Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

Duh...sasa wenye majina mengi kazi tunayo!

Jina la kuzaliwa (la kilugha) naitwa Samulakai. Wakati naanza shule miaka hiyo walimu walioniandikisha wakaniita Samu Makai. Hiyo Makai sio jina la ukoo, ni la baba. Nimeenda kanisani wakanipa jina la kizungu....Salutaris. Nilivyoomba passport wakataka majina matatu....nikaandika Samu Makai Magori. Magori ni jina la ukoo lakini halimo kwenye vyeti vyangu vya shule. Nimefunga ndoa ya kikristo, cheti kikaandikwa Salutaris Samu Magori.

Mtaani hapa wananiita Baba Silke. Silke ni jina la mwanangu. Kazini wananiita Makai. Nikienda kijijini wananiita Samulakai. Kanisani wananiita Salu au Salutaris. Nikienda kwa mzee wangu hupenda kuniita Samu. Na hapa JF mnaniita SMU.

Sasa hapo 'namechisha" vipi majina?
 
Mkuu jina huwa ni lipi? Kama mdau mmoja hapo juu alivyoeleza kuwa na majina zaidi ya mawili, vivyo hivyo hata mimi pia Jina langu Allency, nilivyoanza kazi wakaanza niita la ukoo likianza na N, wakati official name linaanza na I na lipo kwa passport na official docs, so hapo kwako jina langu ni lipi????


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Habarini wana jf,
Kumekuwa na matatizo mengi sana katika mahusiano yetu ya kila siku,hasa ya kamapenzi na hata kijamii(na wenzetu).Mahusiano hayakai,watu kila siku wanasalitiana,na hata wengine kuchukiana bila sababu.Wengi wamekuwa na majibu yanayofanana huku wengine wakifika mbali kwa kusema kuwa huwezi pendwa au kumpenda mtu pasipo matumizi ya fedha.Lakini ki uhalisia fedha inanafasi ndogo sana tena ndogo mno katika mapenzi,

sababu ya mapenzi kudumu au kupendana baina ya fulani na fulani ni uwiano wa majina,
najua utastuka lakini huo ndo ukweli halisi,majina yanachukua nafasi kubwa sana katika kudumisha na hata furaha katika mapenzi iwe kwa wapenzi wetu na hata wengine wanao tuzunguka na hata pia wale tunaotaka kufanya nao biashara,endapo hakutakuwa na uwiano sahihi wa majina yenu basi uhusiano wenu kamwe hautadumu na hata ukidumu hautakuwa na furaha hivyo hivyo hata katika biashara yenu pia,endapo utafanya biashara na mtu ambae hamna uwiano katika majina yenu ni ngumu sana kufanikiwa na hata mkifanikiwa biashara yenu itaandamwa sana na matatizo mpka pale mtapofilisika.

UTAJUAJE UWIANO WA MAJINA YENU,
Elimu hii ya uwiano wa majina ilikuwa ikitumika sana na wazee wetu na ndio elimu hii hii inayotumika kuwaliza watu kwa kuwatoza gharama kubwa ili wasaidiwe
endapo unataka kuanzisha mahusiano ya kimapenzi,kirafiki na hata kibiashara na mtu,ki uwiano unatakiwa muwe mmezidiana herufi saba au zaidi mfano jerry na rachel wanaweza kuwa wapenzi na kudumu na hata kibiashara lakini jerry na mary hawawezi kuwa wapenzi wala kushirikiana katika biashara na hata wakiwa wapenzi hawawezi kudumu wala kuwa na mahusiano ya furaha.
kanuni hii pia unaweza kuitumia au hata kuithibitisha endapo unataka kupima mapenzi ya watu wawili au kutaka kujua nani anakupenda zaidi kwa kuangalia herufi za mwanzo za majina yao,yule ambae herufi yake ya kwanza ya jina lake na lako zimezidiana(zimepishana herufi saba au zaidi) na herufi yko ya kwanza jua huyo ndo mwenye mapenzi na wewe zaidi kushinda mwengine na hivyo hivyo kwenye kutafuta mpenzi
Elezea kwa mifano Mkuu, unajuaje kuwa yule anampenda zaidi mwenzake au hawawezi kudumu kwenye mahusiano...tumia mifano ya majina halafu utupe njia ya utambizi
 
Huenda ikawa labda sababu mie nimepitwa herufi zaidi ya kumi na tano hukooo. Na ndio sababu bado tunadunda tu miaka nenda rudi.

Ila nawaza tu hivyo kipindi hicho unachokisemea hakuna wazee ambao mahusiano yao yaliishia njiani?
 
Fact yangu ni kwamba ulioongea hapo huo ni upuuzi na nia ya kuwaibia watu wenye matatizo ya mahusiano
Jina halipendi unaopenda ni moyo ungeniambia kuwa jina la mtu linaweza kusadifu tabia yake kidogo inamantiki japo hii dhana inaande kupotea kabisa

Ingekuwa hivyo kusingekuwa na maumivu ya mapenzi kwa sababu wote mnakuwa hamna hisia sababu ya majina hayajapishana herufi saba,

Mapenzi ni hisia inayoanzia kwenye macho hadi moyoni

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata moyo haupendi moyo kazi yake kusukuma damu tu kiini cha hisia ni nafsi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh...sasa wenye majina mengi kazi tunayo!

Jina la kuzaliwa (la kilugha) naitwa Samulakai. Wakati naanza shule miaka hiyo walimu walioniandikisha wakaniita Samu Makai. Hiyo Makai sio jina la ukoo, ni la baba. Nimeenda kanisani wakanipa jina la kizungu....Salutaris. Nilivyoomba passport wakataka majina matatu....nikaandika Samu Makai Magori. Magori ni jina la ukoo lakini halimo kwenye vyeti vyangu vya shule. Nimefunga ndoa ya kikristo, cheti kikaandikwa Salutaris Samu Magori.

Mtaani hapa wananiita Baba Silke. Silke ni jina la mwanangu. Kazini wananiita Makai. Nikienda kijijini wananiita Samulakai. Kanisani wananiita Salu au Salutaris. Nikienda kwa mzee wangu hupenda kuniita Samu. Na hapa JF mnaniita SMU.

Sasa hapo 'namechisha" vipi majina?
Mkuu kama umeoa pambana uimarishe ndoa yako aya mavitu tuachie sisi tulio nje ya ulingo....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...hii ishu inaukweli ila ukienda kwa mihemko huwezi ielewa
 
Majina? Mbona Kuna Watu Wana Majina Mawili Na Yote Yanatumika Na Kufahamika Kwa Wengi, Sasa Ni Jina Gani Linaathiriwa Na Hii Nadharia?
 
Back
Top Bottom