tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,956
- 25,348
Kuna taarifa kwamba Pinder amewapanga wabunge kadhaa (majina kapuni) wamtetee bungeni leo ili asiende na maji. Kwa kufanikisha utetezi wao wanadai kwamba Pinder hajahusika yeye binafsi katika ufisadi huu bali ni watendaji wa chini yake ndio wanapaswa kuchukuliwa hatua.
Kete ya pili wanayotumia 'watetezi' hawa ni kwamba ikiwa Pinder alihusika kwenye ufisadi huu basi asingeagiza uchunguzi ufanyike. So the guy is clean and innocent.
Aidha, kuna timu kubwa imetumwa kumtetea Pinder kwenye social media, hasa JF, kwa lengo la kuupotosha umma na kuwafanya wananchi wasadiki kwamba Pinder anaonewa bure.
Kisingizio kingine kitakachotumiwa kumsafisha ni uwepo wa makundi ya urais, 2015 yanayochafuana.
Anyway, ngoja tusubiri tuone hao vibaraka wake wamejipangaje kumtetea kwa kuwa naona kama wanatumia hoja mfu kumsafisha mtu ambaye amechafuka kiasi cha kutosafishika tena. Mbivu na mbichi tutazipata leo bungeni wakati utetezi wa serikali (utakaotolewa na Pinder mwenyewe) utakaporindima.
Nawasilisha
:israel:
Kete ya pili wanayotumia 'watetezi' hawa ni kwamba ikiwa Pinder alihusika kwenye ufisadi huu basi asingeagiza uchunguzi ufanyike. So the guy is clean and innocent.
Aidha, kuna timu kubwa imetumwa kumtetea Pinder kwenye social media, hasa JF, kwa lengo la kuupotosha umma na kuwafanya wananchi wasadiki kwamba Pinder anaonewa bure.
Kisingizio kingine kitakachotumiwa kumsafisha ni uwepo wa makundi ya urais, 2015 yanayochafuana.
Anyway, ngoja tusubiri tuone hao vibaraka wake wamejipangaje kumtetea kwa kuwa naona kama wanatumia hoja mfu kumsafisha mtu ambaye amechafuka kiasi cha kutosafishika tena. Mbivu na mbichi tutazipata leo bungeni wakati utetezi wa serikali (utakaotolewa na Pinder mwenyewe) utakaporindima.
Nawasilisha
:israel: