Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Wateja wetu wote katika Jukwaa hili mita zinazofungwa kwa wateja kwa sasa zote ni zile zinazofungwa kwenye nguzo Wassion na aina nyingine ni EDMI ndizo zinazo patikana katika ofisi zote za TANESCO .

Mita hizo zote zinatumia remote au kiwasilianishi kama wengine wanavoita na remote hizo zipo za aina mbili kuna zile zinazo hitaji kuchomekwa ukutani kwenye socket switch ndio uingize umeme na kuna zile ambazo si lazima chomeke ukutani kwenye swichi ndio uweke umeme,aina hii ya pili hutumia antena kuwasiliana na mita remote hizo zote zina ubora sawa.

KUHUSU Tarrif mgawanyo wa makundi ya matumizi ya umeme unafanyika kutokana na kiwango cha matumizi ya mteja mfano kuna mtu kauliza kuwa kwanini mtu mmoja anauziwa unit moja sh 100 na mwingine ni zaidi ya hapo , jawabu ni kuwa makundi ya matumizi yapo kama ifuatavyo

Kundi la kwanza ni wale wateja wanao tumia unit ambazo hazivuki units 75 kwa mwezi, wateja hawa mara nyingi ni wale wenye matumizi madogo kabisa wengi wao hawa a vifaa vingi vya umeme mostly wako vijijini .wateja hawa hulipia unit moja shs 100 kama atatimiza kigezo cha kuto vuka units 75 kwa mwezi . na ikiwa atavuka units 75 kila unit inayo zidi baada ya zile 75 za mwanzo atachajiwa tshs 350 , na ikiwa mteja huyo atavuka units 75 kwa miezi mitatu mfulululizo mteja huyo atahamishwa daraja na kwa mashatri hayo mteja huyo hataweA kurudi daraja hili dogo tena.

Kundi lapili ni lile la wateja wanao tumia units zaidi ambao huanzia units 0 283.4 hadi hawa ndio wale wanao itwa Tarrif 1 hawa bei ya units ni shs 292 nahapa atatumia mita ya single phase yenye volts 220 -250 au ataweza kutumia ile ya three phase ile yenye volts 400 ikiwa atakuwa anamatumizi yanayo fikia units 7500 katika kundi hili bei inafanana kwa units hizo zote .

na kundi la tatu ni lile la wateja wa matumizi ya kati ambao hutumia units zaidi ya hizo 7500 na bei ya units moja ni shs 195 kwa unit moja na kundi la nne ni kundi la wateja wakubwa ambao unit moja wanauziwa shs 157 hawa hutumia umeme mkubwa sana mfano wale wanao jengewa line kabisa ya 33 Kv etc wateja hawa pamona na kundi lile la wateja wa kati wote huchajiwa kitu kina itwa KVA charges ambayo ni constant like kwa wale wa T2 tarrif 2 ni tshs 15004 na T3 ni 13200 nii ni ile gharama ya kiwango cha juu cha mahitaji tunaita maximum demand charges

Shukrani sana kwa kutupatia ufahamu huu.
 
naomba kujua kwa matumizi ya nyumbani, sh 10000 inabidi kupata units ngapi, hapa ni kwa matumizi ya nyumbani. ukifafanua hapa nathani tutaenda vizuri. kwa kifupi mimi huwa napata unit 28.1
 
Mkuu kuhusu kuna form nimeskia zipo TANESCO unajaza kwa wale wananchi wenye matumizi madogo ya umeme unakuwa unalipa 9700 kwa mwezi,je hiyo inabidi uwe na mita maalumu za watu wachini au kwa mteja yoyote mwenye matumizi madogo hiyo huduma inamuhusu?
Hii ni kwa wale wateja wenye matumizi yasiyozidi unit 75 kwa mwezi hawa ndo wanastahili kuwa kwenye tarrif 4
 
Asante kwa maelezo mazuri TANESCO.

Umesema sababu mojawapo ya umeme kupotea ni earth lod kutokuwa shaba halisi.

Naomba kujua sababu zingine zinazoweza kuleta leakage ya umeme kwenye nyumba.

