Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje, amesema kuwa uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania uliendeshwa kwa utulivu mkubwa katika maeneo mengi, akibainisha kuwa wagombea wote 17 wa Urais hawakuwahi kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais ambapo Dkt. Samia Suluhu Hassan alishinda, wala kudai kuwa kulikuwa na wizi wa kura- jambo analoliona kama hoja muhimu katika mjadala unaoendelea kuhusu uhalali wa matokeo na matukio yaliyofuata.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na TV47 nchini Kenya, Wenje ambaye kwa sasa ni kada wa chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameeleza kuwa kati ya vyama 18 vilivyoshiriki uchaguzi, vyama 17 vilikuwa na wagombea wa Urais ambao hakua yeyote kati yao aliyewasilisha malalamiko ya kupinga matokeo kwa tume wala mahakamani.
"Tulikuwa na wagombea 17 wa Urais. Matokeo yalitolewa na kura tuliona lakini kitu cha muhimu zaidi ni kwamba hawa wagombea wengine wa Urais walikubali kwamba Rais Samia ameshinda na hamna yoyote aliyelalamika na hakuna mtu alipinga matokeo ya Urais"
Akizungumza katika mahojiano maalumu na TV47 nchini Kenya, Wenje ambaye kwa sasa ni kada wa chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameeleza kuwa kati ya vyama 18 vilivyoshiriki uchaguzi, vyama 17 vilikuwa na wagombea wa Urais ambao hakua yeyote kati yao aliyewasilisha malalamiko ya kupinga matokeo kwa tume wala mahakamani.
"Tulikuwa na wagombea 17 wa Urais. Matokeo yalitolewa na kura tuliona lakini kitu cha muhimu zaidi ni kwamba hawa wagombea wengine wa Urais walikubali kwamba Rais Samia ameshinda na hamna yoyote aliyelalamika na hakuna mtu alipinga matokeo ya Urais"