THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 419
- 654
KAMA NITAKUKWAZA WEWE UNAYE SOMA UZI HUU NAOMBA UNISAMEHE MAANA NAKWENDA KUONGELEA ELIMU YA KWELI KUHUSU DINI NA CHANZO CHAKE.
Tutazungumza kwa urefu zaidi jinsi dini fulani fulani zilivyoanza na kusitawi. Utakuta inanurisha si kujua tu jinsi kila dini ilivyo tofauti na nyinginezo bali pia jinsi inavyofanana nazo. Pia utaweza kujua jinsi kila dini inavyoingia katika mpangilio wa wakati wa historia ya kibinadamu na historia ya dini, jinsi kitabu au maandishi yayo matakatifu yanavyohusiana na mengine, jinsi mwanzilishi au kiongozi wayo alivyovutwa na mawazo mengine ya kidini, na jinsi imekuwa na uvutano juu ya mwenendo na historia ya ainabinadamu. Ukizingatia mambo haya akilini, kujifunza juu ya jitihada ya ainabinadamu ya kutafuta Mungu ambayo imechukua muda mrefu Mungu kutakusaidia uone kwa uwazi zaidi ukweli juu ya dini na mafundisho ya kidini.
SITOPENDELEA DINI YEYOTE NITAJITAHIDI KUELEZEA KWA MAPANA KILA DINI NA KUFICHUA MAMBO YA SIRINI KABISA YA KILA DINI.HATA DINI ZA ASILI NITAZIELEZEA KWA KIWANGO CHA KAWAIDA SITOZAMA NDANI.KUMBUKA SITOAIBISHA DINI BALI NITAIELEZEA KAMA ILIVYO.
LAKINI YEYOTE ANARUHUSIWA KUNIKOSOA NA KUPANUA MADA HII MAANA INA MASWALI NA MAJIBU KWA AJIRI YA KUSHIRIKI MAJADILIANO.HII NI ELIMU YA WAZI KWA WOTE HIVYO UNARUHUSIWA KUTOA HOJA ZAKO LAKINI ZIWE NA UDHIBITISHO MAANA NAMI NITAONGEA KWA KUNUKUU VITABU VILIVYO TOA HOJA HIZI ZOTE KUHUSU ELIMU YA KWELI KUHUSU DINI NA IMANI.
Sura 1
Kwa Nini Kupendezwa na Dini Nyingine?1-7.
Ni nini baadhi ya madhihirisho ya dini mbalimbali za ulimwengu?BILA kujali waishi wapi, bila shaka umejionea mwenyewe jinsi dini inavyoongoza maisha za mamilioni ya watu, labda na yako pia. Katika nchi ambazo Uhindu unazoewa, mara nyingi utawaona watu wakifanya puja—sherehe ambayo yaweza kuhusisha kutoa sadaka kwa vijimungu vyao, kwa namna ya nazi, maua, na matofaa. Kuhani anapaka rangi nyekundu au ya manjano, yaani tilak, kwenye vipaji vya nyuso za waumini. Mamilioni pia humiminika kila mwaka kwenye mto Ganges watakaswe na maji yao.Katika nchi za Katoliki, utaona watu wakisali katika makanisa na makathedro huku wameshika kisalaba au tasbihi. Shanga za tasbihi zinatumiwa kuhesabia sala zinazotolewa kwa ujitoaji wao kwa Mariamu. Na si vigumu kutambua watawa wa kike na makasisi, wanaotofautishwa na kanzu zao nyeusi. Katika mabara ya Kiprotestanti, vikanisa na makanisa ni tele, na siku ya Jumapili wafuasi kwa kawaida huvaa nguo zao bora na kukusanyika waimbe nyimbo za dini na kusikia mahubiri.
Mara nyingi makasisi wao huvaa mavazi meusi na kola ya kikasisi yenye kuwatofautisha.Katika nchi za Kiislamu, unaweza kusikia sauti za waadhini, wapiga mbiu Waislamu wakiipiga kwenye vinara vya misikiti mara tano kila siku, kuwaita waamini kwenye s̩alãt, au sala ya sherehe. Wao huiona Qurani Tukufu kuwa kitabu cha Kiislamu cha maandiko matakatifu. Kulingana na imani ya Kiislamu, kilifunuliwa na Mungu akapewa nabii Muhammad na malaika Gabrieli katika karne ya saba W.K.Kwenye barabara za mabara mengi ya Kibuddha, watawa wa Dini ya Buddha, kwa kawaida wakiwa wamevaa majoho ya dhahabu-nyekundu, meusi, au mekundu, huonekana kuwa ishara ya mtu kuwa wa dini.
Mahekalu ya kale yanayoonyesha Buddha mtulivu ni uthibitisho wa zamani za kale wa imani ya Kibuddha. Dini ya Shinto ikiwa inazoewa katika Japan, inahusu maisha za kila siku kukiwa na vihekalu vya familia na matambiko kwa wazazi wa kale waliokufa. Wajapan huhisi huru kusali kwa ajili ya mambo ya kimwili kabisa, hata juu ya kufaulu katika mitihani ya shuleni.
Utendaji mwingine wa kidini unaojulikana ulimwenguni pote ni ule wa watu wanaoenda nyumba kwa nyumba na kusimama kwenye barabara wakiwa na Biblia na vitabu vya Biblia. Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakionekana wazi, karibu kila mtu anawatambua watu hao kuwa Mashahidi wa Yehova.8. Historia ya ujitoaji kidini inaonyesha nini?Unamna-namna huu mkubwa wa ujitoaji wa kidini ulimwenguni pote waonyesha nini? Kwamba kwa maelfu ya miaka ainabinadamu wamekuwa na uhitaji na tamaa ya kiroho. Binadamu ameishi na majaribu na mizigo, tashwishi na maswali yake, kutia ndani kitendawili cha kifo. Hisia za kidini zimeonyeshwa katika njia nyingi kwa watu kugeukia Mungu au vijimungu vyao, wakitafuta baraka na utulizo. Dini pia hujaribu kushughulikia maswali makubwa: Kwa nini sisi tupo hapa? Tuishije? Wakati ujao una nini kwa ajili ya ainabinadamu?9. Ni katika njia gani watu walio wengi wana namna zao za ujitoaji kidini maishani mwao?Kwa upande mwingine, kuna mamilioni ya watu wasiodai kuwa na dini yoyote wala imani yoyote katika kijimungu chochote. Wao ni waatheisti. Wengine, waagnosti, huamini kwamba Mungu hajulikani na yaelekea hawezi kujulikana. Hata hivyo, hilo kwa wazi halimaanishi kwamba wao ni watu wasio na kanuni wala maadili, kama ambavyo kudai kuwa na dini kusivyomaanisha kwamba mtu anazo. Hata hivyo, mtu akikubali dini kuwa “ujitoaji kwa kanuni fulani; utumainifu imara au uaminifu; udhamiriaji; shauku ya kufuata dini au ufungamano,” basi watu walio wengi, kutia waatheisti na waagnosti, wana namna fulani ya ujitoaji wa kidini maishani mwao.—The Shorter Oxford English Dictionary.10. Je! dini ina mshindo juu ya ulimwengu wa kisasa? Toa kielezi.Kwa kuwa kuna dini nyingi mno katika ulimwengu unaozidi kuwa mdogo zaidi na zaidi kwa sababu ya usafiri na uwasiliano wa kasi zaidi, mshindo wa imani mbalimbali huhisiwa ulimwenguni pote, tutake-tusitake. Kasirani iliyotokea mnamo 1989 kuhusu kitabu The Satanic Verses, kilichoandikwa na mtu ambaye watu wengine walimtaja kuwa ‘Mwislamu kafiri,’ ni uthibitisho ulio wazi wa jinsi fikira ya kidini yaweza kujidhihirisha kwa kiwango cha duniani pote. Kulikuwako wito kutoka viongozi wa Kiislamu kuwa kitabu hicho kipigwe marufuku na hata mtungaji wacho auawe. Ni nini kinachofanya watu wamenyuke vikali sana katika mambo ya dini?11. Kwa nini si kosa kuchunguza imani nyingine?Ili kujibu hilo, tunahitaji kujua jambo fulani juu ya chanzo cha dini za ulimwengu. Ni kama Geoffrey Parrinder anavyotoa taarifa katika World Religions—From Ancient History to the Present: “Kuchunguza dini tofauti-tofauti kwa lazima hakumaanishi mtu anakosa uaminifu kwa imani yake mwenyewe, bali huenda ikazidishwa kwa kuona jinsi watu wengine wametafuta uhalisi wa mambo na wakathawabishwa sana na jitihada yao ya kutafuta.” Maarifa huongoza kwenye kupata kuelewa, na kuelewa kwenye uvumilio wa watu wenye maoni tofauti.Kwa Nini Kuchunguza?12. Ni mambo gani ambayo kwa kawaida huamua dini ya mtu?Je! wewe umepata kufikiri au ukasema, ‘Mimi nina dini yangu mwenyewe. Hilo ni jambo la kibinafsi kabisa.
Mimi siizungumzi pamoja na wengine’? Ni kweli dini ni jambo la kibinafsi kabisa—karibu tangu kuzaliwa mawazo ya kidini au ya kiadili yanapandikizwa katika akili yetu na wazazi na watu wa ukoo. Tokeo ni kwamba, kwa kawaida sisi hufuata mafikira ya kidini ya wazazi wetu na ya wazazi wa wazazi wetu. Kwa ujumla dini imekuwa utamaduni wa familia. Matokeo ya hatua hiyo yamekuwa nini? Kwamba katika visa vingi wengine wametuchagulia sisi dini yetu. Karibu imetegemea mahali na wakati tulipozaliwa. Au, kama mwanahistoria Arnold Toynbee alivyoonyesha, kuambatana kwa mtu na imani fulani mara nyingi huamuliwa na “tukio la kijiografia la mahali alipozaliwa.”13, 14. Kwa nini si jambo la akili kuwaza kwamba dini aliyozaliwa nayo mtu ni yenye kuidhinishwa na Mungu moja kwa moja?Je! ni jambo la akili kudhania kwamba dini ambayo ilipandikizwa wakati wa mtu kuzaliwa kwa lazima ndio ukweli mzima?
Kama ulizaliwa Italia au Amerika Kusini, basi, bila ya uchaguzi wowote, yaelekea ulilelewa ukiwa Mkatoliki. Kama ulizaliwa katika India, basi yaelekea moja kwa moja ulikuwa Mhindu au, kama unatoka Punjabi, labda wewe ni wa Dini ya Sikh. Kama wazazi wako walitoka Pakistan, basi kwa wazi ungekuwa Mwislamu. Na kama ulizaliwa katika nchi ya Siasa za Kijamaa katika makumi machache ya miaka yaliyopita, huenda ikawa hukuwa na uchaguzi wowote bali kulelewa ukiwa mwaatheisti.—Wagalatia 1:13, 14; Matendo 23:6.
Kwa hiyo, je! dini aliyozaliwa nayo mtu inakuwa moja kwa moja ndiyo ya kweli, yenye kuidhinishwa na Mungu? Kama wazo hilo ndilo lingefuatwa kwa maelfu ya miaka iliyopita, wengi kati ya ainabinadamu wangekuwa wangali wanazoea ushamani wa kikale na ibada za nguvu za uzazi za kale, kwa msingi wa kwamba ‘kilichokuwa kizuri vya kuwatosha wazazi wangu wa kale waliokufa ni kizuri vya kunitosha.’
Tutazungumza kwa urefu zaidi jinsi dini fulani fulani zilivyoanza na kusitawi. Utakuta inanurisha si kujua tu jinsi kila dini ilivyo tofauti na nyinginezo bali pia jinsi inavyofanana nazo. Pia utaweza kujua jinsi kila dini inavyoingia katika mpangilio wa wakati wa historia ya kibinadamu na historia ya dini, jinsi kitabu au maandishi yayo matakatifu yanavyohusiana na mengine, jinsi mwanzilishi au kiongozi wayo alivyovutwa na mawazo mengine ya kidini, na jinsi imekuwa na uvutano juu ya mwenendo na historia ya ainabinadamu. Ukizingatia mambo haya akilini, kujifunza juu ya jitihada ya ainabinadamu ya kutafuta Mungu ambayo imechukua muda mrefu Mungu kutakusaidia uone kwa uwazi zaidi ukweli juu ya dini na mafundisho ya kidini.
SITOPENDELEA DINI YEYOTE NITAJITAHIDI KUELEZEA KWA MAPANA KILA DINI NA KUFICHUA MAMBO YA SIRINI KABISA YA KILA DINI.HATA DINI ZA ASILI NITAZIELEZEA KWA KIWANGO CHA KAWAIDA SITOZAMA NDANI.KUMBUKA SITOAIBISHA DINI BALI NITAIELEZEA KAMA ILIVYO.
LAKINI YEYOTE ANARUHUSIWA KUNIKOSOA NA KUPANUA MADA HII MAANA INA MASWALI NA MAJIBU KWA AJIRI YA KUSHIRIKI MAJADILIANO.HII NI ELIMU YA WAZI KWA WOTE HIVYO UNARUHUSIWA KUTOA HOJA ZAKO LAKINI ZIWE NA UDHIBITISHO MAANA NAMI NITAONGEA KWA KUNUKUU VITABU VILIVYO TOA HOJA HIZI ZOTE KUHUSU ELIMU YA KWELI KUHUSU DINI NA IMANI.
Sura 1
Kwa Nini Kupendezwa na Dini Nyingine?1-7.
