Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Wazee,
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.
Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.
Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka takribani 15 ofisi za serikali zimeanza kukosa hata karatasi za kufanyia printing za barua na documents mbalimbali. Kuna mdau mmoja yupo wizara ya maji anasema magari ya wakurugenzi yamepaki miezi kadhaa kutokana na kukosa hela ya kununua mafuta. Mengine yanadaiwa na DT Dobie, Toyota (T) Ltd, n.k. malipo ya matengenezo tangu mwaka jana. Madereva wanaenda ofisini kupiga stori na kusibiri mishahara mwisho wa mwezi. Watumishi wengi wanaenda likizo bila malipo. Mdau aliendelea kunihabarisha kwamba hata programu ya kitaifa ya maji ni kama imesimama na wafadhili wakiwemo wajerumani, waholanzi, benki ya dunia, n.k. wamepanga kujiondoa kwenye programu.
Kama habari hizi ni za kweli, basi kikwete nchi imemshinda na kwa dalili hizi tunarudi kulekule alikotutoa mzee mkapa wakati serikali ilikuwa haina fedha hata za kununua karatasi kwa matumizi ya ofisi. Cha ajabu wakati mambo hayo yakiw mabaya hivyo serikalini, wafanyabiashara wakubwa wanaendelea kuporomosha majengo marefu mijini.