Elimu ya ujasiriamali: Kuelekea kwenye maendeleo endelevu Tanzania

Tutor B

JF-Expert Member
Jun 11, 2011
9,025
6,554
clip_image002.jpg
ELIMU YA UJASIRIAMALI: KUELEKEA KWENYE MAENDELEO ENDELEVU TANZANIA

Baika – Mr. (March 2018)

1.0. Utangulizi

U

limwengu unabadilika kwa kasi kubwa. Kwa hakika jamii yoyote ambayo haijajiandaa kikamilifu kuendana na kasi ya mabadiliko hayo, kuna uwezekano wa kuwa jamii yenye kutegemea misaada. Jamii hiyo haitakuwa na mbadala zaidi ya kutembeza bakuli kwa ajili ya kuomba chochote. Na cha kusikitisha zaidi, hali hii haitaathiri kizazi kilichopo tu, bali hata kizazi kijacho ambacho hakitakuwa na uwezo wa kulipa madeni yaliyokopwa na baba zao. Kwa hali hiyo, laana ya utamaduni wa kuwa ombaomba itaendelea kuwepo kwa vizazi hadi vizazi kwa kuwa mtoto wa ombaomba ni ombaomba pia.


Uchumi wa dunia unaonesha kuwa nchi nyingi zilizoendelea zimeimarika katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Zinaweza kuamua nini cha kufanya, jinsi ya kufanya na nini cha kufanya lini kwa ajili ya maendeleo yao. Hali hii ni tofauti kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania ambazo bajeti zake kwa zaidi ya asilimia 60 hutegemea kile kinachojulikana kama misaada ya washirika wa maendeleo (wafadhili). Nchi kama hizo hukosa uhuru wa kufanya uamuzi. Nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania kwa mfano, zimejaliwa raslimali ambazo zinaweza kubadilishwa kuwa mali. Lakini suala ni jinsi ya kuzigeuza raslimali hizo ili kuwa vitu halisi. Elimu isiyofaa yenye mapungufu ndiyo kikwazo kikubwa kinachokwamisha kuzibadilisha raslimali hizo kuwa vitu halisi.


Elimu ya Tanzania inasemekana kuwa ni elimu inayowaandaa watu kuwa waajiriwa wa maofisini, japokuwa nafasi za kazi ni chache ukilinganisha na idadi ya watu wanaotafuta kazi za kuajiriwa. Kwa ufupi, elimu yetu haijengi ubunifu na udadisi ambao ungewawezesha watu ama kujiajiri (ujasiriamali) au kuzipanua fursa za ajira ambazo zingewawezesha watu wengi kupata ajira. Fursa za ajira hazijatumiwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha kuweza kuwachukua watu wote wenye sifa za kuajiriwa. Mwasenda Development intervention; ni shirika lisolo la kiserikali (NGO); linaloibua fikra za elimu ya ujasiriamali inayoweza kuibadilisha nchi kutoka kwenye utegemezi na kuwa nchi yenye kujitegemea.



2.0. Maana ya Ujasiriamali

Dhana ya ujasiriamali imeelezwa kwa namna tofautitofauti. Baadhi ya watu hufikiri kuwa ujasiriamali ni kufanya biashara tu. Baadhi wanauangalia ujasiriamali katika muktadha mpana unaohusisha ujuzi na maarifa ya mtu katika kutumia fursa zilizopo. Tranchet na Rienstra, (2009), kwa mfano, wanaelezea dhana ya ujasiriamali kama uwezo binafsi wa mtu wa kubadilisha mawazo na kuwa vitendo.


Ujasiriamali unajumuisha ubunifu, kutengeneza kitu kipya na kuwa tayari kukabiliana na ugumu; vilevile kuwa na uwezo wa kupanga na kuendeleza miradi ili kufikia malengo. Dhana hii humsaidia mtu katika maisha yake ya kila siku akiwa nyumbani na katika jamii. Huwafanya waajiriwa kuwa na uelewa kuhusu muktadha wa kazi zao na kuwa katika nafasi nzuri katika kutumia fursa. Pia ujasiriamali hutoa msingi kwa wajasiriamali kujenga shughuli za kijamii au kibiashara. Olomi, (2009) anakubalina na dhana kuwa ujasiriamali kwa ujumla unaweza kuelezewa kama namna ya kufikiri, kutafakari na kutenda inayosababisha utengenezaji, uimarishaji, utambuzi na ufanyaji mpya wa vitu kwa maslahi ya mtu mmoja mmoja, kikundi cha watu na jamii.



Baadhi huelezea ujasiriamali kwa kutumia sifa za mjasiriamali. Sifa kubwa za mjasiriamali ni pamoja na :

1) Kuwa tayari kupambana na hatari yoyote

2) Huchukua uamuzi mapema na hasubiri tatizo likue

3) Mvumbuzi

4) Mbunifu

5) Mwenye kuleta tija

6) Mwenye kujitegemea

7) Mwenye kutumia fursa zilizopo

8) Mwenye kufikia malengo yake

Kwamba, ujasiriamali ni mtazamo katika akili ya mtu katika kutafuta fursa, kuwa tayari kukabiliana na matatizo na kuwa na uwezo wa kutengeneza faida, kwa kuanzisha ama biashara mpya au kuongeza tija katika taasisi. Ujasiriamali hujumuisha shughuli nyingi ikiwa ni pamoja na kuwa na wazo, kutengeneza na kuendesha biashara. Kwamba mjasiriamali ni mtu anayefikiri kwa ubunifu na uvumbuzi akiwa tayari kukabiliana na hatari inayoweza kusababishwa na fursa zilizopo kwa lengo la kuzalisha faida, ajira na ustawi wa kijamii na kiuchumi. Ujasiriamali siyo lazima uhusishe kuanzisha biashara lakini pia kuleta tija au kubadili utamaduni wa shirika au taasisi. Wajasiriamali huanzisha kampuni ambazo huwa injini katika ukuaji wa uchumi na utengenezaji wa utajiri. Kompyuta, simu za mkononi, mashine za kufulia, ATM, kadi za benki na huduma za usafirishaji ni mifano wa mawazo ya ujasiriamali yaliyobadilishwa kuwa bidhaa au huduma.


3.0. Historia ya Elimu ya Ujasiriamali

Asili ya elimu ya ujasiriamali katika vyuo na vyuo vikuu ilianzia Marekani ambapo kozi ya kwanza ya MBA ilianzishwa mwaka1947 katika Shule Kuu ya Biashara ya Harvard chini ya kichwa cha habari “Uendeshaji wa Biashara Mpya” (Katz 2003). Kuanzia miaka ya 1980 na kuendelea, elimu ya ujasiriamali ilianza kuenea kwanza Ulaya Kaskazini, na kisha kuenea katika sehemu za Ulaya ya Kati na Ulaya ya Kusini katika miaka ya 1990. Elimu ya ujasiriamali baadaye ilienea katika sehemu zingine za dunia. Kimataifa, Amerika ya Kaskazini ndio mfano wa kuigwa katika ustawi wa miradi na pia Amerika ya Kaskazini ni kiongozi katika elimu ya ujasiriamali. Hakuna asiyejua mchango mkubwa wa kiuchumi wa Kampuni ya Microsoft, Amazon, Intel, Cisco au Google na makampuni mengine yenye ustawi mkubwa huko Marekani.


Ukilinganisha na nchi zingine, Marekani ndiyo nchi yenye historia kubwa katika elimu ya ujasiriamali, na pia ndiyo nchi yenye mpangilio, utamaduni na mazingira rafiki ya ujasiriamali kuliko nchi yoyote duniani (Kourilloff, 2000). Nchini Tanzania, elimu ya ujasiriamali haikuwepo enzi za ujamaa wakati wa Azimio la Arusha. Wakati huo Watanzania walisadikishwa kuchukia kila kitu kinachohusiana na ubepari, ujasiriamali ukiwemo. Mjasiriamali alichukuliwa ni kama shetani na alilinganishwa na mnyama katili wa mwituni. Msemo “Ubepari ni Unyama” ulisikika kwenye radio kila baada ya taarifa ya habari. Ujasiriamali uliwavutia tu wale ambao walichukuliwa kuwa ni watu waliopotoka kimaadili. Watumishi wa umma walizuiwa kujishughulisha na biashara (Rutihinda, 2002). Kwa kuwa karibu watumishi wote wa umma walikuwa ni Waafrika, hii ina maanisha kuwa shughuli za kibiashara zilibaki kuwa za Watanzania wenye asili ya Asia pamoja na wale wazawa ambao walikuwa hawana ajira katika ofisi za umma. Watu wa aina hii walikuwa ni wale ambao hawakuwa na kiwango kikubwa cha elimu (Olomi, 2009). Hata hivyo, maendeleo ya hivi karibuni katika ulimwengu, pamoja na sababu za ndani zimeilazimisha nchi kuridhia mabadiliko. Baada ya kuanguka kwa ujamaa na Azimio la Arusha, nchi ilianza kubadilika kimfumo. Mamlaka zinazohusiana na masuala ya elimu zilianza kuiona elimu ya ujasiriamali kuwa ni muhimu kwa maendeleo ya nchi katika miaka ya 2000 katikati. Walianza kuiweka elimu ya ujasiriamali kwenye mihtasari yao.


