Elimu ya Uraia Tanzania

Elimu ya Uraia Tanzania

Kama huamini, rejea idadi ya kura za chaguzi mbalimbali katika maeneo ambayo angalau vyombo vya habari kama magazeti, redio na tv vinapatikana kirahisi. Mfano mzuri ni uchaguzi wa hivi karibuni jimbo la Igunga jinsi ccm ilivyogaragazwa kwenye vimiji vidogo vidogo kama Igunga mjini.
 
Zamani wakati wa Nyerere UJINGA na UMASKINI walikuwa ni maadui lakini sasa hao ndiyo marafiki wa karibu (maswahiba) wa magamba.
 
Kama huamini, rejea idadi ya kura za chaguzi mbalimbali katika maeneo ambayo angalau vyombo vya habari kama magazeti, redio na tv vinapatikana kirahisi. Mfano mzuri ni uchaguzi wa hivi karibuni jimbo la Igunga jinsi ccm ilivyogaragazwa kwenye vimiji vidogo vidogo kama Igunga mjini.
Ni kweli kabisa. Lakini sasa hivi wahabarishaji si tu vyombo vya habari lakini hata wale ambao wanaufahamu wa uraia kama wanfunzi wa sekondari, wanavyuo na wasomi wengine mbalimbali. Hawa ni mabalozi wazuri sana wauraia huko vijijini kwetu. Lakini tatizo pia linakuwa wengi wetu haturudi vijijini kwetu hivyo watu wengi wanapishana na elimu hiyo.
 
Umbumbumbu wa wanaCCm na sio watanzania wengine.
 
Kwakweli nionavyo hakuna katiba mpya itakayoandikwa tunajidanjanya hawa ccm wameshalewa madaraka cha msingi tuelimishe wananchi kwa ujumla wawe wanajitokeza kupiga kura ili pamoja na hii katiba mbovu washindwe kuiiba. Kwasababu Nchi zetu za kiafrika nyingi hadi damu imwagike ndio watawala wliolewa madaraka washtuke. Simple analysis niliyofanya inaonesya kwamba watu wengi hawapigi kura hasa mijini wanaongea sana lakin siku ya kupiga kura hawaendi
 
Nakusuport kumbuka ari iliyopo hivi sasa ya kuwachukia magamba inatokana na elimu kubwa iliyotolewa na cdm hivo hata kama katiba ikibaki lakini watu wakielimishwa vya kutosha bado uwezekano wakuliondosha hili janga la kitaifa upo mkubwa na cdm ikichukua ichi au wabunge 2015 wakiongezeka ndio tuandike katiba na uhakika kabisa hii katiba itakayoandikwa itakuwa kituko zaidi.
 
Natofautiana na wewe kwa kitu kimoja, hata huko kuzugumzia katiba bado ni elimu ya uraia. Hivyo mimi naona mambo yote yaende pamoja hapo tutakuwa tumepiga ndege wawili kwa jiwe moja. Nakubaliana na wewe kuwa ccm inaweza kuondoka hata kwa katiba hii iliyopo. wananchi watakapo ikataa hao NEC hawezi kuiba kura kwa wingi huo, nao wanapima upepo ukoje. tatizo linalo tukabiri upinzani ni kura za kimajimbo, majimbo yale ccm wanayoshinda ndiko wanatumia kuongeza kura na kupunguza kura za majimbo ya upinzani umeshinda.
 
Watanzania wliowengi hawana elimu ya uraia kuhusiana na siasa. Kuna watu kwa kukosa elimu ya uraia wanadhani ukiwa vyama vya upinzani basi wewe ni adui jambo ambalo linasababisha vurugu kwenye mikutano ya kisiasa. Kuwa chama tofauti si uadui ni tofauti ya kiitikadi. Kama ilivyo dini kila mtu ana uhuru wa kuchagua dini kutokana na imani yake. hivyo serikali, asasi za kiraia, vyama vya siasa na hata mashirika ya dini na yasiyo ya kiserikali yatoe elimu ya uraia ili kulinusuru taifa letu.

Kwa mantiki hiyo basi serikali iache mara moja kutumia nguvu za polisi katika mikutano ya Chadema kwani wao wamekuwa na muda mrefu wa kujirekebisha lakini wameshindwa hivyo waachwe watanzania wasikilize sera za chama mbadala. Wajikite kutekeleza yale waliyoahidi kama wataweza na kama hawawezi wakae pembeni.
 
Nikiangalia kipindi cha minibuzz, watu wanafikiri elimu ya uraia, haki ya kupiga kura itasaidia kuwezesha kupata viongozi bora.
Mimi naungana na mshiriki mmoja ambaye kwake kupiga kura si jambo muhimu.
Kiukweli kama hakuna mfumo wa kuwadhibiti na kuwawajibisha viongozi wetu wawapo madarakani na baada ya kipindi chao cha uongozi, tusitegemee kupata maendeleo na kuweza kujipambanua dhidi ya maadui wetu kama maradhi, umaskini na rushwa.
Maana ya uongozi imeshabadilishwa, badala ya kutumikia, sasa ni kutumia.
Nionavyo mimi tunachohitaji ni jinsi gani viongozi wetu tunawawajibisha baada ya kuwaweka madarakani, hiyo itasaidia kuwadhibiti dhidi ya ufisadi na kutowajibika.
 
Back
Top Bottom