Faida za kusoma vitabu

saidi bunduki

Member
Mar 10, 2018
24
23
Kutoka mtandao wa

www.mrbunduki.com

Kama kuna orodha ya vitu vinavyochukiwa zaidi na Watanzania basi ni kusoma vitabu. Sijui ni kwasababu gani hasa.
  • Kuenea kwa teknolojia?
  • Kazi nyingi?
  • Uvivu?
  • Hakuna watunzi wazuri?
  • Hatujui umuhimu wake?
Mi nahisi itakuwa ni mazoea tu ama uvivu kama ni teknolojia huko kwa wazungu ndo imeenea zaidi, lakini mbona wao suala la kusoma wameliweka mbele zaidi? Laniki pia tumejaaliwa watunzi wazuri sana wa vitabu mbali mbali katika nchi yetu na pia teknolojia hiyo hiyo imeturahisishia kuweza kusoma vitabu katika simu na kompyuta zetu popote tulipo;-
  • Okeeey tuyaache hayo, najua si wote ambao ni wavivu katika hili. Lakini kama nawe ni miongoni mwa hao, leo nakuletea faida 7 tu za kusoma vitabu.
  • huenda baada ya hapo utapata kitu ambacho kinaweza kukusaidia katika maisha yako ya kila siku.
Nami nitajitahidi kuandika kwa ufanisi na kwa ufupi zaidi ili nisikuchoshe

***************************************
Kusisimua akili na kuupa ubongo mazoezi
Ingawa watu wengi hawapendi kusoma lakini ifahamike kuwa kusoma ni jambo ambalo huimarisha sana ubongo katika kufikiri, kuzingatia na kuelewa. Unajisikiaje unaposoma kitu hasa kinachokuvutia kama mfano wa makala hii nzuri?😜😜😜
Unaposoma mara nyingi akili yako inakuwa katika kile ambacho unakisoma. Basi hivi huufanya ubongo wako kuwa makini zaidi kuliko yule ambaye haushughulishi. Kwakuwa wanafunzi wanahitajika kuhimizwa zaidi katika kusoma ili kukuza bongo zao, nawe mtu mzima mwenzangu ni vema ukaanza kidogo kidogo kuuzoesha ubongo wako.

Utajiri wa lugha na misamiati

Haijalishi unachokisoma kipo katika lugha gani. Kama ni lugha ya Kiswahili basi utapata maneno mapya ambayo huenda hukuwa unayajua na kama ni lugha yoyote ya kigeni ndio utapata maneno mengi zaidi. Na muda wa kuwa unachokisoma ni chenye kuvutia hivyo ni rahisi zaidi kutafuta kamusi na kujua mengi zaidi.

Kupunguza msongo wa mawazo

Kama tulivyosema hapo awali, unaposoma huwa akili yako inaelekea katika kile unacho kisoma zaidi hivyo hupunguza mawazo na kujisikia huru katika akili yako. Na baadaye unaweza kupata suluhisho la kile ambacho kilikuwa kinakusumbua.
Kuimarisha uwezo wa uandishi
Si lazima uwe muandishi wa vitabu ndio msomi wa vitabu, imarisha uwezo wako wa kuandika, kuzungumza, kufikirti kwa kusoma vitabu kwani pia ni sehemu ya kuongeza busara.

Kusaidia kulala

Kusoma hakukusaidii kulala ila kunasaidia kulala kuliko bora zaidi na kuufanya usingi wako kuwa wa amani. Pia kama unaona katika muda huo unataka kulala lakini huna usingizi basi chukua kitabu chenye hadithi nzuuuri na usome utaona matokeo yake. Hivyo kusoma husaidia pia kuvuta usingizi mnono na ndoto nzuuri kabisa.

Kuitia muangaza siku yako

Hivi umeshawahi kuwaza kuwa vitabu vinaweza kuleta furaha katika siku yako nzima? Hii hutokea pale ambapo umesoma stori nzuuri ambayo aidha imekuvutia ama imekufundisha kitu na hususan kikawa na manufaa kwako.