4.1. Je, Wajasiriamali huzaliwa au hufundishwa?

Watu wamekuwa wakibishana iwapo wajasiriamali hufundishwa au huzaliwa. Baadhi ya watu wanasema kuwa wajasiriamali huzaliwa. Wanasema kwamba hakuna haja ya kuwafundisha au kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali watu kwa sababu mtu huzaliwa akiwa na tabia za kijasiriamali ambazo humfanya awe mjasiriamali moja kwa moja. Wanabainisha kuwa watu wenye tabia au sifa za ujasiriamali hufanya vizuri katika shughuli za kijasiriamali kwa kuwa wana tabia walizozaliwa nazo ambazo hulelewa kupitia elimu rasmi. Wanasema kwamba cha msingi ni kupatikana kwa utamaduni wa kijasiriamali katika jamii husika.


Hata hivyo wengine wanabainisha kuwa ujasiriamali unasomewa. Ujasiriamali si “muujiza’, “si siri’ na hauhusiani na nasaba ya mtu. Ni taaluma. Na kama zilivyo taaluma zingine mtu anaweza kujifunza ujasiriamali”. Hata hivyo swali kuwa mtu anaweza kujifunza ujasiriamali ama la siyo suala la msingi. Kinachohitajika ni utamaduni utakaoufanya uchumi wa taifa ukue (Drucker, 1985). Wajasiriamali waliofanikiwa ni wale wenye elimu ya ujasiriamali. Egeln (2000) anabainisha kuwa utafiti umeonesha kuwa wajasiriamali waliofanikiwa katika Bara la Ulaya ni wale wenye elimu ya kutosha ukilinganisha na wale wasiokuwa na elimu kubwa katika ujasiriamali. Barani Ulaya waanzilishi wengi wa miradi inayohusiana na teknolojia mpya ni wale wenye elimu ya chuo kikuu. Utafiti uliofanyika nchini Ujerumani umeonesha kuwa biashara zilizoanzishwa na watu wenye elimu ya kiwango cha shahada ya kwanza, biashara zao hukua kwa haraka kuliko miradi inayoanzishwa na watu wenye kiwango cha chini ya elimu.

Olomi, (2009) anabainisha kuwa elimu ni muhimu kwa wajasiriamali. Aliona kwamba wale wenye elimu ya ujasiriamali hufanya vizuri katika biashara zao ukiliganisha na wale wasiokuwa na elimu ya ujasiriamali. Anabainisha kuwa wajasiriamali wenye elimu ya ujasiriamali wana uwezo wa kufanya mabadiliko makubwa katika biashara zao ukilinganisha na wale wasiokuwa na elimu ya ujasiriamali. Anahitimisha kwa kusema kwamba katika biashara kitu cha msingi si kiwango cha elimu aliyonayo mtu bali ni uwezo wake wa kutimiza malengo pamoja na ufanisi katika mchakato wa elimu. Tranchet na Rienstra (2009) wanasema kwamba katika nchi nyingi, utamaduni na ukosefu wa uelewa katika ujasiriamali vinaweza kuwa vikwazo katika ubunifu na ukuaji wa uchumi. Kwa kuongeza maarifa na kujenga ujuzi muhimu katika ngazi zote za elimu, kizazi kipya chenye mawazo ya ujasiriamali kinaweza kuubadilisha na kuukuza uchumi wa dunia. Wanafunzi wanaojikita katika fani ya ujasiriamali huwa si watu wa kukubali kila kitu, huwa si watu wenye kujiangalia wao tu, ni watu wenye utayari wa kupambana na hatari yoyote, ni watu wanaokaribisha mabadiliko, wana nguvu katika kiwango cha juu, wana sifa kama zile za wajasiriamali waliofanikiwa (Sexton na Browman, 1985).


Pia, tafiti zinaonesha kuwa wanaojifunza ujasiriamali wana uwezekano mkubwa wa kuanzisha biashara ukilinganisha na wale ambao wanaosoma kozi za biashara. Ulimwengu umekuwa kama kijiji. Ili kuweza kudumu katika utandawazi, mtu anapaswa kuwa na maarifa ya kutosha ili aweze kuishi katika ulimwengu huu. Ulimwengu umeshuhudia mafanikio makubwa katika biashara. Mafanikio hayo yanahusishwa na utamaduni wa watu wake ambao unawahamasisha wajasiriamali kukuza uchumi wa taifa. Kwa maneno mengine, elimu ya ujasiriamali hujenga utamaduni wa kijasiriamali katika akili za watu, na hivyo ni muhimu kwa maendeleo ya jamii husika.



5.0. Malengo ya elimu ya ujasiriamali

Kama ilivyo katika fani zingine, Elimu ya ujasiriamali ina malengo yake. Kwa mfano malengo makuu ya elimu ya ujasiriamali katika vyuo na vyuo vikuu vya Marekani kwa kawaida ni kuendeleza uwezo wa kijasiriamali katika akili za walengwa na kukuza utambuzi wa kijamii katika mikakati inayohusu ujasiriamali (Tume ya Ulaya, 2008). Tanzania imejaliwa raslimali nyingi. Ni kama ndiyo kitovu cha raslimali duniani. Lakini changamoto ni jinsi ya kuzigeuza raslimali hizi ili ziweze kuleta tija na kutumika kama inavyostahili ili ziweze kumnufaisha mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Kushindwa kuzibadili raslimali hizi kunatokana na kuwa na maarifa na ujuzi kidogo katika kutambua nafasi ya elimu ya ujasiriamali. Watu wengi hufikiri kuwa ujasiriamali hauhusiani na elimu: Kwamba kila mtu anaweza kufanya shughuli za kijasiriamali bila kuwa na semina au mafunzo juu ya ujasiriamali. Hii si sahihi.

Malengo ya elimu ya ujasiriamali yanajumuisha:-

a) Mabadiliko katika mtazamo wa watu ili wawe wajasiriamali katika makazi yao.

b) Kutatua tatizo la ajira kwa kuzalisha watengeneza kazi miongoni mwa wasomi,

c) Kugundua na kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla;

d) Kuiona dunia kama fursa na wala si sehemu mbaya ya kuishi.



6.0. Hali ya Elimu ya Ujasiriamali nchini Tanzania

Kama zilivyo nchi zingine ambazo zimepitia hatua mbalimbali katika maendeleo, Tanzania pia imepitia hatua mbalimbali katika mabadiliko ya mfumo. Baada ya miaka saba tu ya uhuru, iliridhia kuwa na mfumo wa ujamaa katika maendeleo yake. Vilevile, mfumo wa elimu ulikuwa wa kijamaa. Nchi ilijenga elimu ya kujitegemea ambapo mtu aliandaliwa kujitegemea katika maisha yake ya baadaye. Kusema kweli, falsafa hii ilikuwa nzuri kwa ustawi wa watu. Kwa kuangalia maudhui ya falsafa, Elimu ya Kujitegemea ililenga katika kuzalisha watengenezaji wa ajira badala ya watafuta ajira ambayo pia ndiyo malengo ya elimu ya ujasiriamali. Hata hivyo, kwa kuwa wafanyabiashara walichukuliwa kama watu waliopotoka kimaadili na hawakuwa na elimu kubwa elimu ya ujasiriamali haikupewa msisitizo. Rutihinda (2002) kwa mfano, amebainisha kwamba nchini Tanzania, enzi za ujamaa, Watanzania walisadikishwa kuchukia karibu kila kitu kinachohusu ubepari, ukabaila, ukaburu n.k. Mjasiriamali alichukuliwa kama shetani na alifananishwa na mnyama mkali wa mwituni. Msemo kama “Ubepari ni Unyama” ulisikika kwenye radio kila baada ya taarifa ya habari. Ujasiriamali ulionekana kufaa kwa wale tu waliopotoka kimaadili ambao wana uelewa mdogo. Watumishi wa umma walipigwa marufuku kujishughulisha na biashara. Baada ya kuanguka kwa mfumo wa ujamaa na elimu ya kujitegemea, Tanzania haikuridhia ujamaa wala ubepari – hapo ndo ulikuwa mwanzo wa anguko la Tanzania kukosa mwelekeo.

Hata hivyo, katiba ya taifa inatamka wazi kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa inayofuata sera ya ujamaa na kujitegemea ingawa kiuhalisia ni nchi ya kibepari. Huduma bora za jamii kama elimu na afya kwa sasa ni za kulipia na siyo bure tena kama zilivyokuwa hapo mwanzoni. Kwamba, hata muundo na maudhui ya elimu yamebadilika kutoka kwenye mfumo wa elimu ya kujitegemea na kuwa kitu kingine katika kipindi hiki cha soko huria na ubinafsishaji. Hakika, sera na mtaala mpya umeandaliwa na kuwekwa kwenye utekelezaji. Kuanzishwa kwa Sera ya Elimu ya Juu, sera ya TEHAMA katika shule za msingi, Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na vya Kati, kwa uchache tu ni mifano bayana ya sera zinazoendana na ubinafsishaji na soko huria.


Sera ya Elimu ya mwaka 1995 ambayo ndiyo mama wa sera zingine zote katika ngazi zote za elimu haisemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Inatilia mkazo maarifa na ujuzi utakaomfanya mlengwa ajitegemee baada ya kumaliza mafunzo yake. Sera ya elimu ya juu inatilia mkazo kuhusu elimu itakayotolewa kwa wanafunzi na ambayo itawapatia maarifa na ujuzi utakaowawezesha kujiajiri. Mihtasari ya vyuo vikuu inatofautiana sana. Hakuna mfanano wa mambo yanayotakiwa kufundishwa katika vyuo vikuu vilivyosajiriwa nchini Tanzania. Kila chuo kikuu huandaa kozi na maudhui kwa kufuata taratibu na falsafa yao. Matokeo yake, kila chuo kikuu hutumia uzoefu wake katika kupanga na kufundisha somo husika. Kwamba kukosekana kwa mfanano juu ya kile ambacho kinatakiwa kufundishwa na jinsi ya kufundishwa, na kile ambacho kimepewa baraka na Tume ya Vyuo Vikuu huzidi kuongeza ukubwa wa tatizo.

Vyuo vikuu vingi hufundisha ujasiriamali. Cha kushangaza, hufundisha ujasiriamali kama mada au mada ndogo ambayo hujumuishwa katika Taaluma ya Maendeleo. Katika vyuo au vyuo vikuu vingine nchini Tanzania ujasiriamali hufundishwa kama somo la hiari! Hata vile vyuo vikuu ambavyo hutoa mafunzo ya uzamili, vyuo vingi hujumuisha ujasiriamali katika shahada ya Uzamili katika Uongozi wa Biashara, lengo likiwa ni kuwapatia wanafunzi utamaduni wa ujasiriamali utakaowawezesha kuongoza taasisi zao kwa kufuata utaratibu wa kijasiriamali.

Pia ujasiriamali hufundishwa kama mada kuu au mada dogo. Hata vile vyuo au vyuo vikuu vichache ambavyo vimeanzisha mafunzo ya shahada za uzamili au stashada za kawaida na za juu katika ujasiriamali vimekuwa vikipanga kozi kwa kufuata utaratibu wao; wakati mwingine vikikosa mwelekeo katika somo. Ndiyo maana baadhi ya vyuo na vyuo vikuu hufundisha ujasiriamali kama mojawapo ya vigezo vya uzalishaji au somo linalohusu uendeshaji wa biashara (biashara za mitaani) tu! Mbaya zaidi, somo hufundishwa na watu ambao hawana maarifa ya kutosha kuhusu somo. Vyuo vikuu vingi huajiri watu wenye shahada za uzamili za MBA ambao hufanya kazi kama wahadhiri wasaidizi. Hawana uelewa kuwa watu wenye shahada za MBA wana elimu ndogo ya ujasiriamali na hivyo wanawanyima wanafunzi haki ya kupata elimu bora ambayo wanastahili kuipata. Katika shule za sekondari hali ni mbaya vilevile. Muhtasari wa elimu ya sekondari hausemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Katika ngazi za juu za elimu ya sekondari, ujasiriamali unachukuliwa kama kigezo cha uzalishaji kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita wanaosoma somo la uchumi. Pia katika Masomo ya Jumla, ujasiriamali hauchukuliwi ama kama mada kuu au mada ndogo. Wanafunzi wengi wa sekondari wanaomaliza elimu yao hawaelewi chochote kuhusu ujasiriamali kama taaluma bali husikia tu kuwa ujasiriamali unahusishwa na biashara ndogondogo za mitaani!

Muhtasari wa Elimu ya Msingi hausemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Huzungumzia kuhusu maarifa ya jamii ambayo yamelenga kuwapatia wanafunzi maarifa na ujuzi wa kuwa wabunifu na wavumbuzi. Hata hivyo walimu wanaofundisha maarifa ya jamii hawana maarifa ya kutosha kuwawezesha wanafunzi wawe wa uwezo wa ziada wa kufikiria. Kwa kawaida wanatilia mkazo katika utengenezaji wa vyungu na upambaji na kazi zingine zinazofanana na hizo na ambazo zimekuwa ndiyo utaratibu wa maisha ya kila siku. Wanakosa mbinu na ujuzi wa kuwafanya wanafunzi wafikirie na kubuni mambo yasiyo ya kawaida. Ukosefu wa elimu ya ujasiriamali kwa shule za msingi ni miongoni mwa sababu za kuandaa watafuta kazi badala ya watengeneza kazi.


7.0. Athari za Kukosekana Msisitizo kuhusu Elimu ya Ujasiriamali

Nguvu ya ujasiriamali imethibitisha kuwa yenye matokeo makubwa katika nchi nyingi ambazo huchukulia elimu ya ujasiriamali kama ndiyo inayotengeneza kazi, injini katika ukuaji wa uchumi na silaha ya kupambana na umasikini kwa uchache tu. Kourilloff (2000) anabainisha kwamba hakuna anayeweza kuhoji mchango mkubwa wa kiuchumi wa kampuni ya Microsoft, Amazon, Intel, Cisco au Google na makampuni mengine makubwa nchini Marekani ambayo ni matokeo ya wajasiriamali. Kwamba kwa kulinganisha na nchi zingine, Marekani ndiyo nchi yenye historia ndefu katika elimu ya ujasiriamali, na pia miongoni mwa nchi zenye utamaduni rafiki juu ya ujasiriamali duniani. Marekani imejipambanua kuwa ni nchi inayoongoza katika ubunifu na uvumbuzi kuliko nchi zote.

Ukweli ni kwamba iwapo nchi haitatilia mkazo elimu ya ujasiriamali itasababisha kuwa na tatizo la ajira, ukuaji mdogo wa uchumi, umasikini na upeo mdogo wa kufikiri kwa watu wake.

Elimu ya ujasiriamali huchangia katika ukuaji wa uchumi. Imegundulika kuwa wajasiriamali wa ndani huchangia kwa kiwango kikubwa katika Pato la Taifa (GDP). Kwa mfano, mtu anapaswa kujiuliza kuhusu mchango wa Makampuni ya IPP au Bakhresa katika uchumi wa taifa hasa kwa kuzingatia mapato ambayo nchi hupata kupitia (kodi) na utengenezaji wa ajira, achilia mbali mchango wa makampuni hayo katika upatikanaji wa huduma za jamii. Iwapo elimu ya ujasiriamali haitatiliwa mkazo, nchi itakuwa tegemezi kwa bidhaa za nje na hivyo kushindwa kupiga vita ujinga, maradhi na umasikini.


8.0. Mahitaji ya Elimu ya Ujasiriamali yenye Ufanisi nchini Tanzania

Elimu ni mchakato usioisha wa kupata ujuzi na maarifa. Mtu anaweza kupata maarifa kwa njia rasmi au isiyo rasmi. Elimu rasmi ni ile tunayoipata kutoka kwenye taasisi za elimu kama vile mashule. Elimu isiyo rasmi ni aina ya elimu ambayo haimlazimu mtu kwenda shule. Inaweza kupatikana muda wowote na popote. Lengo kubwa la elimu ni kutengeneza maisha bora kwa watu. Tunapozungumzia elimu ya ujasiriamali tunamaanisha elimu inayotilia mkazo katika kufikiri kwa ubunifu katika kutumia fursa zilizopo kwa lengo la kutengeneza ajira ambazo husaidia katika ustawi wa kijamii na ukuaji wa uchumi. Hii ndiyo aina ya elimu ambayo inaweza kuyafanya maendeleo ya taifa kuwa endelevu; elimu ambayo MDI tunaitilia mkazo kwa watanzania wote - hasa vijana.


Maendeleo endelevu ni aina ya maendeleo yanayokidhi mahitaji ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho. Ni aina ya maendeleo ambayo hayatikisiki upesi bali yanaweza kudumu na kuhimili vikwazo vya, kijamii, kifikra na kiuchumi. Nchini Tanzania elimu ya ujasiriamali inahitajika sana ili kuzitumia kwa ufanisi fursa na raslimali zilizopo. Tanzania imejaliwa maziwa, mito, bahari, mabwawa, vituo vya utalii n.k. ambayo siyo kwamba yamejaa samaki tu bali yamejaa pia viumbe wengine kama vile viboko, mamba n.k. Nchi imejaliwa ardhi kubwa ambayo haijatumika, misitu na wanyama mwitu na wale wa kufugwa. Pia nchi imejaliwa kuwa na gesi na madini kama vile almasi, dhahabu, Tanzanite, makaa ya mawe kwa uchache tu. Hata hivyo, vitu vyote hivi havijatumiwa kikamilifu ili kuleta maendeleo ya watu. Kwa maneno mengine, tunakosa maarifa na ujuzi wa kiujasiriamali katika kuzibadilisha fursa hizo kuwa maendeleo. Iwapo tunataka maendeleo endelevu lazima tutengeneze/tuandae watu ambao wanaweza:

• Kuendeleza bidhaa zilizopo na kutengeneza bidhaa mpya.

• Kugundua huduma na njia mpya zinazotilia mkazo matumizi halisi katika kiwanda au shirika

• Kugundua na kutumia masoko mapya ambayo kiwanda au shirika halijayatumia

• Kugundua na kutumia nyenzo mpya za utoaji raslimali ambazo hazijawahi kutumika

• Kuwa tayari kupambana na hatari yoyote kwa faida ya nchi

Nchini Tanzania tunahitaji watu ambao wanaweza kuleta tija katika uzalishaji kwenye taasisi au mashirika. Utafiti uliofanyika hivi karibuni umeonesha kwamba huduma za afya nchini Tanzania ni duni sana. Kwa mfano, asilimia 53 ya wagonjwa wanaofika hospitalini huhudumiwa baada ya kusubiri kwa muda wa masaa mawili au matatu na asilimia 19 ya wagonjwa ambao hufikishwa hospitalini huombwa rushwa. Haya yote hutokea kutokana na kukosekana kwa elimu ya ujasiriamali. Hawaijali raslimali watu na wanadhani kuwa uzalishaji unaweza kupatikana kwa njia ya hongo. Ili kuleta ufanisi na tija katika upatikanaji wa huduma na bidhaa, taasisi au shirika lolote linapaswa kuwajumuisha wajasiriamali ambao wanaweza kuleta tija kwenye huduma na bidhaa kwa lengo la kuongeza uzalishaji.



Pia tumeshuhudia kushuka kwa ubora wa elimu kunakoendana na matokeo yasiyoridhisha kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini Tanzania. Mengi yamesemwa kuhusu suala hilo. Mambo hayo yanajumuisha miundombinu isiyoridhisha na vifaa visivyoridhisha vya kufundishia na kujifunzia. Hata hivyo kuna sababu nyingine ambayo huwa tunaisahau. Sababu yenyewe ni kwamba tunakosa ubunifu na uvumbuzi miongoni mwa walimu na wanafunzi katika michakato ya ujifunzaji na ufundishaji. Wanatumia njia za zamani za ufundishaji na ujifunzaji. Juhudi za kugundua njia mpya za ufundishaji na ujifunzaji ni ndogo. Kinachosababisha hali hii ni ukosefu wa utamaduni wa kijasiriamali ambao unaweza kubadili mtazamo wa mtu katika kukabiliana na ulimwengu. Wakati walimu na wanafunzi katika nchi zingine wakijaribu kuvumbua na kubuni njia mpya za ujifunzaji na ufundishaji, sisi bado tunashikilia njia za zamani za ujifunzaji, ufundishaji na upimaji wa wanafunzi wetu. Matokeo yake, baadhi ya wanafunzi (wakati mwingine, kwa kushirikiana na walimu wao) wanafanya udanganyifu katika mitihani.


Pia ukweli uliodhahiri ni kwamba kutokujua kusoma na kuandika kunaongezeka. Kwa mfano, kulikuwa na wanafunzi 308 wa Kidato cha Kwanza wasiojua kusoma na kuandika katika kata ya Nansimo katika wilaya ya Bunda. Pia, mkoa wa Arusha unaongoza katika udanganyifu kwenye mitihani. Unaongoza kwa asilimia 48. Pia ilibainika kwamba ni asilimia 14 tu ya wahitimu wa shule za msingi walifaulu mtihani wa hisabati mwaka jana. Hali hii kwa mujibu wa utafiti ilitokana na ukosefu wa uvumbuzi na ubunifu miongoni mwa walimu wa hisabati katika kulifanya somo hilo lieleweke vizuri. Pia ukosefu wa mbinu zinazowapatia wanafunzi motisha ya kulipenda somo la hisabati huchangia katika ufaulu duni wa wanafunzi. Iwapo walimu wangefundishwa kuhusu ujasiriamali (ujasiriamali wa mashirika), hali hii ingekuwa imepungua kama siyo kuondolewa kabisa.


9.0. Nini kifanyike?

Ili kuwa na elimu ya ujasiriamali yenye ufanisi kwa ajili ya maendeleo endelevu ya mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla, mambo yafuatayo inabidi yafanyike:

• Mihtasari/programu na moduli za elimu ya ujasiriamali ni lazima ziwe na malengo ya kuendeleza ari ya ujasiriamali kwa wanafunzi (kujenga motisha na ufahamu). Hii inajumuisha kuendeleza uwezo wa kijasiriamali ili kuweza kubainisha na kutumia fursa zilizopo, kuwapatia wanafunzi ujuzi unaohitajika katika kuanzisha biashara na kuziendesha ili zikue. Katika hali hizi zote, ni muhimu kuwahamasisha wanafunzi ili waweze kufikiri na kutenda kama wajasiriamali na pia ili wawe wenye kuwajibika kimaadili na kijamii.

• Ujasiriamali ni sharti ufundishwe na wataalamu ambao wanafahamu jinsi ya kulifundisha somo hili. Inapaswa kufahamika kwamba ujarisiarimali ni vitendo na kwamba ili kuwapatia motisha wanafunzi, njia/mbinu mbalimbali za kufundishia inabidi zitumike. Kwa mfano, ni muhimu somo la ujasiriamali lifundishwe na wajasiriamali wenye moyo wa kufanya hivyo. Mbinu ya kuiga ni muhimu zaidi katika ufundishaji wa ujasiriamali kwa sababu watu hupenda kumsikiliza yule wanayemwamini na yule aliyefanya kitu kwenye jamii.

· Shule ni sharti zifungamanishwe na kazi. Uhusiano huu wa shule na kazi husaidia kupunguza matarajio ya kazi kwa vijana na pia husaidia kupunguza tatizo la ajira kwa wasomi walioajiriwa na wale wasio na ajira.


10.0. Hitimisho

Elimu ya ujasiriamali si ya zamani kama zilivyo fani nyingine kama vile sayansi ya siasa, falsafa na sosholojia, lakini ujasiriamali umeleta mabadiliko makubwa tangu kuanza kwake. Kompyuta, mashine za ATM, simu za mikononi, kwa uchache tu ni bidhaa zinazotokana na ujasiriamali. Ijapokuwa mtu anaweza kuwa na sifa za ujasiriamali, ni sharti afundishwe somo hilo ili kumpatia maarifa na ujuzi wa kushindana katika ulimwengu kwa ujumla wake. Ufundishaji makini wa ujasiriamali utawezesha kupatikana kwa maendeleo endelevu na hivyo kuwawezesha watu kuwa na maisha mazuri katika nchi zao.

MDI inafanya kazi ili kuleta ubora wa afya, elimu na kuimarisha maisha ya binadamu kwa kuziwezesha jamii kubadili mtazamo wa kifikra na ushawishi katika utengenezaji wa sera, kuibua mijadala yenye kuleta mabadiliko chanya, kufanya utafiti yakinifu, uchambuzi na utetezi wa sera, na kushirikiana na washirika katika kuendeleza maslahi ya jamii kwa ujumla.
 
clip_image002.jpg
ELIMU YA UJASIRIAMALI: KUELEKEA KWENYE MAENDELEO ENDELEVU TANZANIA

Baika – Mr. (March 2018)

1.0. Utangulizi

U

limwengu unabadilika kwa kasi kubwa. Kwa hakika jamii yoyote ambayo haijajiandaa kikamilifu kuendana na kasi ya mabadiliko hayo, kuna uwezekano wa kuwa jamii yenye kutegemea misaada. Jamii hiyo haitakuwa na mbadala zaidi ya kutembeza bakuli kwa ajili ya kuomba chochote. Na cha kusikitisha zaidi, hali hii haitaathiri kizazi kilichopo tu, bali hata kizazi kijacho ambacho hakitakuwa na uwezo wa kulipa madeni yaliyokopwa na baba zao. Kwa hali hiyo, laana ya utamaduni wa kuwa ombaomba itaendelea kuwepo kwa vizazi hadi vizazi kwa kuwa mtoto wa ombaomba ni ombaomba pia.


Uchumi wa dunia unaonesha kuwa nchi nyingi zilizoendelea zimeimarika katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Zinaweza kuamua nini cha kufanya, jinsi ya kufanya na nini cha kufanya lini kwa ajili ya maendeleo yao. Hali hii ni tofauti kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania ambazo bajeti zake kwa zaidi ya asilimia 60 hutegemea kile kinachojulikana kama misaada ya washirika wa maendeleo (wafadhili). Nchi kama hizo hukosa uhuru wa kufanya uamuzi. Nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania kwa mfano, zimejaliwa raslimali ambazo zinaweza kubadilishwa kuwa mali. Lakini suala ni jinsi ya kuzigeuza raslimali hizo ili kuwa vitu halisi. Elimu isiyofaa yenye mapungufu ndiyo kikwazo kikubwa kinachokwamisha kuzibadilisha raslimali hizo kuwa vitu halisi.


