ismail hassan
JF-Expert Member
- Jul 16, 2017
- 685
- 1,612
hongera sana mkuu.. Na karibu sana kwenye kilimo cha mkongeMwishoni mwa mwaka 2018 nilisoma andiko la Mr Mbaraka (Mtafiti wa Mkonge) ambalo liko kwenye uzi huu. Nilipendezewa nalo na kumpigia Simu. Akanielekeza sehemu ya kupata miche. Nikaenda Mlingano Tanga kupata picha ambayo nilipanda shambani kwangu Morogoro. Niliongezea na miche mingine kutoka katika shamba la Mkonge la Morogoro hapo Mkambalani (Mikese). Kwa kweli baada ya mwaka na miezi Kama 8 shamba langu linaonyesha matumaini na Nina nia ya kuongeza shamba. Lengo langu nikifishe walau hekita 40 kwa miaka 2 ijayo.
View attachment 1633420
Ni vijana wa mjini ambao hawawezi kuchangamkia furusa hii, je hao wengine wanaipataje aridhi?Vijana tuchangamkie hiki kilimo kinaweza kuwa mkombozi. Nasikia wakulima wa korosho wanalalamikia ukosefu wa magunia wakati mwingine. Tukiwa na Mkonge wa kutosha hili tatizo kitaisha maana tunaweza kuingia katika kutengeneza magunia zaidi kwa ajili ya korosho na mazao mengine.
Tanzania bado tuna ardhi kubwa sana sana. Tatizo la watu wengi wanapenda maeneo ambayo ni karibu na mijini. Kuna maeneo Tanzania ukienda hata hununui ardhi, serikali ya kijiji inakupatia ardhi, juhudi zako ni kusafisha hiyo ardhi na kuanza kulima.Ni vijana wa mjini ambao hawawezi kuchangamkia furusa hii, je hao wengine wanaipataje aridhi?
Ni mkoa upi huo nije nilime miti ya matunda?Tanzania bado tuna ardhi kubwa sana sana. Tatizo la watu wengi wanapenda maeneo ambayo ni karibu na mijini. Kuna maeneo Tanzania ukienda hata hununui ardhi, serikali ya kijiji inakupatia ardhi, juhudi zako ni kusafisha hiyo ardhi na kuanza kulima.
Kukosa ardhi huwa siamini kama ni kikwazo.
Unaongelea matunda gani? Mikoa tofauti Tanzania inazalisha matunda tofauti. Inabidi kujua aina ya matunda.Ni mkoa upi huo nije nilime miti ya matunda?
Amini usiamini... Morogoro ni mkoa mmojawapo kama alivyosema mdau hapo awali ..tunapenda ardhi ya mjini huko interior vijijini kwenye mapori hatufiki na pia kusafisha eneo ukipewa na kijiji napo changamoto.Ni mkoa upi huo nije nilime miti ya matunda?
Mkuu tunaweza kuwasiliana tafadhariLengo langu nikifishe walau hekita 40 kwa miaka 2 ijayo.
Naomba nijuwe mkonge ukishailima inaweza ikadumu kwa miaka mingapi ndo inakufa?muda wowote, na huvunwa baada ya miaka 4 mpaka 5
Naomba nijuwe mkonge ukishailima inaweza ikadumu kwa miaka mingapi ndo inakufa?
Nicheki mkuu. Ninalo ila wilaya ya Chunya nauza sehemu na mimi nipande sehemu inayobaki. Nauza ekari angalau kumiNatafuta mtu anayeuza ardhi kwa ajili ya shamba la katani
..nenda ofisi za wilaya zifuatazo , mvomero, handeni,korogwe, same, mwanga, pangani, Bagamoyo ..onana na mkuu wa idara kilimo, au afisa ardhi mueleze lengo lako .Natafuta mtu anayeuza ardhi kwa ajili ya shamba la katani
Wilaya gani naweza kupata mashamba huko Tanga kwaajili ya kilimo cha mkonge? Bei ya shamba kwa ekari moja ikoje huko? Asantemuda wowote, na huvunwa baada ya miaka 4 mpaka 5
Inamaana hakuna mapori huko ya kununua na kufyeka mwenyewe? Mapori yote Tanga yamekwisha, sivyo?lipo hekta 12 sawa na ekari 30..mill 48.
Huwa hayapatikani kama ulivyodai, mara nyingi watu hupanda wenyewe na maeneo kupata ckuiz ni ngumu...Ni kama bahati juzi kupata mtu anayeuza shamba lake maeneo ya korogwe ..ukitaka namba sema nikupatie
Wilaya gani naweza kupata mashamba huko Tanga kwaajili ya kilimo cha mkonge? Bei ya shamba kwa ekari moja ikoje huko? Asante
Mkuu,ni korogwe mpaka magoma huko kwa mandondo maeneo hayapatikani?kwa sasa kwa maeneo kongwe kama Korogwe inakuwa ngumu kidogo. Japo ukibahatisha wewaza kupata. Na ni kwa bei ambayo imechangamka.
Watu wengi kwa sasa wanaenda handeni mana bei iko chini, kwa ekari unaweza pata hata kwa laki moja (hii ilikuwa mwaka jana) huenda bei ikawa imepanda zaidi mana watu wengi wanakimbilia huko.
Mkuu,ni korogwe mpaka magoma huko kwa mandondo maeneo hayapatikani?
Mkuu,ni korogwe mpaka magoma huko kwa mandondo maeneo hayapatikani?
Vipi na biashara na kilimo cha viungo Tangamagoma ndo usiguse kabisa maana mkonge wenye singa nzuri Tanzania unatokea magoma na ni sehemu yenye mkonge mwingi mno ikifuatiwa na hale. Magoma, kwamandondo, mashewa mpaka mavovo, maramba yote wameshaamka. bora maeneo ya matarawanda, makorora, mahenge na kwamndolwa unaweza pata marneo. kwa magoma ni ngumu mno na ukipata bei itakuwa ya juu mno.