Eng. Hersi Saidi: Kampuni haitamiliki mali za Yanga SC

franckkimm

JF-Expert Member
Aug 25, 2016
440
852
Rais wa klabu ya Yanga Eng. Hersi Said kupitia kipindi cha Jahazi kinachorushwa na radio Clouds hapo jana alieleza namna klabu ya Yanga inavyojiandaa kupokea wawekezaji baada ya mabadiliko ya kikatiba kukamilika kwa asilimia 100

Eng. Hersi Said amesema kuwa kwa mujibu wa mabadiliko ya katiba na uendeshaji wa klabu ya Yanga, Rais wa klabu ndiye mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya klabu tofauti na klabu zingine kama Simba ambazo mwenyekiti wa klabu ni mjumbe wa bodi ya wakurugenzi.

“Bodi ya wakurugenzi ina watu tisa [9] Young Africans inapeleka watu watano, kwahiyo uwepo wa Yanga ni mkubwa zaidi kuliko mwekezaji”.

“Rais wa Yanga ndiye mwenyekiti wa bodi, Mangungu ndugu yangu akiingia pale yeye ni mjumbe”.

” Mwekezaji ananunua asilimia 49 lakini analipa mara moja, na atamiliki hizo hisa bila kikomo, iwe ni mmoja au wawili, atakayenunua hisa moja itakuwa ni ya kwake milele mpaka atakapoiuza”.

“Mwanachama wa Yanga atalipia ada yake kila mwaka, kwa muda mrefu mwanachama atakuwa na mchango mkubwa kuliko mwekezaji”.

“Mwanachama amekuwa na mchango wa kuipa nguvu hii timu toka 1935 kuhakikisha kwamba anakwenda uwanjani ananunua jezi”. Eng. Hersi alisema.

Kwa upande mwingine pia Eng. Hersi aliweka wazi namna ambavyo klabu inatengeneza mfumo ambao mwekezaji atakuta muundo bora wa utawala.

“Tunajenga mfumo ambao mwekezaji akija anakuta muundo bora wa utawala, kimapato”.

“Malengo yetu ni kuhakikisha kuwa na timu imara kiuchumi ili yule anayekuja awe na uhakika wa kile anachowekeza kwenye timu”.

“Hivyo tumezingatia sana usalama wa biashara kwa kila ambaye ana nia ya kuwekeza kwenye Klabu yetu”.

“Ili kulinda maslahi ya wawekezaji tumehakikisha kuwa lazima tuwe na Makubaliano ya kimkataba”.

“Vile vile tumelinda maslahi ya Klabu kwa kuhakikisha kuwa kinachopelekwa kwenye kampuni ni nembo na biashara ya timu”.

“Mali zote za Yanga zinabaki kuwa mali ya Yanga na sio mali ya kampuni. Kampuni mpya ya Yanga haitaimiliki Yanga, bali Yanga ndio itamiliki kampuni. Mwekezaji hana haki na mali za klabu kama vile uwanja na majengo".

Source:CloudsFm ( jahazi )

Sent using Jamii Forums mobile app
 
“Rais wa Yanga ndiye mwenyekiti wa bodi, Mangungu ndugu yangu akiingia pale yeye ni mjumbe”.
Hivi huyu Hersi tumpe miaka mingapi pale Yanga? Si tuondoe ukomo kabisa? Au mnasemaje Wananchi?

Kwa ufupi, yeye Hersi ndiye Rais wa Yanga, Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi wa uwekezaji wa mdhamini (ambaye ndiye mwekezaji mtarajiwa)
 
Rais wa klabu ya Yanga Eng. Hersi Said kupitia kipindi cha Jahazi kinachorushwa na radio Clouds hapo jana alieleza namna klabu ya Yanga inavyojiandaa kupokea wawekezaji baada ya mabadiliko ya kikatiba kukamilika kwa asilimia 100

Eng. Hersi Said amesema kuwa kwa mujibu wa mabadiliko ya katiba na uendeshaji wa klabu ya Yanga, Rais wa klabu ndiye mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya klabu tofauti na klabu zingine kama Simba ambazo mwenyekiti wa klabu ni mjumbe wa bodi ya wakurugenzi.

“Bodi ya wakurugenzi ina watu tisa [9] Young Africans inapeleka watu watano, kwahiyo uwepo wa Yanga ni mkubwa zaidi kuliko mwekezaji”.

“Rais wa Yanga ndiye mwenyekiti wa bodi, Mangungu ndugu yangu akiingia pale yeye ni mjumbe”.

” Mwekezaji ananunua asilimia 49 lakini analipa mara moja, na atamiliki hizo hisa bila kikomo, iwe ni mmoja au wawili, atakayenunua hisa moja itakuwa ni ya kwake milele mpaka atakapoiuza”.

“Mwanachama wa Yanga atalipia ada yake kila mwaka, kwa muda mrefu mwanachama atakuwa na mchango mkubwa kuliko mwekezaji”.

“Mwanachama amekuwa na mchango wa kuipa nguvu hii timu toka 1935 kuhakikisha kwamba anakwenda uwanjani ananunua jezi”. Eng. Hersi alisema.

Kwa upande mwingine pia Eng. Hersi aliweka wazi namna ambavyo klabu inatengeneza mfumo ambao mwekezaji atakuta muundo bora wa utawala.

“Tunajenga mfumo ambao mwekezaji akija anakuta muundo bora wa utawala, kimapato”.

“Malengo yetu ni kuhakikisha kuwa na timu imara kiuchumi ili yule anayekuja awe na uhakika wa kile anachowekeza kwenye timu”.

“Hivyo tumezingatia sana usalama wa biashara kwa kila ambaye ana nia ya kuwekeza kwenye Klabu yetu”.

“Ili kulinda maslahi ya wawekezaji tumehakikisha kuwa lazima tuwe na Makubaliano ya kimkataba”.

“Vile vile tumelinda maslahi ya Klabu kwa kuhakikisha kuwa kinachopelekwa kwenye kampuni ni nembo na biashara ya timu”.

“Mali zote za Yanga zinabaki kuwa mali ya Yanga na sio mali ya kampuni. Kampuni mpya ya Yanga haitaimiliki Yanga, bali Yanga ndio itamiliki kampuni. Mwekezaji hana haki na mali za klabu kama vile uwanja na majengo".

Source:CloudsFm ( jahazi )

Sent using Jamii Forums mobile app
hajazungumzia swala la MBAPPE kuja jangwani dirisha kubwa?
by the way huyu msonjo ni mtu haswa
 
Kwa ufupi, yeye Hersi ndiye Rais wa Yanga, Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi wa uwekezaji wa mdhamini (ambaye ndiye mwekezaji mtarajiwa)
Wenye akil wawili FC watashangilia maana hawaoni hili.

Subiri siku akitoka hapo bila kubadili iko kipengele cha katiba halafu anaefata akawa sio mtu wa muwekezaji patanoga.
 
Dah! Yule mwekezaji wa upande wa Mashariki ya mbali alipopewa tu timu kupitia zile bilioni zake hewa; akajimilikisha uwanja wa mazoezi! Na akataka pia kujimilikisha jengo pekee la klabu kwa ujanja ujanja tu!

Asingekuwa yule mzee mwenye busara zake kuificha hati miliki ya jengo; muda huu angekuwa ameshaingia tayari benki na kuvuta mkopo wa biashara zake binafsi, kwa dhamana ya jengo la klabu. Ujanja ujanja tu mwiingi!!

NB:- sijamtaja mtu wala jina la klabu. Kwa hiyo sihitaji kubwekewa hapa na mbwa yoyote yule.
 
Kwa ufupi, yeye Hersi ndiye Rais wa Yanga, Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi wa uwekezaji wa mdhamini (ambaye ndiye mwekezaji mtarajiwa)
Ikimaanisha hamna check n balance, rais hata wajibika kwa bodi. Monarchical leadership -king can do no wrong.
 
Rais wa klabu ya Yanga Eng. Hersi Said kupitia kipindi cha Jahazi kinachorushwa na radio Clouds hapo jana alieleza namna klabu ya Yanga inavyojiandaa kupokea wawekezaji baada ya mabadiliko ya kikatiba kukamilika kwa asilimia 100

Eng. Hersi Said amesema kuwa kwa mujibu wa mabadiliko ya katiba na uendeshaji wa klabu ya Yanga, Rais wa klabu ndiye mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya klabu tofauti na klabu zingine kama Simba ambazo mwenyekiti wa klabu ni mjumbe wa bodi ya wakurugenzi.

“Bodi ya wakurugenzi ina watu tisa [9] Young Africans inapeleka watu watano, kwahiyo uwepo wa Yanga ni mkubwa zaidi kuliko mwekezaji”.

“Rais wa Yanga ndiye mwenyekiti wa bodi, Mangungu ndugu yangu akiingia pale yeye ni mjumbe”.

” Mwekezaji ananunua asilimia 49 lakini analipa mara moja, na atamiliki hizo hisa bila kikomo, iwe ni mmoja au wawili, atakayenunua hisa moja itakuwa ni ya kwake milele mpaka atakapoiuza”.

“Mwanachama wa Yanga atalipia ada yake kila mwaka, kwa muda mrefu mwanachama atakuwa na mchango mkubwa kuliko mwekezaji”.

“Mwanachama amekuwa na mchango wa kuipa nguvu hii timu toka 1935 kuhakikisha kwamba anakwenda uwanjani ananunua jezi”. Eng. Hersi alisema.

Kwa upande mwingine pia Eng. Hersi aliweka wazi namna ambavyo klabu inatengeneza mfumo ambao mwekezaji atakuta muundo bora wa utawala.

“Tunajenga mfumo ambao mwekezaji akija anakuta muundo bora wa utawala, kimapato”.

“Malengo yetu ni kuhakikisha kuwa na timu imara kiuchumi ili yule anayekuja awe na uhakika wa kile anachowekeza kwenye timu”.

“Hivyo tumezingatia sana usalama wa biashara kwa kila ambaye ana nia ya kuwekeza kwenye Klabu yetu”.

“Ili kulinda maslahi ya wawekezaji tumehakikisha kuwa lazima tuwe na Makubaliano ya kimkataba”.

“Vile vile tumelinda maslahi ya Klabu kwa kuhakikisha kuwa kinachopelekwa kwenye kampuni ni nembo na biashara ya timu”.

“Mali zote za Yanga zinabaki kuwa mali ya Yanga na sio mali ya kampuni. Kampuni mpya ya Yanga haitaimiliki Yanga, bali Yanga ndio itamiliki kampuni. Mwekezaji hana haki na mali za klabu kama vile uwanja na majengo".

Source:CloudsFm ( jahazi )

Sent using Jamii Forums mobile app
Ninachoweza kusema ni kuwa Yanga wamechukua Transformation ya Simba kama Learning Document then wamecustomize kupata Document iliyobora zaidi. Hongera zao kwa ujanja huo.
 
Back
Top Bottom