Enzi za Magufuli watu walijenga nyumba, sasa hivi watu wananunua vyakula

Wizara ya fedha wataona aibu kutangaza mapato kwa mwezi maana yatakuwa yameshuka sana eznzi za magu trilion 2 kwa mwezi sasa hivi inaweza kuwa bilion 800hadi trilion 1 tu
Nasikia mwezi wa tatu wamekusanya 500bil na mwezi wa nne 620 bil.
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Hivi una kichaa au? Nyumba zipi unaongelea au za milele? Nahisi unatafutia watu ban humu.
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Naona unaongea vice versa Ila wacha nikujibu kwa jinsi ulivyoandika tufanye ni kweli basi.

In short, watu kwa sasa hawaangalii nyumba kama ndio asset kwa sasa especially mabenki na biashara zimeanza kuwa huru zaidi na mitaji iliyozuiwa na TRA pamoja na wale waporaji kwa sasa inarudi mtaani.

Wengi wanaangalia kutunza mitaji na kuwekeza sababu at least kuna Mwanga wa biashara maana enzi za bwana yule biashara uliyoweza kufanya ni labda uwe MATAGA tu otherwise watakunyang'anya pesa zako.

Nyumba watu waliamua kuhamia hata kama haijaisha sababu pesa ya kodi ilikuwa hakuna, hali ngumu so mtu aliona heri ahamie kwake hata kama ameweka milango ya nje tu huko ndani unaweka mapazia then maisha yanasonga.

Kwa sasa hatujengi tunaangalia biashara so jiandae kuwa na ufundi mzuri sababu hela ukiingia mtaani hatutatumia vibarua kama wewe itakuwa zamu ya maengineer wa nyumba na architect kusimamia mijengo nyie mliokuwa mnalamba mananihii mjiandae kurudi kuchunga mbizi. Jobless.
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Huu wakati watu walijenga , sio kwa sababu ya hela, No ni kwasababu walikuwa hawana uhakika na Kesho yao..
#WakatiWaJkwatuhawakuwaWaoga
 
Wizara ya fedha wataona aibu kutangaza mapato kwa mwezi maana yatakuwa yameshuka sana eznzi za magu trilion 2 kwa mwezi sasa hivi inaweza kuwa bilion 800hadi trilion 1 tu
Mlikuwa mnaaminishw mapato sioni 2 wakati kukusanya trioni 1.
Magufuli keshakufa na uongo wake.
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Wajane wa dhalim wacheni kelele zenu kama vipi mfuateni.
 
kwa mimi, itoshe tu kusema;

1. uongozi ni shida sana nchi hii, ni shida haswaa! usipokuwa na moyo na imani utajinyongeanyongea mambwiga wengi tu maana wanakera sana!!

2. naendelea kujiuliza na kushangaa mbinu au dawa a.k.a 'mzizi' alioutumia mwendazake hadi akafanikiwa kuwashika watu akili kiasi hiki, aisee inanishangaza sana.....nasema dawa kwa sababu si hali ya kawaida hii. nafikiria na mimi kusafiri kuelekea pande hizo nikajipatie dawa ya kuongoza kataasisi kangu haka.
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Wacha hizo! nyumba nyingi zilijegwa awamu ya nne pamoja na mapungufu yake.
Awamu ya tano ujenzi ulishuka sana fedha kwa wananchi zilipatikana za kujikimu kwa chakula tu na si kwa maendeleo na ujenzi wa nyumba.
 
Nyie Mmetesa Watu Sana...Mmeumiza watu sana saiv mnajifanya Malaika..Ni Wapi walijenga?? Mambo yenu yameisha tulieni...
 
Mbona siku chache sana, mlijenga wachache sana, labda wastaafu na traffic, na wakuu wa idara madc, wakuu wa taasisi, magu amesababisha umaskini mkubwa, ni muda tu baada ya kazi kubwa ya mama tutarudi kwanye mstari!
 
Enzi za Magufuli kazi zilikuwa nyingi watu wakajenga Sana ila tokea mama Samia suluhu awe Rais Basi Kasi ya ujenzi imeshuka sana.

Mtu anaona kuliko milioni tano yake aipeleke kwenye mambo ya ujenzi hata Kama Ni kanyumba Cha kupangisha Ni Bora akanunua mazao ya chakula Kama vile ulezi n.k ili yaje yamsaidie baadae maana unaweza ukajenga na still ukabakia maskini Ni heri uweke store vyakula.

Kifupi hali sio hali wakuu tazameni Sana kwa jicho la ukaribu.
Mbona kama kinyume chake?
Naanza kuamiini kuwa awamu ya tano pamoja na ugumu wake kuna watu waliishi peponi.
 
Wizara ya fedha wataona aibu kutangaza mapato kwa mwezi maana yatakuwa yameshuka sana eznzi za magu trilion 2 kwa mwezi sasa hivi inaweza kuwa bilion 800hadi trilion 1 tu
Kama ni pesa halali , haina shida hata kama zimeshuka,
Trilioni mbili zilikuwa machozi jasho na damu ya watanzania wenzako walioshurutishwa kuzitoa kwa nguvu kwa sheria kandamizi na dhulma, mama hazitaki pesa za damu ya watu.
 
Wizara ya fedha wataona aibu kutangaza mapato kwa mwezi maana yatakuwa yameshuka sana eznzi za magu trilion 2 kwa mwezi sasa hivi inaweza kuwa bilion 800hadi trilion 1 tu
Trillion mbili ambayo ilikuwa inaharibu uchumi wa watu,no wawekezaji,kukamua wafanyabiashara hamna kipindi amabcho wafanyabiashara wameteseka Kama kipindi cha magu
 
Ndani ya miezi miwili umeshaanza kuhukumu. Tulia mama ajenge mifumo ya kuboresha maisha ya watu
Kwa namna Hali inavyokwenda sidhani Kama kutakuwa na unafuu kwa wanachi walio wengi...subiri utaona miezi sita ujao...ndipo mtaona kuwa JPM alikuwa genius
 
Pepo mchafu toka
Eeehhh pepo mchafu toka na umfuate Beelzebub mkuu Jiwe haraka.
Nadhindwa hata kukujibu huu uharo wako.
Tangu Ibilisi wenu akate moto Sasa hakuna anayewakodi kwenda kumtilia Mbowe fujo
 
Back
Top Bottom