Ni nini baadhi ya madhihirisho ya dini mbalimbali za ulimwengu?BILA kujali waishi wapi, bila shaka umejionea mwenyewe jinsi dini inavyoongoza maisha za mamilioni ya watu, labda na yako pia. Katika nchi ambazo Uhindu unazoewa, mara nyingi utawaona watu wakifanya puja—sherehe ambayo yaweza kuhusisha kutoa sadaka kwa vijimungu vyao, kwa namna ya nazi, maua, na matofaa. Kuhani anapaka rangi nyekundu au ya manjano, yaani tilak, kwenye vipaji vya nyuso za waumini. Mamilioni pia humiminika kila mwaka kwenye mto Ganges watakaswe na maji yao.Katika nchi za Katoliki, utaona watu wakisali katika makanisa na makathedro huku wameshika kisalaba au tasbihi. Shanga za tasbihi zinatumiwa kuhesabia sala zinazotolewa kwa ujitoaji wao kwa Mariamu. Na si vigumu kutambua watawa wa kike na makasisi, wanaotofautishwa na kanzu zao nyeusi. Katika mabara ya Kiprotestanti, vikanisa na makanisa ni tele, na siku ya Jumapili wafuasi kwa kawaida huvaa nguo zao bora na kukusanyika waimbe nyimbo za dini na kusikia mahubiri.
Mara nyingi makasisi wao huvaa mavazi meusi na kola ya kikasisi yenye kuwatofautisha.Katika nchi za Kiislamu, unaweza kusikia sauti za waadhini, wapiga mbiu Waislamu wakiipiga kwenye vinara vya misikiti mara tano kila siku, kuwaita waamini kwenye s̩alãt, au sala ya sherehe. Wao huiona Qurani Tukufu kuwa kitabu cha Kiislamu cha maandiko matakatifu. Kulingana na imani ya Kiislamu, kilifunuliwa na Mungu akapewa nabii Muhammad na malaika Gabrieli katika karne ya saba W.K.Kwenye barabara za mabara mengi ya Kibuddha, watawa wa Dini ya Buddha, kwa kawaida wakiwa wamevaa majoho ya dhahabu-nyekundu, meusi, au mekundu, huonekana kuwa ishara ya mtu kuwa wa dini.
Mahekalu ya kale yanayoonyesha Buddha mtulivu ni uthibitisho wa zamani za kale wa imani ya Kibuddha. Dini ya Shinto ikiwa inazoewa katika Japan, inahusu maisha za kila siku kukiwa na vihekalu vya familia na matambiko kwa wazazi wa kale waliokufa. Wajapan huhisi huru kusali kwa ajili ya mambo ya kimwili kabisa, hata juu ya kufaulu katika mitihani ya shuleni.
Utendaji mwingine wa kidini unaojulikana ulimwenguni pote ni ule wa watu wanaoenda nyumba kwa nyumba na kusimama kwenye barabara wakiwa na Biblia na vitabu vya Biblia. Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakionekana wazi, karibu kila mtu anawatambua watu hao kuwa Mashahidi wa Yehova.8. Historia ya ujitoaji kidini inaonyesha nini?Unamna-namna huu mkubwa wa ujitoaji wa kidini ulimwenguni pote waonyesha nini? Kwamba kwa maelfu ya miaka ainabinadamu wamekuwa na uhitaji na tamaa ya kiroho. Binadamu ameishi na majaribu na mizigo, tashwishi na maswali yake, kutia ndani kitendawili cha kifo. Hisia za kidini zimeonyeshwa katika njia nyingi kwa watu kugeukia Mungu au vijimungu vyao, wakitafuta baraka na utulizo. Dini pia hujaribu kushughulikia maswali makubwa: Kwa nini sisi tupo hapa? Tuishije? Wakati ujao una nini kwa ajili ya ainabinadamu?9. Ni katika njia gani watu walio wengi wana namna zao za ujitoaji kidini maishani mwao?Kwa upande mwingine, kuna mamilioni ya watu wasiodai kuwa na dini yoyote wala imani yoyote katika kijimungu chochote. Wao ni waatheisti. Wengine, waagnosti, huamini kwamba Mungu hajulikani na yaelekea hawezi kujulikana. Hata hivyo, hilo kwa wazi halimaanishi kwamba wao ni watu wasio na kanuni wala maadili, kama ambavyo kudai kuwa na dini kusivyomaanisha kwamba mtu anazo. Hata hivyo, mtu akikubali dini kuwa “ujitoaji kwa kanuni fulani; utumainifu imara au uaminifu; udhamiriaji; shauku ya kufuata dini au ufungamano,” basi watu walio wengi, kutia waatheisti na waagnosti, wana namna fulani ya ujitoaji wa kidini maishani mwao.