Faida tatu za kuvuta sigara

Faida tatu za kuvuta sigara

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,345
Nimeitoa hukoo Facebook kwa bwana wa kuitwa Ramadhan Lutambi

1.Mvuta sigara hazeeki,
Hazeeki kwa sababu hufa mapema kwa kifua kikuu.

2.Mvuta sigara haumwi na mbwa.
Haumwi na mbwa kwa vile Kifua na mapafu yanapooza mapema hivyo hulazimika kutembea na bakora.

3.Mvuta sigara nyumbani kwake haingii mwizi.
Haingii mwizi kwa kuwa inafika wakati mvuta sigara halali kwa kukohoa usiku kucha. Hivyo mwizi anajua bado yupo macho.

‪Aliye‬ elewa amwambie na mwenzie.
 
Mvuta sigara anachangia kuongeza kasi ya idadi ya michepuko.

Anachangia kwasababu mvuta sigara hawezi kumridhisha kimapenzi mke/mpenzi wake.
 
Aisee hii safi sana! Ingefaa mno kule jokes na vimbwanga.
 
hawa jamaa wakinyeshewa na mvua ni zaidi ya kero
 
Kwani ni utani huu?
Hiyo thread ya faida za kuvuta sigara si utani Khantwe, ila imekaa kama aina ya kejeli hivi. Kejeli, utani, mzaha, vituko, vyote vinatumbukizwa jukwaa la jokes/ gossip/ udaku.
 
Last edited by a moderator:
Mvuta sigara anachangia kuongeza kasi ya idadi ya michepuko.

Anachangia kwasababu mvuta sigara hawezi kumridhisha kimapenzi mke/mpenzi wake.

Nalo neno hili...
 
Upo msituni unatembea hamad! kugeuka nyuma unamuona simba anakuja utafanyaje? Tupia ma ujanja yako hapa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom