Terrible Teen
JF-Expert Member
- May 1, 2017
- 936
- 2,645
Ndugu wana JF. Mwandishi wa habari ndugu Erick Kabendera leo Novemba 07 alifikishwa tena Mahakamani kwa ajili ya kesi yake kutajwa. Kama ilivyo ada kwa mfumo wetu mbovu wa utoaji haki ni kwamba kesi imehairishwa sababu upelelezi haujakamilika na pia Hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo ameteuliwa kuwa Jaji.
Nikirudi kwenye msingi wa uzi huu, tangu mwanzo kumekuwa na viashiria kuwa mashtaka ya Erick ni ya kubambikiwa hasa kutokana na mazingira ya kukamatwa kwake ambapo wenye mamlaka walikuwa wakibadili sababu kila wakati hadi walipompiga kesi isiyokuwa na dhamana.
Aidha, Erick Kabendera hivi majuzi aliwaagiza mawakili wake kumuomba msamaha mtu yeyote ambaye atakuwa amekwazika sababu ya shughuli zake za uandishi wa habari. Ni dhahiri kuwa mashtaka ya Erick yametokana na kazi yake na ukosoaji kupitia kazi zake.
Maono yangu ni kuwa, Mwenye Mamlaka aliyesababisha Erick afunguliwe mashatka haya amuachie huru ndugu huyu mapema iwezekanvyo kabla ya mwaka kuisha. Vinginevyo anajua nini kilimpata wiki mbili zilizopita. Anajua kuwa Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema alimfanyia alichofanya ili kumkumbusha kuwa naye ni binadamu na ameumbwa kwa nyama. Anajua kuwa kwa zaidi ya masaa 6 haukuwa na fahamu.
Mwisho , nimeona mateso anayopitia Erick leo. Kuna kila dalili anapata ulemavu wa kudumu. Mama yake ni mgonjwa sana. Ila kuna mtu kwa chuki tu anayafanya haya. Jumapili anakaa siti ya mbele kanisani. Namauonya kuwa mwaka huu hautapita kabla Mungu hajafanya uamuzi wake wa moja kwa moja. Mawakili wa Serikali , nawaonya pia mwaka huu hautaisha kabla ya Mungu kuliiinua Taifa lake dhidi ya uonevu.
Nikirudi kwenye msingi wa uzi huu, tangu mwanzo kumekuwa na viashiria kuwa mashtaka ya Erick ni ya kubambikiwa hasa kutokana na mazingira ya kukamatwa kwake ambapo wenye mamlaka walikuwa wakibadili sababu kila wakati hadi walipompiga kesi isiyokuwa na dhamana.
Aidha, Erick Kabendera hivi majuzi aliwaagiza mawakili wake kumuomba msamaha mtu yeyote ambaye atakuwa amekwazika sababu ya shughuli zake za uandishi wa habari. Ni dhahiri kuwa mashtaka ya Erick yametokana na kazi yake na ukosoaji kupitia kazi zake.
Maono yangu ni kuwa, Mwenye Mamlaka aliyesababisha Erick afunguliwe mashatka haya amuachie huru ndugu huyu mapema iwezekanvyo kabla ya mwaka kuisha. Vinginevyo anajua nini kilimpata wiki mbili zilizopita. Anajua kuwa Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema alimfanyia alichofanya ili kumkumbusha kuwa naye ni binadamu na ameumbwa kwa nyama. Anajua kuwa kwa zaidi ya masaa 6 haukuwa na fahamu.
Mwisho , nimeona mateso anayopitia Erick leo. Kuna kila dalili anapata ulemavu wa kudumu. Mama yake ni mgonjwa sana. Ila kuna mtu kwa chuki tu anayafanya haya. Jumapili anakaa siti ya mbele kanisani. Namauonya kuwa mwaka huu hautapita kabla Mungu hajafanya uamuzi wake wa moja kwa moja. Mawakili wa Serikali , nawaonya pia mwaka huu hautaisha kabla ya Mungu kuliiinua Taifa lake dhidi ya uonevu.