Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 21,498
- 37,792
Nilidhani nimeona mengi, nimesikia mengi na nimeshuhudia mengi Kwa umri wangu 35+ kumbe bado Nina safari ndefu. Hivi Waliosema kua uyaone walimaanisha ukue Hadi ufikishe miaka mingapi ndo uanze kuyaona hayo waliyotaka tuyaone?
Nimekutana na kioja toka Kwa Profesa mpaka nikasema wazazi wetu zamani hawakututendea haki. Walituaminisha Profesa ni Msomi mkubwa ambaye kazi yake ni kufanya tafiti na kuibua Wasomi wengine. Kwamba Profesa ni incubator ya Wasomi. Ni tanuri la kufua watu watoke wakiwa pure bila purities.
Au hao Maprofesa tuliohadithiwa wako Nchi za dunia ya Kwanza na ya pili huku dunia Nyeusi kuna Mapropesa?
Kweli Propesa wetu ambaye Wasomi wengi wamepita mikononi mwake anatuaminisha dalili kubwa yaa mafanikio ya Nchi kimaendeleo ni Tulia kuwa Rais wa IPU?
Yaani Tulia kuwa Rais wa IPU kunaonyesha mbele ya mataifa kwamba Tanzania Hakuna Ufisadi, nchi haina madeni yaliyotopea, Wananchi hawako kwenye umasikini?
Kwamba Tulia kuwa Rais wa IPU ni dalili kwamba dunia inatuamini Sana kwamba kwetu Hakuna ufujaji wa fedha za Umma na uchumi wetu ni imara?
Maprofesa tuoneeni huruma Sisi tuliodanganywa na Wazee wetu kwamba nyie mna akili Sana na uwezo wenu wa kuchambua Mambo ni wa kiwango cha juu.
Nimekutana na kioja toka Kwa Profesa mpaka nikasema wazazi wetu zamani hawakututendea haki. Walituaminisha Profesa ni Msomi mkubwa ambaye kazi yake ni kufanya tafiti na kuibua Wasomi wengine. Kwamba Profesa ni incubator ya Wasomi. Ni tanuri la kufua watu watoke wakiwa pure bila purities.
Au hao Maprofesa tuliohadithiwa wako Nchi za dunia ya Kwanza na ya pili huku dunia Nyeusi kuna Mapropesa?
Kweli Propesa wetu ambaye Wasomi wengi wamepita mikononi mwake anatuaminisha dalili kubwa yaa mafanikio ya Nchi kimaendeleo ni Tulia kuwa Rais wa IPU?
Yaani Tulia kuwa Rais wa IPU kunaonyesha mbele ya mataifa kwamba Tanzania Hakuna Ufisadi, nchi haina madeni yaliyotopea, Wananchi hawako kwenye umasikini?
Kwamba Tulia kuwa Rais wa IPU ni dalili kwamba dunia inatuamini Sana kwamba kwetu Hakuna ufujaji wa fedha za Umma na uchumi wetu ni imara?
Maprofesa tuoneeni huruma Sisi tuliodanganywa na Wazee wetu kwamba nyie mna akili Sana na uwezo wenu wa kuchambua Mambo ni wa kiwango cha juu.