Lakini pia, taarifa za mtaani zinasema ni vizuri kuweka chumvi na mkaa pale kwenye earth lod. Je hii inasaidia umeme kutokupotea?
Leakage ya umeme mara nyingi inasababishwa na weak/poor wiring system including earth rod
 
1. Je! ni kweli kuwa umeme unatofautiana bei ya unit kutokana na aina ya mita uliofungiwa?

2. Je ! kwa mita hizi mpya nimefunga umeme 3 phace low voltage kwa bahati mbaya umeme ukaisha wote, ninapoweka mwingine nitumie namba ngapi maana inasumbua.
Mkuu maswali yako hayako clear kama nimekuelewa bei ya unit haitegemei mita inategemea ww matumizi yako yapoje na hayo ndo yatapelekea uwekwe kwenye kundi lipi yaani ww ni mteja wa aina gani kama ni tarrif 1,4 nk swali lako la pili sijaelewa ila kama umeishiwa umeme nenda kanunue ila ufahamu kuwa kuna zile unit 150 ulizopewa mwanzo utapaswa kulipia bei yake ni around 50 na kitu hivi
 
Wateja wetu wengi wamekuwa wakijiuliza iwapo wamefungiwa mita sahihi kutokana na matumizi yao ya umeme? Ama mita ambazo wamefungiwa ni za Viwandani na kulalamika wanatumia umeme mwingi zaidi tofauti na matumizi wanayotumia

Mita za LUKU zinazofungwa majumbani ni sahihi kwa matumizi ya nyumbani, ufungaji wa mita za majumbani hutegemea sana upimwaji wa matumizi /mahitaji ya umeme katika nyumba husika.

Mteja anafanyiwa tadhimini kabla ya kuunganishiwa umeme, wakati wa uunganishaji wa umeme inaangaliwa maombi kama Mteja ameomba kufungiwa njia moja (single phase) ama njia tatu (three phase) na haiwezekani Mteja aombe njia moja ya umeme afungiwe njia tatu.

Iwapo matumizi ya umeme ya Mteja yakiongezeka kufika unit 7500 hapo atalazimika kutumia mita za njia tatu (three phase) zenye uwezo wa Volts 400 kutoka mita ya njia moja yenye Volts 220 -250.

Wateja wengi hawafahamu hasa anapo tumia umeme ukafikia units 300 anadhani TANESCO ilikosea kumfungia umeme/mita. Sio kweli, kinachotakiwa ni Mteja kuwa na matumizi mazuri ya umeme ili kupunguza gharama.

Aidha, mita za LUKU za njia tatu kwa baadhi ya Wateja wenye mahitaji makubwa ya umeme wamefungiwa majumbani mwao hasa ambao tangu tathmini inafanyika ilionekana mahitaji ya umeme yatafika units 7500 maeneo mengine ni ya Kibiashara na ambako matumizi ya umeme wa njia moja hautofaa huwa wanafungiwa huo wa njia tatu.

Kwa wastani wa units 10 usiku na 6 mchana maana yake Mteja ana zaidi ya units 300 kwa mwezi yaani 16x30 utapata units mia nne (400) hayo si matumizi madogo, pia yapo mambo mengi ya kuyaangalia linapokuja suala la matumizi ya umeme, cha kwanza hiyo mita iko sahihi? TANESCO huwa inapima mita kulingana na maombi ya Mteja, ikiwa itagundulika kuwa mita ni mbovu Mita hiyo huondolewa eneo la Mteja, na Mteja atasahihishiwa account zake kulingana na kile kipindi mita haikusoma ipasavyo,

Jambo la pili ni Mteja anatakiwa kukagua mfumo wa umeme wa nyumba yake na kuhakikisha hakuna hitilafu (leakage) yoyote inayo pelekea umeme kuvuja na kumuongezea matumizi Mteja (Wiring system) na pia Mteja kuhakikisha earth load iwe shaba halisi.

Tatu ni vifaa anavyo tumia Mteja vina uwezo gani wa kutumia umeme? Nirahisi ku hesabu umeme tunaotumia na kutoa malalamiko kwa TANESCO, na Shirika litafanya ukaguzi ili kubaini matumizi hayo pengine ni sahihi, kila kifaa kina kiasi cha umeme kinachotumia kwa dakika ama masaa kadhaa. Inashauriwa Mteja kutumia vifaa vinavyotumia umeme mdogo (Energy Server), pia inashauriwa kuepuka vifaa vya mitumba sababu vingi vinatumia umeme mwingi.
Salam mkuu,asante kwa Maelezo ila mm ninatatizo kila ifikapo saa moja Umeme unakatika kwng tu na unarudi mda kuanzia saa tatu Sikh zingine HD sita nimetoa taarifa bila mafanikio nipe muongozo mkk
 
naomba kujua kwa matumizi ya nyumbani, sh 10000 inabidi kupata units ngapi, hapa ni kwa matumizi ya nyumbani. ukifafanua hapa nathani tutaenda vizuri. kwa kifupi mimi huwa napata unit 28.1
Inategemea upo ktk kundi lipi ila kwa mujibu wa maelezo yako upo tarrif 1 ambapo bei ya unit 1 ni tzs 292 kwa hiyo kwa tzs 10000 unapata unit 28.1
 
LUKU zinawekwa mahali ambapo TANESCO wanaona salama.

ukichukulia wateja wapo 20 ni vigumu kufunga mita 20 kwenye nguzo hivyo ndio maana nyingine zinawekwa majumbani juu ambapo Mteja hawezi kufika mahali salama

Luku niliyo nayo ni ya kawaida ipo juu sana ambapo mpaka niweke ngazi ndipo naifikia, je kuna uwezekano wa kuuziwa luku nitakayotumia kama remote ili niondokane na shida ya kupanda juu kwa ngazi kila ninapoingiza umeme?
 
Mimi naomba ufafanuzi kuhusu umeme ule wa vijijini(rea)
Mbona matangazo yenu na wanachotufanyia ni tofauti?Ukiritimba mwingi tatizo nini?
 
Inachukua muda gani kuvutiwa umeme majumbani baada ya kukamilisha taratibu zote za ulipaji?
 
Swali. Tumefungiwa mita mpya, ila tunapoenda kulipia tunaambiwa mita haijasiliwa ilipotoka makao makuu kwa hivyo inabidi ibasilishwe. Je hamuwezi kumsajilia mteja huko makao makuu wakati mita anaendelea kuitumia?
 
Asante kwa maelezo mazuri TANESCO.

Umesema sababu mojawapo ya umeme kupotea ni earth lod kutokuwa shaba halisi.

Naomba kujua sababu zingine zinazoweza kuleta leakage ya umeme kwenye nyumba.

Lakini pia, taarifa za mtaani zinasema ni vizuri kuweka chumvi na mkaa pale kwenye earth lod. Je hii inasaidia umeme kutokupotea?
Yanii huuu ni uongo ulio pindukia ikumbukwe umeme ni taaluma kama taaluma nyingine tena ni taaluma nyeti kuliko nyeti tulizo nazo na wala taaluma hii isichangwanye na imani za kishirikina

Mtu asiye jua umeme hawezi jua kazi ya earth rod. Mfumo wa wiring wa nyumba wa kisasa lazime uwe na kitu kinacho itwa PE yaani protective earth. Kwa kifupi kama hufahamu,

Protective earth ni namna ambayo vifaa vyote vinavyo tumia umeme yaani electic appliances in case vikawa na leakage ya umeme kwenye outer case au kiwambo cha nje basi protective earth itafanya kazi ya kuukusanya ule umeme na kuupeleka kwenye earth au udongo. Mfano. Nadhani ushawahi kuona Fridge au deki hata feni ambayo ukiigusa inakupiga shot au inatetemesha basi jua fika hicho kifaa kina leakege ya umeme au umeme unavuja. Kwasababu umeme unavuja huo umeme ilitakiwa ukusanywe na upelekwe ardhini. Soo kaz ya Protective earth ni kuupeleka umeme unaovuja kwenda ardhini

Na inabidi ujiulize ni kwanini kwenye udongo au ardhini??????

Ni kwasababu hata earth lod ya transformer ipo kwenye udongo ivyo huo umeme unavuja kutoka kwenye vifaa vyako vya umeme huzunguka na kurudi tena kwenye transformer kupitia earth au udongo. Kumbuka ardhi inapitisha umeme

Earth rod

Hiki ni chuma kinachoweka ardhini ili kuunganisha protective earth na earth yenyewe (ardhi). Maranyingi material yake ni copper yaani shaba.

Kwanini ni shaba???

Kwa mtu aliye soma umeme anajufika shaba au copper is a one of mostly good conductor of electricity yaani ni kipitisha kizuri cha umeme kuliko vyote kwasababu kina ukinzani mdogo (Law resistance) Pia kinahimili joto
Pia sifa nyingine ya shaba huwa haishiki kutu (Rusting) hivyo basi ukiwa na earth rod ya shaba ni uhakika tosha kuwa una kifaa madhubuti cha kupeleka umeme ardhini

Chumvi na mkaa
Kama nilivyo sema ardhi au udongo unapitsha umeme. Na ili ardhi ipitishe umeme vizuri inabidi iwe na unyevu. Kama wote tunavyo jua Chumvi ina unyevu hata ukiiweka mkononi lazima upate unyevu pia mkaa una absorb moisture yaani unatunza unyevu na hii ndio sabab chumvi na mkaa huwekwa kwenye earth rod na hii ni technic tuuu lakini nishasoma vitabu vingi sijawahi kuona hii kitu

MATUMIZI YA UMEME YANAYO SABABBISHWA NA LEAKEGE

Kuna matumizi ya umeme yasio ya lazima ambayo husababishwa na uvujaji wa umeme kwenye wiring ya nyumba. Hii hutakana na sababu nyingi sana. Moja ikiwa ni designe ya kifaa chenywe kilivyo undwa na pia ni greater kati ya wire wa live na neutral au earth.
Ukinzani uliopo ndio husababisha kuonyesha kuwa kiasi hicho cha umeme kimetumika.
Na kiuhalisia ni kweli kimetumika ila bila manufaa yoyote

Nini cha kufanya

Ni muhimu kukagua wiring yako kama ina shida au vipi na pia ni muhimu kupima na kujua leakage ya vifaa vyako ambavyo ni frequent used. Mfano. Fridge linaweza tumika hata masaa 72 bila kuzima so kama lina leakage jua litamaliza umeme wa kuosha


Protective Earh Briefly
PE inafaida kubwa sana kwenye wiring ya nyumba yoyote au kiwanda linapokuja suala la radi. Kwani husaidia kukusanya umeme unaotokana na radi na kuupeleka ardhini

Japo PE ndio inyokula umeme unaovuja kwenye vifaa. Ivyo inashauriwa kuwa na PE kwenye nyumba yako maana faida ni kubwa kuliko hasara ambayo unaweza pata

Swali lako la msingi

Earth lod inapokuwa shaba halisi ndio husababisha kupotea kwa umeme sanaa kuliko unapokuwa na Lod fake.

Nakupa Fact.

Earth lod ya shaba ndio hupitisha umeme vizuri tena kwa uhakia kwenda ardhi ila fake hipitisha kwa mashaka kwasababu ya factors kama kutu au chuma chenyewe kilicho tumika

Mafundi uchwara hawajuii hiki kitu ndio huwaingiza chaka wateja na kuwaweka rehani kwa matatizo mengi

Solution.

Kupotea kwa umeme hakutibiwi kwa kubadirishla lod. Ila ni kujua ubovu yaani fault na hasa leakage inayosababisha umeme uvuje na kuitibu. Na sio kupoteza pesa kwa kuanza kunua lod na kuchimba chimba pembeni ya nyumba yako.

Nadhani ushawahi kukutana mtu au wew mwenyew kuona Circuit breaker ya nyumba yako inazima zima kila mara. Na unaona mtu analaumu sana


Hapa hutakiwi kulaumu ila ndo mida wa kujisifu kuwa wiring yangu na PE yangu ni nzima na inafanya kazi kwa usahihi swala ni kutafuta taizo


Kwa yeyote mwenye shida just call
0712425141
0763554400
Occybeats@live.com
 
1. Je! ni kweli kuwa umeme unatofautiana bei ya unit kutokana na aina ya mita uliofungiwa?

2. Je ! kwa mita hizi mpya nimefunga umeme 3 phace low voltage kwa bahati mbaya umeme ukaisha wote, ninapoweka mwingine nitumie namba ngapi maana inasumbua.
Ni aina ya mtumiaji ila sio mita
Cuz wew na rafiki yako mnaweza mkawa na mita sawa lakini matumiz yenu tofauti
Hivyo mnauziwa umeme kutokana na matumizi
 
Back
Top Bottom