Em Naombeni Mwongozo Wenu JF Great Thinkers ...!

Mkuu kindafu,

Thanks much kwa mawazo mazuri, na wengine wote bila kukusahau 'Mzee' kwa na mchango wako hapo juu.

Inshu ni kwamba mtoto ni wa class II na anasomea shule nzuri tu English Medium ambapo kimsingi naweza sema anapata huduma karibu zote muhimu kuanzia usafiri wa school bus kwa kwenda na kurudi kutoka shuleni, breakfast, pamoja na lunch kabla ya kurudishwa nyumbani mchana, japo shule yenyewe ni ya kutwa.

Sasa ni ukweli kabisa kwamba mimi kama mzazi nilijaribu kufanya udadisi kwa mtoto ili kupata kufahamu hiyo pesa anayoombaga huwa ni ya matumizi yepi ya ziada, na ni kwa nini anaombaga sh. 200/- tu na si zaidi kama jinsi na ninyi mlivojaribu ku'raise concern wakuu.

Sasa baada ya kufanya udadisi nlichokuja gundua ni kuwa ile breakfast itolewayo shuleni ninayoilipia kwa term in advance kumbe huwa ni uji pekee bila kitafunwa chochote, japo uji wenyewe ni ule wenye mchanganyiko wa virutubisho, ambao hujulikana maarufu kama 'uji wa ulezi'!

Na nilipoendelea kudadisi zaidi ndipo pia nikagundua ya kwamba, tofauti na jinsi nilivyoielewa mimi ile dhana ya kwamba ni 'strictly prohibited kwa mzazi yeyote kumfungashia mtoto wake chakula cha ziada kutoka nyumbani (cuz, at least that was one of the school's general rules of admission), kumbe pale kwenye school compound huwa kuna kiduka ambacho, aidha ni mradi wa shule (au mradi wa waalimu maybe) ambako ndiko watoto huuziwaga vitafunwa ifikapo muda wa breakfast; yani kwa mana hii ni kwamba, kumbe wakati wengine wanakunywa uji bila vitafunwa, kuna watoto wengine huwa wanakunywa uji na vitafunwa according to sizes of their pockets!

So, tofauti ya kimtazamo inayojitokeza sasa kati yangu mimi na wife wangu ni kuwa, wakati mimi naona ni kumtendea haki mtoto wangu ili asijiskie unyonge na au kutamani watoto wenzie wanapokula good-time, wife wangu yeye anaamini ya kwamba shule ilikuwa na maana nzuri sana ku'provide breakfast ya uji pekee bila vitafunwa kwa watoto wote ili kuleta usawa (uniformity) katika uvaaji, ulaji n.k, na kwa maana hiyo mimi kumpatia mtoto pocket money kwa ajili ya vitafunwa n.k ni kumfundisha mtoto tabia mbaya sana, sasa hii sijui mnaona imekaaje wakuu, maana kwa upande mngine naona wife nae kama ana ka'point' flan vile ... ??

Nawasilisha.

Nadhani hapa tatizo sio wewe, mkeo wala mwanenu. Tatizo ni hiyo shule anayosoma. Ongea na walimu waamue kuwapa watoto commom breakfast (uji and snack or uji pekee) au wasitoe kabisa breakfast hapo shule na kila mzazi amfungashie mwanae snack.

Kumpa mtoto mia mbili, au hata mia tano au hata elfu ni kukubaliana na ukware wa hao walimu kuamua kuwalisha watoto wenu chochote wawapo shuleni bila consent yenu.
 
Eti, hivi ni kweli kwamba kumpatia binti yako "pocket money", let's say Tshs. 200/- (Tshs. Two hundred Only) kila aombapo pindi aondokapo asubuhi kwenda shule ni kumfundisha mtoto tabia mbaya??

Coz, at least that's what she accassionally asks from a father, but is upheld by a mother as impacting "bad-manners" to a babygirl ..."

Mie sioni kama ni tabia mbaya, nakumbuka wakati nasoma nilikuwa nikipewa shilingi 25 kila siku pamoja na nauli ya dala dala na hizi zilikuwa nyingi hata ukitaka kujichana zilikuwa zinatosheleza kabisa na weekend bado ukabaki na pesa za kwenda movie ila kama kwenda kuruka majoka basi ilikuwa inabidi upige bomu lingine ili ukaruke majoka. Kama uwezo unakuruhusu basi ongeza hado 500, 200 kwa sasa ni pesa ndogo sana kwa siku.
 
Hamna ubaya wowote kumpatia mwanao pocket money ila usizidishe sana kiwango yaani badala ya kumpa ile inayomtosheleza kwa siku (kama shilingi 200/=) ukampa elfu kumi hela ya kutumia shuleni kwa siku moja hapo utakuwa unamharibu mwanao. Ipo siku utakuwa huna na mtoto akagoma kwena shule na pia waweza kumfungashia chakula toka hapo nyumbani.
 
Wakati mwengine wanawake wanakuwa wakali kwa watoto wa kike kwa mambo ya kawaida kabisa.
Kama uko vizuri, mpatie 500/= daily.
Mkuu 500.- is on a high side,mimi nashauri mtoto apewe sh 300.- ambayo inatosha kununua mandazi mawili mazuri ya bakhresa.Mtoto hapashwi kuwa starved si sawa,apewe mia tatu na mama aache unoko.
 
Back
Top Bottom