Elimu ya Tanzania inasemekana kuwa ni elimu inayowaandaa watu kuwa waajiriwa wa maofisini, japokuwa nafasi za kazi ni chache ukilinganisha na idadi ya watu wanaotafuta kazi za kuajiriwa. Kwa ufupi, elimu yetu haijengi ubunifu na udadisi ambao ungewawezesha watu ama kujiajiri (ujasiriamali) au kuzipanua fursa za ajira ambazo zingewawezesha watu wengi kupata ajira. Fursa za ajira hazijatumiwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha kuweza kuwachukua watu wote wenye sifa za kuajiriwa. Mwasenda Development intervention; ni shirika lisolo la kiserikali (NGO); linaloibua fikra za elimu ya ujasiriamali inayoweza kuibadilisha nchi kutoka kwenye utegemezi na kuwa nchi yenye kujitegemea.



2.0. Maana ya Ujasiriamali

Dhana ya ujasiriamali imeelezwa kwa namna tofautitofauti. Baadhi ya watu hufikiri kuwa ujasiriamali ni kufanya biashara tu. Baadhi wanauangalia ujasiriamali katika muktadha mpana unaohusisha ujuzi na maarifa ya mtu katika kutumia fursa zilizopo. Tranchet na Rienstra, (2009), kwa mfano, wanaelezea dhana ya ujasiriamali kama uwezo binafsi wa mtu wa kubadilisha mawazo na kuwa vitendo.


Ujasiriamali unajumuisha ubunifu, kutengeneza kitu kipya na kuwa tayari kukabiliana na ugumu; vilevile kuwa na uwezo wa kupanga na kuendeleza miradi ili kufikia malengo. Dhana hii humsaidia mtu katika maisha yake ya kila siku akiwa nyumbani na katika jamii. Huwafanya waajiriwa kuwa na uelewa kuhusu muktadha wa kazi zao na kuwa katika nafasi nzuri katika kutumia fursa. Pia ujasiriamali hutoa msingi kwa wajasiriamali kujenga shughuli za kijamii au kibiashara. Olomi, (2009) anakubalina na dhana kuwa ujasiriamali kwa ujumla unaweza kuelezewa kama namna ya kufikiri, kutafakari na kutenda inayosababisha utengenezaji, uimarishaji, utambuzi na ufanyaji mpya wa vitu kwa maslahi ya mtu mmoja mmoja, kikundi cha watu na jamii.



Baadhi huelezea ujasiriamali kwa kutumia sifa za mjasiriamali. Sifa kubwa za mjasiriamali ni pamoja na :

1) Kuwa tayari kupambana na hatari yoyote

2) Huchukua uamuzi mapema na hasubiri tatizo likue

3) Mvumbuzi

4) Mbunifu

5) Mwenye kuleta tija

6) Mwenye kujitegemea

7) Mwenye kutumia fursa zilizopo

8) Mwenye kufikia malengo yake

Kwamba, ujasiriamali ni mtazamo katika akili ya mtu katika kutafuta fursa, kuwa tayari kukabiliana na matatizo na kuwa na uwezo wa kutengeneza faida, kwa kuanzisha ama biashara mpya au kuongeza tija katika taasisi. Ujasiriamali hujumuisha shughuli nyingi ikiwa ni pamoja na kuwa na wazo, kutengeneza na kuendesha biashara. Kwamba mjasiriamali ni mtu anayefikiri kwa ubunifu na uvumbuzi akiwa tayari kukabiliana na hatari inayoweza kusababishwa na fursa zilizopo kwa lengo la kuzalisha faida, ajira na ustawi wa kijamii na kiuchumi. Ujasiriamali siyo lazima uhusishe kuanzisha biashara lakini pia kuleta tija au kubadili utamaduni wa shirika au taasisi. Wajasiriamali huanzisha kampuni ambazo huwa injini katika ukuaji wa uchumi na utengenezaji wa utajiri. Kompyuta, simu za mkononi, mashine za kufulia, ATM, kadi za benki na huduma za usafirishaji ni mifano wa mawazo ya ujasiriamali yaliyobadilishwa kuwa bidhaa au huduma.


3.0. Historia ya Elimu ya Ujasiriamali

Asili ya elimu ya ujasiriamali katika vyuo na vyuo vikuu ilianzia Marekani ambapo kozi ya kwanza ya MBA ilianzishwa mwaka1947 katika Shule Kuu ya Biashara ya Harvard chini ya kichwa cha habari “Uendeshaji wa Biashara Mpya” (Katz 2003). Kuanzia miaka ya 1980 na kuendelea, elimu ya ujasiriamali ilianza kuenea kwanza Ulaya Kaskazini, na kisha kuenea katika sehemu za Ulaya ya Kati na Ulaya ya Kusini katika miaka ya 1990. Elimu ya ujasiriamali baadaye ilienea katika sehemu zingine za dunia. Kimataifa, Amerika ya Kaskazini ndio mfano wa kuigwa katika ustawi wa miradi na pia Amerika ya Kaskazini ni kiongozi katika elimu ya ujasiriamali. Hakuna asiyejua mchango mkubwa wa kiuchumi wa Kampuni ya Microsoft, Amazon, Intel, Cisco au Google na makampuni mengine yenye ustawi mkubwa huko Marekani.


Ukilinganisha na nchi zingine, Marekani ndiyo nchi yenye historia kubwa katika elimu ya ujasiriamali, na pia ndiyo nchi yenye mpangilio, utamaduni na mazingira rafiki ya ujasiriamali kuliko nchi yoyote duniani (Kourilloff, 2000). Nchini Tanzania, elimu ya ujasiriamali haikuwepo enzi za ujamaa wakati wa Azimio la Arusha. Wakati huo Watanzania walisadikishwa kuchukia kila kitu kinachohusiana na ubepari, ujasiriamali ukiwemo. Mjasiriamali alichukuliwa ni kama shetani na alilinganishwa na mnyama katili wa mwituni. Msemo “Ubepari ni Unyama” ulisikika kwenye radio kila baada ya taarifa ya habari. Ujasiriamali uliwavutia tu wale ambao walichukuliwa kuwa ni watu waliopotoka kimaadili. Watumishi wa umma walizuiwa kujishughulisha na biashara (Rutihinda, 2002). Kwa kuwa karibu watumishi wote wa umma walikuwa ni Waafrika, hii ina maanisha kuwa shughuli za kibiashara zilibaki kuwa za Watanzania wenye asili ya Asia pamoja na wale wazawa ambao walikuwa hawana ajira katika ofisi za umma. Watu wa aina hii walikuwa ni wale ambao hawakuwa na kiwango kikubwa cha elimu (Olomi, 2009). Hata hivyo, maendeleo ya hivi karibuni katika ulimwengu, pamoja na sababu za ndani zimeilazimisha nchi kuridhia mabadiliko. Baada ya kuanguka kwa ujamaa na Azimio la Arusha, nchi ilianza kubadilika kimfumo. Mamlaka zinazohusiana na masuala ya elimu zilianza kuiona elimu ya ujasiriamali kuwa ni muhimu kwa maendeleo ya nchi katika miaka ya 2000 katikati. Walianza kuiweka elimu ya ujasiriamali kwenye mihtasari yao.


4.1. Je, Wajasiriamali huzaliwa au hufundishwa?

Watu wamekuwa wakibishana iwapo wajasiriamali hufundishwa au huzaliwa. Baadhi ya watu wanasema kuwa wajasiriamali huzaliwa. Wanasema kwamba hakuna haja ya kuwafundisha au kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali watu kwa sababu mtu huzaliwa akiwa na tabia za kijasiriamali ambazo humfanya awe mjasiriamali moja kwa moja. Wanabainisha kuwa watu wenye tabia au sifa za ujasiriamali hufanya vizuri katika shughuli za kijasiriamali kwa kuwa wana tabia walizozaliwa nazo ambazo hulelewa kupitia elimu rasmi. Wanasema kwamba cha msingi ni kupatikana kwa utamaduni wa kijasiriamali katika jamii husika.


Hata hivyo wengine wanabainisha kuwa ujasiriamali unasomewa. Ujasiriamali si “muujiza’, “si siri’ na hauhusiani na nasaba ya mtu. Ni taaluma. Na kama zilivyo taaluma zingine mtu anaweza kujifunza ujasiriamali”. Hata hivyo swali kuwa mtu anaweza kujifunza ujasiriamali ama la siyo suala la msingi. Kinachohitajika ni utamaduni utakaoufanya uchumi wa taifa ukue (Drucker, 1985). Wajasiriamali waliofanikiwa ni wale wenye elimu ya ujasiriamali. Egeln (2000) anabainisha kuwa utafiti umeonesha kuwa wajasiriamali waliofanikiwa katika Bara la Ulaya ni wale wenye elimu ya kutosha ukilinganisha na wale wasiokuwa na elimu kubwa katika ujasiriamali. Barani Ulaya waanzilishi wengi wa miradi inayohusiana na teknolojia mpya ni wale wenye elimu ya chuo kikuu. Utafiti uliofanyika nchini Ujerumani umeonesha kuwa biashara zilizoanzishwa na watu wenye elimu ya kiwango cha shahada ya kwanza, biashara zao hukua kwa haraka kuliko miradi inayoanzishwa na watu wenye kiwango cha chini ya elimu.

