Fahamu namna bora ya kutengeneza Kachori

Muda mwingine unataka kubadilisha mlo mkuu.
Huo sio mlo ni mboga hiyo mkuu! Hushibi chochote hapo bila kuweka kitu chochote kizito na hiyo ndo sifa ya mboga😜
Hata chips huwa ni mboga ila hamjui tu!!
 
Mbona naona Youtube wanatumia all purpose wheat flour?

Kwa hiyo inaweza kuwa sababu za kiwa laini saana?
Wewe SI unataka utengeze Gamba la juu,,Sasa sijui huo unga una apply vipi,maana hizo ball sharti uzichovye kwenye Ute wa yai,then unaweka kwenye unga unachovya Tena kwenye Ute then unapitisha kwenye bread crumbs ndio unadumbukiza kwenye kikaango
 
Wewe SI unataka utengeze Gamba la juu,,Sasa sijui huo unga una apply vipi,maana hizo ball sharti uzichovye kwenye Ute wa yai,then unaweka kwenye unga unachovya Tena kwenye Ute then unapitisha kwenye bread crumbs ndio unadumbukiza kwenye kikaango
Asante Elungata hii process yako ni ndefu sina hata bread crumbs na kutengeneza ni hatua nyingine mkuu.
 
Daby, Chemsha viazi,vichuje kwenye chujio,viponde,unaweza kuweka vitunguu swaum,korienda,pili pili kama ukipenda,chumvi,kisha koroga uji wa ngano, weka rangi kwa sababu umesema binzari huielewi,so unachovya kwenye ngano unatia kwenye mafuta,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chemsha viazi,vichuje kwenye chujio,viponde,unaweza kuweka vitunguu swaum,korienda,pili pili kama ukipenda,chumvi,kisha koroga uji wa ngano,weka rangi kwa sababu umesema binzari huielewi,so unachovya kwenye ngano unatia kwenye mafuta,

Sent using Jamii Forums mobile app

Shukrani nilikuwa sichuji....labda ndiyo maana maji na ulaini nilikuwa nauskia.
 
Je huwa unahakikisha viazi ni vikavu(havina maji) kabla ya kuviponda?
Yawezekana pia unaviivisha sana.

Hutumii ute wa yai?
 
Daby unahakika unatengenza Potato Balls au Fried mashed potato? Bora ubakie na utaalam wa Maandazi na mengineo.

Kuna vitu sijaviona kama Kiini cha yai(usiulize yai la kuku au bata) sio lazima lakini. Breadcrums( unaweza nunua supermarket, sio lazima ukaushe mkate juani). Kwenye kulainika kw aviazi inategemea na unachemshaje viazi vyako..na aina ya viazi

Chemsha viazi bila kumenya viziive sana, usivikate vipade weka vizima.
 
Naomba majina ya rangi unazo tumia....

Kuhusu viazi kuiva kiukweli leo nilijitahidi nilikaa kuvisubiri havikuiva saana.

Ngano unatumia ipi? Ingekuwa vizuri kama ungenipa mahitaji yote na hatua mkuu.

Shukrani.
rangi za ubuyu zinakua kwenye vikopo vidogo

viazi visiive sana waweza tumia viazi vizimavizima pia hio ukichanganya na minof ya samaki, kitunguu maji,kitunguu saum, chumvi, giligilani zinaitwa katles
 
Nisiviponde niviweke hivyo hivyo vilivyo?

Sijaelewa mkuu.
yap yan kiazi unakikata mara mbili kama n kikubwa

chemsha na maji kidogo visiorojoke

tayarisha unga wako wa ngano

weka rangi yako ya ubuyu hio njano, chumvi na maji kiasi koroga huo mkorogo wa unga wangano usiwe mwepesi

chukua karai weka mafuta weka jikoni

chota kiazi kitumbukize kwenye huo mchanganyiko wa ngano had uone ile ngano imejieneza vizur kwenye kiaz

kama mafuta yameshapata moto weka kiazi ulichokidip kwenye hilo rojo la unga wa ngano kaanga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom