Fahmi Dovutwa Nashindwa kumuelewa

FortJeasus

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
603
397
Miongoni mwa wanasiasa wapuuzi niliopata kuwajua,Fahmi Nassoro Dovutwa,mwenyekiti wa chama cha UPDP(sitaki kujua hata kirefu chake) ni mojawao.

Mwaka 2010 alijitoa katika kinyanganyiro cha Uchaguzi Mkuu alipokuwa anawania nafasi ya Urais kwa sababu za kipuuzi ambazo nisingependa kuzirejea hapa.Si vibaya kukumbusha kuwa,wakati akiendesha kampeni zake wakati huo,moja ya vipaumbele vyake ilikuwa kuanzisha kiwanda cha silaha kwa madhumuni ya kuinua mauzo ya nje pamoja na matumizi ya ndani ili kuimarisha usalama wa rai na mali zao pamoja na ulinzi wa taifa kwa ujumla!

Kwa sasa huyu mwananchi mwenzetu dhaifu mno kifikra na kimatendo yupo Dodoma ''akitunga'' Katiba!Badala ya kutoa mchango wake wa mawazo kuhusu Rasimu ya Pili ya Katiba,kipaumbele kwake ni maudhui ya mkutano wa TCD na Rais siku ya jumatatu iliyopita.Hapa chini nimeweka maelezo yake,kutoka gazeti la Mwananchi,ili kila mmoja wetu aone namna watu wanaojiita wanasiasa wanavyofikiri na kutenda.

Dodoma. Sumu iliyomwagwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Seif Shariff Hamad imeanza kuwatafuna baadhi ya viongozi Taasisi ya Demokrasia nchini (TCD), akiwamo mwenyekiti wake, John Cheyo.

Akiwa mkoani Mwanza, Maalim Seif aliwatuhumu viongozi watatu wa TCD kuwa ni wasaliti kwa kile alichodai kukataa kusaini makubaliano kati ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi hao walipokutana Dodoma Septemba 8.

Maalimu Seif alisema Cheyo, Mwenyekiti wa Taifa wa TLP, Augustino Mrema na Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa hawakutia saini makubaliano hayo.

Waliotajwa kutia saini ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa.

Hata hivyo, akizungumza bungeni mjini Dodoma jana, Dovutwa alisema kauli hiyo ya Maalim Seif imemletea matatizo makubwa kwa vile tayari ameanza kupokea vitisho vya maisha yake.

Dovutwa alisema katika kikao chao na Rais Septemba 8 walikubaliana mambo mawili ya msingi, moja kuifanyia marekebisho Katiba ya sasa na pili Bunge liendelee hadi litakapofikia ukomo wake Oktoba 4.

"Suala hili limeshaleta chuki kwenye jamii na wengine maisha yetu yameshakuwa katika matatizo kwa kauli ya kiongozi mmoja mkuu wa Serikali kutoka CUF," alisema.

Alisema kitendo cha wao kukubaliana halafu viongozi wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kumwacha yeye, Mrema, Cheyo na Mangula kuzungumza na wanahabari kilikuwa ni kitendo cha hatari.

"Document (nyaraka) inayosemwa sisi tulikataa kuisaini, tulikataa kuisaini kwa sababu ilikuwa na mitego. Ile ‘document' tumeambiwa tusaini dakika za mwisho kwenda mlangoni kwa Rais hatukuwa na muda wa kuisoma,"alisema.

Kwa mujibu wa Dovutwa, katika nyaraka hiyo kulikuwa na kipengele cha hatari ambacho kilikuwa kinataka Bunge lisitishwe na baada ya kusitishwa, itungwe sheria kumdhibiti Rais ajaye mara baada ya kuingia madarakani aitishe mjadala wa Bunge la Katiba.
"Kama hivyo ndivyo, yaani Rais anaingia madarakani mnamtwisha na mgogoro.

Nchi itakalika? Kwa hiyo tunakwenda pale mwanzo kwamba hawataki nchi itawalike,"alisisitiza.

Chanzo:Mwananchi



 
Hiyo posho ya 300,000 kwa siku imehamia kwenye ubongo!Kawa mtumwa na msaliti kwa umma!
 
