuulizia, kama nikitoka kidogo, halafu niwaache nyumbani, nitaharakisha kilichonitoa ili niwawahi watoto, ndio maana wanangu wananipenda sana, kama ulivyosema mtoa mada, kuwaogesha, kuwapikia, kuwafulia, kuwasaidia wafanye h/w, na hata kucheza nao, wanafurahi sana vitu hivi niwafanyie mimi, kuliko dada wa kazi.

utakuwa unaenjoy sana. hongera
 
Kila jambo na wakati wake. Kuna wakati wa kucheka na kulia, wakati wa kulima na kuvuna, kuna wakati wa njaa na shibe. Majira nayo hubadilika. Nadhani jambo la msingi ni kufanya maamuzi kwa kuzingatia ''stuaation and condition'.
 
Kila jambo na wakati wake. Kuna wakati wa kucheka na kulia, wakati wa kulima na kuvuna, kuna wakati wa njaa na shibe. Majira nayo hubadilika. Nadhani jambo la msingi ni kufanya maamuzi kwa kuzingatia ''stuaation and condition'.

nikweli ila nachoamini ni kuwa, kwenye maisha kuna misingi ambayo haibadiliki hatakama mazingira au nyakati zitabadilika kwa kiasi gani. Mf kubeba mimba na kuzaa ni sifa ya mwanamke daima japo kunawanawake wasiozaa kama ujasiri ni sifa ya mwanaume japo kuna wanaume waoga.
Tunapo badili misingi ya asili kama hii kwa visingizio vya uongo kama mazingira nk ndo unakuta tunakuwa na ndoa za jinsia moja kisa kila mmoja anataka kufanya jukumu la mwenzake, vituo vya kulea watoto wadogo wakati wazaziwao wanapokuwa makazini, hapa napo mama kakimbia jukumu lake la msingi kakimbilia la baba.

Kuna mambo hayapaswi kubadilishwa ktk maisha, lasivyo tutajitengenezea madhara makubwa.
 
Nimeipenda mada hii asante sana mtoa mada. Tukumbuke kuwa kila kitu kinapendeza kikiwa moderate kwa mfano mama kama wewe ni mwajiriwa au umejiajiri basi hakikisha unatenga muda wa kuihudumia familia yako. Inapendeza mama anapokua nyumbani kwani inamsaidia kuwajua watoto wake kwa karibu na hata kuijua tabia ya kificho ya mtoto. Kuhusu tabia ya mtoto sio guarantee kwamba atakua mwema ingawa inasaidia kupunguza tabia zisizofaa au mazoea mabaya. Upo umuhimu wa kuliangalia jambo hili kwa jicho la 3. Wamama wengine wanavunjwa moyo na wenzi wao kwa sababu ya kukosa uaminifu na hata kuwapa manyanyaso baadhi ya wamama. Huko nyuma mambo yalikua shwari sababu gharama za maisha hazikua kama leo ona mfn shule kipindi kile ilikua za serikari tu hasa za msingi na hata secondary nazo karibu 95% zilikua za serikari na gharama zilikua nafuu. Leo hii maisha yako juu lkn bado mama anatakiwa apunguziwe majukumu hasa ya utafutaji.
 
haswa... hilo ndilo nalosema mimi KUBALANCE MUDA. tunaelemewa sana na kazi za ofisini tunakosa muda wa kuhudumia famiia zetu kitu ambacho si sahihi. Unakuta mama wa nyumbani anakuwa na familia bora kuliko mama wa ofisini.

Exactly! Tunatakiwa tujitahidi asubuhi tukiamka tufanyebaadhi ya majukumu yetu ili kuonyesha uwepo wa mama katika familia, andaa breakfast wewe, safisha nyumba wewe, muandalie mumeo maji ya kuoga na kumpasia nguo wewe, kama unamtoto anasoma muandalie mazingira ya kwenda shule wewe......
Jioni ukirudi sio unakimbilia kwa bed eti kisa umechoka Noo...... Julia hali kwanza familia yako kuanzia wale ulio waacha nyumbani na walioenda shule pia unaangalia maendeleo yao...

