Enzi za Mwinyi zimeanza kurejea magari ya serikali yamepaki hayana mafuta!

Dumelambegu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
1,052
257
Wazee,
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.

Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.
 
Dume,
Ni kweli kabisa hali ni mbaya kupita maelezo. Binafsi sijawahi kushuhudia hali hii tangu niajiriwe serikalini. Imefika wakati mkurugenzi wetu mmoja anatumia hela yake mfukoni kununua karatasi za kuprintia documents za serikali. Nadhani muda si mrefu nchi itacollapse.
 
Kingcobra, unataka nchi icollapse mara ngapi!!! Ukweli ni kuwa sasa tunaelekea kwenye kiza kizito. Wengi wetu hatuoni mbele.
 
Wazee,
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.

Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.

Mpaka tutakapokubali kupumuliwa kisogoni!
 

Mpaka tutakapokubali kupumuliwa kisogoni!
Halafu hili sharti limetolewa katika wakati mugumu wa nchi yetu na zingine zinazoendela! Nafikiri wameyaona mazingira kuwa yanaruhusu kutoa sharti lolote. Kwa ugumu wa maisha, wasiokuwa wavumilivu lazima wapumuliwe kisogoni mkuu.
 
Hivi za maadhimisho zinatoka wapi? au zinatoka pia mifukoni mwa wakurugenzi, mawaziri na watu binafsi kwenye wizara na idara za serikali?

Kwa hali hii hii nchi iko mahali pasipo salama hata kidogo na kibaya zaidi ni kuwa hakuna juhudi za uhakika zinazochukuliwa na watawala wa nchi hii zaidi ya kupanda ndege kila siku
 
Wametumia pesa Igunga wakakodi chopa wakagawa pesa kama embe mtini,kuna askari jamaa yangu aliniambia palikuwa na pesa haijawahi kutokea...mbali ya hilo pesa iliyobaki wakanunua jengo USA na zingine wamewapa wezi wa Dowans,sasa pesa itoke wapi tena?
 
Wametumia pesa Igunga wakakodi chopa wakagawa pesa kama embe mtini,kuna askari jamaa yangu aliniambia palikuwa na pesa haijawahi kutokea...mbali ya hilo pesa iliyobaki wakanunua jengo USA na zingine wamewapa wezi wa Dowans,sasa pesa itoke wapi tena?
Kama mambo hayo kweli yanafanyika, basi nchi hii haina 'rais' bali ina 'rahisi'.
 
mambo mengi yanakuja..magari yatazimika barabarani bila kusaau kujikausha kuhusu mishahara ya watu.hakika hali itakua mbaya sana.
 
brah brah tu! hamna kazi kila siku kulalama hapa, kwani aliyemchagua jk sio nyie? unafiki mtupu. na bado mtalia sana, mwaka wa kwanza tu huo bado minne. watz sisi mdomo sana ila waoga kama kobe. hivi unakumbuka muswada wa ugaidi ulivyopita fasta fasta? ngoja siku si nyingi na muswada wa haki sawa kuruhusu mashoga utapita tu. ngoja hela ziishe. kwani govt si ni bunge? na bunge si ni ccm? ha ha ha haa! majuhaland !
 
Wazee,
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.

Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.
Habari hizi umezichukua kutoka pale viwanja vya biafra, au pale viwanja vya jangwani tujuze chanzo.
 
Wazee,
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.

Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.


kwani mkuu ulitaka wafanyabiashara wafanye nini na unadhani inawahusu hii kitu ya govt kufilisika? Au una ajenda ya siri gani mpaka kufikia kusema hilo?
 
Habari hizi umezichukua kutoka pale viwanja vya biafra, au pale viwanja vya jangwani tujuze chanzo.
Tatizo unakariri hujui hata chanzo ni nini. Yeye anasema anafanya serikalini na anayaona sasa chanzo ni yeye unataka chanzo gani tena? Au unadhani chanzo lazima kiwe gazeti?

Ukweli nchi ipo rehani. Jk alikuta hela za Mkapa akaziponda bila kufanya kazi. Yeye kusafiri tu sasa matokeo ni hayo
 
kama wamekosa za mtihani kidato cha 2 watapata za mafuta wapo busy na maadhimisho

Maadhimisho pia ni kitendawili kwani hata huo uwanja wenyewe wa kuadhimishia miaka 50 ya Uhuru....uwanja wa kihistoria ...ujenzi wake unasua ......na kuna uwezekano mkubwa usikamilike ndani ya muda kwa ajili ya sherehe hizo....ukata.
 
Msiwe na wasi wasi wakuu, fedha zipo na maisha yataendelea kama kawaida kama kila mtu ataacha kulalamika na kutimiza wajibu wake.
 
Alichoambiwa mkuu Dume ni kweli kabisa, hali ya serikali ni mbaya hasa hii Wizara ya Maji,kwani mimi mwenyewe ni muathirika wa miradi hii ya maji,ofc yetu tulifanya kazi ya facilitation, katika baadhi ya wilaya ya mikoa ya kusini toka mwaka 2008/9 ila hadi sasa sehemu kubwa ya malipo hatujapewa..na ukiuulizia unaambiwa WB walishatoa hizo hela,zilipokwenda hatujui..wacha WAJITOE tu..
 
Kama hali ndiyo hii kwanini wasiondokane na upuuzi huu wa sherehe ya miaka miaka 50 ya Uhuru
wa Tanzania bara? Afterall 9/12/1964 hakukuwa na nchi inayoitwa Tanzania bara, hivyo hawajui
hata wanasherehekea uhuru wa nchi gani? (SIC)
 
Kama hali ndiyo hii kwanini wasiondokane na upuuzi huu wa sherehe ya miaka miaka 50 ya Uhuru
wa Tanzania bara? Afterall 9/12/1964 hakukuwa na nchi inayoitwa Tanzania bara, hivyo hawajui
hata wanasherehekea uhuru wa nchi gani? (SIC)

Please read 9/12/1961 not otherwise!
 
Kama hali ndiyo hii kwanini wasiondokane na upuuzi huu wa sherehe ya miaka miaka 50 ya Uhuru
wa Tanzania bara? Afterall 9/12/1964 hakukuwa na nchi inayoitwa Tanzania bara, hivyo hawajui
hata wanasherehekea uhuru wa nchi gani? (SIC)
Kwa uswahili wa RAHISI wetu itakuwa vigumu kuacha maadhimisho. Si unajua watu wa pwani wanavyopenda minuso?!
 
Back
Top Bottom