mkulu senkondo
JF-Expert Member
- Feb 19, 2017
- 1,895
- 3,654
Kwa sasa unapata ujasiri wa kutamka maneno kama hayo! Lakini ungenyimwa wakati unaanza kusoma ungekuwa wa kwanza kuwa kimbelembele kama mfuko wa shati kwa kuanza kuandamana na kuililia serikali kama ndio mzazi wako! Kama wewe unaona serikali ya ccm inakutesa, nakushauri anza kwa kumwekea mwanao mazingira mazuri ya kutokuja kukopa.....sio kuwahamasisha na kuwalisha watu mawazo mfu kama haya!Walinipotezea muda kusomea didgrii ambayo sijawahi ata kuitumia..! Chakushangaza bado eti wananidai hivi wanaelewa hasara kiasi gani nilipata kwa miaka 3.
Nasema hivi maana walinisomesha tena kwa kunipangia mwenyewe kozi ambayo sikuomba ubabe na ukatili wa hali ya juu.Kwa sasa unapata ujasiri wa kutamka maneno kama hayo! Lakini ungenyimwa wakati unaanza kusoma ungekuwa wa kwanza kuwa kimbelembele kama mfuko wa shati kwa kuanza kuandamana na kuililia serikali kama ndio mzazi wako! Kama wewe unaona serikali ya ccm inakutesa, nakushauri anza kwa kumwekea mwanao mazingira mazuri ya kutokuja kukopa.....sio kuwahamasisha na kuwalisha watu mawazo mfu kama haya!
Lakin mtoa mada amejikita kwenye utajiri hilo la mafanikio ni suala lingineUnatafsiri VIP utajiri ndugu? Unadhan kua na hela ndio utajiri? Unajua kutofautisha mwenye Mali na MTU aliefanikiwa?? Unajua kuutofauyisha utajiri na mafanikio??? Labda unachanganya HIV vitu viwili
Pole sana! Lakini sasa kwa nini ufanye kitu ambacho hukipendi? Yaani ulikosa kabisa namna ya kubadilisha? Isitoshe mbona mtu anapotaka kujiunga na elimu ya juu yeye mwenyewe ndio huchagua akasome kozi anayotaka! Hicho chuo kinachochagulia watu bachelor kipo wapi na ni kipi?Nasema hivi maana walinisomesha tena kwa kunipangia mwenyewe kozi ambayo sikuomba ubabe na ukatili wa hali ya juu.
Unaelewa kazi ya TCU kweli, inazofanya na ambazo imekuwa ikifanya tangu mwanzo?? Ni upuuzi mtupu, pia HESLB kupangia watu kuwa kusoma kozi Fulani ndiyo apewe mkopo ni upuuzi mkubwa. Uelewi unachosema wewe.Pole sana! Lakini sasa kwa nini ufanye kitu ambacho hukipendi? Yaani ulikosa kabisa namna ya kubadilisha? Isitoshe mbona mtu anapotaka kujiunga na elimu ya juu yeye mwenyewe ndio huchagua akasome kozi anayotaka! Hicho chuo kinachochagulia watu bachelor kipo wapi na ni kipi?
Mkuu umeua!Walinipotezea muda kusomea didgrii ambayo sijawahi ata kuitumia..! Chakushangaza bado eti wananidai hivi wanaelewa hasara kiasi gani nilipata kwa miaka 3.
Hatujawahi kujua tunachokitaka! Umesahau. Yule walisema mpole na dhaifu, huyu wanasema dictator.Hapa ndio unafiki wa watanzania unapojidhihirisha! Sasa mnatajaje? Mtu asiposoma mnamwita kilaza/bashite wanaosoma, mnawaambia wanapoteza muda! Sasa mnataka nini?
Wanaudhi sana!Mkuu umeua!
Mimi naomba nianzie kwanza ulipoishia kuwa umesema watanzania wanasoma ili kupata makaratasi bila kujua kuwa makaratasi hayo yana faida gani, labda niulize kwanza, haya makaratasi unayo, au na wewe ni Bashite+ maana tusije kuwa tunasoma Uzi wa watu waliopiga failure halafu wanakuja kulalamika huku.Nimekuwa nikijiuliza Mara nyingi kuwa elimu inayotolewa nchini Tanzania hulenga nini na ni faida kwa nani? Sio Siri imechukua muda mrefu kutambua kuwa elimu ya Tanzania hususani ya juu huwapoteza watu katika direction ya maisha. Serikali ingeweka mfumo ambao mtu akisoma awe na uwezo wa kuajiriwa na kujiajiri pia tofauti na ilivyosasa.
Mtu anamaliza chuo kikuu akirudi mtaani hana tofauti na yule aliyekomea la saba labda tofauti ya kuvaa yaani msomi atakuwa anamodoa nguo zake lakini wa la saba anavaa kipapaa.
Wale ambao wameajiriwa ni watumwa, mfano mwalimu anakipindi kimoja kwa wiki lakini analazimika kuhudhuria shuleni muda wote wa kazi yaani SAA 7:30 mpaka 3:30 harusiwi kutoka njee ya kituo cha kazi kufanya Mishe zake.
Umewahi sikia kuna mwalimu tajiri? Umewahi sikia kuna nurse tajiri? Umewahi sikia kuna askari tajiri? Umewahi sikia kuna dactari tajiri? Utajiri umeumbwa kwa ajili ya nani? Kwanini ung'ang'anie kutafuta ajira? Watu wamekuwa wakisoma ili wapate makaratasi(vyeti) bila kujua makaratasi hayo yanamchango gani kimaisha.
TAFUTA FEDHA USITAFUTE ELIMU
We nenda directly kuwa unataka kutushawishi kujiunga forever living
Mnaanziaga mbali sana