Alloyce PR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 590
- 706
“Tumesoma historia tukafundishwa kuwa asili yetu ni sokwe, na hata katika mitihani unatakiwa kukiri simulizi hilo bila kuhoji. Kwa mwelekeo huo wa kufikiri usioacha nafasi ya tafakuri huru, ungetarajia kweli kupata mvumbuzi au mgunduzi? Badala yake tunazalisha vijana wanaoamini uzungu ni kipimo cha akili na uafrika ni alama ya upungufu.
Elimu ya aina hiyo imelea jamii inayokubali kila kinacholetwa bila kuchambua, jamii inayofuata mkumbo bila utashi. Matokeo yake, wengi hujenga fikra zinazofanana; na yeyote anapothubutu kufikiri tofauti huambiwa: ‘Kama mzungu ameshindwa, wewe utaweza wapi?’ Hapo ndipo tunapopaswa kujiuliza tatizo ni uwezo wetu, au namna tulivyofundishwa kuutazama uwezo huo?”
— Alloyce, P.R.
Elimu ya aina hiyo imelea jamii inayokubali kila kinacholetwa bila kuchambua, jamii inayofuata mkumbo bila utashi. Matokeo yake, wengi hujenga fikra zinazofanana; na yeyote anapothubutu kufikiri tofauti huambiwa: ‘Kama mzungu ameshindwa, wewe utaweza wapi?’ Hapo ndipo tunapopaswa kujiuliza tatizo ni uwezo wetu, au namna tulivyofundishwa kuutazama uwezo huo?”
— Alloyce, P.R.