Olomi, (2009) anabainisha kuwa elimu ni muhimu kwa wajasiriamali. Aliona kwamba wale wenye elimu ya ujasiriamali hufanya vizuri katika biashara zao ukiliganisha na wale wasiokuwa na elimu ya ujasiriamali. Anabainisha kuwa wajasiriamali wenye elimu ya ujasiriamali wana uwezo wa kufanya mabadiliko makubwa katika biashara zao ukilinganisha na wale wasiokuwa na elimu ya ujasiriamali. Anahitimisha kwa kusema kwamba katika biashara kitu cha msingi si kiwango cha elimu aliyonayo mtu bali ni uwezo wake wa kutimiza malengo pamoja na ufanisi katika mchakato wa elimu. Tranchet na Rienstra (2009) wanasema kwamba katika nchi nyingi, utamaduni na ukosefu wa uelewa katika ujasiriamali vinaweza kuwa vikwazo katika ubunifu na ukuaji wa uchumi. Kwa kuongeza maarifa na kujenga ujuzi muhimu katika ngazi zote za elimu, kizazi kipya chenye mawazo ya ujasiriamali kinaweza kuubadilisha na kuukuza uchumi wa dunia. Wanafunzi wanaojikita katika fani ya ujasiriamali huwa si watu wa kukubali kila kitu, huwa si watu wenye kujiangalia wao tu, ni watu wenye utayari wa kupambana na hatari yoyote, ni watu wanaokaribisha mabadiliko, wana nguvu katika kiwango cha juu, wana sifa kama zile za wajasiriamali waliofanikiwa (Sexton na Browman, 1985).


Pia, tafiti zinaonesha kuwa wanaojifunza ujasiriamali wana uwezekano mkubwa wa kuanzisha biashara ukilinganisha na wale ambao wanaosoma kozi za biashara. Ulimwengu umekuwa kama kijiji. Ili kuweza kudumu katika utandawazi, mtu anapaswa kuwa na maarifa ya kutosha ili aweze kuishi katika ulimwengu huu. Ulimwengu umeshuhudia mafanikio makubwa katika biashara. Mafanikio hayo yanahusishwa na utamaduni wa watu wake ambao unawahamasisha wajasiriamali kukuza uchumi wa taifa. Kwa maneno mengine, elimu ya ujasiriamali hujenga utamaduni wa kijasiriamali katika akili za watu, na hivyo ni muhimu kwa maendeleo ya jamii husika.



5.0. Malengo ya elimu ya ujasiriamali

Kama ilivyo katika fani zingine, Elimu ya ujasiriamali ina malengo yake. Kwa mfano malengo makuu ya elimu ya ujasiriamali katika vyuo na vyuo vikuu vya Marekani kwa kawaida ni kuendeleza uwezo wa kijasiriamali katika akili za walengwa na kukuza utambuzi wa kijamii katika mikakati inayohusu ujasiriamali (Tume ya Ulaya, 2008). Tanzania imejaliwa raslimali nyingi. Ni kama ndiyo kitovu cha raslimali duniani. Lakini changamoto ni jinsi ya kuzigeuza raslimali hizi ili ziweze kuleta tija na kutumika kama inavyostahili ili ziweze kumnufaisha mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Kushindwa kuzibadili raslimali hizi kunatokana na kuwa na maarifa na ujuzi kidogo katika kutambua nafasi ya elimu ya ujasiriamali. Watu wengi hufikiri kuwa ujasiriamali hauhusiani na elimu: Kwamba kila mtu anaweza kufanya shughuli za kijasiriamali bila kuwa na semina au mafunzo juu ya ujasiriamali. Hii si sahihi.

Malengo ya elimu ya ujasiriamali yanajumuisha:-

a) Mabadiliko katika mtazamo wa watu ili wawe wajasiriamali katika makazi yao.

b) Kutatua tatizo la ajira kwa kuzalisha watengeneza kazi miongoni mwa wasomi,

c) Kugundua na kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla;

d) Kuiona dunia kama fursa na wala si sehemu mbaya ya kuishi.



6.0. Hali ya Elimu ya Ujasiriamali nchini Tanzania

Kama zilivyo nchi zingine ambazo zimepitia hatua mbalimbali katika maendeleo, Tanzania pia imepitia hatua mbalimbali katika mabadiliko ya mfumo. Baada ya miaka saba tu ya uhuru, iliridhia kuwa na mfumo wa ujamaa katika maendeleo yake. Vilevile, mfumo wa elimu ulikuwa wa kijamaa. Nchi ilijenga elimu ya kujitegemea ambapo mtu aliandaliwa kujitegemea katika maisha yake ya baadaye. Kusema kweli, falsafa hii ilikuwa nzuri kwa ustawi wa watu. Kwa kuangalia maudhui ya falsafa, Elimu ya Kujitegemea ililenga katika kuzalisha watengenezaji wa ajira badala ya watafuta ajira ambayo pia ndiyo malengo ya elimu ya ujasiriamali. Hata hivyo, kwa kuwa wafanyabiashara walichukuliwa kama watu waliopotoka kimaadili na hawakuwa na elimu kubwa elimu ya ujasiriamali haikupewa msisitizo. Rutihinda (2002) kwa mfano, amebainisha kwamba nchini Tanzania, enzi za ujamaa, Watanzania walisadikishwa kuchukia karibu kila kitu kinachohusu ubepari, ukabaila, ukaburu n.k. Mjasiriamali alichukuliwa kama shetani na alifananishwa na mnyama mkali wa mwituni. Msemo kama “Ubepari ni Unyama” ulisikika kwenye radio kila baada ya taarifa ya habari. Ujasiriamali ulionekana kufaa kwa wale tu waliopotoka kimaadili ambao wana uelewa mdogo. Watumishi wa umma walipigwa marufuku kujishughulisha na biashara. Baada ya kuanguka kwa mfumo wa ujamaa na elimu ya kujitegemea, Tanzania haikuridhia ujamaa wala ubepari – hapo ndo ulikuwa mwanzo wa anguko la Tanzania kukosa mwelekeo.

Hata hivyo, katiba ya taifa inatamka wazi kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa inayofuata sera ya ujamaa na kujitegemea ingawa kiuhalisia ni nchi ya kibepari. Huduma bora za jamii kama elimu na afya kwa sasa ni za kulipia na siyo bure tena kama zilivyokuwa hapo mwanzoni. Kwamba, hata muundo na maudhui ya elimu yamebadilika kutoka kwenye mfumo wa elimu ya kujitegemea na kuwa kitu kingine katika kipindi hiki cha soko huria na ubinafsishaji. Hakika, sera na mtaala mpya umeandaliwa na kuwekwa kwenye utekelezaji. Kuanzishwa kwa Sera ya Elimu ya Juu, sera ya TEHAMA katika shule za msingi, Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na vya Kati, kwa uchache tu ni mifano bayana ya sera zinazoendana na ubinafsishaji na soko huria.


Sera ya Elimu ya mwaka 1995 ambayo ndiyo mama wa sera zingine zote katika ngazi zote za elimu haisemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Inatilia mkazo maarifa na ujuzi utakaomfanya mlengwa ajitegemee baada ya kumaliza mafunzo yake. Sera ya elimu ya juu inatilia mkazo kuhusu elimu itakayotolewa kwa wanafunzi na ambayo itawapatia maarifa na ujuzi utakaowawezesha kujiajiri. Mihtasari ya vyuo vikuu inatofautiana sana. Hakuna mfanano wa mambo yanayotakiwa kufundishwa katika vyuo vikuu vilivyosajiriwa nchini Tanzania. Kila chuo kikuu huandaa kozi na maudhui kwa kufuata taratibu na falsafa yao. Matokeo yake, kila chuo kikuu hutumia uzoefu wake katika kupanga na kufundisha somo husika. Kwamba kukosekana kwa mfanano juu ya kile ambacho kinatakiwa kufundishwa na jinsi ya kufundishwa, na kile ambacho kimepewa baraka na Tume ya Vyuo Vikuu huzidi kuongeza ukubwa wa tatizo.

Vyuo vikuu vingi hufundisha ujasiriamali. Cha kushangaza, hufundisha ujasiriamali kama mada au mada ndogo ambayo hujumuishwa katika Taaluma ya Maendeleo. Katika vyuo au vyuo vikuu vingine nchini Tanzania ujasiriamali hufundishwa kama somo la hiari! Hata vile vyuo vikuu ambavyo hutoa mafunzo ya uzamili, vyuo vingi hujumuisha ujasiriamali katika shahada ya Uzamili katika Uongozi wa Biashara, lengo likiwa ni kuwapatia wanafunzi utamaduni wa ujasiriamali utakaowawezesha kuongoza taasisi zao kwa kufuata utaratibu wa kijasiriamali.