Namuunga mkono 1000%. Mlitegemea Faumi Dovutwa alambe lini posho ya Ubunge jamani?? Dovutwa analipa fadhila kwa m/kiti mwenzake wa ccm kumkumbuka na kumwita akachukue mtaji wa kugombea ubunge mwakani.
Dovutwa alijua kuwa hatakaa apate tena mkwanja ka huo na akiondoka mle ndani, UKAWA hawawezi kumpa. Yule ni MCHUMIA TUMBO TUUUUU. Hana lolote hivyo alijitutumua pale kumuonesha Sita kuwa wapo pamoja. Laana hii haitamwacha vyema ndo maana anajihami ati anatishiwa maisha, sio watu wanamtishia maisha ni mizimu inamtishia kwani amekula hela kabla hajaenda kwao kuzitolea kafara.
Mtu unataka urais na wazo kichwani la kuanzisha vita, atapigana na nani huyooo
 
To be honest, kwa mtu makini ni kupoteza muda ktk siasa za vyama vya upinzani kumuongelea mtu kama John Momose Cheyo, Augustine Lyamtonga Mrema na Fahami Dovutwa. Jamani these guys they are no longer opposition party leaders any more. Ukifikiria strength and popularity yao na vyama vyao ni muhimu wao kufanya haya yanayoendelea ktk mchakato huu wa kutunga katiba mpya.
 
To be honest, kwa mtu makini ni kupoteza muda ktk siasa za vyama vya upinzani kumuongelea mtu kama John Momose Cheyo, Augustine Lyamtonga Mrema na Fahami Dovutwa. Jamani these guys they are no longer opposition party leaders any more. Ukifikiria strength and popularity yao na vyama vyao ni muhimu wao kufanya haya yanayoendelea ktk mchakato huu wa kutunga katiba mpya.

Vyama vya siasa ambazo ofc zao ni briefcase na siyo taasisi ni mzigo.
 
Nimeona hicho kichwa cha Habari kuwa anatishiwa maisha.......hata sikuhangaika kuisoma hiyo Habari maana nilijuwa Ndugu Hashim hana lolote zaidi ya kutengeneza majungu na kutaka asikike,huyo wa kumtishia maisha ni nani na katika kipi kwenye siasa alilofanya mpk awe target.......Labda kama kuchukua mke wa mtu au anadaiwa huko mtaani kwao,hapo anaweza Tishiwa maisha..........
 
huyoo jamaa kagombea uraisi hata mamaake mzazi hajui kama anagombea unafikiri anajitambua kweli.......
mnafiki tu
 
Watanzania wengi wapuuzi na hawako makini na critical issues.
 
Nimeona hicho kichwa cha Habari kuwa anatishiwa maisha.......hata sikuhangaika kuisoma hiyo Habari maana nilijuwa Ndugu Hashim hana lolote zaidi ya kutengeneza majungu na kutaka asikike,huyo wa kumtishia maisha ni nani na katika kipi kwenye siasa alilofanya mpk awe target.......Labda kama kuchukua mke wa mtu au anadaiwa huko mtaani kwao,hapo anaweza Tishiwa maisha..........

Ha ha ha ha ha ha dah
 
Miongoni mwa wanasiasa wapuuzi niliopata kuwajua,Fahmi Nassoro Dovutwa,mwenyekiti wa chama cha UPDP(sitaki kujua hata kirefu chake) ni mojawao.

Mwaka 2010 alijitoa katika kinyanganyiro cha Uchaguzi Mkuu alipokuwa anawania nafasi ya Urais kwa sababu za kipuuzi ambazo nisingependa kuzirejea hapa.Si vibaya kukumbusha kuwa,wakati akiendesha kampeni zake wakati huo,moja ya vipaumbele vyake ilikuwa kuanzisha kiwanda cha silaha kwa madhumuni ya kuinua mauzo ya nje pamoja na matumizi ya ndani ili kuimarisha usalama wa rai na mali zao pamoja na ulinzi wa taifa kwa ujumla!

Kwa sasa huyu mwananchi mwenzetu dhaifu mno kifikra na kimatendo yupo Dodoma ''akitunga'' Katiba!Badala ya kutoa mchango wake wa mawazo kuhusu Rasimu ya Pili ya Katiba,kipaumbele kwake ni maudhui ya mkutano wa TCD na Rais siku ya jumatatu iliyopita.Hapa chini nimeweka maelezo yake,kutoka gazeti la Mwananchi,ili kila mmoja wetu aone namna watu wanaojiita wanasiasa wanavyofikiri na kutenda.



Chanzo:Mwananchi



mimi hata sioni wa kupiga kelele nao pale uyo cheyo hata bill gate ampe tuff ashindi kwani mzee na nina shaka anaugua ebora yule si mzima! Uyo mrema ndio hivyo leo kesho atakufa hana mbele wala nyuma! Uyo dovutwa anajipendekeza kwa jk na jk bc nina cho mpendeya hata hana mpango nae! Mimi nasema waachane nao ayo majinga
 
To be honest, kwa mtu makini ni kupoteza muda ktk siasa za vyama vya upinzani kumuongelea mtu kama John Momose Cheyo, Augustine Lyamtonga Mrema na Fahami Dovutwa. Jamani these guys they are no longer opposition party leaders any more. Ukifikiria strength and popularity yao na vyama vyao ni muhimu wao kufanya haya yanayoendelea ktk mchakato huu wa kutunga katiba mpya.
ujitambui wewe
 
dovutwa na wachumia tumbo wenzake njaa zinawasumbua na njaa zao zimewakaa m@k@|i0ni badala ya kukaa tumboni. hawa mawakala wa magamba ni wa kuwapuuza tu.
 
SUMU ILIYOMWAGWA na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad imeanza kuwatafuna baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Demokrasia nchini (TCD), akiwamo Mwenyekiti wake, John Cheyo.

Akiwa Mwanza, Maalim Seif aliwatuhumu viongozi watatu wa TCD kuwa ni wasaliti kwa kile alichodai kukataa kusaini makubaliano kati ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi hao walipokutana Dodoma Septemba 8.

Maalimu Seif alisema Cheyo, Mwenyekiti wa Taifa wa TLP, Augustino Mrema na Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa hawakutia saini makubaliano hayo.

Waliotajwa kutia saini ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk Wilbroad Slaa.

Hata hivyo, akizungumza Bungeni Dodoma jana, Dovutwa alisema kauli hiyo ya Maalim Seif imemletea matatizo makubwa kwa vile tayari ameanza kupokea vitisho vya maisha yake.

Dovutwa alisema katika kikao chao na Rais Septemba 8, walikubaliana mambo mawili ya msingi, moja kuifanyia marekebisho Katiba ya sasa na pili Bunge liendelee hadi litakapofikia ukomo wake Oktoba 4.

“Suala hili limeshaleta chuki kwenye jamii na wengine maisha yetu yameshakuwa katika matatizo kwa kauli ya kiongozi mmoja mkuu wa Serikali kutoka CUF,” alisema Dovutwa.

Alisema kitendo cha wao kukubaliana halafu viongozi wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kumwacha yeye, Mrema, Cheyo na Mangula kuzungumza na wanahabari kilikuwa ni kitendo cha hatari:

“Document (nyaraka) inayosemwa sisi tulikataa kuisaini…tulikataa kuisaini kwa sababu ilikuwa na mitego. Ile ‘document’ tumeambiwa tusaini dakika za mwisho kwenda mlangoni kwa Rais hatukuwa na muda wa kuisoma,” alisema Dovutwa.

Kwa mujibu wa Dovutwa, katika nyaraka hiyo kulikuwa na kipengele cha hatari ambacho kilikuwa kinataka Bunge lisitishwe na baada ya kusitishwa, itungwe sheria kumdhibiti Rais ajaye mara baada ya kuingia madarakani aitishe mjadala wa Bunge la Katiba:

“Kama hivyo ndivyo…yaani Rais anaingia madarakani mnamtwisha na mgogoro…Nchi itakalika?…Kwa hiyo tunakwenda pale kwamba hawataki nchi itawalike,” alisisitiza Dovutwa.

Kwa upande wake, juzi akizungumza Bungeni kuhusu yeye kutosaini makubaliano hayo, Cheyo alisema:

“Wewe ukisema eti mheshimiwa Cheyo hakusaini pointi za mazungumzo zile…(wazungu wanasema zilikuwa ni pointi za mazungumzo) kwamba tunaenda kuzungumza juu ya hili na hili si lazima usaini kwamba haya ndio makubaliano.”

Aliongeza: “Makubaliano yanapatikana baada ya mazungumzo,” alisema Cheyo, wakati akijitetea kwanini hakusaini makubaliano hayo kama ambavyo Maalim Seif, alidai mjini Mwanza..

Chanzo: Daniel Mjema wa Mwananchi
 
Back
Top Bottom