Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,710
- 9,063
Nimekaa nimetafakari sana kuhusu mbwembwe za Rais wetu wakti wa kampeni alivyokuwa akipiga push up mwaka 2015 kwenye majukwaa!!
Push up za JPM ilikuwa kuwashawishi Watz kuwa kazi ya Urais ilikuwa ni rahisi na ataiweza pasipo shaka yoyote!
Lakini cha kushangaza leo mwaka 1 na miezi kadhaa JPM anaonekana kuelemewa na kazi za Ikulu! Rais ameanza kuonyesha dalili za kuchoka na kukata tamaa mapema kuliko Watz walivotazamia!
Angalia matukio yanayofuatana mfululizo ambayo yako kinyume kabisa na Katiba na Sheria za nchi hii!
Kwa kifupi tunaweza sema kuwa kumbe zile push zilikuwa za kuja kupambana na Wapinzani kwa kuwasweka ndani na kuua upinzani! Alipomtumbua Mama Malecela, Waziri Kitwanga, Watumishi hewa na Walioghushi vyeti. Lakini leo kashindwa na kijamaa kidogo kilichozungusha ZERO form 4 na kukiona kama mungumtu wa Darisalama! Hakiguswi,hakikemewi wala kutumbuliwa! Kila anachofanya Bashite kiwe kibaya au kizuri anasifiwa kwa kuambiwa APIGE KAZI! Akivamia Studio za Media Achape Kazi, akisingizia Watu kuwa wana Dawa za kulevya lakini Polisi wakichunguza na kukuta ni uongo, Chapa Kazi maana Hapa ni Kazi Tu!
Media wakiandika na kutangaza kuhusu Migogoro ya Wakulima na Wafugaji ni Uchochezi, wakitangaza kuna Ukame na Njaa ni Uchochezi, wakihoji hela za Tetemeko la Ardhi Kagera kwanini hazikusaidia wahanga, ni Uchochezi! Ukweli ni kwamba Magufuli Ikulu imemchosha bado mapema asubuhi! Tumwombee ili Mungu amtie nguvu.
Push up za JPM ilikuwa kuwashawishi Watz kuwa kazi ya Urais ilikuwa ni rahisi na ataiweza pasipo shaka yoyote!
Lakini cha kushangaza leo mwaka 1 na miezi kadhaa JPM anaonekana kuelemewa na kazi za Ikulu! Rais ameanza kuonyesha dalili za kuchoka na kukata tamaa mapema kuliko Watz walivotazamia!
Angalia matukio yanayofuatana mfululizo ambayo yako kinyume kabisa na Katiba na Sheria za nchi hii!
Kwa kifupi tunaweza sema kuwa kumbe zile push zilikuwa za kuja kupambana na Wapinzani kwa kuwasweka ndani na kuua upinzani! Alipomtumbua Mama Malecela, Waziri Kitwanga, Watumishi hewa na Walioghushi vyeti. Lakini leo kashindwa na kijamaa kidogo kilichozungusha ZERO form 4 na kukiona kama mungumtu wa Darisalama! Hakiguswi,hakikemewi wala kutumbuliwa! Kila anachofanya Bashite kiwe kibaya au kizuri anasifiwa kwa kuambiwa APIGE KAZI! Akivamia Studio za Media Achape Kazi, akisingizia Watu kuwa wana Dawa za kulevya lakini Polisi wakichunguza na kukuta ni uongo, Chapa Kazi maana Hapa ni Kazi Tu!
Media wakiandika na kutangaza kuhusu Migogoro ya Wakulima na Wafugaji ni Uchochezi, wakitangaza kuna Ukame na Njaa ni Uchochezi, wakihoji hela za Tetemeko la Ardhi Kagera kwanini hazikusaidia wahanga, ni Uchochezi! Ukweli ni kwamba Magufuli Ikulu imemchosha bado mapema asubuhi! Tumwombee ili Mungu amtie nguvu.