Kuongeza ubunifu

Kuna tofauti katika kusoma na kuangalia movie. Katika kusoma huwa unatumia akili niyngi zaidi kuliko pale ambapo unatazama. Ukitazama ni rahisi zaidi fikra zako kuhama na kufikiri jambo jingine tofauti na pale unapo soma akili yote hufikiri kile unachokisoma na kukielewa vizuri na bila shaka unaweza kupata mbinu mpya katika mambo yako. Hii ndio maana tukasema tunaongeza ubunifu.

TUSOME NINI?

Kila mtu ana vitu ambavyo vinamvutia kuvijua, lakini Kuna vitu ambavyo ni muhimu kwa wote. Kwa mfano vitabu vya dini na mafundisho yake n.k. Hapa viongozi wa dini wamefaulu kwa kiasi kikubwa Sana.

Lakini pia vipo vitabu muhimu vya mafunzo mbali mbali vyenye manufaa kwako Kama vitabu vya afya, hadithi za kale, sayansi n.k.

HIVYO BASI
 
Mkuu hapo kwenye vitabu wadau watapita kimya kimya. Unless ungeongelea vitabu vya kupata papuchi au Jinsi ya kuwa Marioo, Pamoja na Ngono, Bila kusahau kula tunda KIMASIKHARA.
 
Mbona na hiki ni Kitabu Sasa!! Mie nimesoma vichwa vya habari tu km wenzangu...
 
Nmeshindwa tu kusoma hii thread kitabu nitawezea wapi mkuu

Sent using Gun Trigger
 
Ni kweli aisee m huwa nadownload siyo msom wa siku nyingi kweny hv vitabu visivyo vya shule ila ndo nmeshaanza na matokeo ni mengi aisee utajiboreshea maisha kuna vtu vyng vya kukufundisha,hasa self improvement
 
Tuwe wakweli mkuu
Ili usome kitabu mkuu inabidi uwe umeshiba,akili inautulivu, moyo una amani,
hapo utakuwa msomaji wa vitabu muzuri tu.

Tazama maisha ya watanzania wengi
chakula duni
maisha magumu-(pesa za kununulia vitabu)
@Malezi ( utamaduni) wa kusoma hatuna
N.k

Kitabu soma umeshiba utakielewa la sivyo ...😂😂
 
App yenu inagoma kudownload hyo bongoclass
Kutoka mtandao wa

www.mrbunduki.com

Kama kuna orodha ya vitu vinavyochukiwa zaidi na Watanzania basi ni kusoma vitabu. Sijui ni kwasababu gani hasa.
  • Kuenea kwa teknolojia?
  • Kazi nyingi?
  • Uvivu?
  • Hakuna watunzi wazuri?
  • Hatujui umuhimu wake?
Mi nahisi itakuwa ni mazoea tu ama uvivu kama ni teknolojia huko kwa wazungu ndo imeenea zaidi, lakini mbona wao suala la kusoma wameliweka mbele zaidi? Laniki pia tumejaaliwa watunzi wazuri sana wa vitabu mbali mbali katika nchi yetu na pia teknolojia hiyo hiyo imeturahisishia kuweza kusoma vitabu katika simu na kompyuta zetu popote tulipo;-
  • Okeeey tuyaache hayo, najua si wote ambao ni wavivu katika hili. Lakini kama nawe ni miongoni mwa hao, leo nakuletea faida 7 tu za kusoma vitabu.
  • huenda baada ya hapo utapata kitu ambacho kinaweza kukusaidia katika maisha yako ya kila siku.
Nami nitajitahidi kuandika kwa ufanisi na kwa ufupi zaidi ili nisikuchoshe

***************************************
Kusisimua akili na kuupa ubongo mazoezi
Ingawa watu wengi hawapendi kusoma lakini ifahamike kuwa kusoma ni jambo ambalo huimarisha sana ubongo katika kufikiri, kuzingatia na kuelewa. Unajisikiaje unaposoma kitu hasa kinachokuvutia kama mfano wa makala hii nzuri?
Unaposoma mara nyingi akili yako inakuwa katika kile ambacho unakisoma. Basi hivi huufanya ubongo wako kuwa makini zaidi kuliko yule ambaye haushughulishi. Kwakuwa wanafunzi wanahitajika kuhimizwa zaidi katika kusoma ili kukuza bongo zao, nawe mtu mzima mwenzangu ni vema ukaanza kidogo kidogo kuuzoesha ubongo wako.

Utajiri wa lugha na misamiati

Haijalishi unachokisoma kipo katika lugha gani. Kama ni lugha ya Kiswahili basi utapata maneno mapya ambayo huenda hukuwa unayajua na kama ni lugha yoyote ya kigeni ndio utapata maneno mengi zaidi. Na muda wa kuwa unachokisoma ni chenye kuvutia hivyo ni rahisi zaidi kutafuta kamusi na kujua mengi zaidi.

Kupunguza msongo wa mawazo

Kama tulivyosema hapo awali, unaposoma huwa akili yako inaelekea katika kile unacho kisoma zaidi hivyo hupunguza mawazo na kujisikia huru katika akili yako. Na baadaye unaweza kupata suluhisho la kile ambacho kilikuwa kinakusumbua.
Kuimarisha uwezo wa uandishi
Si lazima uwe muandishi wa vitabu ndio msomi wa vitabu, imarisha uwezo wako wa kuandika, kuzungumza, kufikirti kwa kusoma vitabu kwani pia ni sehemu ya kuongeza busara.

Kusaidia kulala

Kusoma hakukusaidii kulala ila kunasaidia kulala kuliko bora zaidi na kuufanya usingi wako kuwa wa amani. Pia kama unaona katika muda huo unataka kulala lakini huna usingizi basi chukua kitabu chenye hadithi nzuuuri na usome utaona matokeo yake. Hivyo kusoma husaidia pia kuvuta usingizi mnono na ndoto nzuuri kabisa.

Kuitia muangaza siku yako

Hivi umeshawahi kuwaza kuwa vitabu vinaweza kuleta furaha katika siku yako nzima? Hii hutokea pale ambapo umesoma stori nzuuri ambayo aidha imekuvutia ama imekufundisha kitu na hususan kikawa na manufaa kwako.

Kuongeza ubunifu

Kuna tofauti katika kusoma na kuangalia movie. Katika kusoma huwa unatumia akili niyngi zaidi kuliko pale ambapo unatazama. Ukitazama ni rahisi zaidi fikra zako kuhama na kufikiri jambo jingine tofauti na pale unapo soma akili yote hufikiri kile unachokisoma na kukielewa vizuri na bila shaka unaweza kupata mbinu mpya katika mambo yako. Hii ndio maana tukasema tunaongeza ubunifu.

TUSOME NINI?

Kila mtu ana vitu ambavyo vinamvutia kuvijua, lakini Kuna vitu ambavyo ni muhimu kwa wote. Kwa mfano vitabu vya dini na mafundisho yake n.k. Hapa viongozi wa dini wamefaulu kwa kiasi kikubwa Sana.

Lakini pia vipo vitabu muhimu vya mafunzo mbali mbali vyenye manufaa kwako Kama vitabu vya afya, hadithi za kale, sayansi n.k.

HIVYO BASI
  • Baada ya makala hii fupi nimekauandalia baadhi ya vitabu ambavyo kwa namna moja ama nyingine vinaweza kukupa faida katika maisha yako. jaribu kupitia hivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli aisee m huwa nadownload siyo msom wa siku nyingi kweny hv vitabu visivyo vya shule ila ndo nmeshaanza na matokeo ni mengi aisee utajiboreshea maisha kuna vtu vyng vya kukufundisha,hasa self improvement
Umenena vyema, mi binafsi ni msomaji kiasi, ingawa nakuwa mvivu wa hapa na pale, ila mwaka huu nimeazimia nisome vitabu sana, ingawa nimeanza kwa kusua sua kutokana na ubize wa hapa na pale, ila hadi sasa nimesoma vitabu saba, na namalizia cha nane.
Nime base kwenye
Self help
Psychology
Business na management
 
Jaribu kwasasa kila kitu kipo Sawa..

www.bongoclass.com

Hii ni website , unaweza kuingia na kusoma vitabu mbali mbali. Unaingia online kisha bonyeza offline pale uta download app yetu ukiwa online kisha mafaili utakayo yafungua ukiwa online unaweza kuyapata baadae ukiwa offline.

www.mrbunduki.com.

Hii ni blog ndogo Tu inayojihusisha na utunzi wa mashairi, tenzi, riwaya na mikasa mbali mbali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom