Watanzania hawadanganyiki kama wewe unavyodhani.
Mkuu unahakika na unachosema? Kama kweli mtu ana akili timamamu anaweza kuona wazi kuwa huu ni uongo. I can assure you kuwa kaa tukiendelea ufuatiliaji wa utekelezaji wa ahadi hizi naweza kukwambia kuwa unaweza kuwa wa kwanza kulia.
Unajua inachukua muda gani kuufanya mji uwe wa viwanda? Can you beleieve that JK ana uwezo wa kufanya hata wilaya iwe ya viwanda?
Can you believe that kuna uwezekano wa kujenga barabara hata moja? Miaka mitano iliyopita hawajenga barabara hata moja, sasa kuna uwezekano wa kujenga barabara kweli? Hizi ndio ahadi za JK, kama kweli unaakili unajua kabisa kuwa hii ilikuwa danganya toto.
1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya
Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba
Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
Kujenga bandari Kasanga Rukwa
Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
Kulinda haki za walemavu- Makete
Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
Kujenga barabara MusomaMto wa Mbu Arusha-Arusha
Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma Kaliua,Tabora
Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma
Kuwafidia wanakijiji ngombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-
Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha Arusha mjini
Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti Ngorongoro
Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara
kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa
ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma
kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) Ruvuma
Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania Ruvuma
Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
Mtwara kuwa mji wa Viwanda Mtwara
Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha