FACTS 11: Kama wanasayansi wangesoma BIBLIA, Technology ya sasa ingekuwa Zamani Sana

Inaonekana umekutana na wanadini wasioelewa tunachokijadili wakakupotosha ukapotoka.
Sio bibilia inayojadiliwa hapa. Hapa sio kutafuta waumini bali ni biblical evidence kuonyesha kuwa bibilia ni scientifically accurate. na hujazungumzia hata kipengele kimoja
jamani si wewe umesema kuwa wanasayansi wangesoma bibilia sayansi ingekuwa mbali? si ni wewe? unakubali nini na kukataa nini? kila unapozungumzia bibilia unazungumzia dini, sawa na kuzungumzia Quran unazungumzia uisilamu, ukisema Veda UNAzungumzia uhindu nk,
 
jamani si wewe umesema kuwa wanasayansi wangesoma bibilia sayansi ingekuwa mbali? si ni wewe? unakubali nini na kukataa nini? kila unapozungumzia bibilia unazungumzia dini, sawa na kuzungumzia Quran unazungumzia uisilamu, ukisema Veda UNAzungumzia uhindu nk,
UMEANDIKA VZR
Lkn ukiangalia content zangu pale juu threadini ninazumzia kitu kusemwa miaka 3000+ iliyopita na kuja kugundulika scientifically miaka ya 1400 au 1500+. Kumbe basi kama wangeyazingatia haya miaka hiyo wakati maandishi ya bibilia yalikuwa bado katika magombo mambo mengi ya Sasa yangegunduliwa zamani kwa reference ya mifano juu ambayo hujaipinga kwa hoja mashiko. Zingatia mada usizingatie what you think you know.
 
hizi ni simulizi tu za watu wenye hekima, wakati taifa la iziraeli walipoingia kwenye matatizo watu wenye hekima wakaandika maandiko hayo kuwapa mwongozo wa jinsi kuvumilia na kuondokana na matatizo

Ayubu alikuwa anaishi mji wa UZI muji ambao haujapa kuwapo tangu dunia ianze kuwapo, jaribu kuangalia ramani zote za kibibilia za zamani hakuna mji km huo.

Umemzunguza MUHIBIRI wajua hicho kitabu kiliandikwa na nani? mbona humtaji mwandishi wake?

kwa maelezo yako yoooote uloeleza hapo juu naomba tuanze na asili ya binadamu

kwanza tambua kuwa bibilia hiyo iliandikwa kwa madhumuni ya ujenzi wa taifa la Iziraeli tu hivyo walikusanya mambo mema na mabaya wakayaita yote ni ya Mungu, na uandishi wa bibilia mambo mengi yametokana na simulizi za miungu ambazo zimekarabatiwa mfano unapoamini kwamba utatu wa Mungu, Mungu baba, Mungu mwana na Mungu roho mtakatifu, miungu hawa walikuwapo kabla ya Ibrahimu, cha ajabu wewe unaamini Miungu wa tatu wakati Ibrahimu unayedai kuwa ni baba yako wa imani alisema Mungu mmoja, imekuwaje wewe unaamini miungu wa tatu?, unasema Mungu wako ana mtoto mmoja ambae ni Yesu kwa upande wapili (Waisilamu) wanadai Mungu hazai kwakuwa hana mke,

science ni neno la kigiriki lenye maana ya maarifa, maana yake maarifa ni science na bibilia yako inasema hivi kumcha bwana ni chanjo cha maarifa yaani Science kwa maana nyingine Science inatokana na Mungu sio Dini.

kwa hiyo dini ni tegemeo la wajinga na wapumbavu, baali Mungu ni tegemeo la watu wenye busara, hekima na maarifa
pole yako unootegemea dini, Mungu hatafutwi kupitia dini anatafutwa kupitia maarifa ambayo ni Science

Sikatai kwa kila msaafu wa dini yapo mambo mazuri yanopaswa yazingatiwe, na mengine ni mambo yaliyopitwa na muda kwa bahati mbaya dini zinakazania mambo yaliyopitwa na wakati

Swali la kizushi, km leo Mungu angelipuliza kipenda na kutangaza kuwa amefuta adhabu ya kifo binadamu hatutokufa tena na kila kitu binadamu anachokihitaji atapata bila masharti yeyote, hivi kuna atae enda nyumba ya ibada kuomba? na km ataenda ataenda kuomba nini?

dini zilianzishwa na wanadamu kumshawishi Mungu awaondolee kifo, ndio sababu kila dini inastahili yake ya kumwendea Mungu, wengine hulia, wengine hupiga magoti, wengine husali uchi, lkn staili zote hizo zimeshindwa kumridhisha Mungu kuwaondelea wanadamu kifo, dini zilipoona kwamba wanadamu wanaendelea kufa wakaja na ushawishi mwingine kwa maana ya kwamba hata binadamu akifa ataenda mbinguni wataishi milele, simulizi ya maisha ya umilele huo zinatofautiana kati ya dini na dini wengine wanadai huko hakuna kula wala kunywa ni kusifu tu, wengine wanassema kule kuna vinywaji vitamu na kuhudumiwa na vimwana wazuri, je ukweli ni upi? nani aliyekwenda mbinguni na kurudi?
Umeeleza mengi binafsi nimependa maana yanahitaji kujibiwa na nitajibu kimoja baada ya kingine kwa kadili nitakavyoweza.
Ukienda middle east yote kuanzia Iraq, egypt, allepo Ilan israel penyewe Kuna archeological evidence za kumwagikia za vitu unavyodai ni story za kutunga ili kuliwaza watu.

Mkuu sentensi yako ya kwanza tu inaaibishwa na makoleo yanayofukua kila kukicha biblical facts ambazo wengi walidhani ni nadharia leo hata ninawi inafukuliwa, moto wa Sodom na Gomorrah unadhibitishwa practically hata ningekuwa na Uwezo wa kuwanutralize isis na pesa ya nauli tungetembea kila site then ndio nikuombe urudie hiyo sentesi. Hata higher clitics hawawezi kupinga kijuujuu hivyo.

Nitarudi asubuhi nitoe maoni yangu juu ya hizi changamoto zako
 
hizi ni simulizi tu za watu wenye hekima, wakati taifa la iziraeli walipoingia kwenye matatizo watu wenye hekima wakaandika maandiko hayo kuwapa mwongozo wa jinsi kuvumilia na kuondokana na matatizo

Ayubu alikuwa anaishi mji wa UZI muji ambao haujapa kuwapo tangu dunia ianze kuwapo, jaribu kuangalia ramani zote za kibibilia za zamani hakuna mji km huo.

Umemzunguza MUHIBIRI wajua hicho kitabu kiliandikwa na nani? mbona humtaji mwandishi wake?

kwa maelezo yako yoooote uloeleza hapo juu naomba tuanze na asili ya binadamu

kwanza tambua kuwa bibilia hiyo iliandikwa kwa madhumuni ya ujenzi wa taifa la Iziraeli tu hivyo walikusanya mambo mema na mabaya wakayaita yote ni ya Mungu, na uandishi wa bibilia mambo mengi yametokana na simulizi za miungu ambazo zimekarabatiwa mfano unapoamini kwamba utatu wa Mungu, Mungu baba, Mungu mwana na Mungu roho mtakatifu, miungu hawa walikuwapo kabla ya Ibrahimu, cha ajabu wewe unaamini Miungu wa tatu wakati Ibrahimu unayedai kuwa ni baba yako wa imani alisema Mungu mmoja, imekuwaje wewe unaamini miungu wa tatu?, unasema Mungu wako ana mtoto mmoja ambae ni Yesu kwa upande wapili (Waisilamu) wanadai Mungu hazai kwakuwa hana mke,

science ni neno la kigiriki lenye maana ya maarifa, maana yake maarifa ni science na bibilia yako inasema hivi kumcha bwana ni chanjo cha maarifa yaani Science kwa maana nyingine Science inatokana na Mungu sio Dini.

kwa hiyo dini ni tegemeo la wajinga na wapumbavu, baali Mungu ni tegemeo la watu wenye busara, hekima na maarifa
pole yako unootegemea dini, Mungu hatafutwi kupitia dini anatafutwa kupitia maarifa ambayo ni Science

Sikatai kwa kila msaafu wa dini yapo mambo mazuri yanopaswa yazingatiwe, na mengine ni mambo yaliyopitwa na muda kwa bahati mbaya dini zinakazania mambo yaliyopitwa na wakati

Swali la kizushi, km leo Mungu angelipuliza kipenda na kutangaza kuwa amefuta adhabu ya kifo binadamu hatutokufa tena na kila kitu binadamu anachokihitaji atapata bila masharti yeyote, hivi kuna atae enda nyumba ya ibada kuomba? na km ataenda ataenda kuomba nini?

dini zilianzishwa na wanadamu kumshawishi Mungu awaondolee kifo, ndio sababu kila dini inastahili yake ya kumwendea Mungu, wengine hulia, wengine hupiga magoti, wengine husali uchi, lkn staili zote hizo zimeshindwa kumridhisha Mungu kuwaondelea wanadamu kifo, dini zilipoona kwamba wanadamu wanaendelea kufa wakaja na ushawishi mwingine kwa maana ya kwamba hata binadamu akifa ataenda mbinguni wataishi milele, simulizi ya maisha ya umilele huo zinatofautiana kati ya dini na dini wengine wanadai huko hakuna kula wala kunywa ni kusifu tu, wengine wanassema kule kuna vinywaji vitamu na kuhudumiwa na vimwana wazuri, je ukweli ni upi? nani aliyekwenda mbinguni na kurudi?
1:hizi ni simulizi tu za watu wenye hekima, wakati taifa la iziraeli walipoingia kwenye matatizo watu wenye hekima wakaandika maandiko hayo kuwapa mwongozo wa jinsi kuvumilia na kuondokana na matatizo
----> umeamua kurahisisha. Matatizo gani, Lini, Yalisababishwa na nani, Mbona bado wanamatitizo mengi pamoja na uwepo wa maandishi hayo, nielezee mfano wa nchi iliyoondolewa matatizo kwa maandishi,
Mfano tu Jerusalem Imebomolewa Mara Mbili, Imezungukwa na kutekwa mara 23, Imeshambuliwa mara 52, Mara 44 imekuwa captured and recaptured. Niambie kwa source na evidence wazo hilo walilitoa wapi na anani alilileta . Yaani kwa ufupi natakiwa uelezee Who, When, Where,What, Why and How kama uko tayari tujadili kwa hoja. Maana bibilia haijaelezea au kuandikwa na waisrael tu maana hata Ruth hakuwa muisrael, Baba wao wa imani Ibrahim hajawahi kuwa muisrael na wengine wengi.
Ayubu alikuwa anaishi mji wa UZI muji ambao haujapa kuwapo tangu dunia ianze kuwapo, jaribu kuangalia ramani zote za kibibilia za zamani hakuna mji km huo.

----> UZI
240px-Edom.png

kwanza sio kila mji umeandikwa kwenye kitabu upo kwenye ramani, ingekuwa hivyo na bustani ya edeni na miji ya awali kabla ya gharika ingekuwepo. Unapouliza kuhusu UZ, inabidi uulize miji kama Misri,Kushi, kanani maana yote iliwanza kwa kwa majina ya watu au familia, kutambulika hadi kufikia kiwango cha kutoka kwenye ramani inategemea na Ukubwa, na umaarufu ya mji yawezekana mji ukawa ndani ya mji mwingine mkubwa kabisa zaidi ya huo na ukamezwa.

Baadhiu ya ushahidi wa Uwepo wa UZ physically
1: Soma Mwanzo 10:23, 1 Nyakati 1:17 UZ ni jina la mtu kama walivyo au familia na baadae ikawa mji kama ambavo famila na nyingine Misri,Edom,etc ikiwemo familia ya mzee yakobo (Israel) ikaja kuwa nchi unayodhani iko nyuma ya nadhalia zako.

2:Ayubu 4:1 Rafiki yake ayubu Elifadhi anasomwa kama mtemani ambao walikuwa wanakaa edomu maana yake alitoka ediomu akaenda UZ kumsalimia Ayubu so huwezi kutenganisha edom na uz.

3:SOma ayubu 1:15,17 UZ ilikuwa subject ya attack ya wakaldayo ambao wap wanajulikana.

Lamentations 4:21 reads: "Rejoice and be glad, O daughter of Edom, that dwellest in the land of Uz"
hapo unaweza kuona kuwa land of uz ipo maeneo ua edomu . Ni kitu ambacho kilikuwepo na sio uzushi.


Umemzunguza MUHIBIRI wajua hicho kitabu kiliandikwa na nani? mbona humtaji mwandishi wake?
Hapa sielewi unataka nini, mwandishi wa kitabu au huamini kama kilikuwepo. hilo ni somo lingine, sijaelewa lengo lako ukimfahamu ndio utaamini au unataka nini.

Bibilia iliandikwa kwa dunia nzima, ndio maana sio waisrael wote wanaamini hiyo tunaoiita bibilia. ZIonism haiamini katika kufa na kufufuka kwa yesu. Sijui unaongelea waisraeli wapi.

Kuhusu kuwepo kwa miungu watatu hakuna uhusiano na kuwepo kwa utatu. natamua uwepo wa Osirus-Isis-Horus (utatu mtakatifu wa kipagani) na vingine vingi ambavyo vinarandana na vya shetani na hata hao wayahudi wenyewe walivipitia na kumuacha Mungu. Lakn ukikaa ukatulia utagundua hizo ni counterfit za shetani na hazina uhusiano na Mungu anavyoelezwa kwenye bibilia. Kuhusu ni Mmoja au mmoja katika watatu hiyo ni mada yake na hapa sio mahala pake kwa sas.
Swali la kizushi, km leo Mungu angelipuliza kipenda na kutangaza kuwa amefuta adhabu ya kifo binadamu hatutokufa tena na kila kitu binadamu anachokihitaji atapata bila masharti yeyote, hivi kuna atae enda nyumba ya ibada kuomba? na km ataenda ataenda kuomba nini?

Assumption hii ni invalid hadi ujue kwa nini tunakufa. Mahaka ya Mungu ni ya haki sio kama za huku duniani, Aliposema Utakufa hakika, ilikuwa hivyo. Hilo swali ungeliuliza kama adam asingekiuka makubaliano jee maisha yale yangeendelea duniani hadi sasa je tungekuwa tunaenda ibadani, Bado Mungu na adam na mke wake walikuwa na ukaribu sana kama baba na watoto wake au Mungu na Viumbe vyake. Kwa nini Ujiulizi hayo maswali kati ya malaika na Mungu wanaishije kwa nini wasiache kumuabudu kama wanaishi nae kila siku huko na hawana shida yoyote?


dini zilianzishwa na wanadamu kumshawishi Mungu awaondolee kifo, ndio sababu kila dini inastahili yake ya kumwendea Mungu, wengine hulia, wengine hupiga magoti, wengine husali uchi, lkn staili zote hizo zimeshindwa kumridhisha Mungu kuwaondelea wanadamu kifo, dini zilipoona kwamba wanadamu wanaendelea kufa wakaja na ushawishi mwingine kwa maana ya kwamba hata binadamu akifa ataenda mbinguni wataishi milele, simulizi ya maisha ya umilele huo zinatofautiana kati ya dini na dini wengine wanadai huko hakuna kula wala kunywa ni kusifu tu, wengine wanassema kule kuna vinywaji vitamu na kuhudumiwa na vimwana wazuri, je ukweli ni upi? nani aliyekwenda mbinguni na kurudi?

hapa mzee unaonyesha kwamba huelewi unachokizungumzia. niambie aliyeanzisha hivyo vutu na hayo malengo yawezekana kwenye msururu wa dini na madhehebu wakawepo wenye mtazamo huo. Lakini mimi naamini chochote kuhusu dini ibada kusali kimeelezwa kenye bibilia na ndio chakufuatwa bila kwenda kushoto wala kulia. na huko unapoongea kwenye kadamnasi mtandao ndipo unatakiwa kujengea hoja zako sio maneno ya kusikia au hisia. vinginevyo unakuwa hueleweki unataka au unapinga nini.
 
Baadhiu ya ushahidi wa Uwepo wa UZ physically
1: Soma Mwanzo 10:23, 1 Nyakati 1:17 UZ ni jina la mtu kama walivyo au familia na baadae ikawa mji kama ambavo famila na nyingine Misri,Edom,etc ikiwemo familia ya mzee yakobo (Israel) ikaja kuwa nchi unayodhani iko nyuma ya nadhalia zako.

2:Ayubu 4:1 Rafiki yake ayubu Elifadhi anasomwa kama mtemani ambao walikuwa wanakaa edomu maana yake alitoka ediomu akaenda UZ kumsalimia Ayubu so huwezi kutenganisha edom na uz.

3:SOma ayubu 1:15,17 UZ ilikuwa subject ya attack ya wakaldayo ambao wap wanajulikana.