Pia unaangalia nini ambacho kimepelea ndani, maana kuna wakati mwingine tunajisahau mchele au mafuta yanaisha ndani hatujui mpaka mdada wa kazi aseme... HAPANA sisi ndio wapangaji wa bajeti nyumbani, lazima ujue kipi kimeisha na kipi cha kuongeza.

Kuna usemi unasema KAZI ZA MWANAMKE HAZIISHI na kuwa mama yahitaji moyo wapendwa la sivyo migogoro ya familia haitaisha....!

Ni raha ilioje kuona watoto wako wakikuwa katika maaadili ya kupendeza na kumcha Mungu huku furaha na upendo ukiwa umetawala kati yako na mume wako KWAAJILI YA UWEPO WAKO KWAO..!

Tutataka haki sawa lakini baba atabaki kuwa baba na mama atabaki kuwa mama..

Ila wanaume na nyinyi msijibweteke maana kulea familia ni jukumu letu sote!!
 
Habari wanajamii wote popote mlipo hapa duniani. natanguliza heshima za dhati kwenu nyote na itifaki imezingatiwa.

Napenda niwashirikishe wanajamii wenzangu kuhusu faida za kuwa mama wa nyumbani na naomba niseme kuwa kwa miaka ya hivi karibuni, jamii imekuwa ikimdharau sana mama wa nyumbani na kumuona mvivu na hana mchango wowote kwenye maendeleo ya familia yake eti kisa haingizi CASH. jamii imeenda mbali hata kudiriki kumtungia maneno ya kashfa na kejeli kwamba ni golikipa yani ni kama kandege kanakosubiria kufumbua mdomo na kupokea chakula kutoka kwa mama yake pasipokuwa na mchango wowote katika kutafuta chakula hicho.

Tukumbuke kwamba wamama zetu walio wengi waliweza kutulea na kutuwezesha kuwa na maadili mema kwa kuwa walikuwa karibu yetu masaa 24. kuanzia tulipozaliwa wamama zetu walio wengi;

1. wametunyonyesha si chini ya miaka 2

2. wametuogesha utoto wetu wote (mama anapokuogesha anahakikisha umetakata na anakukagua mwili mzima kama siku hiyo umeumia au una kidonda basi mama atajua mara moja na kukuhudumia ipasavyo)

3. kukupikia uji/chai na kuhakikisha amekunywesha kila siku. kama unaumwa atajua. ni furaha kubwa sana kwa mtoto kulishwa na mama yake.

4. kukuandaa kwenda shule huku akikusisitiza usome kwa bidii

5. kufuatilia kwa ukaribu masomo yako na kuhakikisha unaishi kwa adabu pale nyumbani maana yupo muda wote kufatilia mwenendo wako (bakora za kutosha).

Wakati huo baba yeye yuko bize kibaruani kuhakikisha analeta mahitaji yote ya familia yake na cha kushangaza maisha yalikuwa mazuri na matamu sana. kulikuwa hakuna dharau. Mama alikuwa anamuheshimu baba maana anajua mchango wake katika familia. Baba naye alikuwa anamuheshimu mkewe maana alikuwa anajua mchango wake katika familia. hivyo kila mtu alikuwa na wajibu wake na familia nyingi (sio zote) silizoishi kwa mfumo huu zimekuwa familia bora.

Je, kulikoni nyakati hizi???

- pesa imekuwa ndo kila kitu. kumekuwa na vita ya pesa kiasi kwamba si baba wala mama anayependa kupitwa na hii kitu

- pesa imekuwa ndio msingi wa familia... hapendwi mtu bali pesa. leo hii mwanamke ukijitolea kuwa mama wa nyumbani ili uwalee watoto wako ipasavyo, uwepo muda wote watoto watakapokuhitaji, unaonekana wa ajabu, jamii na hata mume wako hatokuelewa. lakini ukiondoka nyumbani saa 12 asubuhi na kurudi saa 4 usiku ukitokea kazini (kutafuta pesa), hapo unaonekana mjanja na mpambanaji wa kweli huku nyuma watoto wako wanaharibikiwa.