Pia ujasiriamali hufundishwa kama mada kuu au mada dogo. Hata vile vyuo au vyuo vikuu vichache ambavyo vimeanzisha mafunzo ya shahada za uzamili au stashada za kawaida na za juu katika ujasiriamali vimekuwa vikipanga kozi kwa kufuata utaratibu wao; wakati mwingine vikikosa mwelekeo katika somo. Ndiyo maana baadhi ya vyuo na vyuo vikuu hufundisha ujasiriamali kama mojawapo ya vigezo vya uzalishaji au somo linalohusu uendeshaji wa biashara (biashara za mitaani) tu! Mbaya zaidi, somo hufundishwa na watu ambao hawana maarifa ya kutosha kuhusu somo. Vyuo vikuu vingi huajiri watu wenye shahada za uzamili za MBA ambao hufanya kazi kama wahadhiri wasaidizi. Hawana uelewa kuwa watu wenye shahada za MBA wana elimu ndogo ya ujasiriamali na hivyo wanawanyima wanafunzi haki ya kupata elimu bora ambayo wanastahili kuipata. Katika shule za sekondari hali ni mbaya vilevile. Muhtasari wa elimu ya sekondari hausemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Katika ngazi za juu za elimu ya sekondari, ujasiriamali unachukuliwa kama kigezo cha uzalishaji kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita wanaosoma somo la uchumi. Pia katika Masomo ya Jumla, ujasiriamali hauchukuliwi ama kama mada kuu au mada ndogo. Wanafunzi wengi wa sekondari wanaomaliza elimu yao hawaelewi chochote kuhusu ujasiriamali kama taaluma bali husikia tu kuwa ujasiriamali unahusishwa na biashara ndogondogo za mitaani!

Muhtasari wa Elimu ya Msingi hausemi chochote kuhusu elimu ya ujasiriamali. Huzungumzia kuhusu maarifa ya jamii ambayo yamelenga kuwapatia wanafunzi maarifa na ujuzi wa kuwa wabunifu na wavumbuzi. Hata hivyo walimu wanaofundisha maarifa ya jamii hawana maarifa ya kutosha kuwawezesha wanafunzi wawe wa uwezo wa ziada wa kufikiria. Kwa kawaida wanatilia mkazo katika utengenezaji wa vyungu na upambaji na kazi zingine zinazofanana na hizo na ambazo zimekuwa ndiyo utaratibu wa maisha ya kila siku. Wanakosa mbinu na ujuzi wa kuwafanya wanafunzi wafikirie na kubuni mambo yasiyo ya kawaida. Ukosefu wa elimu ya ujasiriamali kwa shule za msingi ni miongoni mwa sababu za kuandaa watafuta kazi badala ya watengeneza kazi.


7.0. Athari za Kukosekana Msisitizo kuhusu Elimu ya Ujasiriamali

Nguvu ya ujasiriamali imethibitisha kuwa yenye matokeo makubwa katika nchi nyingi ambazo huchukulia elimu ya ujasiriamali kama ndiyo inayotengeneza kazi, injini katika ukuaji wa uchumi na silaha ya kupambana na umasikini kwa uchache tu. Kourilloff (2000) anabainisha kwamba hakuna anayeweza kuhoji mchango mkubwa wa kiuchumi wa kampuni ya Microsoft, Amazon, Intel, Cisco au Google na makampuni mengine makubwa nchini Marekani ambayo ni matokeo ya wajasiriamali. Kwamba kwa kulinganisha na nchi zingine, Marekani ndiyo nchi yenye historia ndefu katika elimu ya ujasiriamali, na pia miongoni mwa nchi zenye utamaduni rafiki juu ya ujasiriamali duniani. Marekani imejipambanua kuwa ni nchi inayoongoza katika ubunifu na uvumbuzi kuliko nchi zote.

Ukweli ni kwamba iwapo nchi haitatilia mkazo elimu ya ujasiriamali itasababisha kuwa na tatizo la ajira, ukuaji mdogo wa uchumi, umasikini na upeo mdogo wa kufikiri kwa watu wake.

Elimu ya ujasiriamali huchangia katika ukuaji wa uchumi. Imegundulika kuwa wajasiriamali wa ndani huchangia kwa kiwango kikubwa katika Pato la Taifa (GDP). Kwa mfano, mtu anapaswa kujiuliza kuhusu mchango wa Makampuni ya IPP au Bakhresa katika uchumi wa taifa hasa kwa kuzingatia mapato ambayo nchi hupata kupitia (kodi) na utengenezaji wa ajira, achilia mbali mchango wa makampuni hayo katika upatikanaji wa huduma za jamii. Iwapo elimu ya ujasiriamali haitatiliwa mkazo, nchi itakuwa tegemezi kwa bidhaa za nje na hivyo kushindwa kupiga vita ujinga, maradhi na umasikini.


8.0. Mahitaji ya Elimu ya Ujasiriamali yenye Ufanisi nchini Tanzania

Elimu ni mchakato usioisha wa kupata ujuzi na maarifa. Mtu anaweza kupata maarifa kwa njia rasmi au isiyo rasmi. Elimu rasmi ni ile tunayoipata kutoka kwenye taasisi za elimu kama vile mashule. Elimu isiyo rasmi ni aina ya elimu ambayo haimlazimu mtu kwenda shule. Inaweza kupatikana muda wowote na popote. Lengo kubwa la elimu ni kutengeneza maisha bora kwa watu. Tunapozungumzia elimu ya ujasiriamali tunamaanisha elimu inayotilia mkazo katika kufikiri kwa ubunifu katika kutumia fursa zilizopo kwa lengo la kutengeneza ajira ambazo husaidia katika ustawi wa kijamii na ukuaji wa uchumi. Hii ndiyo aina ya elimu ambayo inaweza kuyafanya maendeleo ya taifa kuwa endelevu; elimu ambayo MDI tunaitilia mkazo kwa watanzania wote - hasa vijana.


Maendeleo endelevu ni aina ya maendeleo yanayokidhi mahitaji ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho. Ni aina ya maendeleo ambayo hayatikisiki upesi bali yanaweza kudumu na kuhimili vikwazo vya, kijamii, kifikra na kiuchumi. Nchini Tanzania elimu ya ujasiriamali inahitajika sana ili kuzitumia kwa ufanisi fursa na raslimali zilizopo. Tanzania imejaliwa maziwa, mito, bahari, mabwawa, vituo vya utalii n.k. ambayo siyo kwamba yamejaa samaki tu bali yamejaa pia viumbe wengine kama vile viboko, mamba n.k. Nchi imejaliwa ardhi kubwa ambayo haijatumika, misitu na wanyama mwitu na wale wa kufugwa. Pia nchi imejaliwa kuwa na gesi na madini kama vile almasi, dhahabu, Tanzanite, makaa ya mawe kwa uchache tu. Hata hivyo, vitu vyote hivi havijatumiwa kikamilifu ili kuleta maendeleo ya watu. Kwa maneno mengine, tunakosa maarifa na ujuzi wa kiujasiriamali katika kuzibadilisha fursa hizo kuwa maendeleo. Iwapo tunataka maendeleo endelevu lazima tutengeneze/tuandae watu ambao wanaweza:

• Kuendeleza bidhaa zilizopo na kutengeneza bidhaa mpya.

• Kugundua huduma na njia mpya zinazotilia mkazo matumizi halisi katika kiwanda au shirika

• Kugundua na kutumia masoko mapya ambayo kiwanda au shirika halijayatumia

• Kugundua na kutumia nyenzo mpya za utoaji raslimali ambazo hazijawahi kutumika

• Kuwa tayari kupambana na hatari yoyote kwa faida ya nchi

Nchini Tanzania tunahitaji watu ambao wanaweza kuleta tija katika uzalishaji kwenye taasisi au mashirika. Utafiti uliofanyika hivi karibuni umeonesha kwamba huduma za afya nchini Tanzania ni duni sana. Kwa mfano, asilimia 53 ya wagonjwa wanaofika hospitalini huhudumiwa baada ya kusubiri kwa muda wa masaa mawili au matatu na asilimia 19 ya wagonjwa ambao hufikishwa hospitalini huombwa rushwa. Haya yote hutokea kutokana na kukosekana kwa elimu ya ujasiriamali. Hawaijali raslimali watu na wanadhani kuwa uzalishaji unaweza kupatikana kwa njia ya hongo. Ili kuleta ufanisi na tija katika upatikanaji wa huduma na bidhaa, taasisi au shirika lolote linapaswa kuwajumuisha wajasiriamali ambao wanaweza kuleta tija kwenye huduma na bidhaa kwa lengo la kuongeza uzalishaji.



Pia tumeshuhudia kushuka kwa ubora wa elimu kunakoendana na matokeo yasiyoridhisha kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini Tanzania. Mengi yamesemwa kuhusu suala hilo. Mambo hayo yanajumuisha miundombinu isiyoridhisha na vifaa visivyoridhisha vya kufundishia na kujifunzia. Hata hivyo kuna sababu nyingine ambayo huwa tunaisahau. Sababu yenyewe ni kwamba tunakosa ubunifu na uvumbuzi miongoni mwa walimu na wanafunzi katika michakato ya ujifunzaji na ufundishaji. Wanatumia njia za zamani za ufundishaji na ujifunzaji. Juhudi za kugundua njia mpya za ufundishaji na ujifunzaji ni ndogo. Kinachosababisha hali hii ni ukosefu wa utamaduni wa kijasiriamali ambao unaweza kubadili mtazamo wa mtu katika kukabiliana na ulimwengu. Wakati walimu na wanafunzi katika nchi zingine wakijaribu kuvumbua na kubuni njia mpya za ujifunzaji na ufundishaji, sisi bado tunashikilia njia za zamani za ujifunzaji, ufundishaji na upimaji wa wanafunzi wetu. Matokeo yake, baadhi ya wanafunzi (wakati mwingine, kwa kushirikiana na walimu wao) wanafanya udanganyifu katika mitihani.


Pia ukweli uliodhahiri ni kwamba kutokujua kusoma na kuandika kunaongezeka. Kwa mfano, kulikuwa na wanafunzi 308 wa Kidato cha Kwanza wasiojua kusoma na kuandika katika kata ya Nansimo katika wilaya ya Bunda. Pia, mkoa wa Arusha unaongoza katika udanganyifu kwenye mitihani. Unaongoza kwa asilimia 48. Pia ilibainika kwamba ni asilimia 14 tu ya wahitimu wa shule za msingi walifaulu mtihani wa hisabati mwaka jana. Hali hii kwa mujibu wa utafiti ilitokana na ukosefu wa uvumbuzi na ubunifu miongoni mwa walimu wa hisabati katika kulifanya somo hilo lieleweke vizuri. Pia ukosefu wa mbinu zinazowapatia wanafunzi motisha ya kulipenda somo la hisabati huchangia katika ufaulu duni wa wanafunzi. Iwapo walimu wangefundishwa kuhusu ujasiriamali (ujasiriamali wa mashirika), hali hii ingekuwa imepungua kama siyo kuondolewa kabisa.


9.0. Nini kifanyike?

Ili kuwa na elimu ya ujasiriamali yenye ufanisi kwa ajili ya maendeleo endelevu ya mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla, mambo yafuatayo inabidi yafanyike:

• Mihtasari/programu na moduli za elimu ya ujasiriamali ni lazima ziwe na malengo ya kuendeleza ari ya ujasiriamali kwa wanafunzi (kujenga motisha na ufahamu). Hii inajumuisha kuendeleza uwezo wa kijasiriamali ili kuweza kubainisha na kutumia fursa zilizopo, kuwapatia wanafunzi ujuzi unaohitajika katika kuanzisha biashara na kuziendesha ili zikue. Katika hali hizi zote, ni muhimu kuwahamasisha wanafunzi ili waweze kufikiri na kutenda kama wajasiriamali na pia ili wawe wenye kuwajibika kimaadili na kijamii.

• Ujasiriamali ni sharti ufundishwe na wataalamu ambao wanafahamu jinsi ya kulifundisha somo hili. Inapaswa kufahamika kwamba ujarisiarimali ni vitendo na kwamba ili kuwapatia motisha wanafunzi, njia/mbinu mbalimbali za kufundishia inabidi zitumike. Kwa mfano, ni muhimu somo la ujasiriamali lifundishwe na wajasiriamali wenye moyo wa kufanya hivyo. Mbinu ya kuiga ni muhimu zaidi katika ufundishaji wa ujasiriamali kwa sababu watu hupenda kumsikiliza yule wanayemwamini na yule aliyefanya kitu kwenye jamii.

· Shule ni sharti zifungamanishwe na kazi. Uhusiano huu wa shule na kazi husaidia kupunguza matarajio ya kazi kwa vijana na pia husaidia kupunguza tatizo la ajira kwa wasomi walioajiriwa na wale wasio na ajira.


10.0. Hitimisho

Elimu ya ujasiriamali si ya zamani kama zilivyo fani nyingine kama vile sayansi ya siasa, falsafa na sosholojia, lakini ujasiriamali umeleta mabadiliko makubwa tangu kuanza kwake. Kompyuta, mashine za ATM, simu za mikononi, kwa uchache tu ni bidhaa zinazotokana na ujasiriamali. Ijapokuwa mtu anaweza kuwa na sifa za ujasiriamali, ni sharti afundishwe somo hilo ili kumpatia maarifa na ujuzi wa kushindana katika ulimwengu kwa ujumla wake. Ufundishaji makini wa ujasiriamali utawezesha kupatikana kwa maendeleo endelevu na hivyo kuwawezesha watu kuwa na maisha mazuri katika nchi zao.

MDI inafanya kazi ili kuleta ubora wa afya, elimu na kuimarisha maisha ya binadamu kwa kuziwezesha jamii kubadili mtazamo wa kifikra na ushawishi katika utengenezaji wa sera, kuibua mijadala yenye kuleta mabadiliko chanya, kufanya utafiti yakinifu, uchambuzi na utetezi wa sera, na kushirikiana na washirika katika kuendeleza maslahi ya jamii kwa ujumla.
Safi sana, mkuu.
 
Elimu tunapata sana tatizo hyo mitaji ya kufanya hizo biashara.
Elimu tunapata sana tatizo hyo mitaji ya kufanya hizo biashara.
Unapata elimu ya kukufanya uwe mnyenyekevu, usiwe na uwezo wa kuuliza maswali, ukubali hali yoyote ile hata kama huitaki, uumnenyekee kila mtu hata kama anakunyanyasa - hiyo ni elimu yenye misingi ya wakoloni.

Elimu unayopaswa kuipata sio Mathematics, English, Physics, Biology n.k. - hiyo haikusaidii - unakuwa msindikizaji wa wengine.

Pata Ujuzi na Maarifa ya kutumia mazingira yanayokuzunguka ili upambane na changamoto ulizonazo.

Mtaji sio pesa, mtaji ni pamoja na watu, ardhi, bahari, ziwa, n.k. - unavitumiaje hivyo vitu?
 
Unapata elimu ya kukufanya uwe mnyenyekevu, usiwe na uwezo wa kuuliza maswali, ukubali hali yoyote ile hata kama huitaki, uumnenyekee kila mtu hata kama anakunyanyasa - hiyo ni elimu yenye misingi ya wakoloni.

Elimu unayopaswa kuipata sio Mathematics, English, Physics, Biology n.k. - hiyo haikusaidii - unakuwa msindikizaji wa wengine.

Pata Ujuzi na Maarifa ya kutumia mazingira yanayokuzunguka ili upambane na changamoto ulizonazo.

Mtaji sio pesa, mtaji ni pamoja na watu, ardhi, bahari, ziwa, n.k. - unavitumiaje hivyo vitu?
Apo mkuu ndo mtufundishe na mtufafanulie namna ya kutumia rasilimali kama aridhi, watu, maziwa n.k bila kuwa na pesa
 
Apo mkuu ndo mtufundishe na mtufafanulie namna ya kutumia rasilimali kama aridhi, watu, maziwa n.k bila kuwa na pesa
Hivi zamani kabla ya pesa watu walikuwa hawafanyi kazi? Kama walifanya kazi na wakaishi vizuri hadi mfumo ukabadilika na kuanza kutumia pesa ... inadhihirisha wazi kwamba kwa sasa ni raisi zaidi kuliko zamani.
Haya ndiyo ya kufanya ili uondokane na kauli za hakuna pesa ...
1. Angalia kile kinachochukua pesa zako kila siku ndo ukifanye kuwa kazi yako.

Mfano mijini kitu kinachochukua hela nyingi ni mboga .... zalisha mboga mwenyewe.

2. Changamoto za wengine ndo ziwe kazi kwako... utazibadilije changamoto kuwa kazi ...? Hapo ndo kunahitajika elimu ... elimu itapatikanaje .... ?
 
Somo zuri ila limekosa wachangiaji sijui tatizo nini
Hiki ndo kipimo cha watanzania walio wengi .. yakiongelewa mambo ambayo hayamsaidii mtu - wachangiaji wanakuwa wengi sana. Jambo la kumsaidia mtu - anapita tu wala hana hata muda wa kusoma ..
Hiki ndicho kipimo cha uelewa wa watanzania wenzetu.
 
Maarifa yanapatikana katikati ya maandishi. Jitahidi usome
 
Somo refu sana,mi mwenyew nimejisikia uvivu nasoma comment labda nitapata mwanga wa kitu kilichoelezewa lakin wap
Jenga utamaduni wa kusoma maandiko marefu ili uweze kupata kilicho bora. Mara nyingi maandiko machache huwa ni ufupisho
 
Back
Top Bottom