Lamentations 4:21 reads: "Rejoice and be glad, O daughter of Edom, that dwellest in the land of Uz"
hapo unaweza kuona kuwa land of uz ipo maeneo ua edomu . Ni kitu ambacho kilikuwepo na sio uzushi


Hapo mzee hakuna cha maana ulicho jibu.
Biblia haiwezi kujipa ushahidi yenyewe inabidi utoe ushahidi at least kwejye maandiko mengine.
Kumbe kifupi mji wa UZI hauja wahi kuwepo
 

Hapo mzee hakuna cha maana ulicho jibu.
Biblia haiwezi kujipa ushahidi yenyewe inabidi utoe ushahidi at least kwejye maandiko mengine.
Kumbe kifupi mji wa UZI hauja wahi kuwepo
Nimetumia bibilia makusudi maana muuliza swali katumia bibilia.
na kwamujubu wa mkuu hapo (Hadi atakapokana) anakubaliana na miji mingine ya kibibilia kwa sababu inaweza kuwa traced back archaeologically na historically hadi nje ya bibilia kasoro huo alio na mashaka nao. Ndio maana nimemuambia kama ramani ya tanzania haionyeshi mji wa gamboshi alafu kesho ukasikia kuna watu wametoka magu kijiji cha masanza kona na kuvamia Gamboshi, Utajiuliza maswali machache tu kwamba wenda gamboshi ni mji mdogo uliokuwa hauna hadhi ya au ukubwa wa kuwa katika ramani. Kuwepo kwa familia ndani ya bibilia zilizozaa miji na mataifa na ukiambiwa mwanafamilia mmoja mfano UZ akakaa sehemu flani automatically kutokuwepo kwa record za physical uz kwenye ramani ya bibilia haimaanishi haipo. na kama alikuwepo masanza kona akazaa watoto na ukoo baadae mji au taifa, basi haizuii gamboshi kuzaa na kufanya kukawa na mji mdogo au kijiji kiitwacho gamboshi japo kinaweza kuwa kidogo . Bibilia haisemi nchi kwa maana ya taifa lA UZ bali (a Land of uz), ni sehemu tu inawezakuwa mji nchi au kitongoji.

old-testament-nations.gif

Mfano hiyo lamani haijaonyesha mizi midogomidogo zaidi ya 10,000. Haimaanishi kuwa haipo mkuu.

Nimemjibu kwa kutumia Bibilia kwa sababu na yeye msingi wa swali lake ni RAMANI YA KWENYE BIBILIA SIO hii ya kwenye atras tunayotumia huku duniani nje ya bibilia.
 
MWANZO: 6-8
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.

MPAKA HAPO, tunathibitishiwa kuna anga katikati ya maji na maji, yaani una li mpira kuubwa lililojazwa maji then unayagawa chini na juu ili katikati kuwe na nafasi, ambayao Mwenyezi Mungu aliifanya iwe ndio Anga, na kuipa jina "Mbingu" yaani MBINGUNI au unisahihishe kama si hivyo....

TUKIENDELEA NA MSTARI WA 9-10
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Sasa basi kama mwanzo maji yaligawanishwa chini na juu, basi bila kupoteza ukweli ni lazima Yale maji ya chini yalitafuta level yake na ina maanisha yalikuwa katika flat level.
mstari wa 9 kama unavyojieleza, ardhi ilipatikana baada ya hayo maji kuamrisha yajitenge, je hiyo ardhi haikuwa FLAT utoka katika maji yaliyojitenga? Chukulia kwa mfano, unaimwagilia sakafu iliyotoka kujengwa, maji yanapoanza kukauka huwa hayakauki kwa pamoja hata kama mwanzo yalienea eneo lote, so pale palipokauka ndio pawe nchi kavu na palipo na maji pawe ndio bahari.
maji yakaitwa bahari na pakavu pakaitwa nchi, ambapo Ndipo sisi viumbe wake tunaishi yaani mimi na wewe.

je kwa maandiko hayo, tunaishi katika eneo flat au juu ya mviringo?
basi kama wahubirio dunia ni tambarare wanapingana na BIBLIA nijuze, wanapingana na andiko lipi linaloielezea dunia kuwa ni Mviringo?
Ndugu hivi vitabu haviko straight forward.... ndio maana ni rahisi kupewa majibu yoyote tu... kila wanavyoulizwa wana majibu.

Pastor au sheikh ambae haijui sayansi at all lakini ameisoma biblia au quran kwa undani hawezi kukupa majibu kama yanayotolewa na wale waliopitia kwenye darasa la sayansi. Huyu wa sayansi atajifanya anachimekea maneno oxygen, atmosphere... kwa kifupi anaongeza chumvi.

Hayo maneno kwenye bible wala quran hayapo....
 
Ndugu hivi vitabu haviko straight forward.... ndio maana ni rahisi kupewa majibu yoyote tu... kila wanavyoulizwa wana majibu.

Pastor au sheikh ambae haijui sayansi at all lakini ameisoma biblia au quran kwa undani hawezi kukupa majibu kama yanayotolewa na wale waliopitia kwenye darasa la sayansi. Huyu wa sayansi atajifanya anachimekea maneno oxygen, atmosphere... kwa kifupi anaongeza chumvi.

Hayo maneno kwenye bible wala quran hayapo....
Unapojadili bibilia huitaji pastor wala shehe, jadili kwa mtazamo uliopo mezani. Kama mleta mada niko pembeni kosoa kwa mtazamo wako kulingana na upotovu husika ulioudukua ndani ya mada. ukitaka kuleta stori za shehe mara mchungaji huwa anasema hivi au vile utafeli maana bibilia ni mtambuka, uhalisia au ukweli wake haumilikiwi na kikundi cha watu flani au viongozi hata sisi waumini tunaweza kuja na mitazamo flani ikakubalika.
ingia kwenye content ya thread njoo tujadili changamoto zke kwa mitazamo huru
 
Umeeleza mengi binafsi nimependa maana yanahitaji kujibiwa na nitajibu kimoja baada ya kingine kwa kadili nitakavyoweza.
Ukienda middle east yote kuanzia Iraq, egypt, allepo Ilan israel penyewe Kuna archeological evidence za kumwagikia za vitu unavyodai ni story za kutunga ili kuliwaza watu.

Mkuu sentensi yako ya kwanza tu inaaibishwa na makoleo yanayofukua kila kukicha biblical facts ambazo wengi walidhani ni nadharia leo hata ninawi inafukuliwa, moto wa Sodom na Gomorrah unadhibitishwa practically hata ningekuwa na Uwezo wa kuwanutralize isis na pesa ya nauli tungetembea kila site then ndio nikuombe urudie hiyo sentesi. Hata higher clitics hawawezi kupinga kijuujuu hivyo.

Nitarudi asubuhi nitoe maoni yangu juu ya hizi changamoto zako
mkuu naomba nielewe vyema, sikusema mambo yote ya yaliyo andikwa kwenye misaafu ya kidini ni uongo, yapo mambo mazuri na mengine yamepitwa na wakati, hivyo kazi ni kwako kuchanganua, ktk historia ya mtu yeyote yule au taifa lolote lina mambo mazuri na mabaya, watu huwa wnachuja wanachukua mazuri na mabaya wanaachana nayo, ndivyo ilivyo hata kwa misaafu, kuna mazuri na mabaya watu wanatakiwa wachuje, wachukue mema mabaya wayaache, wawaachie waanzilishi wa dini
 
Je science imeweza kushawishi Mungu aondowe kifo? Mbona usomeki unapinga biblia na misahafu mingine lakini unaingia humo humo kutafuta uhalali wa hoja yako mbona hauthibitishi kwa sayansi yako natumai umelewa maharifa kidogo uliyoyapata juu ya uso wa dunia hii wewe unaweza kuwa msomi kuliko Paul?
 
Je science imeweza kushawishi Mungu aondowe kifo? Mbona usomeki unapinga biblia na misahafu mingine lakini unaingia humo humo kutafuta uhalali wa hoja yako mbona hauthibitishi kwa sayansi yako natumai umelewa maharifa kidogo uliyoyapata juu ya uso wa dunia hii wewe unaweza kuwa msomi kuliko Paul?
Ufahamu wa Paul kisayansi ulikuwa mdogo sana wakati ule ukilinganisha na ufaham wa wanasayansi wa leo, Paul ungelimwambia wakati ule kwamba wanadamu ipo siku watasafiri angani angelikuona wewe ni mwendawazimu, huenda angefika mbali zaidi na kudai unapinga Mungu, umerukwa na akili, kwani alikuwa akiamini na kujua kuwa ni ndege tu na ma;laika ndio walioruhusiwa na Mungu kuruka angani,

mfano Galileo Galilei apogundua kuwa ulimwengu kuwa ni mviringo km mpira wanadini hawa walimshutumu kwamba anampinga Mungu, kumbuka wakati Armstrong walipotua kwenye mwezi ninyi wana dini mliaani sana kitendo hicho, kuwa ni kitendo cha kuchomkoza Mungu, mkapitisha hukumu kwamba wanastahili kunyongwa hata kufa, dini zinapumbaza akili ya mwanadamu, hazitaki kumpa uhuru wa kufikiri na kuuliza, mara zote wanadai AMINI tu Mungu haulizwi kuuliza mambo juu ya Mungu ni kukufuru Mungu, na ndivyo alivyo Paul
 


Hapo mzee hakuna cha maana ulicho jibu.
Biblia haiwezi kujipa ushahidi yenyewe inabidi utoe ushahidi at least kwejye maandiko mengine.
Kumbe kifupi mji wa UZI hauja wahi kuwepo
Je kutokuwepo au kuwepo kwa mji huo ndio kuondowa ushaidi wote uliomo ndani ya Biblia? Na kama ni kusema iliandikwa na wenye hekima kipindi cha matatizo je matatizo leo hayapo miongoni mwa jamii na hao wenye hekima hawapo? kwa nini wasiandike tena maandiko zaidi ya hayo ili kuzisaidia jamii zao? Soma zaburi 1:1 ili ujipime!
 
Je kutokuwepo au kuwepo kwa mji huo ndio kuondowa ushaidi wote uliomo ndani ya Biblia? Na kama ni kusema iliandikwa na wenye hekima kipindi cha matatizo je matatizo leo hayapo miongoni mwa jamii na hao wenye hekima hawapo? kwa nini wasiandike tena maandiko zaidi ya hayo ili kuzisaidia jamii zao? Soma zaburi 1:1 ili ujipime!
Sasa nikisoma Zaburi tena inakuwa kazi kwangu kuelewa.

At least ushahidi wa mambo ya biblia utoke nje ya biblia yenyewe.
Maana kitabu hakiwezi kujitetea chenyewe na kikawa credible
 
Yaani watu bwana wanawaza kwamba tukisoma ndio tutajua ukweli....soma mathayo sijuu ngapi. Ukisoma ndio inakufanya ujue?... ubongo wa binadamu umejengwa kwenye misingi ya logic and arthmetics. Logical na illogical issues mnaamini tu... ndio maana wale wengine wanaamin ukijitoa muhanga basi unaenda peponi... na hawa wengine nao wanaamini aliyepona kwenye ajali ya ndege was because alikuwa anasoma bible... ridiculous.
 
Yaani watu bwana wanawaza kwamba tukisoma ndio tutajua ukweli....soma mathayo sijuu ngapi. Ukisoma ndio inakufanya ujue?... ubongo wa binadamu umejengwa kwenye misingi ya logic and arthmetics. Logical na illogical issues mnaamini tu... ndio maana wale wengine wanaamin ukijitoa muhanga basi unaenda peponi... na hawa wengine nao wanaamini aliyepona kwenye ajali ya ndege was because alikuwa anasoma bible... ridiculous.
hapa point sio kusoma, ili uambiwe usome first assumption ni kwamba na wewe unaamini au umeonekana ukitumia bibilia kama reference ya baadhi kwenye baadhi ya hoja zako kwa kuipinga au kuikataa. vinginevyo unadeclare wewe ni outsider then tutakuletea ushahidi wa nje ya bibilia wa archeology, fossils, palentology, history na hata science kukupa na kukuonyesha uhalali wa yaliyomo ndani ya bibilia kama ukiamua kuyakubali maana sio lazima
 
Ufahamu wa Paul kisayansi ulikuwa mdogo sana wakati ule ukilinganisha na ufaham wa wanasayansi wa leo, Paul ungelimwambia wakati ule kwamba wanadamu ipo siku watasafiri angani angelikuona wewe ni mwendawazimu, huenda angefika mbali zaidi na kudai unapinga Mungu, umerukwa na akili, kwani alikuwa akiamini na kujua kuwa ni ndege tu na ma;laika ndio walioruhusiwa na Mungu kuruka angani,

mfano Galileo Galilei apogundua kuwa ulimwengu kuwa ni mviringo km mpira wanadini hawa walimshutumu kwamba anampinga Mungu, kumbuka wakati Armstrong walipotua kwenye mwezi ninyi wana dini mliaani sana kitendo hicho, kuwa ni kitendo cha kuchomkoza Mungu, mkapitisha hukumu kwamba wanastahili kunyongwa hata kufa, dini zinapumbaza akili ya mwanadamu, hazitaki kumpa uhuru wa kufikiri na kuuliza, mara zote wanadai AMINI tu Mungu haulizwi kuuliza mambo juu ya Mungu ni kukufuru Mungu, na ndivyo alivyo Paul
Nilikushauri na ninakushauri tena kwa mara nyingine,haya mambo rudi kajifunze upya maana naona kabisa bado hujayajua ipaswayo kufikia kuanza ku argue na watu kwenye furum kama hapa....