Hivi kweli hii ni sawa???

Mimi naamini kuwa tumeingia kichwa kichwa katika hii dhana ya usawa na tunakoelekea itatugharimu. Kwa nini?

1. Wanawake siku hizi hawana muda wa kunyonyesha watoto wao kisa wanawahi kazini. kumbuka maziwa ya mama ndio pekee yenye uwezo wa kujenga immunity ya mtoto kwa maisha yake yote. inashauriwa mtoto anyonyeshwe walau miaka miwili (jambo ambalo mama zetu walilijua na kulifanyia kazi japo hawakuwa wamesoma sana). huyu mtoto aliyenyonyeshwa kwa miezi miwili tu atakuwa salama kweli?

2. Dhana hii imewafanya wanaume kuwa wavivu na kukimbia majukumu yao. wanaogopa kubeba mzigo wa familia zao hivyo kutafuta wanawake wenye vipato tayari ili kukwepa majukumu. wake zao wasipokuwa na kazi huwanyanyasa na kuwaona tegemezi (golikipa).

3. Watoto wetu siku hizi wanaharibikiwa kwani wazazi wote wako bize kutafuta pesa, hakuna mwenye muda na mtoto. hakuna anayejua ameamka vipi, kama amekunywa chai ama la, ameenda shule ama la, huko shule maendeleo yake yapoje, labda kapigwa na mtu shule, au dada au kaka wa kazi kamfanyia kitu kibaya, hakuna anayejali.

4. Madhara makubwa ya hii dhana ni kwa wanawake kwani wanajikuta wamejiover-load na shughuli nyingi sana. mfano utakuta mtu ni mjamzito (tumbo kule) hapohapo anahaingaika na kazi kila siku ya Mungu mpaka anajifungua, bosi haelewi una kichefuchefu wala kizunguzungu anachotaka kazi iende.
ukijifungua unanyonyesha miezi 3 tu unakimbia kazini, katoto unakaachia hausigeli ambaye humwamini, unafanya kazi huku presha iko juu. mume naye haelewi. mtoto anakosa bonding na mama yake kitu ambacho ni muhimu sana kwa ustawi wa mwanadamu.

5. Na mengine mengi.....


Sisemi mwanamke asijishugulishe, nachosema mwanamke asiwe bize sana na kusaka pesa, awe na muda wa kulea familia yake (mume na watoto). hata kama ni ujasiriamali usiwe full time ili apate muda wa kulea watoto wake ipasavyo.

Tukubali tukatae, kazi ya kulea watoto na kuhakikiha wanakuwa na maadili mazuri ni ya mama kwa asilimia 90.

HITIMISHO;

-HESHIMA ZANGU ZA DHATI NA ZA KUTOKA MOYONI MWANGU ZIWAENDEE WANAUME WOTE WANAOTAMBUA KUWA JUKUMU LA KULETA MAHITAJI YA NYUMBANI NI LA KWAO NA WANAFANYA HIVYO KWA MOYO WAO WOTE

-WAHESHIMIWE PIA WANAUME WALIO NA WAKE AMBAO NI MAMA WA NYUMBANI NA WANATAMBUA MCHANGO WAO KATIKA FAMILIA NA WALA HAWAWADHARIRISHI WAKE ZAO KWA KUWAITA MAGOLIKIPA AU KUWANYIMA MAHITAJI

-WAHESHIMIWE WANAWAKE WOTE WANAOFANYA DOUBLE JOBS YAANI KUZAA KWA UCHUNGU NA KULA KWA JASHO (wakati wanaume wao wanafanya moja tu ya kula kwa jasho hiyo nyingine hawaielewi). MUNGU AWAFANYIE WEPESI WAMAMA HAO.

Kwa mtazamo wangu USAWA (Beijing) umeletwa kuwakandamiza wanawake na kuharibu familia na si kuwatetea na kuwainua wanawake.

AMANI KWENU WOTE.

Queen shkamoo!!

Uneongea point sana, watoto wakiwa mazuzu hata tuwapeleke st anthony sjui wapi ni kwa sababu ya malezi.
 
Back
Top Bottom