Elimu bure bila kuboresha maslahi ya walimu

Elimu bure bila kuboresha maslahi ya walimu

Ssayari

Member
Joined
Oct 15, 2015
Posts
16
Reaction score
8
Wakuu hivi ELIMU bure bila kuwajali walimu kweli lengo litafikiwa?
Watz wanafurahishwa na kauli hii lakini je wanajua faida na hasara za ELIMU bure? Kwa taarifa ya uhakika niliyo nayo walimu wa Mwanza jiji katika shule za msingi wamelazimishwa na Afsa elimu kufundisha bure madarasa ya la pili, nne na saba wakati wa likizo.

Hii ni kutekeleza agizo la ELIMU bure, je, walimu hao watakaofundisha madarasa hayo hawana haki ya kupumzika/kukaa likizo baada ya kufanya Kazi mwaka mzima?

Achilia mbali likizo, acha wafundishe, je, kwakuwa ni muda wa ziada hawana haki ya kulipwa posho za kufundisha kipindi cha likizo?

Huku siyo kuwaonea walimu? Walimu HAWA watafundisha kweli kwa dhati? Nahisi Afsa ELIMU Huyu atakuwa amekiuka haki za walimu.
 
mzee magufili aangalie sana..

mwalimu hana nyumba.

mwalimu hana usafiri.

mwalimu kula yake ya taabu

mwalimu anakopa anapigwa % kubwa

mwalimu anakatwa Payee nzito

mwalimu hasomesha wanae, kula, kuvaa, nk

ninyi mnamhadaa nyumba, vyeo
 
binafsi kufundisha mda wa likizo ni lazima nilipwe mshahara wa mwezi huo kama posho vinginevyo tutatoana roho
 
Tunasema hivi elimu bure kuanzia 2016 january kuanzia std 1 - form 4 inawezekana na changamoto zake tumejiandaa kuzikabiri kadiri ya zitakavyojitokeza.
 
Acha uwongo, wengine tuna nyumba, usafiri na tunakula vizuri, wewe ndo hujielewi na hajitambui
 
huo uoga gani sasa wa kulazimishwa kufundisha hadi likizo kwani walimu wameshakuwa watumwa
 
Wakuu hivi ELIMU bure bila kuwajali walimu kweli lengo litafikiwa?
Watz wanafurahishwa na kauli hii lakini je wanajua faida na hasara za ELIMU bure? Kwa taarifa ya uhakika niliyo nayo walimu wa Mwanza jiji katika shule za msingi wamelazimishwa na Afsa elimu kufundisha bure madarasa ya la pili, nne na saba wakati wa likizo.
Hii ni kutekeleza agizo la ELIMU bure,je, walimu hao watakaofundisha madarasa hayo hawana haki ya kupumzika/kukaa likizo baada ya kufanya Kazi mwaka mzima?

Achilia mbali likizo,acha wafundishe, je,kwakuwa ni muda wa ziada hawana haki ya kulipwa posho za kufundisha kipindi cha likizo?

Huku siyo kuwaonea walimu? Walimu HAWA watafundisha kweli kwa dhati? Nahisi Afsa ELIMU Huyu atakuwa amekiuka haki za walimu.

Acha kulalamika we ticha uchwara, hiyo ni likizo ya wanafunzi na sio wafanyakazi. Mwalimu ana likizo moja tu kwa mwaka ambayo unapewa hadi nauli.
 
Acha kulalamika we ticha uchwara, hiyo ni likizo ya wanafunzi na sio wafanyakazi. Mwalimu ana likizo moja tu kwa mwaka ambayo unapewa hadi nauli.

Asante mkuu kwa kumwerewesha,binafsi nachukia watu wanaopenda kulialia,mi mwenyewe mwalimu naipenda kazi,napenda kuitwa mwalimu mpaka mke wangu nishamzuia kuniita honey,dear sweet,huwa ananiita mwalimu tu.
 
Asante mkuu kwa kumwerewesha,binafsi nachukia watu wanaopenda kulialia,mi mwenyewe mwalimu naipenda kazi,napenda kuitwa mwalimu mpaka mke wangu nishamzuia kuniita honey,dear sweet,huwa ananiita mwalimu tu.
Una uhakika na unachokisema ati Mimi ni "Mwalimu uchwara?"

Unauhakika walimu wanaoenda likizo mwisho wa mwaka hakuna ambao wamegawiwa vipindi katika madarasa ambayo Afsa Elimu ameagiza yafundishwe wakati wa likizo?

Jibu lake hapo ni kwamba lazima walimu waliopaswa kwenda likizo mwisho wa mwaka lazima wapo waliochukua vipindi katika madarasa hayo.Kwahiyo wewe ndiyo unaonekana akili yako huitumii ipasavyo kuchanganua mambo kitaalamu, Mimi nilitoa hii taarifa huku nikijua yote hayo ingawa Mimi siyo "ticha uchwara" ila wewe nahisi ni Mwalimu na ni ticha uchwara haswaaa!Kwasababu inaonekana umekariri kasheria hako tu!

Hujui hata kutofautisha likizo na kupumzika baada ya Kazi,Mwalimu anayohaki ya kupumzika pia kama ambavyo mwanafunzi anayohaki ya kupumzika baada ya kusoma mwaka mzima.

Inawezekanaje mwfz awe na haki ya kupumzika na Mwalimu asipate haki hiyo? Kati ya Mwalimu na mwfz nani kafanya kazi kubwa kwa mwaka? Jibu unalijua,Mwalimu hufanya Kazi kubwa sana ya kufundisha n.k.

Msemo wako Mwalimu huwa hafungi, km kweli no hivyo kwanini shule hufungwa? Basi ilipaswa shule zisifungwe, walimu wafundishe muda wote! Sababu kuu ya kufunga shule mojawapo ni kupumzisha akili kwa Mwl na mwfz na pili ni BAADA ya kukamilisha mpango Kazi au silabasi/mhula.

Kwaufupi toa hoja za msingi acha kutukana bila hoja za msingi, PENGINE UJUMBE UMEKUGUSA KWAKUWA WEWE NI MMOJA WA WALE MNAOHUJUMU WALIMU. WEWE NI SAWA NA BAADHI YA WALIMU WALIOBAHATIKA KUPATA UONGOZI NGAZI ZA JUU NA KUSAHAU SHIDA ZA WALIMU ILI HALI WAKATI NI WALIMU WALIKUWA WANALIA KWA KUTOPATA HAKI ZAO.
 
hiyo elimu bure itamtokea puani mtu tusubiri,walimu wameshakataa tamaa moyo wakufundisha haupo tena.mwalimu mshahara hauna tofauti namlinzii
 
Akitaka atekeleze Sera hii vzri na januari aboreshe maslahi ya walimu hasa mishahara,posho,nauli,nyumba n.k.Vinginevyo ni maigizo kama walimu walivyozoea.
 
Back
Top Bottom