Elimu ya Paul ilikuwa kubwa sana na hili hulijui,na inawezekana hakuna binadamu mwenye elimu kama ya Paul leo,unayakimbilia haya mambo na kuyapinga sijui kwanini,nakuona una jambo moyoni mwako linalokufanya uchukie sana dini kitu ambacho siyo kizuri kabisa....

Suala kama la Paul tu linakufanya uonekane hujui kabisa unachokijadili...

Niliwahi kukuambia kwamba unapaswa utofautishe dini na wanadini,mwanadini akiiba au kuua haimaanishi dini inaruhusu jambo hilo.Biblia inazungumza kuhusu dunia kuwa duara halafu wewe unajenga hoja kuwa wanadini walimshutumu na kumuona Galileo anampinga Mungu,ni wanadini gani hao?Ni Mungu gani unamzungumzia hapa?

Hata kama ni wa-Kristo walikuwa wakimpinga,huoni kwamba wanakwenda kinyume na kitabu kinachowaongoza maana kimesema dunia ni duara? Kwanini usiwalaumu wao kutokuelewa kinachoelezwa kwenye kitabu chao?

Nini kinakufanya ufunge kabisa ubongo wako kiasi hiki?
 
Kama unavyoeleza ni sawa lakini hiyo hiyo bible ilikuwa inatuaminisha ukiuchunguza sana ulimwengu unakufuru Mungu hapendi (rejea mnara wa babeli) hata kuchelewa kwa technology huwenda ilichangiwa zaidi na bible hiyo hiyo

Kujenga mnara kufika mbinguni kwa Mungu? :D
Hayo yalikuwa mawazo ya Kipuuzi, ndiyo maana kazi
ikastishwa mara moja ili waendelee na kazi zitakazowaletea
faida na si kupoteza muda, nguvu na rasilimali.
Swali:Kwani Mungu anapatikana wapi?Anapatikana juu? :D:D
 
Nilikushauri na ninakushauri tena kwa mara nyingine,haya mambo rudi kajifunze upya maana naona kabisa bado hujayajua ipaswayo kufikia kuanza ku argue na watu kwenye furum kama hapa....

....Elimu ya Paul ilikuwa kubwa sana na hili hulijui,na inawezekana hakuna binadamu mwenye elimu kama ya Paul leo,unayakimbilia haya mambo na kuyapinga sijui kwanini,nakuona una jambo moyoni mwako linalokufanya uchukie sana dini kitu ambacho siyo kizuri kabisa

Suala kama la Paul tu linakufanya uonekane hujui kabisa unachokijadili...

Niliwahi kukuambia kwamba unapaswa utofautishe dini na wanadini,mwanadini akiiba au kuua haimaanishi dini inaruhusu jambo hilo.Biblia inazungumza kuhusu dunia kuwa duara halafu wewe unajenga hoja kuwa wanadini walimshutumu na kumuona Galileo anampinga Mungu,ni wanadini gani hao?Ni Mungu gani unamzungumzia hapa?

Hata kama ni wa-Kristo walikuwa wakimpinga,huoni kwamba wanakwenda kinyume na kitabu kinachowaongoza maana kimesema dunia ni duara? Kwanini usiwalaumu wao kutokuelewa kinachoelezwa kwenye kitabu chao?

Nini kinakufanya ufunge kabisa ubongo wako kiasi hiki?

Elimu ya Paul ilikuwa kubwa wakati ule sio sasa hivi, Paul wakati ule alikuwa hajui teknolojia ya sasa, kapitie Pre history, Anciant history, Currenty history, Philosopy na Church History,

Dini ni hatari kwa maendelleo ya binadamu, mpaka leo dini zinapinga Sayansi na we ukiwa mmoja wao, niko upande wa Science na maana sayansi inawaleza watu ukweli, na huu ndio ukweli naweew shahidi. Sayansi inashughulika na maendeleo ya watu hai, bali dini inashughulika na maendeleo ya walio wafu
 
Ninapotaja bibilia na maanisha contents, Ni kweli wakati wa yusufu hakukuwa hata hizo torati maana zilikuja miama zaidi ya 400 baada yake. Ninaposema bibilia namaanisha neno la Mungu na sio tu compilation of 66 books tunalotumia sasa. Kwa maelezo hayo nathani tuko pamoja, Maswali kuhusu bibilia kama compilation ya vitabu vingi hiyo ni mada nyingine mkuu.

 
Back
Top Bottom