Eid inakaribia, Mshahara Serikalini hakuna

Eid inakaribia, Mshahara Serikalini hakuna

Mie Simo

Member
Joined
Oct 17, 2013
Posts
58
Reaction score
24
Pamoja na kuwa Bajeti ya Serikali ilipitishwa kwa mbwembwe hadi leo HAZINA haijaweza kutoa fedha za Matumizi ya Kawaida na wala za Maendeleo. Tunavyoandika hata Ankara za Mishahara hazijatoka na Mwezi Julai ndio unakwisha. Kawaida watumishi wa Serikali hupokea Mishahara tarehe 23 ya kila Mwezi. Watumishi wanaingia kwenye sikukuu ya EID bila senti. Mwenyezi Mungu wanusuru wasianze biashara ya viungo vya binadamu.
 
Mhhhhh!


kp22072014.jpg
 
Hapa inabidi kufanya maarifa yoyote ili angalau familia ijisikie vizuri
 
Umelipwa mshahara wa siku 30 na sasa ni siku 23 una matumizi mabaya....acha ufuska
 
Umelipwa mshahara wa siku 30 na sasa ni siku 23 una matumizi mabaya....acha ufuska

Hesabu toka tarehe 23 mwez uliopita had leo siku ngap?siasa zinawatoa had akil kwa vile wewe unalipwa kwa sku ile buku saba
 
Ofisi nyingi za serikali hawaja-run payroll mpaka sasa....kwahiyo tegemea mchelewesho wa hali ya juu ndugu..
 
Kwahiyo eid el fitr ingekua tarehe 15 ungetaka upate mshahara tarehe 13???
Inaonekana siku kuu imekuchanganya kwakua mweupe mfukoni,
Kua mpole na ujifunze kuweka akiba.
 
Umelipwa mshahara wa siku 30 na sasa ni siku 23 una matumizi mabaya....acha ufuska
usifikiri wote wanalelewa kama unavyo lelewa wewe. Umri wote huo hujui hata bei ya kufuli lol!
 
Pamoja na kuwa Bajeti ya Serikali ilipitishwa kwa mbwembwe hadi leo HAZINA haijaweza kutoa fedha za Matumizi ya Kawaida na wala za Maendeleo. Tunavyoandika hata Ankara za Mishahara hazijatoka na Mwezi Julai ndio unakwisha. Kawaida watumishi wa Serikali hupokea Mishahara tarehe 23 ya kila Mwezi. Watumishi wanaingia kwenye sikukuu ya EID bila senti. Mwenyezi Mungu wanusuru wasianze biashara ya viungo vya binadamu.


Aseee acha n.sheeder yaan.hapa nawaza ntakulaje eid hakuna.cha oc wala mshahara hata kutudanganya na payroll pia hakuna sielew serikali hii
 
Wabongo kwa kulalamika!
Yani ndo kwanza tarehe 23 imeingia lakini asubuhi asubuhi mtu ameshaanza kulalama hata nusu ya siku bado!!!
 
Wapi Papaaa Bingwa wa Uchumi Mwigulu Nchemba

Hana jipya huyo,kapelekwa pale BOT kwa kazi maalumu ya kukwiba kodi za watanganyika ili wapate pesa za kuhonga wapiga kura wakati wa chaguzi.Tegemea hali mbaya kwani uchaguzi wa SM upo karibu,pesa yote itaishia kununa tshirt za kijani,kofia,viroba,kulipia mafuso ya kusomba watu kwenye mikutano,kufadhili tawi lake la act na kupika wali kwenye mikutano.
 
Umelipwa mshahara wa siku 30 na sasa ni siku 23 una matumizi mabaya....acha ufuska

Hivi unazijua siku 30 kweli? Kama ulilipwa tar 23 ya mwezi uliopita,hebu twambia siku hizo 30 zitaishia tarehe ngapi ya mwezi unaofuata? Tayari mapepo yameshaanza kukupanda? Muone Mch Lusekelo akuombee faster!
 
Back
Top Bottom