Wanabaraza wenzangu , nimekaa na kutafakuri kwa kina. Nimesoma na kusikiliza wengi humu jamvini. Sasa naomba kuuliza wote wale wanaoshangilia kukamatwa kwa mafisadi, nipeni sababu za msingi za kunifanya name ninyanyue sauti , kalamu na hata key board kuanza kushangilia kufikishwa kwa mafisadi mahakamani. Kwani tumesahahu wahenga wa kale walisema, atushangilii mimba , mpaka mtoto amezaliwa. Vilele atushangilii embe kutoa majani au maua kuashilia mavuno ya embe dodo, kwa kawaida tunashangilia wakati wa mavuno.
Si unajua tena isije ikawa tukabaki vinywa wazi na yale yale ya mbaazi kukosa maua na kusingizia jua.
Narudia tena swali mbona tunashangilia sana majani badala ya matunda? Enzi ya Sokoine tulishangilia kwa sababu justice was seen to be done .Naomba kuelemishwa.
Si unajua tena isije ikawa tukabaki vinywa wazi na yale yale ya mbaazi kukosa maua na kusingizia jua.
Narudia tena swali mbona tunashangilia sana majani badala ya matunda? Enzi ya Sokoine tulishangilia kwa sababu justice was seen to be done .Naomba kuelemishwa.