—The Shorter Oxford English Dictionary.10. Je! dini ina mshindo juu ya ulimwengu wa kisasa? Toa kielezi.Kwa kuwa kuna dini nyingi mno katika ulimwengu unaozidi kuwa mdogo zaidi na zaidi kwa sababu ya usafiri na uwasiliano wa kasi zaidi, mshindo wa imani mbalimbali huhisiwa ulimwenguni pote, tutake-tusitake. Kasirani iliyotokea mnamo 1989 kuhusu kitabu The Satanic Verses, kilichoandikwa na mtu ambaye watu wengine walimtaja kuwa ‘Mwislamu kafiri,’ ni uthibitisho ulio wazi wa jinsi fikira ya kidini yaweza kujidhihirisha kwa kiwango cha duniani pote. Kulikuwako wito kutoka viongozi wa Kiislamu kuwa kitabu hicho kipigwe marufuku na hata mtungaji wacho auawe. Ni nini kinachofanya watu wamenyuke vikali sana katika mambo ya dini?11. Kwa nini si kosa kuchunguza imani nyingine?Ili kujibu hilo, tunahitaji kujua jambo fulani juu ya chanzo cha dini za ulimwengu. Ni kama Geoffrey Parrinder anavyotoa taarifa katika World Religions—From Ancient History to the Present: “Kuchunguza dini tofauti-tofauti kwa lazima hakumaanishi mtu anakosa uaminifu kwa imani yake mwenyewe, bali huenda ikazidishwa kwa kuona jinsi watu wengine wametafuta uhalisi wa mambo na wakathawabishwa sana na jitihada yao ya kutafuta.” Maarifa huongoza kwenye kupata kuelewa, na kuelewa kwenye uvumilio wa watu wenye maoni tofauti.Kwa Nini Kuchunguza?12. Ni mambo gani ambayo kwa kawaida huamua dini ya mtu?Je! wewe umepata kufikiri au ukasema, ‘Mimi nina dini yangu mwenyewe. Hilo ni jambo la kibinafsi kabisa.
Mimi siizungumzi pamoja na wengine’? Ni kweli dini ni jambo la kibinafsi kabisa—karibu tangu kuzaliwa mawazo ya kidini au ya kiadili yanapandikizwa katika akili yetu na wazazi na watu wa ukoo. Tokeo ni kwamba, kwa kawaida sisi hufuata mafikira ya kidini ya wazazi wetu na ya wazazi wa wazazi wetu. Kwa ujumla dini imekuwa utamaduni wa familia. Matokeo ya hatua hiyo yamekuwa nini? Kwamba katika visa vingi wengine wametuchagulia sisi dini yetu. Karibu imetegemea mahali na wakati tulipozaliwa. Au, kama mwanahistoria Arnold Toynbee alivyoonyesha, kuambatana kwa mtu na imani fulani mara nyingi huamuliwa na “tukio la kijiografia la mahali alipozaliwa.”13, 14. Kwa nini si jambo la akili kuwaza kwamba dini aliyozaliwa nayo mtu ni yenye kuidhinishwa na Mungu moja kwa moja?Je! ni jambo la akili kudhania kwamba dini ambayo ilipandikizwa wakati wa mtu kuzaliwa kwa lazima ndio ukweli mzima?
Kama ulizaliwa Italia au Amerika Kusini, basi, bila ya uchaguzi wowote, yaelekea ulilelewa ukiwa Mkatoliki. Kama ulizaliwa katika India, basi yaelekea moja kwa moja ulikuwa Mhindu au, kama unatoka Punjabi, labda wewe ni wa Dini ya Sikh. Kama wazazi wako walitoka Pakistan, basi kwa wazi ungekuwa Mwislamu. Na kama ulizaliwa katika nchi ya Siasa za Kijamaa katika makumi machache ya miaka yaliyopita, huenda ikawa hukuwa na uchaguzi wowote bali kulelewa ukiwa mwaatheisti.—Wagalatia 1:13, 14; Matendo 23:6.
Kwa hiyo, je! dini aliyozaliwa nayo mtu inakuwa moja kwa moja ndiyo ya kweli, yenye kuidhinishwa na Mungu? Kama wazo hilo ndilo lingefuatwa kwa maelfu ya miaka iliyopita, wengi kati ya ainabinadamu wangekuwa wangali wanazoea ushamani wa kikale na ibada za nguvu za uzazi za kale, kwa msingi wa kwamba ‘kilichokuwa kizuri vya kuwatosha wazazi wangu wa kale waliokufa ni kizuri vya kunitosha.’