Enzi Hizo S02

Salama wakuu........

Leo ngoja tumalize weekend kwa kibao kitamu cha Conjests toka kwao DDC Mlimani Park Orchestra wana Sikinde ngoma ya ukae..
Wimbo huu waimbaji wake ni Bennovill Anthony,Fresh Jumbe,Maalim Hamis Kinyasi na Fancis(baadaye Nassir) Lubua..Gitaa la solo lilipigwa na Kassim Mponda 'Bella Chance',gitaa la rhythm lilipigwa naye Abdallah Gama na gitaa la besi lilipigwa na Julius Mzeru.Drums zilikung'utwa na Said Chipelembe,Tumba zilipigwa na Ally Jamwaka,Trumphet zilipulizwa nao Machaku Salum na Ally Yahaya,Saxaphone zilipulizwa na Shaban Lendi,Joseph Bernard na Juma Hassan Town...........

Wimbo unaanza hivi:

Benovilla Anthony: Nimetembea pande nyingi za dunia,mashariki na magharibi jamani eeh,nikatafuta mpenzi mwenye busara ili kujenga
mapenzi ya kweli,
Nimetembea pande nyingi za dunia,mashariki na magharibi jamani eeh,nikatafuta mpenzi mwenye busara ili kujenga
mapenzi ya kweli.

Benovilla Anthony: Na sasa kwako mpenzi,nimefika ukingoni eeeh,sitegemei kupenda mwingine tena zaidi yako weee Conjestaaaaa,
Na sasa kwako mpenzi,nimefika ukingoni eeeh,sitegemei kupenda mwingine tena zaidi yako weee Conjestaaaaa.
aaaaaaaaah Conjesta sitapenda mwingine tena eeeeehhhhhhh.

Na sasa kwako mpenzi,nimefika ukingoni eeeh,sitegemei kupenda mwingine tena zaidi yako weee Conjestaaaaa,
Na sasa kwako mpenzi,nimefika ukingoni eeeh,sitegemei kupenda mwingine tena zaidi yako weee Conjestaaaaa.

Kiitikio(wote): Mtoto mwenye imani Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani,
Mtoto mwenye imani Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani.

Fresh Jumbe: Mapenzi mazito sioni mwingine wala sisikii la yeyote yule ila ni wewe,
Mtoto mwenye imani(ooooh mama ooooh Conje),Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani,
Mapenzi mazito sioni mwingine wala sisikii la yeyote yule ila ni wewe,
Mtoto mwenye imani(ooooh mama ooooh Conje),Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani.

Francis Lubua: Macho yangu na masikio yangu,mawazo yangu ypte ni kwako weeeee....

Kiitikio(wote): Mtoto mwenye imani Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani,
Mtoto mwenye imani Conjesta nimeamua kukupenda wewe pekee duniani.
 

Hii nyimbo kuna kipande mwishoni zinapigwa drums balaa...
dah Ardhi imemeza jama
 

VIP ni moja ya nyimbo nilizokuwa nazikubali Duniani...... U remaind me those days Balantanda! Naikumbuka D'slaam those days tupo wachache hakuna foleni rahaaa tuu DAH!
 

VIP ni moja ya Nyimbo nilizokuwa nazikubali Duniani...... U remaind me those days Balantanda! Naikumbuka D'slaam those days haina foleni tupo Wachacheeee.
 
Jamani mambo kwa soksi duh redio tanzania walikataa kuurekodi kwa maadili ya kipindi hicho.
 
mim nimezaliwa mwishon mwa miaka ya 80 ila popote nikisikia nyimbo za zaman huwa nafurah sana kweli zaman kulikuwa na burudani sio leo
 
Heshima yako mkuu
 
Ahsante Balantanda, nimefurahia Marquis Du Zaire.
 
Wakuu Balantanda na wengine kuna ule wimbo wa Vijana Jazz Wana pamba moto unaoitwa Zainabu ambao katika safu ya waimbaji walikuwa Jerry Nashon"Dudumizi" ,Adam Bakari"sauti ya zege" na Fred Benjamin. Naomba mwenye mashairi na ikiwezekana hata video yake auweke hapa.
 
Kwa bahati nzuri wakina dada wa siku hizi
Ni wazuri sana wakupendeza
Ni wapole sana kama twiga
Duh miaka dahari hiyo dudumizi analalamika humo.
 
the best song of all time
 
the best one mkuu
 
mkuu hii co mchezo
 
Mkuu asante kwa kumbukumbu hizi.
Kuna hii nyimbo ya makumbele no 2 tukumbushe mashairi na kama una audio tafadhali utuwekee.
Nimejaribu kutafuta kwenye mitandao nimeikosa
 
Daa!Nimefurahi sana kukutana na huu uzi.Marquis ilikuwa ndiyo band yenye wapuliza ala za upepo wengi.Lakini kwenye wimbo Karubandika jamaa hao nasikia waligoma kutia ala zao humo.Hii ilikuwa ni kile kilichoitwa ujuaji wa wale ndugu wawili Kasaloo na Kyanga Songa.Lakini kinyume ilivyotegemewa wimbo huu ulibamba sana.Nadhani wimbo huu ulikuwa ni kati ya zile chache ambazo hazikusindikizwa na midomo ya bata.
 
Ogaaah! Kumbe huo wimbo aliimba Nguza Viking daah asee alitsha
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…